Afande Sirro, ukimuona Lissu kama unavyomuona Magufuli kuwa wote ni wagombea Urais, basi utakuwa na amani na Lissu

Mkuu umeandika vizuri, IGP mpaka Sasa amejitahidi Sana hata kauli yake ya leo sawa ,ila amejitahidi,huyu mzee anapitia kipindi kiguma ambacho wamekipitia IGP wengine ambao sidhani Kama wapo, ila ivyo binafsi nasema mungu aendelee kumpa hekima ,na akiona vipi basi amuachie mtu mwingine apambane na Hali yake ,vyeo vipo ila mbele ya Safari raha ya moyo mtulivu ,usiokua na stress au hata Kama huna pesa ni flaha tosha ,naongea kwa kifupi ila nikiwa na maana pana mkuu
 
Kuna tofauti kubwa kati ya...
Mgombea Urais na Rais
Mropokaji na Mtendaji
HGL, HKL na PCM
Mpenda sifa na Mtu asie jikweza.

Sasa tafuta ujue Lissu yupo kundi gani.
Mtu kasoma HGL anataka kutusumbua sisi. Hebu muambieni Urais sio kubwabwaja tu. Yeye amefanyia jimbo lake nini mpaka leo tumuamini kuwa Rais. Kila siku ana lazimisha kuwa nilazima awe Rais kwani hizo kura anajipigia mwenyewe au yeye ni Mungu mpaka alazimishe watu kuwa yeye ndie Rais iwe isiwe.
Mkumbusheni wanaopiga kura na kuamua ni Watanzania so ASITUFOKEE.

Bado ninatafuta mahali ambapo Lissu amenadi wa BUNGE na MADIWANI wa chama chake akiwa kwenye mikutano yake.
Hapa ndio ninafikia na kuona kuwa huyu mtu hayupo serious kabisa ana umimi mwingi sana ndio maana sioni sera zake zikiwa na mashiko zaidi ya kutuonyesha Ungwini wake tu.
Watanzania hatutaki sheria..... Sheria ibakie kwako na ndugu zako sisi tunataka KIONGOZI anae toa sera zinazotekelezeka.
 
Well said
 
Aisee na wewe unaona umetoa hoja ile mbaya aisee hii nchi hawa ndo wapiga kura wa Jamuhuri ya Muuangano wa Tanzania Aisee
 
Alipoamuwa kukabidhi kichwa chake pale Lumumba ndo akaanza kutenda hayo. Siro halisi mwenye kichwa chake ni yule wa Mwanza enzi hizooo. Huwa anazo busara akiwa ni yeye.
 
Rais anayegombea urais!
 
Magufuli umeshaona anafanya mikutano kwenye giza wakati muda wa campaign mwisho saa 12 jioni.

Lissu kwakweli ni tatizo.
 
Lissu anavunja sheria kwa makusudi. Tuambie wapi magufuli amevunja sheria. Kwahiyo hapa suala siyo kuwa treated vizuri, ni mtu anatakiwa afuate sheria.
1. Akiwa Buchosa alitangaza tender ya barabara kinyume cha maadili ya uchaguzi.

2 Akiwa Bunda alitangaza ubaguzi wa maendeleo kinyume cha katiba ya Jamhuri ya Muungano.

3 Akiwa Bukombe akatangaza tender ya barabara kinyume cha maadili ya uchaguzi.

4. Akiwa Dodoma alitangaza tender ya barabara kinyume cha maadili ya uchaguzi

5 Akiwa Magu alihutubia kwa lugha ya kisukuma na kuwatisha wananchi kinyume cha maadili ya uchaguzi na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

6. Akiwa Tunduma alitoa rushwa ya kutoa hela kwa mpiga kura kinyume cha maadili ya uchaguzi

7 Akiwa Kasulu Kigoma alivamia mkutano wa Tundu lissu kazuramimba kinyume cha maadili ya uchaguzi.

8. Katika kampeni zake amekuwa akihubiri ubaguzi kinyume cha katiba ya nchi.

9. Hafuati ratiba ya uchaguzi kama ilivyopangwa hivyo kwenda kinyume cha maadili ya uchaguzi.

10. Akiwa Simiyu alihutubia mkutano zaidi ya saa 12.30 kinyume cha sheria ya uchaguzi na kanuni za uchaguzi.


Yote hayo niliyoyataja hapo Tume na jeshi la polisi wako kimya kwa sababu anayeyatenda sheria hazimhusu.
 
Lissu anavunja sheria kwa makusudi. Tuambie wapi magufuli amevunja sheria. Kwahiyo hapa suala siyo kuwa treated vizuri, ni mtu anatakiwa afuate sheria.
Tutajie sasa na wewe sheria anazovunja Lissu.
 
Si ivyo tu, kama alivyoshindwa kuwatumia policcm kuwatawanya watu walomsubili mh TAL pale moshi ndio ivyo ivyo Lissu alishindwa kupita bila kukutana na kuongea nao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…