Afariki baada ya kipigo kutoka kwa mumewe

Afariki baada ya kipigo kutoka kwa mumewe

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Mwanamke mmoja Mkazi wa Kijiji cha Kanyarakata Kata ya Mbuluma Wilayani Kalambo Mkoani Rukwa, Albetina Mazwile (42) amefariki baada ya kupigwa fimbo katika sehemu mbalimbali za mwili wake na Mumewe na kupelekea kuvuja damu kwa ndani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, William Mwampaghale amesema chanzo cha Mume kumpiga Mkewe ni chuki binafsi "Tunamshikilia Mwanaume huyu tukikamilisha uchunguzi tutamfikisha Mahakamani"

Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa limefanikia kumkamata mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 42 mkazi wa Kijiji cha Kanyalakata, Kata ya Mbuluma wilayani Kalambo kwa tuhuma za kumchapa fimbo mke wake aitwaye Albetina Mazwile (42) na kupelekea kifo chake.

Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Rukwa, ACP William Mwampaghale amesema mwanaume huyo alianza kumshambulia mkewe kwa fimbo katika maeneo balimbali ya mwili wake na kusababisha kuvuja damu nyingi kwa ndani na baadaye kusababisha mauti.

Anashikiliwa, uchunguzi utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

Aidha, ACP Mwampaghale ametoa kutoa wito kwa wananchi wote kutoa ushirikiano katika kutoa taarifa za uhalifu ili kukomesha vitendo hivyo.
 
So sad, hatupaswi kufika huko. Dah! Jamaa anaenda kumalizia maisha yake jela..

Mungu tuepushe na hasira za papo kwa papo, hii inatokea popote, hata mtu kakukera mtaani, unamjaza ndoo, unashangaa mtu chaliii, kidizi.
 
So sad, hatupaswi kufika huko. Dah! Jamaa anaenda kumalizia maisha yake jela..

Mungu tuepushe na hasira za papo kwa papo, hii inatokea popote, hata mtu kakukera mtaani, unamjaza ndoo, unashangaa mtu chaliii, kidizi.
2pac wa bongo wewe ungejua yaliyomo ndani ya familia zetu usingesema
 
2pac wa bongo wewe ungejua yaliyomo ndani yafamilia zetu usingesema
Mzee kwani nami naishi katika familia gani, natokea hizi hizi, maisha ya mtaani haya haya, ndio maana nikasema Mungu atupe uvumilivu, sababu mtu anakukera kweli unampiga, kaanguka kafa unaenda kunyea ndoo, ndio hapo hasira hasara.

Unadhani jamaa hapo hata iwe alitiwa kidole cha macho na mkewe ila bado ana hatia ya mauaji.
 
Jamaa apigwe mvua za kutosha, pole yao sana wafiwa...
 
Mzee kwani nami naishi katika familia gani, natokea hizi hizi, maisha ya mtaani haya haya, ndio maana nikasema mungu atupe uvumilivu, sababu mtu anakukera kweli unampiga, kaanguka kafa unaenda kunyea ndoo, ndio hapo hasira hasara.

Unadhani jamaa hapo hata iwe alitiwa kidole cha macho na mkewe ila bado ana hatia ya mauaji.
Kingekuwa kidole afadhali pengine mtu mwenyewe moja tu chali halafu unisumbue sumbue Mimi ,ishia hapohapo mama Samia anatulinda nakutujali wanawake, weeeee weeeee jaribu jamaa kapiga debe linamsubiri nyinyi wanawake ifikie hatua punguzeni midomo
 
Kingekua kidole afadhari pengine mtu mwenyewe moja tu chali harafu unisumbue sumbue Mimi ,ishia hapohapo mama Samia anatulinda nakutujali wanawake ,weeeee weeeee jaribu jamaa kapiga debe linamsubiri nyinyi wanawake ifikie hatua punguzeni midomo
Hapo ndio kinakutoka kibao moto kimoja, mtu chali, umauti umemfika, unaishia korokoroni.
 
Wanawake nao wamezidi kwa mdomo na masimango tangu..... Wakiuliwa ndio inaonekana wameonewa.

Msipojichunga mtaisha maana stress za field kusaka riziki halafu unafika home mwanamke anakusimanga.....hahahaaa.
 
Back
Top Bottom