Acha shule fanya biashara

Kuna wafanya kazi. Kwani Mengi alikuwa na elimu ya Masscommunication? Mbona alikuwa ana miliki vyombo vya habari?
Wakina Anton Dialo sijui elimu yake ila mbona anamilik vyombo vya habari?

Mengi alikuwa na ndoto hadi za kiwanda cha Madawa je kasomea Udakitari?

Aisee kinacho hitajoka ni kuinitiate Idea tu.

Ndo maana kukawa na Labour.

Entrepreneurs ni the Owner of factor of productions
1. Land
2.Capital
3.Labour

Mengi au Chrstopher Gachuma anamilika kiwanda cha Soda cha Nyanza bottle kule Mwanza. Huyo ni Darasa la saba, hana elimu ya Food technology but ana milik kiwanda cha Vyakula.

Ana Ma IT ana wahasibu na kila kitu. Je hapigi hatua?

 
Ni bora tukaenda na mifano basi. Wafanya biashara wengi wa Tanzania ni Darasa la saba ukitoa wahindi hao.

Je wamepiga hatua au la?
wamepiga hatua kwa kulinganishwa na nani? maana biahara nyingi za watanzania wazawa hazidumu zaidi ya kizazi kimoja zinakuwa zimeshasamabaratika, tofauti na za wazungu ama wahindi, unadhani tatizo ni nini kama sio elimu?
Hii ndio inapelekea hata top 10 ya matajiri Tanzania ni wahindi na waaarabu, japokuwa wao ni fraction ndogo sana ya population yetu.
Matajiri wa Tanzania wangejifunza namna bora ya ku manage utajiri wao vizuri, ku expand na kuchukua oppotunity mpya nadhani tusingekuwa na hali hii
 
Kwani Maada inasemaje? Nazani ni shule Formal Education.

Tunazungumzia Formal Education na sio Elimu Dunia.

Mada inahusu elimu rasimi
Shule sio majengo wala vyeti..., hata yule anayekwambia wapi mzigo unapatikana ni shule kwahio usiache hata siku moja kujifunza maisha yako yote...., masuala ya vyeti n.k. ni status ambayo unaweza kuitumia pia kuingiza kipato..
 
Mampuni hata ya Wazungu wana funga kila siku. Google uone bisshara za wazungu zinazo filisika kila siku orodha itakushangaza.

Wamepiga hatua Kitanzani unataka tuawalinganishe na Billgate?

Kibongobongo ni matari yes na hawatakufa masikini
 
Kwani Maada inasemaje? Nazani ni shule Formal Education.

Tunazungumzia Formal Education na sio Elimu Dunia.

Mada inahusu elimu rasimi
ndio maana nikasema shule in real sense ni ujuzi mtu anaopata, na kikawaida unapatikana katika formal institutions ingawa mwingine anaweza kuupata chini ya mwembe na mwingine akaenda kwenye hayo majengo a hasiupate.., kina Faraday huwezi kusema hawakuwa educated au mtu anayekwenda university kufanyiwa assignment yupo educated.., au huwezi kusema sababu mfanyabiashara imara akienda shule akili zake za biashara zitafutika.., bottom line its acquiring knowledge
 
Tatizo Bongo ndoto za maskini zinapoteleaga pale kwenye matokeo ya 4m6. Unataka Medicine lakini tokeo halitaki sasa unajikuta huna nmna inabidi ukasome kozi yoyote chuo alimradi upate na mkopo maana hata ukitaka kulazimisha unachotaka labda uanzie ngazi za Diploma unajikuta huna ada, haya ukienda kusoma kozi hizo zingine ndo hapo mtu anamaliza hana interest na alichosomea anarudi mtaani kusema Elimu ya chuo haijamsaidia
 
Mampuni hata ya Wazungu wana funga kila siku. Google uone bisshara za wazungu zinazo filisika kila siku orodha itakushangaza.

Wamepiga hatua Kitanzani unataka tuawalinganishe na Billgate?

Kibongobongo ni matari yes na hawatakufa masikini
ndio kuna zinazokufa na kuna zinazopiga hatua kubwa nyingi zaidi, ndio maana wao ni matajiri kuliko Waaafirka weusi
Pengine umeshindwa kunielewa hapa ninachosema kuwa mtu wa darasa la saba sio kwamba hawezi kufanikiwa
Ila atafanikiwa zaidi endapo akiongeza maarifa yake zaidi ya elimu tu ya shule ya msingi

Nikakutolea mfano kuwa biashara za matajiri wengi weusi sio kubwa ukilinganisha na za wahindi ama waarabu, achilia mbali za wazungu, na pia zinakufa mapema zaidi.
Sababu wahindi, waarabu, wazungu wana elimu, na elimu ni muhimu katika ku manage na kukuza biashara
 

Mkuu unaposema hazipigi hatua una maana gani?labda kwa mtazamo wako.
Kuna rafiki yangu anaitwa Mshamu jamaa kwa Sasa ni mfanyabiashara mkubwa,yes ni mfanyabiashara mkubwa kwani tangu anaanza from scratch akiwa na kibanda tu cha machinga kisicho zidi mtaji wa million moja hadi sasa anaakiba si chini ya million 500 bank.
Ana assets za kutosha ana maduka 2 ya jumla,ana Duka 1 la rejareja,ana mashine za kusaga na kukoboa nafaka 2+ package ya unga.
Ana Duka la mazao ya nafaka 1,ana Chanja 1,Amazon Gest 2 na sasa anajenga Rodge 1 ya kisasa lakini ana Nunua mazao huko vijijini.Hadi hapa ninapoandika hii comment anameshanunua tani 43 za korosho huko Lindi.
Kingine ambacho nilitaka kusahau ni kuwa amesoma mwisho darasa la 4 akaacha shule.

Kwa mtazamo wako Je,jamaa huyu Biashara yake imepiga hatua ama laa.

Nakuhakikushia asilimia kubwa ya matajiri kwa Hapa Tanzania na Dunia ni watu ambao hawana elimu ya darasani ila na wanayo elimu ya pesa.
 
Kwani Maada inasemaje? Nazani ni shule Formal Education.

Tunazungumzia Formal Education na sio Elimu Dunia.

Mada inahusu elimu rasimi

CHACHA ninachokiona Mimi watu wanachanganya Kati ya elimu rasmi na hii elimu ya isiyo rasmi(based on field).
Watu wasichokijuwa kuwa elimu inapatikana mahali popote pale kulingana na lengo la mhitaji/mahitaji ya muhusika hivyo elimu ya darasani haina uhusiano na kuanzisha ama kukua kwa Biashara ya aina yoyote.
Kwa sisi ambao hatuna elimu ya darasani huwa tunawatumia watu wenye formal education as our leverage.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Nimesema hawapigi hatua? hapa nazungumzia relative hapa, kila mtu anapiga hatua ila kuna wanaopiga hatua kwa spidi kubwa zaidi na wanafika mbali
Biashara nyingi za Kibongo japo zinapiga hatua ila zinafanywa kienyeji na zinakufa haraka ukilinganisha na za wazungu, wachina, wahindi ama waarabu ambao wameelimika. Hapa ndio utofauti wa anayepuuza na asiyepuuza elimu unaonekana.

Top 10 ya matajiri Tanzania ni wote ni wahindi na waarabu, na biashara zao zinakuwa kwa kasi. Ukiwa na spirit na kipaji cha ujasiriamali ukiongeza na elimu mafanikio ndio yanakuja haraka na yanakuwa sustainable zaidi. Ndio hapo watu weusi tunapigwa bao kwa sababu ya kudharau elimu
 

Nimekupa story ya one of my friends ambaye alianza Biashara from scratch na sasa wapi alipo nilitegemea ungenipa maoni yako katika Hilo....

Lakini suala la hatua ni pana sana na linategemea malengo/ndoto za mwenye Biashara kwanini nasema hivyo,kila mfanyabiashara anakuwa na lengo lake katika ku win market (local or international level).Kama mfanyabiashara A alikusudia kusambaza huduma kijijini kwao na amefikia kijiji chote basi huyu tunasema amekuwa(amepiga hatua)

Alafu kuhusu elimu hakuna anaekataa umuhimu wa Elimu.Jaribu kusoma Katika post yangu ya kwanza kabisa utajuwa msimamo wangu ni upi katika elimu Mkuu.Ili ufanikiwe katika chochote kile kinahitaji elimu na ujuzi thabiti kuhusu uwanda huo,lakini suala lililopo Je elimu hiyo ni ipi?
Hapa ndo tunapisha sasa, kwasababu mjasiriamali/mfanyabiashara anayo elimu tayari ijapokuwa sio ya shuleni/Chuo.
Education has nothing to do with school and college.
 
mwenyewe sijasema lazima aende shule au college, elimu inapatikana kwingi sasa hivi. Lakini lazima tukubaliane kuna elimu ya msingi ambayo mtu akitaka kujiendeleza hata mwenyewe kiurahisi lazima awe nayo

Pia mfanyabiashara akifikia alipokuwa anaota kupafikia, hatakiwi kusema basi nimeshakamilisha na uwe ndio mpaka wake, kama potential ya kukua zaidi ipo, jitanue zaidi na zaidi

Ndio maana tulikuwa na simu za mezani, wakaona haitoshi, wakaleta za mkononi, wakaona haitoshi, wakaleta zenye intaneti, wakaona haitoshi, wakaleta simu janja na maendeleo yanakuja kwa kutoridhika na ulichonacho
 
Tafuta elimu itakayoendana na biashara yako mkuu.
 
Kipimo unacho wewe mwenyewe maana maisha ni yakwako.
Kwangu mimi kila kitu kinanafasi yake
 
Mwenye elimu anaona elimu haina maana.
Asiye na elimu anahitaji elimu. Tafurani!!!!!
 

Kuhusu elimu naona tumefika muafaka kuwa si lazima iwe college education or school but inaweza kupatikana sehemu yoyote ile inategemea na muhitaji.

Kwa upande wa Biashara hilo ni sahihi kabisa kuangalia namna ya kujitanua zaidi.Na hii inachagizwa na malengo ya mfanyabiashara mwenyewe.
Naona mfano wangu wa kwanza kuhusu rafiki yangu unaukwepa.
 
rafiki kafanyaje, sijakuelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…