Sasa Bosi
kama Saudi Arabia hakuna, Rape, Ushoga,Usagaji, Wizi, Ugoni,
Hao wanaoendelea kuchinjwa wanatenda hayo makosa wakiwa nje ya Saudia ?
Ujue mwanadamu anapoishi ni lazima anafanya makosa, ndiyo maana Mungu ameruhusu toba.
Na kila jamii inatunga adhabu mbalimbali ili kuwaogofya wakosaji kutenda kosa flani.
Jambo linalojadiliwa ni ukubwa wa adhabu dhidi ya kisa husika,
Ndo maana Nchi nyingi zinatoa adhabu ya kifo kwa mtuhumiwa aliyefanya mauaji kwa makusudi, kwa kukusudia.
Sasa ndugu kama hata makosa ya kawaida ya kufumaniwa, kuzini, kumsema kiongozi kwa kumkosoa tu, kuiba pete ya dhahabu nk, hukumu yake iwe kuchinjwa hadharani ?
Tunaambiwa adhabu hizo kali zinawapata haswa wageni na wananchi wa daraja la chini na wanaoonewa kwa chuki za kisiasa na visazi
Matajiri na viongozi wa Saudia wao hawaguswi na ahabu hizo kwani wanauwezo wa kujificha na kujilinda
mfano
Bwana Yesu Kristo alivyopelekewa mwanamke mzinzi ili apigwe mawe hadi kufa. Wauaji hao walikimbia baada ya kuambiwa asiyewahi kutenda kosa hilo awe wa kwanza kumpiga mawe na kumwua binti huyo.
Binti huyo aliletwa peke yake ivi alijizini mwenyewe ?
Mwanaume aliye zini naye alikuwa mtu maarufu, kiongozi, mtu tajiri, ndio maana aliachwa asiuawe.
Hata huko Marekani majimbo mengine hayauwi walioua kwa makusudi.
Huwezi kuzuia makosa kwa kuchinja watu.
njia nzuri ya kuzuia uhalifu ni kuielimisha jamii iweze kumudu maisha, iweze kustarabika, iweze kujitegemea kimaisha, iweze kuzijua haki zake na kuzidai nk
Pia Serikari inatakiwa kutimiza majukumu yake ya, kutoa huduma za jamii kwa kiwango cha kuridhisha.
Kama Elimu, Afya, Ulinzi, Haki,
Demokrasia nk.
Adhabu ya kuua aliyeua kwa makusudi bado wanaopigania haki za binadamu wanapinga ulipaji huu wa kisasi.
Uchinjaji watu hadharani ni udhalimu.
Hauna nafasi katika nchi zilizostarabika kama Nchi yetu nzuri.