ACT: Viongozi wetu waliozuiwa kuingia Angola wamerejea Nchini, tunasikitishwa na ukimya wa Serikali ya Tanzania

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Viongozi wa Chama cha ACT Wazalendo waliokuwa wamezuiwa kuingia nchini Angola wamerejea Tanzania usiku wa Machi 14, 2025, saa 9:40.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa ACT Wazalendo leo Machi 14, 2025, Mwanaisha Mndeme, viongozi waliorejea ni Kiongozi wa Chama, Dorothy Jonas Semu, Naibu Katibu wa Mambo ya Nje, Nasra Nassor Omar, na Katibu wa Haki za Binadamu, Pavu Abdallah.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa chama hicho ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, bado yupo jijini Luanda, Angola, akisubiri kukamilisha taratibu za safari ya kurejea nchini.

ACT Wazalendo imeeleza kusikitishwa na kimya cha Serikali ya Tanzania, hususan Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kuhusu tukio hilo. Taarifa hiyo imeeleza kuwa kutotoa kauli rasmi kunavunja misingi ya kidiplomasia na kuhatarisha mshikamano wa Afrika pamoja na uhusiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Angola.

Chama hicho kimeitaka Serikali kutoa ufafanuzi kuhusu kilichotokea kwa viongozi wake na kueleza hatua zinazochukuliwa, hasa ikizingatiwa kuwa mmoja wa waliokumbwa na tukio hilo ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.

ACT Wazalendo pia kimetaka Serikali kumuita mara moja Balozi wa Angola nchini Tanzania ili kutoa maelezo kuhusu tukio hilo. Chama kimeeleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kulinda heshima ya viongozi wa taifa na mahusiano ya kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.
 
Na wa chandumu wamerejea au Bado?
 
wajifunze kufata protocol na kuheshimu utamaduni, ustaarabu na sheria za kimataifa,

sio kukurupuka tu kama wanaenda kununua maembe sokoni. Angola ina serikali na ina utaratibu wa kupokea viongozi wa hadhi mbalimbali wa serikali na upinzani pia πŸ’
 
Pale tumbo linapofikiria badala ya kichwa
 
Your browser is not able to display this video.


UKIMYA WA SERIKALI YA TANZANIA JUU YA KUZUIWA KWA VIONGOZI WETU ANGOLA HAUKUBALIKI

HALI HALISI YA SASA
Tunapenda kuujulisha umma kuwa Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Ndugu Dorothy Jonas Semu akiambatana na Naibu Katibu wa Mambo ya Nje Ndugu Nasra Nassor Omar na Katibu wa Haki za Binadamu Pavu Juma Abdalla wamerejea nchini Tanzania takribani saa 9:40 usiku wa tarehe 14 Machi, 2025 baada ya kuzuiwa kuingia nchini Angola.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Ndugu Othman Masoud Othman bado yupo Jijini Luanda nchini Angola kwa ajili ya kukamilisha taratibu za usafiri kurejea nyumbani Tanzania. Chama kitaendelea kutoa taarifa mara kwa mara kwa umma juu ya maendeleo ya suala hili.

UKIMYA WA TANZANIA HAUKUBALIKI​

Chama cha ACT Wazalendo kimesikitishwa na ukimya wa Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kulikalia kimya suala hili. Ni jambo linaloshangaza na kusikitisha kwa Serikali ya Tanzania kushindwa kutoa kauli yoyote dhidi ya kitendo hiki kinachokiuka taratibu za kidiplomasia, ari ya mshikamano wa Afrika na undugu wa kihistoria baina ya Tanzania na Angola.

Tunaitaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki itoke hadharani na kufafanua kilichotokea Angola na msimamo wa Serikali juu ya hilo ikizingatiwa kuwa miongoni mwa viongozi waandamizi waliokumbwa na kadhia hiyo yumo pia Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar. Pia, tunarejea rai yetu ya kuitaka Serikali kumuita mara moja Balozi wa Angola nchini Tanzania kujieleza kuhusu kilichotokea kwa viongozi wetu nchini Angola.
 
Mnaenda kufanya siasa kwenye nchi za watu....mkihukumiwa kwa Uasi ..treason huko chini kwa watu...mtakatwa vichwa ...bora mrudi tz kwenu
 
Mnaenda kufanya siasa kwenye nchi za watu....mkihukumiwa kwa Uasi ..treason huko chini kwa watu...mtakatwa vichwa ...bora mrudi tz kwenu
Ccm wamepeleka fitina huko ili wazuiwe.
 
Pale tumbo linapofikiria badala ya kichwa
makamu wa Rais wa nchi, ati anaingia nchi nyingine huru yenye mamlaka kamili kama kibaka au jambazi kweli?

sheria za kimataifa ni utamaduni na ustaarabu wa dunia nzima, kama mtu hajui hilo anafaa kupewa elimu bila aibu πŸ’
 
Hakuna protocol hata moja iliyovunjwa isipokuwa ni ufitini wa ccm huwo.

Hamna mnaloweza kuhoji isipokuwa nguvu za kishetani.
 
Hakuna protocol hata moja iliyovunjwa isipokuwa ni ufitini wa ccm huwo.

Hamna mnaloweza kuhoji isipokuwa nguvu za kishetani.
sasa mbona haijulikani yule makamu wa Rais wa Zanzibar ameingia vip Angola bila Rais na Makamu wa Rais wa nchi hiyo kujua na kumuandalia mapokezi ya heshma kama ulivyo ustaarabu wa kimataifa?πŸ’
 
makamu wa Rais wa nchi, ati anaingia nchi nyingine huru yenye mamlaka kamili kama kibaka au jambazi kweli?

sheria za kimataifa ni utamaduni na ustaarabu wa dunia nzima, kama mtu hajui hilo anafaa kupewa elimu bila aibu πŸ’
Angola haiitambui Zanzibar kama nchi, kwa hiyo suala la umakamu wa raisi Zanzibar haliingii hapa
 
sasa mbona haijulikani yule makamu wa Rais wa Zanzibar ameingia vip Angola bila Rais na Makamu wa Rais wa nchi hiyo kujua na kumuandalia mapokezi ya heshma kama ulivyo ustaarabu wa kimataifa?πŸ’
Na kwambia hivi hujui lolote na kama unajua ni unafiki wako. Huwo ni ushirikiano na ccm kuhujumiwa kutokuingia huko. Kwanini hawajazuiwa sehem nyingine wakati Angola haijpakana na Tanzania?
 
Walishazoea kudekezwa uko Ulaya na Marekani kwakuwa Wazungu wanania mbaya na rasilimali zetu Afrika,,,,!!


ndio wanawanyenyekea Viongozi wa vyama vya Upinzani nakuficha mazaifu yao,!!


Lkn Angola ukijichanganya tu ndio ivo wanatoa ukelele na mlio!!!!

Upinzani Bado tu awajaitaja polisi CCM ya Angola!!!!!

Mana wao kuvunja Sheria ndio Maana ya wao kuwa Upinzani!!!


Awataki kueshimu Sheria yyte popote wawapo ili watu wajue pale kuna wapinzani!!!!

Hiii zana ujinga sijui utawaondoka lini vichwani mwao!!!!!!! Awajapigwa virungu Tuwape pole wapinzan wetu!!!!
 
Angola haiitambui Zanzibar kama nchi, kwa hiyo suala la umakamu wa raisi Zanzibar haliingii hapa
umezubaa sana kifikra gentleman, pole.

but pamoja na Marais na viongozi wengine wastaafu kutoka mataifa mengine Africa na duniani kote, mamlaka za kiusalama za Angola hazikua na taarifa za ujio wa viongozi hao wala hapakua na tarifa za kuwepo kwa mkutano huo uliotarajiwa kuangazia masuala ya kisiasa na kidemokrasia duniani,

na kwahiyo,
delegates walihitajika kuandaliwa usalama wa kutosha na mamlaka za angola kabla ya kutua Angola kama walivyotua utadhani vibaka πŸ’
 
Serikali waseme nini wenye nchi yao wamekataa ni kusubiri nao wakija tuwakatae!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…