LGE2024 ACT Wazalendo: Mawakala wa Vyama vya Siasa wanalazimishwa kwenda kuapa Halmashauri ambako ni mbali na maeneo wanayotoka

LGE2024 ACT Wazalendo: Mawakala wa Vyama vya Siasa wanalazimishwa kwenda kuapa Halmashauri ambako ni mbali na maeneo wanayotoka

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo Ado Shaibu akizungumza na wanahabari leo, Alhamisi Oktoba 10.2024, Dar es Salaam amesema kuwa mawakala wanalazimishwa kufika kwenye ofisi za Halmashauri husika ili kuapa suala ambalo wengi hushindwa kutokana na umbali uliopo kati ya Halmashauri na maeneo wanayotoka

"Kuapishwaji wa mawakala wa undikishaji wapiga kura (kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa), tumepokea taarifa katika maeneo mengi kwamba wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya Halmashauri wameitisha zoezi la viapo vya mawakala kufanyika katika ofisi za Halmashauri husika, kwa jiografia ya nchi yetu, maeneo mengi yako mbali na Halmashauri, hivyo ni ngumu kwa mawakala kufika kwa ajili ya viapo, utaratibu huo utawaacha mawakala bila viapo na ikiwa hawataapishwa maana yake hawatakuwa na sifa za kusimamia zoezi la uandikishaji"

"Newala, kule viongozi wetu wa chama (ACT Wazalendo) wametakiwa kuwapeleka mawakala wote Newala mjini kwenda kuapishwa ambapo baadhi ya maeneo yana zaidi ya Kilometa 70 mfano yale yanayopakana na Msumbiji"

shaibu.jpg
 
10 October 2024


View: https://m.youtube.com/watch?v=NDXZuV1uGq0

Katibu mkuu wa ACT - WAZALENDO Bw. Addo Shaibu asema kukurupuka kwa kila wilaya, halmashauri na kata kufanya zoezi la kuapisha mawakala wa vyama watakaofuatilia uchaguzi wa serikali za mitaa mwezi November 2024 inaimarisha ile shaka kuwa kuna njama za TAMISHEMI kukwamisha vyama vya upinzani wasiwe na mawakala..
 
Wananchi na CHADEMA waliliona jambo hili na kulipa angalizo mapema kuhusu uwezo (capacity), makada wa CCM ambao ofisi zao mabosi ni DED kusimamia chaguzi, uchama na kukosa kutoegamia popote (Neutrality).

ACT-WAZALENDO na vyama vingine 13, Baraza la Vyama vya Siasa, hata pia Msajili wa vyama vya siasa angekuwa mmojawapo wa wadau wenye maslahi kuwa marafiki wa wananchi 3 waliofungua kesi lakini hawakuona umuhimu

TOKA MAKTABA:

24 September 2024
Mahakama Kuu ya Tanzania
Kivukoni Front
Dar es Salaam

MAWAKILI WAVUTANA MAHAKAMANI KESI YA TAMISEMI KUSIMAMIA UCHAGUZI/ SERIKALI YAPEWA SIKU 14 KUJIBU HOJA ZA WANANCHI.


View: https://m.youtube.com/watch?v=IzuZftVKoTY

Hoja za wananchi Kaiza Buberwa, A. Nkya na Bob Wangwe wanaowakilishwa na jopo la mawakili
 
ELIMU YA URAIA KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024

:FIRE: LIVE : WANAOPINGA TAMISEMI KUSIMAMIA UCHAGUZI WAIBUA MAPYA / WAHOJI UKIMYA WA WANANCHI 'KESI YAO'​



View: https://m.youtube.com/watch?v=3SokBJXm6W8
  • Kinachoendelea mahakama kuu ya Tanzania ni Ombi la Kufungua Kesi kwa niaba ya waTanzania wote
  • Shauri lililofunguliwa mahakamani na raia watatu wa Tanzania ambao ni Nkya, Kaiza na Wangwe kwa niaba ya watanzania
  • Umuhimu wa ombi hili kwa watanzania wote
  • Wizara ya TAMISEMI ni batili kusimamia uchaguzi wa viongozi wa vijiji, mitaa na vitongoji
  • Ombi kama raia hao watatu wanaruhusiwa kufungua kesi
  • Yaliyojitokeza
  • Uongozi ni rasilimali namba moja ya kutuletea maendeleo
  • Media House / Waandishi wa Habari ni kama wamesusa kufuatilia Ombi hili la raia 3, pengine ni kwa kutofahamu uzito na umuhimu wa ombi hili
  • Unyoofu uadilifu integrity
 
Kama ni mawakala wa vyama vyote wanaenda huko hilo siyo tatizo ,Vyama vinatakiwa kuhakikisha wanafika huko halmashauri mapema
 
Chaguzi zetu Zina vituko Sana. Eti msimamizi was uxhaguzi ni Bwana mchengerwa wakati nae chama chake kinashiriki huo uchaguzi!
 
Kama ni mawakala wa vyama vyote wanaenda huko hilo siyo tatizo ,Vyama vinatakiwa kuhakikisha wanafika huko halmashauri mapema
Ruzuku wanakula makao makuu tu hawawatendei haki hao mawakala ohhh mjitegemee nauli mkaape wao viongozi wa ACT makao makuu wakisafiri hawajitegemei .Ruzuku ndio inatumika huo ni utapeli
 
😄 wanaenda kuapa kwa wana ccm...
Na bado yajayo yatawafurahisha

Ova
 
Je Mawakala wa CCM kutoka ..hayo maeneo wanafika huko Halmashauri? Kama jibu ni ndio wanafikaje na hao wa ACT washindwe kufika?
 
Back
Top Bottom