Adhabu ya kifo kwa Muhammad Mursa iliyozua simanzi

Adhabu ya kifo kwa Muhammad Mursa iliyozua simanzi

Kama imani yao na utashi wao kama taifa vinaruhusu acha wafanye wanaloona lina manufaa kwao.

But mimi huwa nafarijika kwamba as long as hakuna ataeishi tuseme labda miaka 500 au hata 150 bila kufa soon haya tunayofanyiana binadamu humu duniani tunaenda kuyatolea hesabu iwe kwa kutaka au kwa kulazimishwa,siku inakuja na hivi miaka 100 kibongo bongo 60 tunaitafuta kwa torch mtu anifanyie ubaya anavyoweza ipo siku itadhihirika tu.
 
chini ya sheria hakuna mkamilifu hata mmoja ndio maana Yesu alikuja na kwa njia ya yeye tunaishi kwa neema na nguvu ya msamaha kwa imeandikwa usihukumu usije ukahukumiwa na kisasi ni juu ya MUNGU mwenyewe .hiyo post inasikitisha kwa kwel
 
Kusamehe 7 mara 70 nakumpenda adui ndivyo nilivyofunzwa tangu udogoni
Alipoulizwa yeye mwenyewe, aliionesha Qur'an.

Qur'an ni muujiza unaoishi. Siyo wa kuhadithiwa tu kama mingine yote.
 
Ndio maana Saudia kuna amani kubwa, hakuna ujinga wa majambazi, wauwaji au panya road,
Unauwa kwa kusudia unauwawa tu labda wenye familia ya alie uwawa wakusamehe.
Hii sheria tunahitaji hapa ili tuishi kwa amani na furaha.
 
View attachment 2767997
Umewahi kuona muuaji ambaye polisi wanamlilia, wanahabari wanalia, watu wanakusanyika wakimuombea msamaha, na nchi nzima inalia, lakini pamoja na yote hayo hukumu ya kifo ikatekelezwa? Tukio hili la kusikitisha sana la mauaji ya kukatwa kichwa kwa upanga lililotekelezwa tarehe 20 Septemba mwaka 2023 huko nchini Saudia Arabia. Hii ni tukio linalomhusisha kijana Muhammad Mursal. Unaweza kuona katika picha hapa chini kijana akimbusu mwanamke. Mwanamke huyu ni mama wa kijana huyu, na huyu ni Muhammad Mursal.
View attachment 2767998
Dakika 20 za Mwisho
Jaji Sab anamwambia mama yake aonane na mwanaye kwa dakika 20 za mwisho; baada ya hapo, shingo ya mtoto wake itakatwa! Ni kijana wa miaka 22 tu. Muhammad Mursal alimuua binamu yake aliyeitwa Moeed bin Abdullah bin Mohsen Al-Yami kwa mikono yake mwenyewe, bado haijaelezwa zaidi namna ya uuaji huo ulivyo tendeka. Baada ya hapo, Muhammad Mursal alikamatwa na kuhukumiwa kifo mahakamani.

Kulingana na sheria ya Kiislamu, Ndugu wa marehemu walikuwa na machaguo matatu, wanaweza kukubali adhabu ya hukumu ya kifo, wanaweza kusamehe, au walipe kisasi, yaani jino kwa jino, baada ya hapo hukumu ya kifo kwa upanga hutolewa. Kwa wakati huu ndugu wa marehemu wanachagua hukumu ya kifo kwenda kwa Muhammad Mursal.

Watu wote wa ukoo wa Al-Rizq; watoto, wazee, wanawake wote wanakwenda pamoja kwenye ukoo ambapo mtu ameuawa, na wanapofika kwenye ukoo huo, mashairi na nyimbo huimbwa mbele ya watu hao wote. Wale wanaovaa vilemba huvua vilemba, joho, na mavazi wanayovaa na kuyaweka miguuni mwa watu wa ukoo huo.

Mashairi husomwa na vijana wadogo. Wazee wa ukoo wanainuka na mikono yao imefungwa na kuomba msamaha. Matajiri wana sifa moja: hawainuki kwa urahisi mbele ya mtu yeyote; wanashikamana na majivuno yao. Lakini hapa, watu hawa wameinama mbele ya watu wa ukoo huo na kuanza kuomba msamaha mbele yao hadi wawaweke miguuni mwao na kujitupa mbele yao. Kila vito vya thamani ikiwemo dhahabu na mali waliyonayo hutolewa kama malipizi ya msamaha huu.

Ndugu hawa walikuwa tayari kutoa kila kitu walichokuwa nacho kwa wale ambao ndugu yao aliuawa. Taarifa hizi zilisambaa kwenye vyombo vingi vya habari na watu wengi walionyeshwa kuguswa na haswa waliungana kwa pamoja ili kuisihi familia ya Al-Yami iwasamehe ndugu hawa ili kijana huyu mdogo asiuwawe kwa upanga!

Hii ni kwa sababu Muhammad Mursal ni lazima angeuwawa iwapo msamaha usinge tolewa kwa sababu yeye aliuwa bila kutarajia. Sasa kwamba jambo hili limeonekana katika vyombo vya habari, linakuwa lugha ya Saudi Arabia nzima, na lugha hiyo ni kusamehewa. Sasa mamlaka ya sheria pia yanafuatilia. Mfalme Salaman pia anafuatilia. Dunia nzima inaangalia kwamba hii imekuwa tukio kubwa sana hadi nchi nzima inakusanyika na kuomba msamaha kwa familia ambayo mtu ameuawa, lakini hawasamehi!
View attachment 2767999
Siku ya mwisho ya Muhammad Mursal
Hatimaye, siku inafika wakati Muhammad Mursal alipaswa kuhukumiwa adhabu ya kifo, tarehe 20 mwezi Septemba mwaka 2023. Takriban siku saba kabla, kikao kinafanyika. Watu wanaitwa wa koo na kabila zote mbili zilizokinzana kwa ajili ya kuomba msamaha. Vyombo vya habari vinakusanyika. Mzee wa heshima amesimama mbele ya kipaza sauti, "Asalaam aleykum, sisi tumekuja kwa ajili ya ambaye mama, binti, dada, watoto, na wazee wa taifa wanamuombea. Maombi ya kila mtu yalikuwa kwamba mtu huyu asamehewe, ikiwa hata serikali inapenda kumsamehe huyu mtu ikiwa ni kwa ridhaa yenu ninyi mliotendewa kosa hili, tunawaomba mumsamehe tupo chini ya miguu yenu."

Mzee wa makamo amesimama akiwa amejifunga jambia kiunoni amezunguukwa na ndugu waliokunja sura zao, wamegoma kusamehe wote wamevaa kanzu na vilemba, "Hapana tumekataa msamaha wenu tumekataa mali zote na dhahabu, na ngamia, na vilemba, na kazu na malizote za mamilioni mlizozitoa, tunataka adhabu ya kifo itendeke, kwani kijana wenu aliua kwa kukusudia na haikuwa bahati mbaya, sheria ya Mungu(Allah) itekelezwe auwaye kwa upanga naye atakufa kwa upanga!"

Wakati huo, watu wa vyombo vya habari wanaanza kulia, polisi wanalia, umati unalia, na hata ndugu wa marehemu nao wanalia, lakini adhabu ya kifo inatekelezwa kwa njia ya kinyama kukatwa shingo kwa upanga mkali sana unaotenganisha kichwa na kiwiliwili kwa pigo moja tu. Ulimwengu unajifunza nini kupitia adhabu hii kali aliyopewa kijana Muhammad Mursal? Kwa mujibu wa uislamu kila mtu ni sawa, iwe tajiri, iwe masikini, iwe mfalme, au iwe mtu wa kazi, sheria za Kiislamu zinaweka usawa kwa wote na amri ni sawa kwa wote. Katika sheria ambapo kila mtu ni sawa.

Kulingana na mafundisho ya Kiislamu, kumuua binadamu bila haki ni dhambi kubwa ya pili baada ya shirki, lakini baadhi ya wanazuoni wamesema kwamba yeyote anayemuua Muislamu anajitoa kwenye uislamu. Hivyo adhabu yake ni Jahannam, ambayo atakaa humo milele, na Mwenyezi Mungu atateremsha ghadhabu yake juu yake na kumlaani. Mwenyezi Mungu Mtukufu ameandaa adhabu kubwa kwa ajili yake, lakini baadhi ya wanazuoni wanasema atakaa Jahannam kwa muda mrefu na atapata adhabu kali.
View attachment 2768000 View attachment 2768001
Ovyo KABISA Bora UKRISTO msamaha ni priority namba Moja.
 
Tusali:
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe..........,,............................. .........,,
Utusamehe makosa yetu kama tunavyowasamehe waliotukosea...........,.
..................
Sala hii alifundisha Yesu kristo!
Sala inatumika kinafiq sana hii
 
Hii ije na huku. Tena wale wala rushwa na kutumia madaraka wapigwe mawe wafe.
 
Dini gani hii haina upendo na msamaha
Wangemuacha aishi Mungu angemuadhibu mwenyewe atakavyo
Uislam hauna unafiki wa kujifanya unasamehe huku ukiugulia moyoni.

Watu wanasema waislam makatili lakini utakuta ndio hao hao wanakimbilia kwa waganga kutafuta dawa ya kuadhibu wale waliowakosea.

Sheria za Kiislam zingetumika dunia nzima kungekuwa na adabu mno.
 
Hii Hukumu ingekuja hapa tusingekuwa na Rais yoyote hadi sasa, japo wa sasa hata Tarehe 19 Machi, 2021 asingefika
 
Uislam hauna unafiki wa kujifanya unasamehe huku ukiugulia moyoni.

Watu wanasema waislam makatili lakini utakuta ndio hao hao wanakimbilia kwa waganga kutafuta dawa ya kuadhibu wale waliowakosea.

Sheria za Kiislam zingetumika dunia nzima kungekuwa na adabu mno.
Sheria bila hekima ni tatizo
 
Back
Top Bottom