Hili si jambo jema hata kidogo,iwe ametekwa kwa sababu binafsi kati yake na mtu mwingine,au iwe ametekwa na kupigwa kwa sababu ya kazi yake bado nasema kitendo hiki hakikubaliki,lakini tatizo kubwa ninaloliona hapa ni wale wenzangu mimi tunaotofautiana kiitikadi,sisi wa upande mwingine hasa CDM tunaapokosoa utendaji kazi wa serikali hii ya CCM watu wengine wanakuja na hoja za kupinga na kusifia kuwa ni serikali sikivu na inayojali watu,na mbaya zaidi hata sisi wananchi tumeridhika na maisha haya,tumekubali kusubiri zamu zetu za kutekwa na kupigwa hadi kufa au kusalimika kama alivyobahatika Dr Ulimboka,maana kama tungelikuwa tunakataa kwa vitendo ndani na nje hakika hata wanaohusika kulinda usalama wa raia na mali zao wangekuwa wanafanya kazi zao ipasavyo,lakini leo hii tunakataa ndani tu nikimaanisha kupitia mtandao,kwenye laptop na simu,tunaandika sana baada ya siku mbili tatu tunasahau na kudandia jambo jingine.hapa kinachotakiwa ni kukataa kwa vitendo,ni kupinga kwa vitendo,tunapaswa kupaza sauti zetu kwa nguvu mchana na usiku tukipinga vitendo hivi vya kutekwa na watekaji kutojulikana na wala sababu ya kutekwa kwao,sasa tumebaki kusubiri zamu zetu za kutekwa na wote tulioko humu kwenye JF,Twitter,FB na mitandao mingine ni wajanja wa kuandika tu,na imekuwa kama fasion tu,iweje matukio ya kutekwa yanaendelea lakini hatujawahi kusikia watekaji wamekamatwa na sababu za kufanya unyama huo zikabainishwa?hivi hili sio genge la kihalifu kweli,maana baada ya kutekwa Dr Ulimboka nakumbuka kuna mama nae alitekwa na akauwawa huko kwenye msitu wa mabwepande na gari yake ilichomwa moto,nadhani matukio haya yaliendelea tena nadhani mtakumbuka,mwanasheria wa baraza la mazingira nae yalimkuta,nani yule wa bakwata Arusha,mapadri kule ZNZ yote haya ni matukio yanayotudhihirishia kuwa hakuna usalama wa raia wala hakuna Intelijensia isipokuwa pale CDM wanapotaka kufanya mikutano au maandamano ndipo utawasikia hao Intelijensia.
Wandugu,natoa wito kwamba,sasa tukataeni hali hii ya utekwaji kwa vitendo,ndani na njetupazeni sauti zetu kwa maandamano ya amani na tushinikize wahusika wajihuzuru kwani wizara hii imewashinda,Nchimbi aondoke na Mwema nae aondoke,Kova aende na wengine wote wanashughulika na usalama wa raia na mali zao,maana hakuna hata mtekaji mmoja aliewahi kukamatwa na akafikishwa mbele ya sheria.hata kama watekaji hawa ni serikali yenyewe basi tuikataeni,maana ni unyama unaoweza kumpata kila mtu pale ambapo wakijisikia kufanya hivyo.
Mungu na akujalie upone haraka Kibanda.