Acid reflux ni kivipi inasababisha harufu mbaya kinywani?

Acid reflux ni kivipi inasababisha harufu mbaya kinywani?

Habari wakuu naombeni msaada wenu.

Nasumbuliwa na tumbo kuwaka moto, nahisi kukabwa na kitu kooni, natoa vitu vidogo vidogo kama mabaki ya chakula yaliyo Ganda kwenye Koo, sauti kukata nikiongea kwa sauti ya juu na kutoa harufu mbaya kinywa.

Nahitaji kujua kama sababu ya kutoa harufu mbaya kinywani inasababishwa na acid pia?
Inahitaji kwanza kujua ni tatizo gani unalo, labda ni reflux, labda ni peptic ulclers

Kwanza kapime kuhakiki kama ni peptic ulcers tibu kwanza hili moja. Reflux ni tatizo kubwa zaidi, pengine ni hizo ulcers tu ndio ulizonazo
 
Kwanza, pole sana kwa hali unayopitia. Acid Reflux ni ugonjwa unaoumiza sana.

Je, nini husababisha harufu mbaya ya kinywa?
1. Mdomo kuwa mkavu.
Acid reflux inapunguza sana uzalishwaji wa mate, na hivyo kusababisha hali iitwayo kisayansi xerostomia. Mate husaidia sana kusafirisha mabaki ya chakula na bakteri. Sasa ukosefu wake hupelekea mabaki ya vyakula na mate kubakia kinywani, na kuoza na kupelekea harufu mbaya kinywani.

2. Acid ya tumbo.
Tumboni kwetu tuna acid isaidiayo katika mmeng'enyo wa chakula. Acid hiyo ni HCL. Sasa acid reflux husababisha acid hiyo kurudi kwenye oesophagus na kubeba vyakula ambavyo havijameng'enywa kwa ukamilifu kuelekea kwenye koo na baadae mdomoni. Hii husababisha matonge tonge hayo kuleta harufu mbaya sana kinywani.

Ulichouliza hayo matonge tong ni chakula kilichomeng'enywa nusu. Mkuu Nyani Ngabu siyo tonsil stones.

3. Kurudi kwa Acid kunaweza kusababisha vidonda kwenye umio (oesophagus) na koo. Ile acid inachoma kuta za koo, ukichungulia unaona uwekundu. Ni vidonda. Sasa inasababisha infections ambayo huleta harufu mbaya sana kinywani.

4. Bakteria mdomoni.

Ili kupunguza hali hiyo, tafadhali zingatia sana usafi. Pia, pata matibabu. Acha unywaji wa pombe na vinywaji baridi, acha vyakula vyenye viungo vingi na kunywa maji mengi.

Ugua pole Mkuu.
Dr Restart,
Ushauri wako ni mzuri kweli sana. Mimi nilikuwa na tatizo hilo na nimepata matibabu na ninafuata masharti kama ulivyomshauri mleta hoja na ninaendelea vizuri.

Ila mbona nimekatazwa kula kila aina ya nyama iwe nyekundu au nyeupe! Nimepewa na masharti mengine mengi. Kunywa maji mengi na kuacha vyakula vyenye viungo vingi kunanisaidia sana. Nakupongeza sana mkuu.
 
Ndiyo.

Anza kwanza kwa mganga wa meno. Atakufanyia tathmini ya kitaalamu na kukupatia tiba/ ufumbuzi wa tatizo lako/ pendekezo la nini ufanye au wapi uende kwa msaada zaidi.
Daktari mhusika kabisa wa tonsil stones ni ENT specialist.

Dentist ni specific kinywani. Huko kooni ni kwa ENT. Ijapokuwa hata mtaalam wa meno anaweza kuziona ila anapaswa daktari ambaye ni mtaalam wa kuzijua, kuzichunguza na kung'amua matatizo mengine ni Specialist wa ENT.

Ambaye kwa taarifa ya mhusika alishamtembelea. Japo yeye anasema ETN.
 
Inahitaji kwanza kujua ni tatizo gani unalo, labda ni reflux, labda ni peptic ulclers

Kwanza kapime kuhakiki kama ni peptic ulcers tibu kwanza hili moja. Reflux ni tatizo kubwa zaidi, pengine ni hizo ulcers tu ndio ulizonazo
Peptic ulcers ni nn? Naomba kufahamishwa
 
Daktari mhusika kabisa wa tonsil stones ni ENT specialist.

Dentist ni specific kinywani. Huko kooni ni kwa ENT. Ijapokuwa hata mtaalam wa meno anaweza kuziona ila anapaswa daktari ambaye ni mtaalam wa kuzijua, kuzichunguza na kung'amua matatizo mengine ni Specialist wa ENT.

Ambaye kwa taarifa ya mhusika alishamtembelea. Japo yeye anasema ETN.
Okay, sawa.
 
Dr Restart,
Ushauri wako ni mzuri kweli sana. Mimi nilikuwa na tatizo hilo na nimepata matibabu na ninafuata masharti kama ulivyomshauri mleta hoja na ninaendelea vizuri.

Ila mbona nimekatazwa kula kila aina ya nyama iwe nyekundu au nyeupe! Nimepewa na masharti mengine mengi. Kunywa maji mengi na kuacha vyakula vyenye viungo vingi kunanisaidia sana. Nakupongeza sana mkuu.
Mkuu, kwanza pole na hongera kwa kuanza kupata nafuu kwa tatizo ulilonalo.

Umezuiwa matumizi ya nyama kwa sababu kuu mbili;
a)Moja, mmeng'enyo wa nyama ni wa taratibu sana. Sasa kama upo taratibu maana yake acid itaendelea kuachiwa kwa muda mrefu na hivyo kuendelea kuongeza tatizo.

b)Mwilini kuna valve au tuseme koki, inayofunguka na kuachia. Koki mfano ya mkunduni, nyingine inaitwa lower oesophagical sphincter. Sasa ukila nyama kunasabisha koki hii (LES) kulegea. Na ikilegea inaachia acid kuflow kwenye oesophagus. Na hivyo kusabanisha tatizo kuwa kubwa zaidi.

Hata hivyo unaweza kutumia kwa kiwango kidogo sana.

Endelea kufuata maelekezo Mkuu.
 
Mkuu, kwanza pole na hongera kwa kuanza kupata nafuu kwa tatizo ulilonalo.

Umezuiwa matumizi ya nyama kwa sababu kuu mbili;
a)Moja, mmeng'enyo wa nyama ni wa taratibu sana. Sasa kama upo taratibu maana yake acid itaendelea kuachiwa kwa muda mrefu na hivyo kuendelea kuongeza tatizo.

b)Mwilini kuna valve au tuseme koki, inayofunguka na kuachia. Koki mfano ya mkunduni, nyingine inaitwa lower oesophagical sphincter. Sasa ukila nyama kunasabisha koki hii kulegea. Na ikilegea inaachia acid kuflow kwenye oesophagus. Na hivyo kusabanisha tatizo kuwa kubwa zaidi.

Hata hivyo unaweza kutumia kwa kiwango kidogo sana.

Endelea kufuata maelekezo Mkuu.
Nimekuelewa sana Dr. Restart. Na ndivyo nilivyoambiwa na mtaalamu mwenzako. Kwa kweli naendelea vizuri sana. Mbarikiwe sana nyote. Kwa wengine nawaomba mfuate ushauri wa Dr. Restart. Mimi ni shahidi na ninaendele vizuri kabisa. Nyama nimeacha kwa kiasi kikubwa. Once in a while nakula kidogo nyama. Nakula mboga za majani kwa wingi.
 
Wewe ni doctor wa mitishamba eti?!!!maana hata uandishi unakushinda na nyie ndiyo huwa kila kitu mnajua au mmeshawahi kutibu.

Huwezi ukaonekana msaada kwa mtu kama utafanya ulichofanya hapo juu kuuponda ushauri wa mwenzako kwa sababu wewe ndiye utaeonekana kanjanja zaidi elewa hapa kila mtu anajaribu kusaidia ukizingatia hakuna mwenye kipimo cha maabara cha mleta mada,hiyo hali anayozungumzia mleta mada (kutoka mabaki ya chakula kinywani) mimi ilishawahi kunitokea na nahisi alichoeleza restart hapo juu yupo sahihi.
Unazingatia vitu vidogo sana huenda una akili ndogo pia mimi sijashindwa kuandika ilo neno kama na wewe ni dr uchwara saman kwa hilo,,,kama ulishawahi patwa na hii kitu msaidie ndugu yetu mana huu ugonjwa unatesa wengi sana wanaambiwa ni acid alafu suruhu hamna
 
Back
Top Bottom