Ada na gharama za kumsomesha mtoto English medium kwa miaka 4 ni milioni 10. Atachoambulia huko unakipata kwa Ras Simba kwa mwezi mmoja tu kwa laki 2

Hizo private hata sioni umuhimu wake NOTE. Tusomeshe watoto wetu kwenye zile shule ambazo tuna uwezo nazo achen kuiga kila January itakuwa mbaya
 
Hapo ulitakiwa uandike English fluency.
Kwa uandishi huo, bado haujakijua Kiingereza, na usijifariji kuwa mlikuwa sawa. Hapo ni wewe, achana na watoto wako ambao nao utawapeleka baadaye kwa Ras Simba
Utakosoa sana lakini ukweli unabaki palepale kuwa shule za serikali ni mbovu.english medium za binafsi wanajitahidi.
 
Kwa Ras lion kuna maabara na practical tools/apparatus?

Kwa Ras lion kuna Mwl. wa hesabu,kiswahili,sayansi,uraia,historia n.k.?

Kwa Ras lion kuna Mwl. wa nidhamu,michezo,patron na matron?

Kwa hiyo jibu ni kwamba wewe ndio hauna uelewa.
 
Baadhi ya Shule zinatoa elimu nzuri sana kwa watoto sijui huko unakoishi wewe. Fuatilia shule za Roman, KKKT,Sabath utaona watoto walivyo na uelewa mzuri na kujengwa kimaadili.
Kuna team kataa shule nzuri hapo JF kwa hizo ulizowatajia lazima wazikatae
 
Utakosoa sana lakini ukweli unabaki palepale kuwa shule za serikali ni mbovu.english medium za binafsi wanajitahidi.
Hahaha naona unapigania ugali wako mwalimu wa English Medium. Wabongo wameshastuka now wanawatoa watoto huko Ems wanawaleta Kayumba.

Eti Elimu bora. Elimu bora my foot. Elimu bora unaijua wewe?
Yani wewe ndio umpe mwanangu elimu bora?
 
Hizo private hata sioni umuhimu wake NOTE. Tusomeshe watoto wetu kwenye zile shule ambazo tuna uwezo nazo achen kuiga kila January itakuwa mbaya
๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ
 
Kwa Ras lion kuna maabara na practical tools/apparatus?

Kwa Ras lion kuna Mwl. wa hesabu,kiswahili,sayansi,uraia,historia n.k.?

Kwa Ras lion kuna Mwl. wa nidhamu,michezo,patron na matron?

Kwa hiyo jibu ni kwamba wewe ndio hauna uelewa.
January hii shule zinafunguliwa wiki ijayo watu washakula ada now vichwa vinawaka moto na unakuta mtu hakujipanga now kichwa kinawaka moto tena wa welding oxyacetylene gas na kila akigusa pa kukopa riba 20% kwa mwezi matokeo yake mtu anafungua nyuzi za kumsifia ras simba na kuponda shule za private
 
Kuna siku nimemtembelea jamaa yangu Mmoja, ambaye anawasomesha watoto wake hizi hizi shule zenu mnazoziita English mediums.

Yaani watoto ninawauliza Moja jumulisha Moja jibu ni ngapi???... Wananitolea macho tu, hawajui wajibu Nini..

Ila nilivyoanza kuwauliza one plus one... Two plus two.... Wow walifurahi hao, wakaanza kutiririka tu majibu.

Kwa hiyo nilichokiona pale, huko kwenye hizo English medium schools kubwa zaidi watoto wanachofundishwa ni kuzoea matumizi ya lugha ya kingereza tu basi... Hakuna kingine Cha maana, na elimu Bora haiko hivyo
 
Gharama za kumiliki gari kwa mwezi ni laki 3 za mafuta, wakati unaweza kupanda daladala kwenda na kurudi kila siku buku mbili jero na kwa mwezi 30,000 tu. Mawazo yako hayajatofautiana sana na haya.
๐ŸคฃKila mtu ashinde mechi zake
 
Kuna team kataa shule nzuri hapo JF kwa hizo ulizowatajia lazima wazikatae
Sio mbaya kama kila mtu akifanya kile kinachomfurahisha ๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…๐Ÿ˜…ili mradi tu awe na Akili timamu
 
Kizuri gharama, ila sio vya gharama vyote ni vizuri.
 
Reactions: Tsh
Watu badala ya kuwekeza kwenye viwanja na assets nyingine baadae watoto wao wakimaliza chuo wawape mitaji kwa kuuza baadhi ya hizo assets mijitu inaishi maisha ya kufake( FASHION LIFESTLE) haya tukutane uzeeni.

Ambapo wasomesha watoto English medium watakuwa wanalialia hovyo kuwa serikali itoe ajira๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„ huku mitoto yao mibroila ikiwa bado haijatoka majumbani bado wapo wanakula kulala kwa wazazi.

Watanzania shtukeni acheni kupoteza pesa na kutajirisha wamiliki wa hizi shule. Na bado mitoto inatoka huko english medium unaingia garama tena za tuition๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„na ENGLISH YAO BROCKEN.

1.Huo muda wa pre form 1 na pre form 5 wakati wa LIKIZO ZA KUSUBIRI MATOKEO pelekeni watoto VETA.Huko wachukue ujuzi utakao wasaidia wakishamaliza hizo elimu zao za chuo.

2.Pesa mnazoenda kutupa huko English medium wekezeni kwenye assets kama viwanja,mashamba, kununua bond za serikali na hisa katika kampuni zisizopata hasara๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„ acheni UBINAFSI na uchoyo kama nyie hamkuandaliwa URITHI basi jitaida WATOTO wako na vijukuu na vitukuu vije vikukumbuke hiyo ndo legacy๐Ÿ’ช๐Ÿ’ช๐Ÿ’ช

Kuna shule nyingi tu ada chini ya millioni 1 zingatia zenye ufaulu wa wastani kupanda juu kama huko huwezi mpeleke kayumba ila ongeza usimamizi na mwalimu wa ziada wa kumboost.

#kumpa mtoto Elimu ni wajibu,elimu sio urithi!!!
 
My friend Lugha yoyote duniani unajifunza muda wowote na lugha ni kuongea.Nakuhakikishia hata leo ukitaka kujifunza lugha mpya yoyote unaweza ila jitihada zako katika kuiongea ndo itafanya uwe fluent.

Mimi nilikuwa najua kingereza cha kuombea maji ila nilifika hatua nikasema nataka nijue kingereza chenyewe na niwe fluent na pia niwe na confidence ya kutosha nikaweka mikakati ya kujifunza misamiati mipya na ya kisasa na kutafuta watu wa kuongea nao kupasua yai hahahaa na nimefanikiwa.

Mademu ni wazuri sana wa lugha so kama vipi unaweza ukawatumia kujibrashbrash lugha inase kichwani pia kama unamarafiki wa nje ya nchi nao jitahidi uwe unaongea nao kujiboresha zaidi.

#kupanga ni kuchagua!!!
 
Naunga mkono hoja ndo maana nikasema....... lazima ujitoe hasa hapo juu
 
Kwa Ras lion kuna maabara na practical tools/apparatus?

Kwa Ras lion kuna Mwl. wa hesabu,kiswahili,sayansi,uraia,historia n.k.?

Kwa Ras lion kuna Mwl. wa nidhamu,michezo,patron na matron?

Kwa hiyo jibu ni kwamba wewe ndio hauna uelewa.
Hivyo vitu ulivyotaja havipo kwenye shule za serikali?
Kwa Ras Simba nimeongelea issue ya English language
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ