Binti Magufuli
JF-Expert Member
- Apr 2, 2011
- 7,479
- 5,157
- Thread starter
-
- #121
Samahani dada naomba kama una Full stop wa Khadija Kopa uniwekee hapa, si mpenzi wa Taarabu lakini huu wimbo nimetokea kuupenda mbaya
Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
"Aaaa Mungu kanipa kauli nzuri niongee na watu kwanini wasinipendeeeee"
Msiniite mswahili japo mie mtanzania nazungumza kiswahili na kiswahili asili yangu. Wanajamii taarabu zinamafunzo kweli kweli na huwa hazichoshi kusikiliza. Mfano huyu mdada Leyla Rashidi verse zake zimeenda shule sana.
"Kizingiti cha manani ni mtihani kwa mja, hata uwe mashakani usisite kumtaja"
"Kauli ya molaaaaaaa silaha nzitoooo alipangalo ndilo litakuwaaaa"
Leyla Rashid & Jahazi Modern Taarab - Fungu La Mungu Sikosi - YouTube.
Hivi mnikumbushe na ule wa marupe rupe ndio unasemaje vile?
CC
Wapenzi wenzangu wa nyimbo za mwambao
aah basi wenzanguuuuu
huo si ujabariiiiiii
hayo ni maruperupeeee
nyinyi si mungu mpunguze wenu munkari naye mapepe e ee ee
kosa langu kukaaa nanyi vizuri .............................
Mrembo by Nature sijui ndi hivo, maana nausikiaga tu nahuwa unanivutia kuusikia
Taarab ni music mzuri mno!Travetine Magomeni nilipelekwa mwaka huu kuangalia Taarab kwa mara ya kwanza toka nizaliwe;Kwa kweli nakiri nimepitwa na mengi kwenye music huu!Yule Mzee Yusuf anajua taarab!
Mrembo by Nature wapi naweza pata collection ya taarab za zamani kama vile sikutegemea kama ww una mambo; Sanamu la Michelin;Mambo ipo huku;utalijua Jiji;Nafanya hesabu sipati jawabu(kuruka ukuta);Muhogo wa Jang'ombe na zinginezo nimpe dada yangu kama zawadi bday yake maana yy anapenda mno taarab!
Mm nipo Ikolo-Kyela na kama inawezekana wasiliana na DEMBA tujue bei na malipo yake na how tutapata huo mzigo!
CC DEMBA
Hahahahahah dada Mrembo by Nature mie naja na hiii ya mwanahawa ally
Umaskini wangu haunipi tahayuri
Bure mkinikebekhi ni ya mola takadiri
Mimi sizijali stihizai zenu walimwengu
Katu sitobadilika nikauza utu watu....
Nna amini kupata na kukosa ni jaala yake mungu
Sizijali istihizai zenu walimwengu
sitodhalilika nikauza utu wangu
Natangaza hadharani nimekinai
Nimekinai umaskini wangu
Naapa sitodhalilika nikauza utu wangu
Japo mimi maskiniiii
Kwani lipi la ajabu
Nimeumbwa nimeumbwa
Hakuna mtimilifu sote ni waja wa mungu
Yake mola mtihaniii
Ntapasi naamini
Siinyongi roho yangu
Inshaallah mola muweza atanipa langu fungu.
taarab za zamani hakuna kuchambana kama za sasa.
Juma bhalo(marhum) nikimsikiliza ni burudani kwakweli.
Taarab nzuri ni hizi http://m.youtube.com/playlist?list=pl737184672a53a3ae&hl=en&guid=&gl=gb&client=mv-rim
Heaven on earth wewe fun wa miondoko ipi? mie ilimradi unaitwa muziki tu. baasi hapo hunitoi napenda kila aina ya mziki..mie taarabu imenipitia pembeni.....ila huyu Patricia huwa ananikosha sanaaa.......
Sasa wezi wa mabwana nawaaambia nitawachakachuaaaa
Sina mimi sina, mwingine zaidi yako weweeee
Sina mimi sina, atakayekushinda weweeeee
Ni wewe hakuna mwingine anipendezaye
Wala kulingana nawe simuoni huyooo *2
Ni wewe peke yako unitoshayeee
Nimetaka kukuwekeawimbo wa Coast Taarabu-Kukupenda isiwe tabu, basi tu nimeshindwa.
Nilitaka kukwambia nisije kuta unaimba huo badala ya kuwachakachua wezi wa mabwana
Hewalaaaa...huu wimbo naukumbuka sana kwani enzi hizo za ujana wangu wenyewe tukijiita 'cheki bobu' basi kulikuwa na binti namsarandia akiitwa kwa jina Sina.
Sasa wimbo huu nilipotoa tu dedikesheni kwa binti Sina, ukawa umenirahisishia kazi ngumu ya tongozo (vijana wa zamani wanajua jinsi tongozo lilivyokuwa ni kibarua kigumu kama cha kuchuna ngozi ya kitimoto)...
Heaven on earth wewe fun wa miondoko ipi? mie ilimradi unaitwa muziki tu. baasi hapo hunitoi napenda kila aina ya mziki..
mi naipenda ninapokuwa kwenye mduara...afu mbele yangu kuna lijimama linanyonga mauno na liwowo lainiiii...,afu limama lenyewe liwe linajua kucheza mugongomugongo na kupekechapekecha km linabrashi via2 vile...!!
haa haaa haaa mwenzangu mie sichagui sibagui. atakaye nizika simjui. kila muziki iwe gospel, bolingo, R&B, taarabu, za asili zote twende kazi.Hahaaaaa mie kuna nyimbo za aina fulani hivi napendaga.....si nimekuona unavyoshusha taarabu