Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa

Polisi waanze uchunguzi na gazeti la tanzania daima na chadema. kwani hatuelewi ni kwanini alikimbia huko alipokuwa mhariri wa hilo gazeti la mwenyekiti wa chama.


inaonekana akili yako haina ushirikiano na na viungo vingine.kazae mtoto umwite chadema kama kama unaipenda.
 

kama mtu wa system kazi anayo...au?
 

Nashukuru kwa mchango wako Mkuu,
Kuna mambo makubwa mawili ambayo yanaweza kuwa yanalengwa, moja ni kukiua chama cha CDM kwa kulinki na mambo haya ikiwa hawa wanaoropoka watakuja kusema CDM inahusika. Hapo watakuwa wamewakasirisha wananchi dhidi ya CDM. Pili kutokana na lengo lao wanajua kuwa kwa kuwakasirisha wananchi kwa CDM kufanya hayo basi inaweza kutokea jambo kubwa kwa viongozi wa CDM kwa jina la kulipiza kisasi na tamko likitolewa na hawa wanausalama hakuna mwenye kubisha. Mbinu hizi huanzia mbali sana hadi kumfikia mlengwa, hawa wengine ni "Mbinu za Midani" au Camouflage, tusubiri tuone.

 
Polisi waanze uchunguzi na gazeti la tanzania daima na chadema. kwani hatuelewi ni kwanini alikimbia huko alipokuwa mhariri wa hilo gazeti la mwenyekiti wa chama.
Polisi ilishashindwa kuchunguza matukio ya hivyo, Waitwe FBI kuchunguza hilo, tena wapo hapo kisiwani tu.
 
Mkuu, hili ndiyo tatizo, nchi inapokuwa na taasisi kama polisi ambayo kwa undani ni kama crime syndicate kuna hatari hata ya kuchochea matukio ya uvunjifu wa sheria kuwa ni moja ya day to day work kwa kikundi cha watu wabaya huku watu wengine wakikosa hata imani na utendaji wake na matokeo yake pia ni watu kuanza kujichukulia sheria mikononi.
 
Mkuu una ushahidi ambao unamweka mtu uliyemtaja au umeamua kumtaja tuu
Maana ni bora usingetaja jina la mhusika ila wewe umejiaminisha kabisa kumtaja na jina
..hata mie nimeshangaa kuona anataja mtu..ila huwezi jua mtoa hoja ni nani..?
 
Naam na kabla ya sheria mkononi inaanza minung'uniko na hukumu binafsi, ambazo unaziona humu jamvini. Cha ajabu tunabishana badala ya kuona ukweli na kuwalazimiza wale woote wanaosababisha hali hii. Tunawaona tunawafahamu lakini tuko vilevile kila siku.
Nina uhakika Absalom Kibanda hakufikiri kuwa iko siku naye atatokewa na hili wakati aliposikia S. Kubenea na Tegambwage wamevamiwa au kuwa kuna mtanzania anawaza kuwa naye anaweza kupigwa na polisi bila sababu japo hili linatoke kila siku na wanaoshuudia washangaa au kucheka.
Hatuhitaji kutumia nguvu ispokuwa ni kuwaambia tu kwa kumanisha kuwa wapo kwa ajili yetu na sisi ndio waajili wao!.
Bila sisi wao hawana kitu. Au kuondoa utawala uliopo madarakani.

Asante!.
 
nimeona hivi tu nimekumbuka DR. Ulimboka. Tanzania imefika hapa ilipo? its hard to believe!!!

Tunaanza kuogopana wenyewe kwa wenyewe, watanzania ambao ukimwona mwenzio those days unajua usalama wako upo asilimia mia, leo hii jirani anagonga mlango wako hata kama ni mchana unapata wasiwasi --kweli ndugu zangu? laaaa!!!
 
Kuna shemeji yangu anafanya MOI amesema jamaa yuko kwenye hali mbaya sana. Halafu nikikumbuka kuwa alizaliwa siku moja na Chavez, nashindwa kabisa kujizuia kusikitika.

By IGUDUNG'WA
MUNGU amponye haraka

Unamlazimisha Mungu?

Mwanzo niliona kama Matola anakuonea, nilipoona nijiridhishe nikaona kuwa wewe sio mtu makini kabisa, wewe ni shabiki asiye jua hata anashabikia nini........mara useme unamuonea huruma Kibanda, anatokea mtu anamuombea kwa Mungu amponye, unageuka tena na kuonea wivu maombi ya mwenzio....fool
 
Poleni sana wanafamilia ya Kibanda. Hata kama uchunguzi utafanyika, itategemea ni nani aliyewatuma wavamiaji waliomteka Kibanda.

Na kutokana na mwendelezo wa matukio ya nyuma, na jinsi serikali ilivyozoea kukaa kimya, na wakati mwingine kutoa taarifa ya kupotosha watanzania kama ilivyokuwa katika ( majibu ya uchunguzi wa mauaji ya Mwangosi) ; basi haitakuwa ajabu hata uchunguzi wa tukio hili ukawa na vioja.

Inaonyesha hatua kubwa ya kuweza kufanya ulitakalo, ni kuwanyamazisha waandishi wa habari, ambao wanaandika maovu yanayo waamsha watanzania kujua uozo wa nchi yetu.

Waandishi msiogope, hakuna lenye mwanzo lisilo na mwisho, andikeni, andikeni, andikeni yaliyo ya kweli.
 
Polisi ilishashindwa kuchunguza matukio ya hivyo, Waitwe FBI kuchunguza hilo, tena wapo hapo kisiwani tu.
FBI wakichunguza kila kitu kuna haja ya kuwa na kitengo cha intelligencia na Police force kwa ujumla? yaani kama imefikia hatua wananchi tumeanza kuhoji uwepo wa taasisi hizi basi ni Janga lingine hili.
 
Awamu ya nne ya utawala Tanzania imekuwa na style mpya kabisa ambayo haikupata kutokea huko nyuma.
Matukio haya wala sio ya kufanyia kebehi hata kidogo maana sasa kasi yake imepamba moto. Tusimame kwa umoja wetu na kuyakataa haya
 
Kama kawaida, kwa kupitia jf, be the first to know, kuwa hivi sasa, juhudi zinafanywa kumhamisha Kibanda kwenda nchini Afrika Kusini kwa matibabu zaidi. Juhudi hizi zinaratibiwa na Jukwaa la Wahariri kwa ushirikiano wa karibu na baadhi ya wadau watakao gharimia safari hiyo!.

Japo ni kawaida kwa serikali kupeleka baadhi ya wagonjwa nje ya nchi, preference ya kwanza ya serikali ni kupeleka wagonjwa India kwa sababu its cheaper kuliko Afrika Kusini ambapo gharama ziko juu!.

Hili la Kibanda kupelekwa A. Kusini, linazidi kumshabihianisha Kibanda na Dr. Dr. Ulimboka, wote walivamiwa usiku na watu wasiojulikana, wote walifanyiwa jinai ya kudhuru mwili, wote walihudumiwa kwanza MOI, na baadae kupelekwa nchini Afrika Kusini, juhudi za kwanza ni kusafirishwa kwa michango ya wadau na baadae serikali ikatumbukiza mkono wake.

Mara ya mwisho kukaa na Kibanda ni mwezi Desemba, mara tuu baada ya kuhama Tanzania Daima, tulikutanishwa mahali na mwana jf Omar Ilyas, na miongoni kwa swali kubwa langu kwa Kibanda, nilidadisi ni kwa nini amehama Tanzania Daima kuelekea Mtanzania, alichonijibu nilibaki tuu kushangaa bila kumuamini. Kwa vile jibu lile lilikuwa off the record, lakini maadam haya yamentokea, naanza to connect the dots!.

Kwa sasa, tuendelee kwanza kumtakia uponyaji wa haraka na mengine yatafuatia!.

We keep on wishing him a speedy recovery and get well soon!.

Pasco
 
FBI wakichunguza kila kitu kuna haja ya kuwa na kitengo cha intelligencia na Police force kwa ujumla? yaani kama imefikia hatua wananchi tumeanza kuhoji uwepo wa taasisi hizi basi ni Janga lingine hili.
Hili ulipaswa ulielekeze kwa serikali yako sio kwangu maana Serikali imebuni mtindo mpya wa kusaidiwa na FBI kuchunguza masuala ambayo yapo ndani ya uwezo wa kawaida kabisa wa jeshi la polisi, so hata hili acha tu tuwapelekee FBI.
 

Ata mie alinipa jibu ilo ilo lakini..chadema wala Tanzania daima havihusiki apa!
 
Ooh boy.. tunamuombea apone.. ni matumaini yangu kuwa hili halihusiani na kazi yake ya uandishi.

Mambo ya ulimboka yameanza Tena

Tunaelekea wapi...Why Absalom? Anayesimamia anachokiamini,mwanahabari ...Majambazi! Haiingii akilini..kuna dots za kuunganisha hapa..

Kwa nchi yetu ilivyo sasa hivi kuna uwezekano mkubwa kwamba sababu kubwa ya kutekwa kwake inahusiana na kazi zake. Tusubiri tufahamu sababu, lakini inaweza kabisa isijulikane. Mungu amponye haraka.

Tina , asante kwa taarifa,
Kibanda we wish you a speedy recovery and get well soon!.
Pasco.

Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri Absalom Kibanda amevamiwa na watu wanaodaiwa ni majambazi akiwa anaingia nyumbani kwake. Amejeruhiwa vibaya ikiwa ni pamoja na kutobolewa jicho na sasa anatibiwa hospital ya Taifa Muhimbili (icu)

Wabaya wake wemetimiza dhamira yao


Kama uko duniani huwezi kosa mbaya, siyo jambo la kushangaza., kwani wabaya wake walikuwa akina nani?

Inawezekana ni sababu za kisiasa.

Haya mambo yanatokea sana system inapokuwa imefeli.hapa itaundwa tume! Waandishi mjifunze ili msimamie haki maana huwezi jua kesho ni nani!

Chama tawala kimefeli muda mrefu!

hivi unaweza kuwa mwanahabari wa new habari corporation halafu ukawa na uhasama na serikali ya ccm?

Ukitaka kuishi kwa amani tanzania nilazima uwe mtu wa kupundisha ukweli na kuubadilisha kuwa uongo. by the way you cat off

Tangia Mtanzania lilipoamua kuweka pua kwenye habari hii iliyopostiwa kwenye HII POST nilijua Kibanda anajihatarishia maisha yake.



Mnakumbuka kuwa siku mbili tu baada ya hii habari, RADIO IMAAN iliiripoti na Mtanzania, hasa mhariri wake akalaumiwa sana? Kwa mliobahatika kusikiliza yale matangazo ya RADIO IMAAN na waliokuwa wanaongea, mtajua kuwa Kibanda alikuwa ameuweka usalama wake mashakani.
Malaria Sugu alileta thread aliyohitimisha kwa kusema Aljaazira center inawataka Mtanzania wakanushe habari hiyo ndani ya siku saba


[Kwa bahati mbaya] baada ya ile habari, Mtanzania inasemekana waliendelea kuchunguza kuhusu kile chuo, na punde wangekuja na more detailed report.

Pole sana Kibanda...
 
Last edited by a moderator:
Awamu ya nne ya utawala Tanzania imekuwa na style mpya kabisa ambayo haikupata kutokea huko nyuma.
Matukio haya wala sio ya kufanyia kebehi hata kidogo maana sasa kasi yake imepamba moto. Tusimame kwa umoja wetu na kuyakataa haya
yes tisha toto style ya uongozi - hata mzee ukiona huna hela mfukoni na weekend ndiyo inawadia cha kufanya ni kuwa mkali kwa kila jambo ili asijitokeze either ze-wife au watoto kuomba hela.
Hili huwa siyo suluhisho bali unaongeza matatizo mengine yasiyo ya lazima.
 
Pole sana kibanda,tunakuombea kwa mola upone haraka. Wanaokuita mpiganaji leo wengi wao walikuita majina ya ajabu ilipotoka tarifa ya kuhama kwako toka free media kwenda habari corp...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…