Japo kuwa refa na rise man wake waliboronga jana,lkn hamna mahusiano kati ya kuboronga kwa refa na kutuharibia uwanja wetu. Simba hili tukio ni la pili ukiacha la kwanza na kagera sugar waling'oa viti na jana wanafanya hivyo hivyo. Wiki kama mbili walilalamika uwanja wa uhuru si mzuri kutokana na nyasi bandia wakakubaliwa kutumia uwanja wa taifa, sasa jana wamefanya uchizi wa kiwango cha PhD, mimi kama ningekuwa TFF ningewapiga marufuku kutumia uwanja wa taifa kwa msimu mzima, wakatumie uwanja ule wa uhuru na kitendo alichokifanya mkude cha kihuni, kwani yy ni professional lkn anatabia za wachezaji wa ndondo. Duniani kote marefa kukosea kitu cha kawaida (refa nae binadam) chukulia kama mechi ya msimu uliopita EPL London derby mechi kati ya chelsea na Arsenal, kitendo cha kihuni alichofanya Costa lkn kadi akapewa Gabriel, lkn kuanzia wachezaji mpaka mashabiki hawakureact kihuni kama jana walivyofanya mashabiki na wachezaji wa simba. Narudia tena Simba inabidi wapewe adhabu kali sana tena sana, iwe fundisho ili wasirudie tena na mwamuzi nae apewe adhabu kali kwani nae mechi ya pili hii anaboronga (aliboronga mechi msimu uliopita kati ya yanga na cost Union).