Absalom Kibanda: Mgombea Urais mmoja hakutaka nifike huu mwaka wa Uchaguzi

Absalom Kibanda: Mgombea Urais mmoja hakutaka nifike huu mwaka wa Uchaguzi

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
Mhariri Mkuu wa Kampuni ya New Habari, ambao ni wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania, Bingwa na Dimba, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) ndugu, Absalom Kibanda, amemtupia kombora mgombea Urais wa CCM. Kumbuka Kampuni ya New Habari, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) ni Hussein Bashe ambaye ni Msemaji wa Mgombea urais wa JMT Edward Lowassa.

Hapa nashindwa kuelewa Mhusika ni nani. Sababu siwezi kusema ni Membe sababu Membe alishatoa tamko kukana Kumdhuru Kipanda. Pitia hii thread Membe atoa tamko juu ya kutekwa kwa Kibanda na Waziri Membe akanusha kuhusika tukio la kumdhuru Mhariri Kibanda.

Kumbuka Bashe hawaivi chungu kimoja na Nape Nnauye. Na Nape Nnauye kaachiwa Jimbo la Mtama na Benard Membe. rejea hii Thread Bashe ajibu mashambulizi ya Nape Nnauye.

Akiandika katika ukurasa wake wa twitter kuhusiana na siku yake ya kuzaliwa, amesema, "Huu ni Mwaka ambao, Mgombea mmoja ambaye ni Mtangaza nia hakutamani niuone, Nimemsamehe!" Najiuliza huyo mtangaza nia ambaye hamtakii Mema Kibanda ni yupi?

Absalom Kibanda mwaka 2013, alivamiwa na watu wasiojulikana akiwa ndani ya gari lake wakati akiingia nyumbani kwake huko Mbezi-Beach, jijini Dar es Salaam majira ya saa sita usiku, akatekwa, kupigwa na kujeruhiwa ikiwa na kutobolewa jicho moja.
attachment.php

 

Attachments

  • Kibanda2.png
    Kibanda2.png
    25.5 KB · Views: 6,529
Bernard Membe huyo...alisema...katika nchi hii ana maadui 11 wawili ni wanahabari...na akiwa Rais watahama Nchi.

Poor Membe....Poor Membe...............Poor...........pooor.

Mkuu kwanza niweke wazi hapa.

Mimi si mccm, wala simuungi mkono Membe kwa lolote kwenye suala la Ugombea Urais.

Sasa turudi kwenye mjadara, hivi kunaconnection yoyote ya kuhusika kwa Membe kwenye Sakata la Kibanda? Kwamba Kibanda alikuwa akimuandika vibaya Membe kwenye Makala zake kiasi Membe achukie kiasi cha kumpeleka gorgota kule Mabwepande? Unaweza kunikumbusha Makala moja wapo ili mjadara upate uhai hapa?

BACK TANGANYIKA
 
Litakuwa kundi lile lile lililotaka kumpotezea mbali Dr.Harrison Mwakyembe kabla ya kuja kuona aibu ya mapokeo ya umma, wakamuacha. Dr.Mwakyembe pia ana bahati kuwa hai leo hii eti na katangaza nia sambamba na kuvchukua fomu urais
 
Kwanza kibanda hapaswi kujiita mwenyekiti wa jukwaa la wahariri, anatakiwa kujiita kibaraka wa lowassa. Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri hawezi kusimama getini na kuchagua waandishi wa habari wa kwenda kuzungumza na lowasa. NI hivi, wakati waandishi na wahariri walipokuwa dodoma kuzungumza na lowasa, huyu bwana alisimama mlangoni na kuanza kuchambua wa kuingia na wa kutoingia kutokana na vyombo vya habari ambavyo wanavipenda. kwa maana hiyo, kujiita mwenyekiti wa jukwaa ni kudhalilisha taaluma ya habari.mwenyekiti gani asiyeweza kutetea waandishi wake na badala yake kuwa kiungo cha ubaguzi kwa sababu tu ya kulamba watu kisiasa? kuna sababu gani za kulilia sheria ya kutambua uhuru wa habari wakati wanaotakiwa kuutumikia uhuru huo wakibagua waandishi wao wenyewe?

pia, tukio la kuteswa kwake, tunawezaje kushindwa kusema pengine alibeba mke wa mtu na jamaa alilipiza kisasi kuliko anavyokimbilia kutuaminisha kwamba kuna mgombea ambaye alitaka kukatisha maisha yake? kwa nini kama ana ushahidi huo asiende kwenye vyombo vya sheria? nachukia sana watu wanajivika ngozi za kondoo kwa umma wakati ni mbwa mwitu tu.
 
Mpuuzi sana huyu Kibanda, siku zote alikaa kimya ili iweje na mbona waliulizwa mara zote waliamu kuficha, ulikuwa ni uwoga ama kutuzuga watanzania?
 
Hivi huyu si ndiye aliyesema CHADEMA ndio waliomdhuru....?
 
Kweli ni EL kwani alikuwa anajua kuwa membe atagombea urais hivyo alitaka kumchafulia ili abaki peke yake. Lakini mungu hamfichi mnafiki na sasa anaumwa na kuna wagombea lukuki ambao wana sifa kuliko yeye. Pole fisadi muuaji wana siasa ambao ni kikwazo kwako
 
Waandishi wetu wengi njaa zinawafanya wasiwe wakweli. Nilishangaa Dodoma kwenye press conference na Lowasa wao ndio walikua wanampigia makofi na kushangilia
 
Huu ni umbea wa mtu mzima. Kibanda is a senior journalist kwanini asilipoti kwenye vyombo vya usalama au kumtaja mhusika kwa jina ila sheria ichukue mkondo wake? Alikuwa wapi siku zote leo uchaguzi anajifanya hoo one even if its all 37, the question is why now? Sipendi watu wanaotuhamisha kwenye mada. Huu ni muda wa mhimu sana katika nchi yetu inayohitaji mabadiriko ya dhati.
 
Siasa ni adui yangu...napita hivi kwanza....ila huyu Membe nahic kuwa ndiye atakaye kuja kuwa Rais wetu.
 
Back
Top Bottom