Acheni uongo, huwezi kuvaa hivi kisha uniambie una heshima

samsun

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2014
Posts
7,386
Reaction score
5,965
Tusiongopeane bhana, yaani kabisa umevaa kisketi kifupiiiiii hadi tight ya ndani inaonekana kuwa ni nyeupe na ramani ya chupi ileeeeeeeeee kama haitoshi umevaa na ki blauzi chako mwenyewe kinachoonyesha matiti yako kisha uniambie eti oooh usim jaji mtu kwa mavazi yake, hivi ni kweli kabisa au mnatania ........ Basi sawa wewe unajiheshimu je kilichokufanya utuvalie hivi ni kitu gani ???



Kuna hiki nacho cha kiume kimeshapiga kiduku chake kama cha Balotel, kisha katuachia makalio nje kiasi anatuonyesha li boxer lake jeupe hadi linataka kuwa rangi nyeusi kiasi kwamba anafanya kazi ya kuipandisha suruali kama vile mikanda imepigwa marufuku kuvaliwa lakini ukiuliza ooooh usim jaji mtu kwa kumuangalia kweli kabisa ???

Nasema hivi HESHIMA NI YA MUDA WOTE SIO KWA SABABU HATUKUJUI NDIO HUTUVALIE HIVI AU ETI LEO NDIO UNAENDA KUABUDU NDIO HUJISTIRI.

WEWE UNASEMAJE MDAU,TIRIRIKA.
 
Nilijua kuna kapicha ka bichkoma ha ha ha
 
Hivi wale bibi zetu wa miaka ileeeeee.......walivaaaje!!!?
 
Ni kweli heshima ni nje na ndani (hapo kwenye mapaja nlieka pause nitathmini)
 
Daah, siku moja niko benki kwenye mstari kwenda kwa teller, jamaa aliyekuwa mbele yangu akaenda, kufika pale kainama huku kapiga mlege chupi nje kama jamaa huyu juu kwenye picha; aiseee nikaona wanawake niliokuwa nao kwenye mstari kila mmoja anamwaangalia jamaa alivyotia fora na kisha kunitupia jicho mimi maana nilikuwa mwanaume pekee huko mbele-ilinilazimu nichukue simu yangu na kujifanya niko bize kana kwamba sijamuona yule msela mav*
 
Bwana Samsun umenifanya ni-zoom in mpaka maximum lakini sijaona kufuli la rangi uliyotaja au nyingine! Wewe umefanyaje mpaka umeona? Halafu yawezekana heshima yao ni ya msimu kama weather au seaons zilivyo.

 
Inategemea kwakuwa kila kitu kina halisi na bandia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…