ACT: Tunaitaka Serikali ya JMT, kuacha utowaji wa Leseni kwa eneo la Fungu Mbaraka na Bahari Kuu upande wa Zanzibar

Kwa mujibu wa ibara ya pili ya katiba ya JMT, eneo la JMT ni eneo lote la iliyokuwa Tanganyika na eneo lote la iliyokuwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar!.

Ardhi yote ni mali ya Watanzania chini ya udhamini wa rais wa JMT, ila Rais wa JMT kabla hajalihawanya eneo la Zanzibar, atajadiliana kwanza na rais wa Zanzibar, visiwa vyote vya bahari ya Hindi mkabala na Tanzania ikiwemo Zanzibar na Pemba ni mali ya JMT.
P
 
Zanzibar wana shida ya ulafi na uroho.
 
Nadhani ACT Wazalendo wanakua WAJINGA.

Samia Suluhu Hassan ana MAMLAKA KAMILI juu ya Mipaka ya iliyokua Tanganyika na eneo lote la Zanzibar. ACT wafahamu kuwa Rais wa Zanzibar ana "assume" hayo madaraka kwa Hisani TU.

Pili. Kwenye majadiliano na kampuni hizi za mafuta, nchi huwa inatakiwa kutoa guarantee ya ulinzi. Sasa kama Zanzibar wanataka independence kwenye eneo hili, wana Jeshi la kutoa ulinzi kwenye eneo husika mafuta yakipatikana? kwa sababu ni lazima waangalie picha kubwa ya mbele. JWTZ na majeshi mengine ni suala la JMT na sio jambo la Tanganyika au Zanzibar. Security Guarantee Zanzibar itatoa wapi nyakati za kufanya final investment decision??

Wana uwezo wa kutoa State guarantee? as far as I am concerned, hizi kampuni zitahitaji dhamana kwa jina la JMT sio Zanzibar
 
Gesi ya Mtwara inanufaisha Zanzibar kaa ilivyo madini , Utalii n.k. ikiwemo Ardhi .

Waya wa Umeme kutoka Tanganyika unakarabatiwa kwa bilioni 240 na JMT au Tanganyika. Zbar hawajakataa!!

UDSM inajenga campus, TIA wamekamilisha, Mweka wanajenga chuo Zanzibar, Uhamiaji wanajenga chuo Zanzibar na majengo. Zote hizo ni kodi za Tanganyika, Wazanzibar hawakatai hayo!

Wazanzibar wanajikatia mapande ya Ardhi Tanganyika! Kuna siku Watanganyika watawaulizakuhusu mipaka !
Kilitangazwa na nani? Mpaka wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wapi baada ya Uhuru ? Latham ilikuwa wapi!
Sultan kutamka haina maana iwe hivyo! Tanganyika haikuwahi kutawaliwa na Sultan!
Kumbe Zanzibar ina mipaka! Haya maneno msije kuyasahau maana Tanganyika ina mipaka pia.

Mipaka ya Zanzibar inalindwa na nani? Kama ni JWTZ , ni hawa ambao bajeti yao ni ile ya Tanganyika?
Kuna Watumishi 805 wa Uhamiaji wanaolipwa na Bajeti ya Tanganyika. Hawa wanalinda mipaka ipi huko Zanzibar
Ukimya huu kwa Serekali zote mbilli ile ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na hii ya Zanzibar pamoja na Taasisi zao zote zinazohusika na masuala ya utafutaji na uchimbaji wa mafuta unatia mashaka na kuibua maswali mengi kwa wananchi.
JMT ina Zanzibar ndani yake. Hapa ni Serikali ya JMT na Zanzibar, ACT wanawalumu Watanganyika kwa lipi? Tanganyika imefichwa haina serikali.
5. Serekali ya Zanzibar itoke hadharani na kueleza umma kwa tamko rasmi la serekali kwamba eneo la Fungu Mmbaraka ni eneo la Zanzibar na haipaswi kwa mamlaka nyengine yoyote kufanya shuhuli yoyote bila ya ridhaa ya Serekali ya Zanzibar.
Mpaka haujadiliwi na upande mmoja. ACT tuungane Tanganyika irudi halafu tujadili mipaka na matumizi ya rasilimali. Mtakuwa na rasilimali zenu , Tanganyika haitabeba mzigo wa gharama . Ugomvi utakwisha!

Kwasasa mnajadili mpaka na nani? Humuwezi kujadili na Tanzania kwasababu mpaka wa Tanzania umefika Zanzibar
Msiishie mafuta na gesi, mtuambie hiyo mipaka yenu inalinwa na nani na kwa bajeti kutoka wapi?
Haya maneno myakumbuke maana ipo siku Watanganyika wataitaka serikali ya Muungano kuzuia uporaji wa Ardhi kwa Watu kutoka Zanzibar!
Chama cha ACT Wazalendo, Tunamtaka Raisi Samia Suluhu Hassan asikukubali kutumika kuiziba mdomo Zanzibar kwa kushiriki katika ufunguaji huu wa leseni mpya za vitalu vya mafuta na gesi kwa Tanganyika bila yakutatua mkanganyiko uliopo sasa.
Mna hiari na Rais Samia!

Hata hivyo Chama chetu, hakitasita na kuendelea kua sauti ya Wazanzibari kwa kusimamia Serekali juu ya masuala yote yanayohusu rasilimali za Zanzibar kwa maslahi ya wanachi wa Zanzibar.
Rasilimali za Tanganyika ni za wote , za Zanzibar ni kwa masilahi ya Wazanzibar.
Watanganyika wanawasikia vizuri ipo siku watawajibu, hata kama si leo au kesho haya maandishi yatajibiwa !
Imetolewa leo, tarehe 03/01/2025 na,

Ndg. Said Ali Mbarouk
Msemaji wa Sekta ya Mafuta na Gesi Asilia Zanzibar
0779955778
Tumewaambia Watanganyika siku nyingi , hiki Chama cha ACT ni cha Zanzibar!

JokaKuu Pascal Mayalla
 

..anayegawa hayo maeneo si Mzanzibari mwenzao? Shida yao ni nini?
 
Ndiyo naanza kuelewa kile kitabu kilichokuwa kinazungumziahabari za "chakula cha wageni na cha wote"
 

Kuwa mile sita sio hoja kama automiatic kinakuwa cha Tanganyika. Leteni mipaka yenu kisheria muliainishiwa wakati wa uhuri tuone
 
Kuwa mile sita sio hoja kama automiatic kinakuwa cha Tanganyika. Leteni mipaka yenu kisheria muliainishiwa wakati wa uhuri tuone
Nenda kasome UN maritime law, kila nchi inayopakana na bahari inaweza ku-claim mpaka 200 nautical miles as ‘exclusive economic zone’.

Ukiona hivyo ACT mahatahira wao bado wanaishi kwenye mipaka ya kikoloni zama za ‘scramble for Africa’.
 

nchi zote za Africa zinatokana na mipaka ya kikoloni
 

Mkuu usitafune maneno, Fungu mbaraka ni ya Zanzibar au Tanganyika? tupe jibu
 
nchi zote za Africa zinatokana na mipaka ya kikoloni



Mambo mengine kubishana ni utoto, hakuna mipaka ya bahari duniani (ni mali ya wote).

Kilichopo ni nchi inaruhusiwa kufanya-commercial exploitation ndani ya 200 nautical miles from its coastline.

Nimekwambia na sheria husika inayosema hivyo UN Maritime law, wewe umekadhana hadithi za mipaka ya ‘scramble for Africa’.

Akili zenu zinawatosha wenyewe
 

..Zanzibar wana vikosi vyao vya ulinzi na vinaweza kutoa ulinzi kwa makampuni ya uchimbaji mafuta. ukitaka kuvijua vikosi hivyo fuatilia gwaride katika sherehe za mapinduzi ya Zanzibar.
 
..Raisi wa Muungano ni Mzanzibari.

..Mwanasheria Mkuu wa serikali ya jamhuri Mzanzibari.

..ACT wakaongee na ndugu zao kuhusu kugawa ardhi ya Zanzibar.

..Watanganyika tulipokuwa tunalalamika Mzanzibari kuuza ardhi yetu, ACT na Wazanzibari walikuwa wanatucheka.
 

mkuu kwani Fungu Mbaraka ni bahari? sisi tunazungumza kisiwa wewe unaleta refrence ya Ocean
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…