Afande Sele amjia juu Mpoto, adai kutomsema marehemu kumepitwa na wakati

Afande Sele amjia juu Mpoto, adai kutomsema marehemu kumepitwa na wakati


Msanii Afande Sele amesema kitendo cha watu kumwambia kuwa anafanya vibaya kumsema marehemu (Steven Kanumba) ni kitendo ambacho kimepitwa na wakati na mila zisizofaa.

Afande Sele ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, huku akimjibu Mrisho Mpoto baada ya kumwambia anakosea kumsema marehemu kuwa alikuwa anabaka, na kusema kwamba mila kama hizo hazifai kwenye jamii kwani zinaleta madhara makubwa baadaye.

Afande Sele ameendelea kwa kusema kwamba ni ukweli usiopingika kuwa Kanumba alikuwa anafanya dhambi, hivyo ni jambo ambalo halitakiwi kufichwa ili wengine wajifunze kupitia hilo.

Hivi karibuni kumekuwa na mvutano mkubwa baada ya muigizaji ELizabeth Michael (Lulu) kuhukumiwa kwa kifo cha Kanumba, na baadhi ya watu kusema kuwa alistahili adhabu hiyo huku wenine wakidai ameonewa kwani marehemu alikuwa anamrubuni kutokana na kuwa na umri mdogo kwake.
Afande yupo sahihi. Mpoto ni agent wa ibilisi
 
Culturally wanyama wanasemwa kwa mabaya au mazuri wakiwa wamekufa au kufariki wewe uliwahi kusikia habari za Faru John kabla ya Kifo chake,wewe uliwahi kusikia aliyoyafanya mengi Maleale kabla ya kifo chake,wewe uliwahi kusikia historia ya Kinjekitile kabla ya kifo chake N.K
Hahaha nimekukubali uncle. Njoo uchukue balimi yako hapa Sinza kwa Mugabe
 
Huyu kaka sio mstaarabu hata kidogo yaani, alikuwa wapi kumwambia alipokuwa hai? Haya leo hii anaongea huyo marehemu anasikia?
Kwani marehem hasemwi? Vipi kukusu kumsema MangiMeli, Kinjekitile, Karume n.k? Afande is correct
 
Huo ni upuuzi mtupu kwa nini usingemuonya alivyokuwa hai , eti Leo unajifanya unafunguka huo ni unafiki mkubwa, huna lolote
 
Hii sasa kiki, aliongea mwanzo tukamuelewa bas angenyamaza tu mlengwa mwenyewe keshakubaliana na hali na hataki dhamana sasa wao kinawawasha nn
Kweli kabisa yani imekuwa too much kila siku anaongea jambo lile lile over marehemu anaskia
 
kiukweli afande hayupo sahihi issue ya kuwa kwenye mahusiano na mtu kuanzia miaka 18 imewekwa tu na wanadamu haikushushwa ila tumeweka wanadamu so kumkuta mtu yupo ndani ya mahusiano katika umri huo sio dhambi ila ni kosa kisheria,
ila pia naweza sema sio kosa kwasababu hata sheria ilikuwa inaruhusu watu kuolewa kuanzia miaka 14


Wabongo wengi hawana upeo wa kuchanganua mambo. Unasema sheria imewekwa tu na binadamu, sasa we ulitaka iwekwe na ng'ombe?
 
Hivi wewe utafurahi Binti w
yako wa 14 or 15 akipitiwa na mabazazi ya more than 25?
 
Afande Sele na yeye anatakiwa ajue kwamba amepitwa na wakati
 
Kama kweli yeye mwanamme si amseme Ali Kiba yuko hai na alikuwa anatembea na Lulu kabla ya Kanumba. aoneshe kama kweli yeye sio mnafiki. yeye ana mazuri gani. kipindi kile Lulu alikuwa katika kila magazeti na mabwana zake wanatajwa na yeye alishakiri kutembea na baadhi. wote hao wazima bado sasa awaongelee asisubiri wafe maana hawataweza kujitetea.
 
Ndio amekufa kitambo. Je kuna umuhimu wa kumuongelea leo? Kabla hajafa alikuwa anatembea na huyo mtoto (wakati huo akiwa under 18) na wengi walijua. Walipaswa kuliongelea hili kipindi hicho
Watu walikuwa hawajui kifo kilimuumbua kwanza kila mtu alishangaa
 
Hivi wewe utafurahi Binti w
yako wa 14 or 15 akipitiwa na mabazazi ya more than 25?
Hakuna mtu atakubali lakini mabwana zake wengine si wako wazima awaseme maana Marehemu hakuwa wa kwanza wako kina Kiba sijui na wengi tu atoke awaseme sio kila siku kumsema mtu ameshafariki hawezi kujitetea wakati yeye mweyewe Lulu alisema she is 18 that time na kila siku alikuwa clubs picha magazeti yote ziko na wazazi wake si walikuwepo. tusiwe wanafiki kujifanya malaika wote tuna madhambi lakini ukifa ni kumuombea kwa Mungu ndio mwenye rehma tusijifanye miungu watu.
 
Hakuna mtu atakubali lakini mabwana zake wengine si wako wazima awaseme maana Marehemu hakuwa wa kwanza wako kina Kiba sijui na wengi tu atoke awaseme sio kila siku kumsema mtu ameshafariki hawezi kujitetea wakati yeye mweyewe Lulu alisema she is 18 that time na kila siku alikuwa clubs picha magazeti yote ziko na wazazi wake si walikuwepo. tusiwe wanafiki kujifanya malaika wote tuna madhambi lakini ukifa ni kumuombea kwa Mungu ndio mwenye rehma tusijifanye miungu watu.
She is[emoji735]
She was[emoji736]
 
Kumsema VIBAYA marehemu aliyefanya VIBAYA kutembea na mtoto mdogo na kumtoa out kwenye kumbi za starehe?

Sema tu unavyojisikia. It doesnt really matter.
 
kimsingi alichokisema Afande sele amefanya watu wafikirie zaidi. But normally watu wenye rasta wanakua na hekima flan na kuona mbali. Ni basi tu hawezi kumfikia bob marley but baadhi ya watu Wanamwelewa
 
Tatizo wabongo wamekariri marehemu kusemwa kwa mazuri tu, ila kiukweli kama alizingua inapaswa kusema tu. Mpoto naye apunguze shobo kwanza harakati za mjomba zishamshinda siku hizi sijui kishanunuliwa kama wale madiwani? ila itapendeza zaidi afande zile akipunguza kumoka mmea.. - Get well soon lulu (in harmorapa voice)
 
Back
Top Bottom