Acheni tu taarabu ni tamu, na zinafunza jamii haswaa!

Hahahahaha waapeee

Alokupa kiti wewe cha kukalia,kumbi akanipa mimi
Ni Mungu si mwenginewe usijitie tafrani,na kunitoa thamani
Kwa vipi unibeue mara juu mara chini,humkumbuki manani
Chuki ziondoe kwangu yatizame yalo yako

Sabah Salum Muchacho
 

Umaskini haunidhuru,wala haunipi joto!!

Kama namuona bi mkubwa na wigi lake!! Kuna waliojaaliwa sauti bwana
 
Last edited by a moderator:
Ulipotoka kwenu nyambizi, sisi tulikupokea wewe, na vibahasha vya hirizi, shingoni umevivaa. Ukafundishwa vivazi wewe na kitanda ukapewa wewe, wajifanya siku hizi, wajifanya unajuaaa. Mdomo umeuchonga wajifanya unajua by khadija kopa

Achia ngazi bibi mchuma unaondoka huo, achia ngazi bibi mchuma unaondoka huo. Umeshachelewa naondoka naye umeshaishiwa nina dunda naye. Kipi cha kung'ang'ania hakutaki ebu timu, mtu mzima hovyo unajieshua mtu mzima hovyo unajieshua

Huna lolole hutonibabaisha, nenda usojijua, huna lolote hutonishughulisha nenda usojijua. Huna sura huna mwili vimekutoka vibavu, utavaaje kimini na usafiri mbovuuuu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 

Dah! Long time.
Thanks.
 

Huku kwetu wala hazifiki, wapo kina Marijan, Mbaraka Mwishe..., chidumule enzi hzo, mpoto, mpoki, fm academia, twanga pepeta. nikija pwani utani huu... sana!
 
Alokupa kiti wewe cha kukalia,kumbi akanipa mimi
Ni Mungu si mwenginewe usijitie tafrani,na kunitoa thamani
Kwa vipi unibeue mara juu mara chini,humkumbuki manani
Chuki ziondoe kwangu yatizame yalo yako

Sabah Salum Muchacho

Aahahhaha wacha niendelee na ya mwahawa ally...
Japo mimi masikiniiiii
Katu sijiweki nyuma
Sababu naziamini
Rehema zake karima

Ipo siku ntawini
Mtanyamaza kusema
Ntamegewa na mimi
Zilizo njema rehema

Kwakua maajaaliwa yake rabana
Yake rabana siweki fundo moyoni
Yeye ndie anaetoa humoa amtakae
Wala hajamuonea yule mja akosae
Hana hiyama manani
Napaa sitokufuru nikakesha ugangani

Nipatacho nashukuruuuu
Ndio riziki yangu ilopangwa ardhini
Kanifariji afuru saada na suudi zake

Umaskini haunidhuru wala haunipi joto
Roho tanda nimepoa
Kwa kipi nidhalilike
 

Wewe bongo star search inakuhusu sana, naamini sautiyo ipo mulemule.
 

Maashaallah!!

Kilo changu hakikai,najinyima nawapa nyie
Mie mbaya leo hii,wema mmekua nyie
Nashukuru Alhamdulillah,Mungu awazidishie
Awape mema maslahi,shida msizisikie

Ng'ombe wa maskini
 
Seleleaaaa...
Cheza na mimi mpenzi...cheza nami kwa henezi mambo mazuri ya habibi ndo hayataki haraka!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…