Adhabu ya kifo kwa Muhammad Mursa iliyozua simanzi

Adhabu ya kifo kwa Muhammad Mursa iliyozua simanzi

hii ni video ya tatu kuangalia, ya kwanza niliiona syria, kijana mmoja mkristo alichinjwa kwa kukataa kusilimu, walitengeneza kama mfereji wanachinja na kutupa kwenye bwawa au shimo kitu kama hicho, wanavyomchinja wanashika kichwa vidole wanashika pua kama kuku, damu ilimwagika, aiseee. nikawa najiuliza hawa mungu wao ni wa aina gani?

lakini hata hivyo, Mungu ni wa rehema, anawapenda, badilikeni achacheni na hiyo dini, sio ya Mungu hiyo.
Na wanabarikiwa hadi wanakuwa Matajiri wanamiliki DPW.

Huyu Mungu bado simwelewi anawaacha watu kama haw /a akwa faida ipi?
 
Unauwaje huku unajua kuwa adhabu yake ni kifo
Kutokana na tabia ya kuuana kwa wamedi na waajemi hata hivyo Matukio ya kuuana Nchi hizo ni mengi sana.

Unaweza kukosana na mtu kwa jambo dogo tu na akakujia na Panga usiku akakumaliza.

Jambo au tukio likifanywa kwa mazoea linakuwa jambo la kawaida kwa jamii
 
Kutokana na tabia ya kuuana kwa wamedi na waajemi hata hivyo Matukio ya kuuana Nchi hizo ni mengi sana.

Unaweza kukosana na mtu kwa jambo dogo tu na akakujia na Panga usiku akakumaliza.

Jambo au tukio likifanywa kwa mazoea linakuwa jambo la kawaida kwa jamii
usisahau kutaja namna wanavyowarusha wasichana housegirls toka gorofani, kwasababu zisizo za msingi kabisa.
 
Kutokana na tabia ya kuuana kwa wamedi na waajemi hata hivyo Matukio ya kuuana Nchi hizo ni mengi sana.

Unaweza kukosana na mtu kwa jambo dogo tu na akakujia na Panga usiku akakumaliza.

Jambo au tukio likifanywa kwa mazoea linakuwa jambo la kawaida kwa jamii
Kwa hiyo kuuwana iko kwenye damu zao.
 
Hii sheria ni nzuri sana ingefaa itumike Dunia nzima ili kuleta haki na usawa kwenye jamii bila kujali tajiri au masikini
 
Dini gani hii haina upendo na msamaha
Wangemuacha aishi Mungu angemuadhibu mwenyewe atakavyo
Kuna dini au sheria ipi nyingine duniani, warithi wakikusamehe, yamekwisha?
 
Hii sheria ni nzuri sana ingefaa itumike Dunia nzima ili kuleta haki na usawa kwenye jamii bila kujali tajiri au masikini
Bahati Mbaya sana huko huko inakotumika watu wanacharangana mapanga kila kukicha.

Amani haiji kwa Ncha ya Upanga.
 
Huenda Mungu wao Hana nguvu ya kuadhibu wanamsaidia
Hii ni hukumu ya haki.
Hata ustaarabu na uaminifu wa wazungu ulijengwa kwa damu.
Zamani ilikua ukimdhulumu mtu au kumuua unasakwa kimya kimya nawe unalipiziwa kisasi, ndipo ikawajengea watu uoga wa kutowatendea wengine mabaya kwa hofu ya kulipwa kisasi
 
Uislam ndio unasheria ya haki kwenye jamii kisasi kisasi
 
View attachment 2767997
Umewahi kuona muuaji ambaye polisi wanamlilia, wanahabari wanalia, watu wanakusanyika wakimuombea msamaha, na nchi nzima inalia, lakini pamoja na yote hayo hukumu ya kifo ikatekelezwa? Tukio hili la kusikitisha sana la mauaji ya kukatwa kichwa kwa upanga lililotekelezwa tarehe 20 Septemba mwaka 2023 huko nchini Saudia Arabia. Hii ni tukio linalomhusisha kijana Muhammad Mursal. Unaweza kuona katika picha hapa chini kijana akimbusu mwanamke. Mwanamke huyu ni mama wa kijana huyu, na huyu ni Muhammad Mursal.
View attachment 2767998
Dakika 20 za Mwisho
Jaji Sab anamwambia mama yake aonane na mwanaye kwa dakika 20 za mwisho; baada ya hapo, shingo ya mtoto wake itakatwa! Ni kijana wa miaka 22 tu. Muhammad Mursal alimuua binamu yake aliyeitwa Moeed bin Abdullah bin Mohsen Al-Yami kwa mikono yake mwenyewe, bado haijaelezwa zaidi namna ya uuaji huo ulivyo tendeka. Baada ya hapo, Muhammad Mursal alikamatwa na kuhukumiwa kifo mahakamani.

Kulingana na sheria ya Kiislamu, Ndugu wa marehemu walikuwa na machaguo matatu, wanaweza kukubali adhabu ya hukumu ya kifo, wanaweza kusamehe, au walipe kisasi, yaani jino kwa jino, baada ya hapo hukumu ya kifo kwa upanga hutolewa. Kwa wakati huu ndugu wa marehemu wanachagua hukumu ya kifo kwenda kwa Muhammad Mursal.

Watu wote wa ukoo wa Al-Rizq; watoto, wazee, wanawake wote wanakwenda pamoja kwenye ukoo ambapo mtu ameuawa, na wanapofika kwenye ukoo huo, mashairi na nyimbo huimbwa mbele ya watu hao wote. Wale wanaovaa vilemba huvua vilemba, joho, na mavazi wanayovaa na kuyaweka miguuni mwa watu wa ukoo huo.

Mashairi husomwa na vijana wadogo. Wazee wa ukoo wanainuka na mikono yao imefungwa na kuomba msamaha. Matajiri wana sifa moja: hawainuki kwa urahisi mbele ya mtu yeyote; wanashikamana na majivuno yao. Lakini hapa, watu hawa wameinama mbele ya watu wa ukoo huo na kuanza kuomba msamaha mbele yao hadi wawaweke miguuni mwao na kujitupa mbele yao. Kila vito vya thamani ikiwemo dhahabu na mali waliyonayo hutolewa kama malipizi ya msamaha huu.

Ndugu hawa walikuwa tayari kutoa kila kitu walichokuwa nacho kwa wale ambao ndugu yao aliuawa. Taarifa hizi zilisambaa kwenye vyombo vingi vya habari na watu wengi walionyeshwa kuguswa na haswa waliungana kwa pamoja ili kuisihi familia ya Al-Yami iwasamehe ndugu hawa ili kijana huyu mdogo asiuwawe kwa upanga!

Hii ni kwa sababu Muhammad Mursal ni lazima angeuwawa iwapo msamaha usinge tolewa kwa sababu yeye aliuwa bila kutarajia. Sasa kwamba jambo hili limeonekana katika vyombo vya habari, linakuwa lugha ya Saudi Arabia nzima, na lugha hiyo ni kusamehewa. Sasa mamlaka ya sheria pia yanafuatilia. Mfalme Salaman pia anafuatilia. Dunia nzima inaangalia kwamba hii imekuwa tukio kubwa sana hadi nchi nzima inakusanyika na kuomba msamaha kwa familia ambayo mtu ameuawa, lakini hawasamehi!
View attachment 2767999
Siku ya mwisho ya Muhammad Mursal
Hatimaye, siku inafika wakati Muhammad Mursal alipaswa kuhukumiwa adhabu ya kifo, tarehe 20 mwezi Septemba mwaka 2023. Takriban siku saba kabla, kikao kinafanyika. Watu wanaitwa wa koo na kabila zote mbili zilizokinzana kwa ajili ya kuomba msamaha. Vyombo vya habari vinakusanyika. Mzee wa heshima amesimama mbele ya kipaza sauti, "Asalaam aleykum, sisi tumekuja kwa ajili ya ambaye mama, binti, dada, watoto, na wazee wa taifa wanamuombea. Maombi ya kila mtu yalikuwa kwamba mtu huyu asamehewe, ikiwa hata serikali inapenda kumsamehe huyu mtu ikiwa ni kwa ridhaa yenu ninyi mliotendewa kosa hili, tunawaomba mumsamehe tupo chini ya miguu yenu."

Mzee wa makamo amesimama akiwa amejifunga jambia kiunoni amezunguukwa na ndugu waliokunja sura zao, wamegoma kusamehe wote wamevaa kanzu na vilemba, "Hapana tumekataa msamaha wenu tumekataa mali zote na dhahabu, na ngamia, na vilemba, na kazu na malizote za mamilioni mlizozitoa, tunataka adhabu ya kifo itendeke, kwani kijana wenu aliua kwa kukusudia na haikuwa bahati mbaya, sheria ya Mungu(Allah) itekelezwe auwaye kwa upanga naye atakufa kwa upanga!"

Wakati huo, watu wa vyombo vya habari wanaanza kulia, polisi wanalia, umati unalia, na hata ndugu wa marehemu nao wanalia, lakini adhabu ya kifo inatekelezwa kwa njia ya kinyama kukatwa shingo kwa upanga mkali sana unaotenganisha kichwa na kiwiliwili kwa pigo moja tu. Ulimwengu unajifunza nini kupitia adhabu hii kali aliyopewa kijana Muhammad Mursal? Kwa mujibu wa uislamu kila mtu ni sawa, iwe tajiri, iwe masikini, iwe mfalme, au iwe mtu wa kazi, sheria za Kiislamu zinaweka usawa kwa wote na amri ni sawa kwa wote. Katika sheria ambapo kila mtu ni sawa.

Kulingana na mafundisho ya Kiislamu, kumuua binadamu bila haki ni dhambi kubwa ya pili baada ya shirki, lakini baadhi ya wanazuoni wamesema kwamba yeyote anayemuua Muislamu anajitoa kwenye uislamu. Hivyo adhabu yake ni Jahannam, ambayo atakaa humo milele, na Mwenyezi Mungu atateremsha ghadhabu yake juu yake na kumlaani. Mwenyezi Mungu Mtukufu ameandaa adhabu kubwa kwa ajili yake, lakini baadhi ya wanazuoni wanasema atakaa Jahannam kwa muda mrefu na atapata adhabu kali.
View attachment 2768000 View attachment 2768001
Ila hawa wenzetu wana moyo. Ngoma inapigwa hadharani.
 
Back
Top Bottom