Acheni uongo, tozo hazijafutwa, zimefichwa tu. Kama zingefutwa jemadari wa tozo asingebaki kitini

Acheni uongo, tozo hazijafutwa, zimefichwa tu. Kama zingefutwa jemadari wa tozo asingebaki kitini

Mag3

Platinum Member
Joined
May 31, 2008
Posts
13,413
Reaction score
23,592
Naam tozo bado zipo tena nyingi tu. Jemadari wa tozo Field Marshal, mtaalam wa uchumi mwenye PhD, karudisha tu majeshi nyuma wakati mbinu za chini chini zikifanyika kuzikarabati zisiweze kutambulika kirahisi.

Kama kweli tozo zingefutwa hivi leo Kamanda Mkuu wa Tozo, aliyetutishia wananchi kama hatutaki tuwe wakimbizi Burundi, angekuwa mapumzikoni. Lakini hadi sasa yuko pale pale akipanga safu na mashambulizi mapya.

Tozo ilikuwa ni fursa iliyopambwa kama mwali na manyang'au yasiyo na chembe ya huruma kwa mateso tunayopitia wananchi. Ni bahati ilioje kuwa wapo wazalendo walioishtukia tozo na malengo yake.

Pamoja na vitisho, wazalendo hao hawakukaa kimya, walipaza sauti wakilia kwa uchungu wakipinga kuibiwa hata kile kidogo walichobakiza. Tozo ilikuwa ni udanganyifu, unyang'anyi na wizi wa mchana kweupee!

Ni wizi uliosimamiwa na wale wale tuliowapa dhamana ya kutuongoza tukiwalipa mamilioni kupitia kodi zetu. Bado wakabuni mbinu ya kutukamua zaidi ili waweze kutembelea ma V8 za milioni mia tano kila moja.

Kwa kuwa Field Marshall bado yuko pale pale akiendelea na mipango yake endelevu, sasa ni lazima tuzidi kupaza sauti zetu. Yeye na tozo ni kama pete na kidole huwezi kuwatenganisha...kama ni kufa, lazima wazikwe pamoja!
 
USHAURI SERIKALI IFUTE USHURU WA KUAGIZA MAGARI ILI IPATE KODI ZAIDI.
Kwenye magari kuna pesa gani nyingi mkuu?tusaidie kutufungua macho
[/QUOTE]

Ipo hivi kuna principal mpya ya kodi nimeibuni inaitwa CHEAP TO IMPORT EXPENSIVE TO MAINTAIN.

Hii principal inafanya na tabia za watu.Kwenye expensive to maintain ndipo serikali inapopata mapato yake.IPo hivi.

Serikali iruhusu magari, pikipiki,bajaji yote yaingie free bila ushuru kutokana na tabia za watz kila mtu atataka kumiliki chombo cha moto iwe ni private au ya biashara kwa sababu wengi awafahamu hesabu.
Kodi ya serikali inapatikanaje.

1. Kwenye usajili wa chombo cha moto badala ya laki 5 iwe milioni moja.
2. Mafuta
3. Bima za magari hapa zipande kidogo
4. Ushuru wa parking hapa kuanzia stand za mabus na barabara za mjini
5. Fine za traffic
6. Fire
7. Spare parts hizi ushuru upande kidogo
8. Ushuru wa barabara uwepo
9. Ushuru wa Usajili wa mamlaka husika mfano latra, dawasco, tbs, misitu,nk
10. Ongezea kodi zingine .

Hoja ya ant dumping. Hii ishu haina mashiko kwa ulimwengu wa SAsa sababu ya mambo ya recycling. KWA maana hata SAsa gari chakavu zote zinaenda screpa kisha zinarejeshwa nje ya nchi kama material za kuzalisha gari zingine.

Hoja ya foleni kwamba ohoo gari zitajazana mjini na kuleta msongamano,nani kakwambia magari yote yatabakia Dar. Kama hofu ya Dar,dar kuwepo na special number ijulikane hili gari matumizi yake si nje ya Dar, mikoani huko still foleni sio tatizo,na pia foleni inatatulika kwa kuongeza miundombinu.

So pesa nyingi itapatikana kwenye uendeshaji wa magari.
 
Unaposema hao wakusanya tozo walipewa dhamana ya kutuongoza na watanzania unakosea, hasa kama unatumia kigezo cha ule uchafuzi mkuu wa 2020.

Watu waliopewa dhamana ya kutuongoza wangekuwa na huruma na wale waliowachagua, hao jamaa walijichagua wenyewe, ndio maana wamejaa viburi, na dharau.
 
Unaposema hao wakusanya tozo walipewa dhamana ya kutuongoza na watanzania unakosea, hasa kama unatumia kigezo cha ule uchafuzi mkuu wa 2020.

Watu waliopewa dhamana ya kutuongoza wangekuwa na huruma na wale waliowachagua, hao jamaa walijichagua wenyewe, ndio maana wamejaa viburi, na dharau.
Ni kweli unavyosema ndugu yangu...hatukuwapa, walitwaa! Pamoja na hayo tusinyamaze, lazima tuendelee kupigia kelele hujuma dhidi ya wananchi.l
 
Inasikitisha sana...
1663671598710.png

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba PhD, Kamanda wa TOZO. Kwamba bado yuko ofisini akiendeleza hujuma dhidi ya wananchi ni swala linalofikirisha sana.
 
USHAURI SERIKALI IFUTE USHURU WA KUAGIZA MAGARI ILI IPATE KODI ZAIDI.
Kwenye magari kuna pesa gani nyingi mkuu?tusaidie kutufungua macho
Ipo hivi kuna principal mpya ya kodi nimeibuni inaitwa CHEAP TO IMPORT EXPENSIVE TO MAINTAIN.
Hii principal inafanya na tabia za watu.Kwenye expensive to maintain ndipo serikali inapopata mapato yake.IPo hivi.

Serikali iruhusu magari, pikipiki,bajaji yote yaingie free bila ushuru kutokana na tabia za watz kila mtu atataka kumiliki chombo cha moto iwe ni private au ya biashara kwa sababu wengi awafahamu hesabu.
Kodi ya serikali inapatikanaje
1.Kwenye usajili wa chombo cha moto badala ya laki 5 iwe milioni moja.
2.Mafuta
3.Bima za magari hapa zipande kidogo
4.Ushuru wa parking hapa kuanzia stand za mabus na barabara za mjini
5.Fine za traffic
6.Fire
7.Spare parts hizi ushuru upande kidogo
8.Ushuru wa barabara uwepo
9.Ushuru wa Usajili wa mamlaka husika mfano latra, dawasco, tbs, misitu,nk
10.Ongezea kodi zingine .

.Hoja ya ant dumping. Hii ishu haina mashiko kwa ulimwengu wa SAsa sababu ya mambo ya recycling. KWA maana hata SAsa gari chakavu zote zinaenda screpa kisha zinarejeshwa nje ya nchi kama material za kuzalisha gari zingine.
.Hoja ya foleni kwamba ohoo gari zitajazana mjini na kuleta msongamano,nani kakwambia magari yote yatabakia Dar.Kama hofu ya Dar,dar kuwepo na special number ijulikane hili gari matumizi yake si nje ya Dar, mikoani huko still foleni sio tatizo,na pia foleni inatatulika kwa kuongeza miundombinu
So pesa nyingi itapatikana kwenye uendeshaji wa magari.
[/QUOTE]

Aisee..🙁🙁

Ni mawazo mazuri sana, lakini ni hatari sana maana yatafungua mlango wa rushwa mkubwa zaidi kuliko huu uliopo...

Si hivyo tu, yatasababisha shida na ugumu mkuu wa maisha...

Huwezi kufungua mlango wa matatizo kwa imani kuwa, nitayakabili yakishafika...

Ni heri kinga kuliko tiba...

Inawezekana ni kweli ni utaratibu utakaoleta mapato makubwa kwa nchi. Lakini mapato yataambana na matatizo makuu zaidi kuliko yaliyopo

Kwa hiyo, kwangu mimi, bado naamini utaratibu uliopo sasa ni mzuri zaidi kuliko huu unaopendekeza hapa ..
 
Kakiri mwenyewe kwamba tozo bado zipo lakini...halafu bila haya kadai eti wanaziboresha! Wizi ulioboreshwa, duh! Tumefikaje hapa Watanzania!
Halafu wabunge wa kuchonga wana piga makofi
 
Ndo maana nikasema anachoongea madelu ni porojo, hakuna jipya atakalofanya isipokuwa ajiuzulu tu.....tuliona kule uingereza David Cameron hoja yake ya kubaki EU ilipogonga mwamba ikabidi ajiuzulu, lakini madelu baada ya kushindwa kutetea uhalali wa tozo kaendelea kunga'ng'ania uwaziri, hivi mbona wadanganyika tunachezewa sana?
 
Ndo maana nikasema anachoongea madelu ni porojo, hakuna jipya atakalofanya isipokuwa ajiuzulu tu.....tuliona kule uingereza David Cameron hoja yake ya kubaki EU ilipogonga mwamba ikabidi ajiuzulu, lakini madelu baada ya kushindwa kutetea uhalali wa tozo kaendelea kunga'ng'ania uwaziri, hivi mbona wadanganyika tunachezewa sana?
Hili jambo la tozo, kuna siku tutajua undani wake. Yawezekana hili jambo halikuwa mpango wa mtu moja, wafaidika ni wengi...ni kelele zetu tu ndizo zimetuokoa kwa kiwango kidogo, wameogopa!

Lingekuwa la mtu moja angekuwa ameshatimuliwa lakini kama kawaida ya wahalifu popote pale lazima walindane. Mwigulu hatakiwi kubaki pale hata kwa dakika moja zaidi, ametuibia vya kutosha.
 
Hili jambo la tozo, kuna siku tutajua undani wake. Yawezekana hili jambo halikuwa la mtu moja, wafaidika ni wengi n kelele zetu tu ndizo zimesaidia. Lingekuwa la mtu moja angekuwa ameshatimuliwa lakini kama kawaida ya wahalifu popote pale lazima walindane. Mwigulu hatakiwi kubaki pale hata kwa dakika moja zaidi, ametuibia vya kutosha.
Wamejaza tozo kwenye mafuta, bado hawajatosheka wakaingia kwenye mitandao ya simu, huko nako hazikuwatosha wakaja kwenye mabenki.......halafu mtu huyo huyo anaongea kwa kejeli na dharau kwa wananchi kwamba wahamie burundi, leo anarudi na spinning mpya eti kapunguza tozo na blah blah kibao, hivi yeye ni nani asiyeweza kuachia ngazi waingie wengine wenye uwezo?​
 
Ipo hivi kuna principal mpya ya kodi nimeibuni inaitwa CHEAP TO IMPORT EXPENSIVE TO MAINTAIN.
Hii principal inafanya na tabia za watu.Kwenye expensive to maintain ndipo serikali inapopata mapato yake.IPo hivi.

Serikali iruhusu magari, pikipiki,bajaji yote yaingie free bila ushuru kutokana na tabia za watz kila mtu atataka kumiliki chombo cha moto iwe ni private au ya biashara kwa sababu wengi awafahamu hesabu.
Kodi ya serikali inapatikanaje
1.Kwenye usajili wa chombo cha moto badala ya laki 5 iwe milioni moja.
2.Mafuta
3.Bima za magari hapa zipande kidogo
4.Ushuru wa parking hapa kuanzia stand za mabus na barabara za mjini
5.Fine za traffic
6.Fire
7.Spare parts hizi ushuru upande kidogo
8.Ushuru wa barabara uwepo
9.Ushuru wa Usajili wa mamlaka husika mfano latra, dawasco, tbs, misitu,nk
10.Ongezea kodi zingine .

.Hoja ya ant dumping. Hii ishu haina mashiko kwa ulimwengu wa SAsa sababu ya mambo ya recycling. KWA maana hata SAsa gari chakavu zote zinaenda screpa kisha zinarejeshwa nje ya nchi kama material za kuzalisha gari zingine.
.Hoja ya foleni kwamba ohoo gari zitajazana mjini na kuleta msongamano,nani kakwambia magari yote yatabakia Dar.Kama hofu ya Dar,dar kuwepo na special number ijulikane hili gari matumizi yake si nje ya Dar, mikoani huko still foleni sio tatizo,na pia foleni inatatulika kwa kuongeza miundombinu
So pesa nyingi itapatikana kwenye uendeshaji wa magari.

Aisee..🙁🙁

Ni mawazo mazuri sana, lakini ni hatari sana maana yatafungua mlango wa rushwa mkubwa zaidi kuliko huu uliopo...

Si hivyo tu, yatasababisha shida na ugumu mkuu wa maisha...

Huwezi kufungua mlango wa matatizo kwa imani kuwa, nitayakabili yakishafika...

Ni heri kinga kuliko tiba...

Inawezekana ni kweli ni utaratibu utakaoleta mapato makubwa kwa nchi. Lakini mapato yataambana na matatizo makuu zaidi kuliko yaliyopo

Kwa hiyo, kwangu mimi, bado naamini utaratibu uliopo sasa ni mzuri zaidi kuliko huu unaopendekeza hapa ..
[/QUOTE]
Mfano matatizo yepi yasiyo na majibu
 
...hivi yeye ni nani asiyeweza kuachia ngazi waingie wengine wenye uwezo?​
Ndugu yangu, naona huijui CCM! Hakuna nchi yoyote duniani ambako kitendo kama hiki kingekubalika kwa wananchi, hakuna. Lakini hapa ni kazi iendeleeee, makofi na vigelegele!

Naona wapo ndugu wawili wanajitahidi kui-derail thread hii na kweli wamepania. Sijui kwa nini hawaanzishi ya kwao. Isije ikawa kuna mkono wa Mwigulu mwenyewe!
 
Halafu wabunge wa kuchonga wana piga makofi
Kwani tuna wabunge? Mbunge anatakiwa awe si mwakilishi tu bali mtetezi wa mwananchi. Kwa bahati mbaya tunalo Bunge linalopitisha sheria kandamizi ya kodi lakini wanahakikisha wao hawalipi kodi hizo.

Badala yake wanajilipa mamilioni kama posho kwa kutimiza wajibu wao bungeni na hiyo ni nje ya mishahara yao minono isiyolipiwa kodi. Ni hawa hawa Mwigulu aliwatumia kupitisha zoezi lake la wizi hivyo wote ni wezi.
 
Back
Top Bottom