Absalom Kibanda: Namuogopa Abdurahman Kinana

Absalom Kibanda: Namuogopa Abdurahman Kinana

- ha! ha! ha! ha! ha! saafi sana hii ina maana hamna hoja, mimi sigombei Urais wa Jamhuri kama Rais wenu anayeiba wake za wananchi, hajawa Rais tayari anaiba wake za wananchi je akiwa itakuwaje? ha! ha1 ha!

Le Mutuz!!

dah! aisee kweli ujinga hauchagui umri, umbo, jina wala familia...
 
kina bado anawatoa jasho mpaka mnaanza kupoteana namna hii kiasi leo kibanda ambae amekua akiwachekesha kila siku kwa kuandika mnayopenda kusikia mnamuona nae hana maana kabisa,iko siku mungu wenu slaa mkija kumgundua kama anatumiwa na lowassa mtamuweka kikaangoni but itakua too late
 
kina bado anawatoa jasho mpaka mnaanza kupoteana namna hii kiasi leo kibanda ambae amekua akiwachekesha kila siku kwa kuandika mnayopenda kusikia mnamuona nae hana maana kabisa,iko siku mungu wenu slaa mkija kumgundua kama anatumiwa na lowassa mtamuweka kikaangoni but itakua too late

- Thubutu nani huko Chadema anaweza kumkaaanga Rais Slaa? Hivi bro unajua kuwa kile chama kinaongozwa na Mke wa Slaa na hakuna wa kusema fyoko huko? Kile sio chama ila ni NGO ya Slaa, Mke wake, Ndesamburo, Lissu, Zitto, na Mbowe pamoja na Mtei basi!

Le Mutuz!!
 
- Thubutu nani huko Chadema anaweza kumkaaanga Rais Slaa? Hivi bro unajua kuwa kile chama kinaongozwa na Mke wa Slaa na hakuna wa kusema fyoko huko? Kile sio chama ila ni NGO ya Slaa, Mke wake, Ndesamburo, Lissu, Zitto, na Mbowe pamoja na Mtei basi!

Le Mutuz!!

Seriously una umri gani mkuu. Nauliza hivi nikiwa sina mfungamano na chama chochote kile
 
Mkuu Mtoi
Umeandika mengi kuhusu safu ya uingozi wetu hebu niwekee msafi wa kimaadili hapo Chadema uongozi wako umejaa watu wachafu wa kimaadili na mafisadi watupu nionyeshe ni nani msafi hapo!

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Labda anapalilia u DC...

hujaona kwenye makala anasema alienda na mwenzake kwa kinana sasa ni DC akifikiria hilo anagundua ni saa ya kulamba matapishi kalamu aliyotumia kuhamasisha mabadiliko ndo anaitumia kuyazikia .ni nooma kwa msomi je mwananchi wa kawaida tshert inampumbaza zaid yake
 
Absalom Kibanda kwanza dhamani yake ilikwisha siku nyingi mno amebakia Naibu mhariri mkuu ( ANSBERT NGURUMO) tu wa kona ya maswali magumu. Huyu jamaa labda anatafuta pia kusalimika kwenye kale ka kesi huyu jamaa namuunganisha na Theophil Makunga wa Mwananchi aliyeungana na Nchimbi kusema kuwa polisi hawakuhusika kumuua Mwangosi Iringa.

Ila wakati akitumiwa na Magamba akumbuke kile ambacho madiwani waliodanganywa kusaliti CHADEMA na Umma Arusha mjini wamefanyiwa nini sasa mwanzoni walibebwa na STK kwenda kwenye kesi waliposhindwa wakadanganywa wakate rufaa sasa wanastaili kulipa gharama za kesi Mkurugenzi hapokei simu zao tena waliowaahidi kuwa watawasaidia hawapokei tena cm kazi yao kwisha hao ndo MAGAMBA atambue hilo.
 
Kwa mtu yeyote anayeijua tanzania mabadiliko ya ccm hayawezi kuwapa ushindi hata kidogo vijana wengi hawamjiu kinana,wala mangula au khatibu,bali vijana wengi wapiga kura wanajua ccm ni chama cha mafisadi full stop.

S
isi watu wazima tunamjua kinana alivyo fisadi mkubwa nchini na data zake chadema watazianika miezi mitatu ya mwisho 2015. Kitendo chake cha kuripoti ofisini na kanzu ni ishara tosha ya yaliyojificha kwa kuwalaghai wapuuzi wachache wa kiislamu kuwa CCM ni ya kiislamu.

H
ivi mchungaji msigwa akiigia ofisi za chadema na nguo za kichungaji gazeti la uhuru na tbc wangwaambiaje watanzani chadema ni cha kikristo.

Philip Mang'ula hajui mabadiliko mengine yeyote zaidi ya kuona umaskini ukiendelea kwa watu wa kawaida huku mafisadi hawaguswi,hakuna mwanaume atayeweza kumgusa rostam au lowasa hivyo hatujaona gamba likivuliwa au koti, CCM ni chama cha kulindana kwa maovu siki zote.

K
inana na mangula hawandai mazingira ya taifa la kesho bali wanalinda mafisadi wa leo.tunahitaji mabadiliko 2015 n​a sio kuirudisha ccm ni kosa la jinai.
 
- Tangu lini umesikia Faida ikasoma hasara unaona unavyojivua nguo hapa mtumzima kwamba wewe ni hasara kuliko, ebo jibu hoja wacha kukimbia kivuli hapa, kufilisika mawazo ni kushindwa Udiwani viti 22 kwa 5, nakudai eti unakubalika zaidi na wananchi that is kufiklisika mawazo!! na mtaendelea kupewa za uso tu!!, nyie Chadomo tuliwaachia sana sasa jino kwa jino, mwendo ni nginja nginja!! tena kwa lugha mnayoijua vizuri sana!!

Le Mutuz!!

Huna hadhi ya kujibiwa maana tayari nakuona HASARA
 
Nimeifuatilia sana mada kwa kusoma mawazo ya watu bila kuchangia. Na hapa sitachangia bali nitaendelea kusoma mawazo ya watu.

Kuna huu mchango wa mwandishi nguli ninaye mheshimu sana (Richard Mgamba) mshindi wa tuzo za CCN.

Amechangia haya kwenye makala hii kwenye moja ya mitandao kuhusu makala ya Kibanda.

"Wasifu mzito na historia za kutukuka? Ninaheshimu sana mawazo ya Kibanda lakini nashindwa kujizuia kuhoji baadhi ya sifa alizotoa kwa hao anaowaita wateule. Kwanza ni kweli CCM imefanya ilichokifanya, lakini kinachotia shaka ni sifa wanazopewa hawa watu.

Mathalan, Kinana amekuwa Waziri wa Ulinzi, Spika wa Bunge la Afrika Mashariki, na hatimaye akawa kampeni Meneja wa Mkapa na Kikwete—sijui katika kipindi hicho alilifanyia taifa hili kitu ghani cha kutufanya tuseme ana wasifu mzito na historia iliyotukuka. Kampuni ya kinana na wenzake hawajalipa mabilioni waliyochota NSSF kwenda kujenga kiwanda cha madawa mikocheni—na mradi ukafa mpaka leo. Hizi siyo fedha za serikali, ni fedha zetu sisi watanzania wafanyakazi. Kamuulizeni, akikana mnione.

Pili, Philip Mangula alikuwa katibu mkuu kwa miaka kama kumi hivi wakati wa Mkapa, na akatuhumiwa na wana-mtandao hawa hawa kwamba alihongwa na kundi la Sumaye ili kumuhujumu JK katika mchakato wa 2005. Siyo hilo tu wakati wa kuchotwa kwa mabilioni ya EPA pale benki kuu upo ushahidi mkubwa kwamba alihusika kutoa recommendations kwa baadhi ya wachotaji kwa sharti la kwamba asilimia fulani inakwenda katika chama.

Ushahidi upo na kama mnabisha katafuteni maelezo ya wakili Maregesi katika tume ya kuchunguza ufisadi huu, na pia ya kwake yeye Mwenyewe Mangula mbele ya tume.

Zakhia Meghji ndiye mliyemshambulia hapa katika vyombo vya habari kwamba hafai kuwa waziri eti kwa sababu ni fisadi tangu akiwa mali asili na hatimaye wizara ya fedha. Au mnataka kutuambia kwamba zile kashfa zilikuwa za kutunga ili hatimaye wateule wenu waingie katika baraza la mawaziri?
Mwigulu Nchemba naye anayo historia iliyotukuka ambayo iliandikwa lini na wapi?

Napata shida sana kuona tunakuwa wepesi wa kutoa sifa badala ya kusubiri kuona utendaji wa wahusika hawa. Mangula alipogombea uenyekiti wa CCM akapigwa chini akalalama kama Sumaye na kusema uongozi ndani ya chama umekuwa ni wa kulangua kama bidhaa, lakini leo amerejea katika nafasi ya juu kwenye Chama ambacho uongozi unauzwa kama bidhaa.
Kwa kifupi, hawa jamaa ni wale wale waliokuwepo juzi, jana, na leo—hivyo kuwapa sifa kibao ni ushabiki usio na kifani. Tusubiri tuone makeke haya ya kuanza kwa mbwembwe—na hii ni kawaida ya CCM, maana hata 2006 walianza kwa kutembelea masoko yetu, kukagua madaraja, na sifa kibao, lakini leo, hali imegeuka. Kazi ipo".

Haya ndiyo mambo Kibanda alipaswa kuyatazama anapompamba mtu wa aina ya Kinana na Mangula maana tayari facts zipo lakini kwa kuwa maandiko yake mengi ni ya kimahaba na kimaslahi zaidi amejikuta anaweka mkono wake ndani ya koti la Kinana na kusahau kila kitu.
 
Seriously una umri gani mkuu. Nauliza hivi nikiwa sina mfungamano na chama chochote kile
Unapoteza muda wako kaka.Huyu jama ni HASARA anatokea Mtera jirani na kwa Lusinde unategemea nini kwake?
 
- Thubutu nani huko Chadema anaweza kumkaaanga Rais Slaa? Hivi bro unajua kuwa kile chama kinaongozwa na Mke wa Slaa na hakuna wa kusema fyoko huko? Kile sio chama ila ni NGO ya Slaa, Mke wake, Ndesamburo, Lissu, Zitto, na Mbowe pamoja na Mtei basi!

Le Mutuz!!

Uko sahihi sana mkuu sema hawa chadema kata wa humu hawajui kinachoendelea,wanaburuzwa tu kama misukule,nasikia wametangaza kuajiri makatibu wa wilaya,sasa subiri uone watakaopata ajiri hizo watakua ni kina nani na kutoka kanda gani hapa nchini
 
Absalom Kibanda,
-On the way to NEW HABARI CORPORATION.
 
mkuu ukitaka kuvua gamba ni vyema ukaanza na kiini cha Gamba hilo. vinginevyo utakua unachekesha. kinana tamaa imemrudisha kwenye uongozi umri aliokua nao hawezi kufanya mabadiliko yoyote ndani ya chama kibaya anatembea na mafisadi anakula na wezi anaishi na wauza nyara yeye mwenyewe ni mshirrika ndo mana anazomewa
 
Huu ni wakati wa Vijana kufanya mabadiliko.Hatuhitaji sare kuonyesha hilo,ila kwenye nyuso va vijana,utatambua hilo.Vijana tushikamane ili kuhakikisha CCM inaondoka 2015.Hata vitabu vitakatifu vinasema,mabadiliko yataletwa na Vijana.
 
haya ni mawazo huru ya absalom kibanda, naunga mkono uhuru wa maoni
 
Bado naendelea kusoma michango ya wadau kwenye hii makala iliyo ibua mjadala murua kabisa kufuatilia.

chama sina muda wa kukujibu aanika ufisadi wa chadema kwa vidhibitisho.

Huu hapa ni mchango wa mwandishi wa kujitegemea na wakili wa mahakama kuu Bw Nyaronyo kicheere kwenye moja ya mitandao kuhusu makala ya Kibanda.

"... Kwanza lililosahaulika ni kwamba wakati wa loliondogate (enzi za mwandishi katabalo) ilidhihirika dhahiri shahiri kuwa kinana aliwasindikiza waarabu hadi kia wakisafirisha twiga, fisi, nyumbu, pundamilia hai na mizoga. kasomeni gazeti la mtanzania la miaka hiyo.

Pili, kinana na wenzake akina mwinyi na ole njoolai, na hata meghji walionekana mara kadhaa wakienda kuswali swala ya jamaa loliondo siku mwarabu mwenye mapesa akiwepo loliondo akiwinda. sasa usiniulize njoolai mkiristu na rais mstaafu wanakwenda ijumaa kuswali!

Tatu, kampuni ya faclon dry cleaners ya kinana ilianzishwa kwa kutumia mashine zinazodaiwa kuwa zililetwa nchini kwa ajili ya kufulia nguo za wagonjwa (mashuka, vitambaa, na taulo) kwenye hospitali ya mkoa wa arusha ya mount meru wakati huo kinana akiwa mbunge wa arusha mjini.

nne, kinana na mangula ndio walisimamia kampeni za kuingia madarakani mkapa na kikwete na ndio watu pekee wanaofahamu kwa undani fedha zilipatikana kuwezesha uchakachuaji wa kura na ndio pekee wanaofahamu utaalamu wa kuiba kura. kilichofanyika hapa ni kuwaweka mahali panapostahili washambuliaji hatari wa timu ccm yaani kuwarejesha kwenye namba zao fulustopu. msijifanye kusahau au kutojua".
 
Last edited by a moderator:
Huu ni mchango mwingine kuhusu makala kwenye mjadala mchangiaji akijulikana kwa jina la Mchili.

Yeye anasema...
"Bila ya kujua nia na dhamira ya Absalom Kibanda kwenye safu hii, ningependa kuamini labda anawaasa wapinzani kuwa uwezo wa hawa viongozi wapya kutekeleza azma ya CCM kubaki madarakani kwa njia zozote zile ni mkubwa kuliko wale walioondolewa km Msekwa na Mukama. Kama hivyo ndivyo nadhani amevuka hata mstari kwa kuwapa umahiri wasiostahili.
Having said that, a soldier preparing for war should never underestimate the enemy.La msingi zaidi ulilozungumzia ni uwepo wa hii safu "mpya" wakati wa msimu wa maovu makubwa yaliyotendwa na CCM au serikali yake. Uuzaji wa tunu za taifa pamoja na kugawa raslimali zetu kwa makampuni ya kigeni bila faida ya kimsingi kwa taifa yamefanyika chini ya uongozi huu huu.

Ufisadi uliokithiri ulitendeka wakati hawa wakiwa ni viongozi waandamizi wa Chama. Kwa mfano, Kinana amekuweko kwenye kitchen cabinet ya CCM miaka yote tangu wakati wa Mkapa hadi leo wakati wa Kikwete, na tujuavyo maamuzi mengi ya Chama hufanyika kwa consultation kupitia vyombo vyake, na kwa hiyo CCM imedorora wakati wakitoa mawaidha yao Sekretariat na Nec. Wizi wote wa kura na mikakati ya kushinda kidhalimu kama kununua kadi na kuweka wakala pandikizi kwenye vyama vya upinzani tangu 1995 umefanyika chini ya uongozi wa Kinana.

Unyang'anywaji ushindi chama cha CUF na kubatizwa kwa udhalimu huo huko visiwani 1995, 2000 na 2005 umefanyika chini ya uongozi huu wa CCM. Na hapa wala sijataja Mwembechai au Pemba kwani yamefanywa na serikali inayosimamiwa na uongozi huu "mpya" na haukuwahi kulaaniwa na Chama.Kwa haya na mengine, sioni sababu ya upinzani kuweweseka eti kwa vile kuna viongozi wapya waliotukuka - Kinana, Mangula, Mehji nk.

Wamekuwako wakati nchi ikiingizwa kwenye mfumo wa kifisadi na hawawezi kusimamia vita dhidi ya ufisadi ambayo ndilo tatizo kuu la zama hizi. Na kama inavyonong'onwa, bila shaka na wao ni sehemu ya muhimili wa ufisadi nchini. Hawa si ndio walihalalisha rushwa kwenye kura kwa kuibatiza na kuiita takrima?"
 
Back
Top Bottom