Afisa Utumishi Igunga avamiwa, ajeruhiwa kwa panga shingoni

Kuna watu ni waajabu sana
Hii yote mtu anafanya sababu ya kazi ambayo sio hata ya baba wala ya mama yake duh kweli tumeumbwa tofauti
 
Watoto wa Ushuani bhana! Yaani kila nyumba ya makazi, basi mnategemea iwe ina kamera za ulinzi!!

Afisa Utumishi mbona ni mtu wa kawaida sana!!
Nakukuhakikishia huyo aliandika hivyo hata kamera yenyewe hajui ikoje. Ni matokeo ya kusoma shule kwa kukariri. Huenda alishasoma comment kama hiyo sehemu basi akaikariri.
 
Jamaa wa Dar hv unajua kuwa hata ofc na makazi ya DED, DC na hata DSO hawana Camera?
Mkuu, hata kwa DC na DSO? Sidhani!

Aisee ningekuwa kwenye hizo nafasi ningeweka camera hata kwa gharama zangu binafsi.
 
Watoto wa Ushuani bhana! Yaani kila nyumba ya makazi, basi mnategemea iwe ina kamera za ulinzi!!

Afisa Utumishi mbona ni mtu wa kawaida sana!!
Mimi nadhani ishu siyo ushua/ufukara.

Usalama kwanza! Kufunga camera kwa ajili ya usalama wako binafsi siyo anasa, iwe ni nyumba ya makazi, biashara, ibada n.k, funga camera kama uwezo upo.

Lakini pia swala la status ya mtu haiwezi kuwa kigezo cha kufunga/kutokufunga camera.

Swali la msingi la kujiuliza ni je, unamudu gharama za kufunga camera? Period.
 
Huku halmashauri ukiwa mchapa kazi sana na muadilifu,utatengenezewa fitna hadi utaacha kazi mwenyewe.

Ili uishi vizuri,aidha uwe mcha Mungu sana au mshirikina sana.
Ukiwa haupo upande wowote,basi usionekane bora kwenye kazi,watakutoa roho au kurogwa uache kazi
 
Halmashauri kwa experience yangu sio pa kitoto mimi kuna muda nimewahi fikiria kujiua, mimi huyuhuyu nimewahi kufikiria ku quit.. Namshukuru Mungu nipo najitafuta ingawa sijajipata bado
 
Una uhakika gani kama inahusiana na kazi yake? Inawezakua mambo ya mapenzi au uhalifu wa vibaka.
Ingekuwa ni uhalifu wangempiga telo na kuingia nae ndani kuchukua wanachokitaka, ila wamemvizia na kumpiga panga la kichwa na kukimbia, hawajachukua hata simu iliyodondoka. Hapo ni ishu ya visasi hasa kazini
 
Nilikuwa nauliza. Hivi afisa utumishi naye huwa anachangia hoja katika vikao vya baraza la madiwani?
 
Kwà upande wangu....nina hofu ya Mungu sana, ni mcha Mungu.

Wakati napigwa mazengwe...alitokea Mama mmoja hivi wa makamu akaniambia...." Kijana wangu, watu wazuri kama wewe huwa hawadumu hapa kwetu "
Na tena akaendelea kusema " kuna Mhasibu kama wewe alikuaga anafanya Kazi kama wewe...walimuwekea sumu kwenye chakula akafa, na mwingine waliifanya miguu yake ijae maji...akawa hawezi kuja kazini"


Aliniambia yote hayo kwasababu ...nilimwambia achukue posho yangu laki kadhaa . Akashangaa sana kwà kitendo kile.

Ni Mama wa makamu ambae anafamilia kubwa na wajukuu kibao....afu Mimi nilikua niko bachelor. Nakumbuka ..nilimshika mkono tukaenda kwà cashier...akanipa karatasi nikasign perdiem yangu...yeye akapokea ile hela. Hakuamini....
 
Halmashauri kwa experience yangu sio pa kitoto mimi kuna muda nimewahi fikiria kujiua, mimi huyuhuyu nimewahi kufikiria ku quit.. Namshukuru Mungu nipo najitafuta ingawa sijajipata bado
Kabla ya kufanya maamuzi ya kuquit. Nilitaka kujiua kwà kamba. Then nikafanya maamuzi ya kuomba ruhusa kwenda masomoni kwà gharama zangu mwenyewe.

Faili langu likaanza kupotea. Kila likifunguliwa lingine....linapotea. Daah Halmashauri sio poa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…