Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa


Natumaini kuwa CHADEMA wamesikia na watakujibu. wakati wanamtesa Dr Ulimboka, kulikuwa na mgomo wa madaktari na tukio hilo waliliibua ili kuchochea mgogoro huo.

Walitegemea kuwa baada ya tukio hilo, makali ya mgomo yataongezeka na wao wachukue nchi kilaini kutokana na shinikizo la wananchi kama ilivyotokea libya, tunisia na misri.

Walisahau kuwa Tanzania si nchi ya Kiarabu. mgomo uliisha na Dr Ulimboka amepona. Sanasana wanamfanya ulimboka aishi kwa kificho kutokana na kumsingizia mambo mengi ya aibu ikiwa ni pamoja na kulawitiwa na kuharibiwa nyeti zake. Leo hii kila anakopita anaitwa shoga.

kuhusu hili tukio la bwana kibanda, huyu mtu alikuwa mhimili mkubwa sana kwa CHADEMA wakati akiwa mhariri mkuu wa gazeti la Tanzania Daima.

Walimtumia katika mambo mengi sana ikiwa ni pamoja na propaganda dhidi ya ccm na serikali yake. bila shaka anayo mengi moyoni.

kuondoka kwake Tanzania Daima hakukuwa kwa heri. CHADEMA wakati wote wana hofu kuwa siri zao zitavuja kama wanavyofanya vijana akina SHONZA na MWAMPAMBA. kwa vile kibanda anazo taarifa nyeti kifuani kwake, suluhisho waliloliona ni kumteka ili wamuue.

Pia wamempofua macho ili asiendelee kutumikia katika ajira yake ndani ya New Habari Corporation. Mungu hajataka hayo.

Na hilo walilifanya kwa kuamini kuwa hawataguswa tena kama ilivyokuwa kwa ulimboka kwa vile Kibanda ana kesi dhidi ya serikali na kwa hiyo serikali ndiyo itakayolaumiwa tena.

hizo ni mbinu mbaya za kutaka madaraka na ni mbinu chafu dhidi ya raia wasio na hatia. Halafu lazima watanzania tuhoji uadilifu wa hawa viongozi wa CHADEMA, pamoja na kulelewa na kufanya kazi za kanisa, wamekosa huruma dhidi ya viumbe wasio na hatia.

Wana visasi ambavyo havina mfano wake. Si watanzania mnakumbuka tukio la kifo cha wangwe? tafakari na chukua hatua
.
 

kwa taarifa yako hakuna hata nchi moja imeweka ulinzi kwa kila mwananchi. tanzania itawezekana? vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vinajitahidi lakini havipati msaada wa kutosha kutoka kwa wananchi pamoja na kuja na maboresho kadhaa kama vile ulinzi shirikishi na polisi jamii
 

Tatizo kubwa hawa watu hawana mafunzo ya kutosha. sijui wakichukua nchi hali itakuwaje. security organ zao zinaonyesha failures nyingi.
 

Wanafunzi wanaofeli kabla ya mtihani huwa na akili kama zako. Kama maboresho hayaleti tija kwa jamii maana yake maboresho ya tija bado hayajafikiwa/hayajafanyika.

Kikubwa ni kuendelea kutafuta njia mbalimbali za kukabiliana na tatizo siyo kulikubali tatizo (kusurrender). Bado naamini kabisa serikali iliyoamua kabisa, inaweza kuondoe matukio ya ajabu ajabu kama haya.

Kuhusu vyombo vya usalama kutokupata ushirikiano kutoka kwa wananchi, nakataa, hakuna polisi anayeweza kufanya upelelezi bila kuwahoji wanachi kwa namna moja au nyingine.

La sivyo hakuna kazi inayofanywa na polisi. Polisi upelelezi hawezi kupeleleza kwa kuwahoji polisi upepelezi wezake. Sema labda ushirikiano umepungua kulinda na wananchi kukosa imani kwa vyombo vya dola.

Kama mwananchi, raia mwema, anatoa taarifa ya uhalifu halafu taarifa inapenyezwa kwa mhusika kwa sababu ya ushirikiano uliopo kati ya wahalifu na askari, unategemea kuendelea kupata ushirikiano?.

Kama vyombo vya dola havipati ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wananchi, huo ni udhaifu wa vyombo vyenyewe kwani kazi yake ni kukusanya taarifa kutoka vyanzo mbalimbali na kuzifanyia kazi.
 
Mbona hili tukio linafanana na la Dr Ulimboka? Maana huyu nae ameng'olewa meno na kucha, sielewi hapa huu mchezo ukoje?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 

Nasema tena haiwezekani na kwa tanzania haiwezekani kabisaa maana watu wana visasi na wana tamaa ya kuingia madarakani kwa nguvu.

Hivyo wanatumia kila hali kuzua matukio ili ilaumiwe serikali. ila kama sote kama jamii tukiamua kukataa matendo haya na tukaweka hofu ya Mungu mbele basi hali itatulia.
 

Kweli kabisa, hawa wanasiasa ni watu atari sana, wanawezaje kuvikoroga vichwa vya watu wazima na akili zao.
 
Mbona hili tukio linafanana na la Dr Ulimboka? Maana huyu nae ameng'olewa meno na kucha, sielewi hapa huu mchezo ukoje?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

soma post namba 461 upate undani wake
 
Mbona hili tukio linafanana na la Dr Ulimboka? Maana huyu nae ameng'olewa meno na kucha, sielewi hapa huu mchezo ukoje?

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

Si ili kuendeleza episode na kutaka kuendeleza upuuzi ule wa ULIMBOKA badala ya watu kuleta mada za maana.
 
mazingira ya kazi waandishi wa kazi ni magumu kwa tanzania ,hufurahia sana pale wanapopewa bahasha kwa kuandika habari nzuri ,bahasha isipotolewa kwao mazingira ni yanageuka na kuwa janga ,nampa pole ndugu kibada apone haraka
 
mazingira ya kazi waandishi wa kazi ni magumu kwa tanzania ,hufurahia sana pale wanapopewa bahasha kwa kuandika habari nzuri ,bahasha isipotolewa kwao mazingira ni yanageuka na kuwa janga ,nampa pole ndugu kibada apone haraka

mkuu, kwan alikataa bahasha? nani alimpa na akaikataa? nadhani wewe unao ukweli wa tukio hili. hebu funguka uwaeleze watz kinachoendelea
 

Naona umejiandaa vyema kulumba. KIBANDA alikuwa na ugomvi na Tanzania Daima tangu alipoacha kazi huko, sasa hapa vyombo vya ulinzi vinalaumiwa , nadhani tungeanza na kuwalaumu hawa wahasimu kwa kuvipa kazi zisizo za lazima kwani vyombo vyetu vya ulinzi vina mambo mengi ya kusimamia.
 
Natumaini kuwa CHADEMA wamesikia na watakujibu. wakati wanamtesa Dr Ulimboka, kulikuwa na mgomo wa madaktari na tukio hilo waliliibua ili kuchochea mgogoro huo.

.......

Watu kama nyie ni sumu kubwa kwa taifa hili. Ungekuwa ni mtu mwenye busara, ungeacha vyombo vya usalama ambavyo ndio wataalamu wa uchunguzi wa matukio kama haya vikafanya kazi yake badala ya ku-jump on conclusions zinazoongozwa na hisia hasi na za kishetani kama zako.

Kwa hivyo mtu ye yote anayehama chama na kujiunga au kuunga mkono chama kingine akiugua, akafanyiwa vitendo vya kihalifu, akapata ajali, ama akafariki - basi conclusion ni amefanyiwa na watu wa chama alikotoka! Kweli tutafika kwa uwendawazimu kama huu.
 
Tehthe, hivi huyu sio mtu mmoja anaandika halafu anajiunga mkono na kujipinga hapo hapo kwa ID nyingine?


Atongwele


Today 12:07

#467


Senior Member Array


Join Date : 22nd February 2013

Posts : 229

Rep Power : 347

Likes Received
19

Likes Given
3






mkiristoMwislamu


Today 12:39

#476


Senior Member Array




Join Date : 21st February 2013

Posts : 156

Rep Power : 333

Likes Received
10

Likes Given
0
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…