Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa

Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa

Last edited by a moderator:
Umbeya mtupu; serikali inayoshindwa kulinda usalama wa watu wake haina maana. Elimu mmeshindwa..... Kilimo mmeshindwa........ Umeme mmeshindwa...... Afya mmeshindwa...... Hata usalama wa watu na mali zao umeshindwa? Aibu kuubwa

tunaweza ngono na kung'oa meno ya watanzania wezetu, kuficha hela uswisi, kuimba chama chao cha matapeli cha haribu nchi
 

Nasema tena haiwezekani na kwa tanzania haiwezekani kabisaa maana watu wana visasi na wana tamaa ya kuingia madarakani kwa nguvu.

Hivyo wanatumia kila hali kuzua matukio ili ilaumiwe serikali. ila kama sote kama jamii tukiamua kukataa matendo haya na tukaweka hofu ya Mungu mbele basi hali itatulia.

mbona akili yako haifanyi kazi vizuri? serikali ina kila kitu usalama wa taifa, polisi, jeshi, hela, wanashindwa nini kubaini watekaji kama sio wao wanaotekeleza hayo yote? kama unaonama chadema ndio wanafanya hivyo ingekuwa ametekwa napi, au hata mtoto mmoja wa kiogogo ungeona kama usalama wa taifa unafanya kazi au. Mama malichela alifanyiwa unyama morogoro waliofanya unyama huo wako wapi leo? walisakwa hata uvunguni kwa hili wala msitafute mchawi serikali ndio inahusika kwa 100%
 
Nadhani tunaelekea mwisho wa safari yetu ya kuteswa na kunyanyaswa. Ni dalili za kuanza kwa hatua mpya za kujenga nchi yenye tumaini jema la maisha. Ni kipindi cha mpito kufikia kilele cha kujitawala. Hii ni hatua muhimu sana katika kujenga Taifa lenye falsafa ya Kidemokrasia. Damu ya Kibanda Absalom na wengine wote waliozimwaga damu zao katika ardhi hii yenye dhambi, wametupatia wino wa kuiandika historia ya mapinduzi katika Taifa huru lisilo na Uhuru.

Pole sana mwanahabari wetu, nadhani hilo ni zao hasi la kundi lililoshindwa kuielewa falsafa yako. Tunakuombea Mungu upone salama.
 
Umbeya mtupu; serikali inayoshindwa kulinda usalama wa watu wake haina maana. Elimu mmeshindwa..... Kilimo mmeshindwa........ Umeme mmeshindwa...... Afya mmeshindwa...... Hata usalama wa watu na mali zao umeshindwa? Aibu kuubwa
nao ni mchango pia. ila unashindwa kuelewa chanzo cha tatizo unarukia kwenye matawi na matunda
 
mbona akili yako haifanyi kazi vizuri? serikali ina kila kitu usalama wa taifa, polisi, jeshi, hela, wanashindwa nini kubaini watekaji kama sio wao wanaotekeleza hayo yote? kama unaonama chadema ndio wanafanya hivyo ingekuwa ametekwa napi, au hata mtoto mmoja wa kiogogo ungeona kama usalama wa taifa unafanya kazi au. Mama malichela alifanyiwa unyama morogoro waliofanya unyama huo wako wapi leo? walisakwa hata uvunguni kwa hili wala msitafute mchawi serikali ndio inahusika kwa 100%

Waliomfanyia uhuni mama ...Ikiwemo kumpora pesa,Vito binafsi...na kumdhalilisha kijinsia kwa Hali ya juu....ni wahuni waliokodishwa toka Bagamoyo wakiongozwa na Hussein Gogo.......ndio maana Mara myinginee huwa na wasifu wanasiasa kwa kusamehe.....hungeamini...Kama familia ya mzee ...ingesamehe kitendo hiki...kwa miendendo ya baadhi ya wanafwamilia hiyo Humu ndani tunaona walishasahau Hilo
 
jamaa ni big time looser.huwezi jidanganya kuwa ukimtunza mamba basi ipo siku ukimpa mkono ataulamba,same to ccm,ccm ni washasi sana siku hizi ni kumu kukaa nao usiwa provoke. Hata ukicheka kushangilia mpira wanahisi unacheka ujinga wao.ukisogea wanah4si 2015 imefika na unata waongoa.imenikuta live sehenu.kwa ujumla cc ni km cell za kansa watengeneza problem halafu wanatumia nguvu zaidi kujenga mkanganyiko ili wabaki na confused people.ccm ikipewa hata ikipewa nchi bila upinzanzi wa cdm itaimplode kwa hasara ya watanzania.
Huyu jamaa ni mfano mwingine wa loosers ,km alijiona kuwa nae ni TISS na alichokuwa anafanya ni kuokoa taifa basi ndivyo ilivyokula kwake ,wenzi ndio tiss wa maisha bora,.wala shmuhurumii asiyejihurumia,.asubiri zawadi za akina mwakyembe,mwandosya,ulimboka na wengine kwa bima isiyo rasmi.Nchi hii bado inapokea amri toka hell,ingwa sheikh yahya kaenda chukua post huko.
 
Jaymmoh hapa kenya.mie namtakia afueni ya haraka.natumai walitua salama afrika kusini.ubinadamu kweli uliwatoka wanadamu!
 


cleardot.gif

Wateswe au wauawe wangapi ndipo tustuke?


Na Ndimara Tegambwage
MWANDISHI wa habari Absalom Kibanda, amevamiwa. Akapigwa. Akachokonolewa jicho. Akachomolewa kucha. Akakatwa kidole. Akang’olewa meno. Akaachwa kufa nje ya lango la nyumba yake iliyoko mtaa wa Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam.

Ni usiku wa kuamkia jana, Jumatano. Hivi sasa Kibanda, mhariri mkuu mtendaji wa New Habari Media Group – kampuni inayochapisha magazeti ya Mtanzania, Rai na The African, yuko taabani kitandani.

Aliyofanyiwa Kibanda ni yaleyale aliyofanyiwa Dk. Steven Ulimboka, kiongozi wa madaktari katika mgomo mkuu wa mwaka jana wa kushinikiza serikali kuweka mazingira bora ya kazi katika hospitali zake kwa kununua vifaa, dawa na kutoa mishahara inayostahili.

Dk. Ulimboka aliburutwa kwenye lami. Akakunjwakunjwa kama godoro na kuingizwa kwenye gari dogo. Akapigwa mara kwa mara kwa fimbo, makofi na mateke. Akang’olewa meno na kucha; akatupwa kwenye msitu wa Mabwepande, kilometa 45 nje ya jiji la Dar es Salaam. Aliponea chupuchupu.

Kwahiyo, mbinu zilizotumika kumtesa Kibanda siyo mpya. Zimewahi kutumiwa. Unaweza kusema haraka kuwa waliomtesa mwandishi, ama wamesomea chuo kimoja au ni walewale waliomtesa Dk. Ulimboka.

Je, baada ya Kibanda, nani? Lakini kabla ya Kibanda, nani? Mwaka 2008, watu watatu wakiwa na panga, chupa yenye tindikali na gongo la mti, walivamia chumba cha habari cha gazeti la MwanaHALISI tulimokuwa tumebaki wawili.

Walifanikiwa kummwagia tindikali machoni, mwandishi na mkurugenzi mtendaji wa kampuni inayochapisha gazeti hilo, Saed Kubenea. Hakupofuka kabisa lakini lazima aende India kila baada ya miezi minne kuchunguzwa macho.

Nakumbuka kunyukana na vijana wawili – mmoja mwenye panga na mwingine mwenye gongo – hadi panga lililolenga katikati ya kichwa lilipokoseshwa shabaha, kutua kwenye kisogo kulia na kudondokea nyuma yangu. Nilishonwa nyuzi 15. Nani alikuwa amewatuma?

Desemba 2009, mwandishi Frederick Katulanda wa Mwanza, alivamiwa nyumbani. Wavamizi walikuwa wakipaza sauti na kudai kuwa ana nyaraka za akaunti za benki za halmashauri ya jiji la Mwanza.

Walikuwa na mapanga. Walikuwa wakichagizana kwa kusema, “Kata kichwa! Kata kichwa!” Waliondoka na mafaili. Walimwachia kilema mguuni na makovu mikononi.

Mwaka 2006, waliojiita wananchi wakazi wa jiji la Mwanza, walikusanywa na kufanya maandamano makubwa kwa walichoita “kupinga mwandishi Richard Mgamba kuandika uongo” na kudai kwamba alikuwa Mkenya na “siyo raia wa Tanzania.”

Hii ilikuwa baada ya filamu iitwayo “Darwin’s Nightmare” kuonyesha jinsi wananchi wakazi wa jiji wanavyokula mapanki badala ya samaki.

Mgamba alidaiwa kuwabeba watengeneza filamu na kuwaonyesha maeneo ambako kweli kunguru na binadamu walikuwa wanagombea mabaki (mifupa) ya samaki baada ya viwanda kunyofoa minofu ya kuuza Ulaya. Mgamba alilazimika kuwa “mkimbizi” jijini Dar es Salaam.

Sept 2010 wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu, katika eneo la Nyambiti, jimbo la Sumve wilayani Kwimba, mkoani Mwanza, mwandishi Frederick Katulanda alivamiwa na kupigwa na watu wapatao 15 waliojiita “Green Guard” – wa “chama cha kijani.”

Katika “kumshughulikia,” Katulanda anasema, walikuwa wakionyesha kuwa na ujuzi mkubwa wa judo na karate huku wakidai kuwa anawaandika “vibaya” Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mwaka 2011 mwandishi Richard Massatu alikutwa amekufa katika eneo la Igoma, jijini Mwanza. Vyombo vya habari viliripoti kuwa macho yake yalikuwa yametobolewa na kuwekwa gundi aina ya super glue; mguu wa kushoto na mbavu vilikuwa vimevunjika.

Vyombo vya habari viliripoti kuwa Massatu aliyekuwa mmiliki na mhariri mkuu wa gazeti la Kasi Mpya (sauti ya umma), alionekana mara ya mwisho usiku wa kifo chake akiwa na maofisa wa polisi na usalama katika baa iitwayo Cross Park katika eneo la Igoma.

Daudi Mwangosi, mwandishi wa kituo cha televisheni cha Channel Ten aliuawa kwa kupigwa risasi katikati na mikononi mwa polisi na hasa mbele ya mkuu wa polisi wa mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda.

Hii ilikuwa tarehe 2 Septemba mwaka jana. Kesi bado iko mahakamani. Picha zinazoonyesha Mwangosi alivyolipuliwa, zinatia simanzi kwa kila anayethamini utu.

Mwaka huu, tarehe 3 Januari, maiti ya mwandishi Issa Ngumba iliokotwa katika pori la mlima Kajuruheta, kijiji cha Mhange, wilayani Kakonko katika mkoa wa Kigoma.

Ngumba alikuwa mwandishi wa habari wa Redio Kwizela. Alikutwa amekufa baada ya kutoweka nyumbani kwa siku tatu.

Mwandishi wa habari Erick Kabendera anayeishi Dar es Salaam, anaishi kwa wasiwasi. Wazazi wake waishio Bukoba, wamehojiwa na “ofisa usalama” kwa kile kilichoitwa “uhalali wa uraia wao.”

Kabendera, ambaye ncha ya kalamu yake haipindwi kwa woga wala upendeleo, amekuwa akiripoti kupigiwa simu na kutishiwa kwamba “atarudishwa kwao.” Naye hajui kwao kwingine isipokuwa Tanzania.

Juzi, Jumanne, mwandishi Charles Misango wa TanzaniaDaima, alishindwa kurudi nyumbani kwake, Kimara nje kidogo ya Dar es Salaam.

Kwa siku nzima familia yake ilishinda ikiripoti watu tofauti waliokuwa wakifika nyumbani kwake wakimuulizia na wengine kuzengea nyumba tu.

“Nilipomwambia mhariri wangu juu ya hali hiyo, aliniambia ‘usiwe mjinga; nenda ukalale hotelini.’ Nilikwenda kwa rafiki yangu mwenye ua mkubwa, nikaegesha gari na kulala katika gari langu kwa kuwa alikuwa na wageni wengi,” anasimulia Misango.

Misango ni mmoja wa wahariri wanaokabiliwa na tuhuma za “kuandika uongo.” Kesi yao iko mahakamani jijini Dar es Salaam.

Kuna orodha ndefu ya waandishi wa habari waliotishwa na wanaoendelea kutishwa; waliopigwa na polisi na askari magereza (Ukonga, Dar es Salaama) kwa tuhuma mbalimbali; waliotishiwa maisha kwa simu na hata kwa kufuatiliwa na watu wasiowafahamu.

Miezi mitatu iliyopita, ilivumishwa kuwa Ansbert Ngurumo, mhariri mtendaji wa sasa wa TanzaniaDaima amefariki. Taarifa hii ilipelekwa pia kwenye mtandao mpana na unaoheshimika wa Jamii Forum (JF).

Hakuna ajuaye kama hakukuwa na nia ya kuua au kudhuru Ngurumo. Livumalo lipo na Ngurumo alipewa ushauri wa “kuwa makini” kwani kila uvumi una shina lake.

Ngurumo amekuwa muwazi siku zote kuelezea jinsi baadhi ya walioko madarakani walivyoshindwa kumshawishi kuwapenda, kuwanyenyekea na hata kufanyakazi nao.

Tatizo lililopo ni kwamba kila janga lilipotokea, baadhi ya waandishi walijitenga na kusema, “Shauri yao, nao wamezidi.” Nani amezidi wapi? Kumekuwa na tabia ya kujitenga na kubaguana.

Huko tuendako, baada ya kujikata kutoka shina kuu la wanataaluma, tunakuwa kama vifaranga vya kuku visivyo na ulinzi wa mbawa wala kelele za mama. Tunajianika mmojammoja kwa mwewe kututafuna mmoja baada ya mwingine. Tutaisha!

Nani atalinda maisha ya waandishi wa habari Tanzania? Tayari mmoja yuko kariku kufa kwa woga. Aliwaambia wenzake jana kwenye viwanja vya hospitali ya Muhimbili (MOI), “Labda tutafute makazi nje hadi mwisho wa utawala wa awamu hii nne…”

Huu ni woga, labda ni upumbavu pia. Kwamba kumekuwa na taarifa za madai ya kuua waandishi wawili maarufu wa habari na wanasiasa wawili mashuhuri; siyo sababu ya kukimbia nchi.

Kuwa na umoja katika taaluma, kuandika zaidi na hasa kuandika ukweli; kuchunguza, chambua na kufafanua zaidi – kuweka jamii wazi juu ya kinachoendelea – hivi vinaweza kuwa ngao kuu kwetu sasa na huko tuendako.

Bali tujenge mashaka juu ya mfanano wa mbinu za kutesa na kuua. Watesaji na wauaji waweza kuwa watu walewale. Wako wapi? Tuwasake na kuwaanika. Tunaweza katika umoja wetu.

Mwisho
 
mkuu, kwan alikataa bahasha? nani alimpa na akaikataa? nadhani wewe unao ukweli wa tukio hili. hebu funguka uwaeleze watz kinachoendelea
waandishi weledi na watiifu ni wachache mkuu wengi wao ni wa bahasha
 
Kwa Kibanda kukubali kujiunga na Mwananchi Communication kwa wengine ilionekana kama ameweka wazi msimamo wake juu ya makundi yanayohasimiana ndani ya CCM na kwa msimamo huo inawezekana ikawa sababu ya kundi moja kuwa na hasira, kinyongo na chuki juu yake.
 
Mambo ya ulimboka yameanza Tena

Tulishawazoea hawa, sasa mtu atakuwa akivamiwa na mateja huko alkiwa amelewa na atakuja humu ataanza propaganda zake mara hoo, Wamening'oa meno, kucha kumbe matake wamemfanya kitu mbaya.
 
Kwa Kibanda kukubali kujiunga na Mwananchi Communication kwa wengine ilionekana kama ameweka wazi msimamo wake juu ya makundi yanayohasimiana ndani ya CCM na kwa msimamo huo inawezekana ikawa sababu ya kundi moja kuwa na hasira, kinyongo na chuki juu yake.

CDM hawa, ndo wameona kama kwenda kwake huko anakwenda kuweka hadharani mbinu wanazozitumia CDM kuwalaghai watanzania. Mbona mpaka sasa hivi jamaa yetu mzee wa Karatu kimya? anjipanga ili akija kutunisha nyusi zake tuamini anachokisema hata kama hi hisia zake.
 
tunaweza ngono na kung'oa meno ya watanzania wezetu, kuficha hela uswisi, kuimba chama chao cha matapeli cha haribu nchi
Hii style waliyogundua ya kutekeleza matukio ya kiuhalifu, lazima tutakwisha kwa sababu wanajua kabisa hivi sasa serikali inachonganishwa na wananchi kwa hiyo watakuwa wakifnya kwa uhuru huku wakijua lawama ni kwa serikali, tazama huyu naye. Hivi tunafikiri tunaikomoa serikali au tunajikomoa? badala ya kuipa ushirikiano serikali katika kupambana na hawa halafu tunaendekeza siasa za kupaka matope, hakika tusipoangalia tutakwisha.
 
CDM hawa, ndo wameona kama kwenda kwake huko anakwenda kuweka hadharani mbinu wanazozitumia CDM kuwalaghai watanzania. Mbona mpaka sasa hivi jamaa yetu mzee wa Karatu kimya? anjipanga ili akija kutunisha nyusi zake tuamini anachokisema hata kama hi hisia zake.
CDM inatumiwa kama kibwagizo cha wimbo lakini maudhui ya wimbo yako kwingine. Watu wanauhakika wa usalama wao wanatenda uhalifu ndani ya nchi jinsi watakavyo na hakuna anayewauliza zaidi ya kuambiwa na mamlaka husika kuwa huo sio uhalifu.
 
mbona akili yako haifanyi kazi vizuri? serikali ina kila kitu usalama wa taifa, polisi, jeshi, hela, wanashindwa nini kubaini watekaji kama sio wao wanaotekeleza hayo yote? kama unaonama chadema ndio wanafanya hivyo ingekuwa ametekwa napi, au hata mtoto mmoja wa kiogogo ungeona kama usalama wa taifa unafanya kazi au. Mama malichela alifanyiwa unyama morogoro waliofanya unyama huo wako wapi leo? walisakwa hata uvunguni kwa hili wala msitafute mchawi serikali ndio inahusika kwa 100%

Ukweli hauwezi kulazimishwa mkuu, punguza munkari na utoe hoja umshinde mwenzako badala ya kung'aka. Serikali haiwezi kuhusika eti kwa saababu haijawakamata wahusika, ingekuwa hivyo basi Marekani wanaosaka magaidi huku na kule basi tuwaite ni magaidi kwa vile mpaka leo hawajawakamata baadhi ya magaidi. Ujue kama hicho ni kikundi cha MAFIA kimejiandaa kutekeleza mauaji , basi hata kazi ya kuwabaini inahitaji umakini sana, Mimi naamini Serikali imejipanga vizuri na lazima washukiwa watakamatwa tu. Hizi zingine kelele za kisiasa, hata hivyo hakuna jambo la kushangaza kwa serikali kulaumiwa hasa ukizingatia kuwa majukwaa yanyotumika kufikisha ujumbe wa kupotosha dhidi ya serikali ni majukwaa aidha yanamilikiwa na vyama vya siasa au wansiasa wenyewe.
 
he, makubwa. kwa hali hiyo wataendelea kuandamwa na matukio mabaya kwa vile kuna watu wanawaumiza kwa tamaa za bahasha

wakiendekeza tamaa za kupenda bahasha na kuwasaliti wenzao, lazima wataendelea kuuawawa kwa kuwa wenzao wanaowasaliti watataka kulipiza visasi
 
Back
Top Bottom