Acha lawama, ni wewe ndiye unayepaswa kuwajibika juu ya maisha yako

Acha lawama, ni wewe ndiye unayepaswa kuwajibika juu ya maisha yako

Kulaumu hakubadilishi mambo kuwa mazuri. Bahati mbaya sana watanzania tunapenda sana kulaumu. Kwa mfano: hatupaswi kulaumu serikali bali tunatakiwa kutumia haki yetu kuiondosha madarakani pale inaposhindwa kutumiza majukumu na kama inatumia ulaghai wa kuiba kura, na sisi tutumie nguvu kuwaondoa.
Haswa
 
hiyo ni kwasisi wanaume tu!.
Hata wanawake waache, mwanamke asilalamike mwanaume wake kuchepuka, bali akae chini na kujiuliza kwa nini anachepuka, akigundua mwanaume ni tabia yake na yeye hawezi kuendana na hiyo tabia anapaswa kujistaafisha kwenye hayo mahusiano. Lawama hazihitaji maana huyo mwanaume hakutafutiwa
 
Mwisho wa siku ni wewe:
1. Ukiwa Bora ni wewe
2. Ukiwa lofa ni wewe
3. Ukiwa mjinga ni wewe
4. Ukiwa mzembe ni wewe
5. Ukiwa masikini ni wewe
6. Ukiwa tajiri ni wewe
7. Ukiwa hodari ni wewe
8. Ukiwa mbivu ni wewe
9. Ukisubiria bahati ni wewe
10. Ukichukua hatua yakuona fursa ni wewe
11. Ukiwa na mawazo hasi ni wewe
12. Ukiwa na mawazo chanya ni wewe

...............ongezea kwa sababu ni wewe.......
 
Nakubaliana na wewe 100%. Kwa mfano sasa hivi, tuache kuilaumu CCM na tuingie barabarani kuiondosha kwenye madaraka kwa sababu inazidi kuleta umaskini.
Ingia mwenyewe barabarani kwasababu wewe ni masikini wenzio sisi sio masikini tunafurahia nchi
 
Ingia mwenyewe barabarani kwasababu wewe ni masikini wenzio sisi sio masikini tunafurahia nchi
Jiongelee mwenyewe, huyo tajiri mwenzako umeongea naye saa ngapi?, by the way hakuna tajiri anayesema kuwa ni tajiri.
 
Jiongelee mwenyewe, huyo tajiri mwenzako umeongea naye saa ngapi?, by the way hakuna tajiri anayesema kuwa ni tajiri.
Huo umasikini upo kwenye ukoo wenu sisi kwenye ukoo wetu sio masikini barabarani ingia wewe na ukoo wako ambao ni masikini msiongelee wengine
 
Just calm down!.. jiangalie wewe...wewe ndiye kiongozi wa maisha yako, hata kama ni katika hali duni kiasi gani, muamuzi wako ni wewe.
 
Leo tunakuzwa katika misingi ya kujitetea na kukwepa kuwajibika karibu katika kila eneo. Hatujifunzi na hatutaki kukubali kuwa tunapaswa kuwajibika asilimia mia moja juu ya maisha yetu na badala yake tunawatafuta wa kuwatupia lawama.

Ni kweli yapo mambo mengi yanayoweza kutokea nje ya uwezo etu ila hayaondoi wajibu wetu juu ya maisha yetu. Hatuwezi kuizuia mvua kunyesha ila tunaweza kukwepa au kujilinda mvua isituloweshe.

Mchezo wa lawama " blame game" ni mchezo wa wasiopenda kuwajibika juu yao. Ni mchezo wa kujiliwaza na kuhamishia majukumu yako kwa wengine kana kwamba na wao hawana majukumu yao. Unayemlaumu na yeye analaumu.

Umasikini na uzembe mkubwa umejificha kwenye mchezo wa lawama. Mduara mzima wa umasikini na uzembe kivuli chake kikuu na faraja yake ni lawama. Lawama hutuaminisha kuwa yupo aliyepaswa kuwajibika juu yetu na siyo sisi "anayetusaidia kuishi maisha yetu"...ah!..ah...

Lawama humfanya mtu kujiona yupo sahihi sana "malaika"'ila wengine ndiyo wanaomkosea na kumfanya kuwa alivyo. Ukweli unaouma ni kuwa "tupo tulivyo kwa sababu tunataka haswa kuwa hivi tulivyo". Hakuna lugha rahisi zaidi ya kuumiza Ili kumfanya mtu kuona uchungu juu ya hali yake na kuchukua hatua.

"You are the master of your life"
Vp na wale wanaolamu chama cha siasa ...kuwa wako hapo kwa sababu ya hiko chama🤔🤔
 
Vp na wale wanaolamu chama cha siasa ...kuwa wako hapo kwa sababu ya hiko chama🤔🤔
Mchezo wa lawama haukosi sababu ndugu, unakupa liwazo na pumbazo la kutosha unajisahau kuishi maisha yako unabaki na bila fulani ningee.... bila Chama X ningee..... mwisho wa siku "it is too late to catch the train".
Vicious cyle of ........
Hao jamaa wanajichelewesha wenyewe ila kama wapo humu nina uhakika Jamii forum inatia elimu tosha linabaki suala la mtu binafsi.
 
Ukweli mchungu. Tumebaki kulaumu mifumo tuliyoikuta bila kufanya mabadiliko (kupambana).
 
Back
Top Bottom