African Development Bank yaidhinisha mkopo wa zaidi ya trilioni 1.4 kujenga reli itakayounganisha Burundi na Tanzania

African Development Bank yaidhinisha mkopo wa zaidi ya trilioni 1.4 kujenga reli itakayounganisha Burundi na Tanzania

Huyo bibi hizo pesa anazirudisha kwa mshahara wake?
Kupitia diplomasia ya Uchumi na Kupitia kuaminika kwake ndio maana Tanzania imepewa pesa hiyo baada ya kuwa rated vizuri.

Kazi ya Uongozi wa Samia na utazirudiaha wewe Kwa Kodi ila sifa ni za Samia,sawa bwashee?
 
Kupitia diplomasia ya Uchumi na Kupitia kuaminika kwake ndio maana Tanzania imepewa pesa hiyo baada ya kuwa rated vizuri.

Kazi ya Uongozi wa Samia na utazirudiaha wewe Kwa Kodi ila sifa ni za Samia,sawa bwashee?
Ninaelipa ndio nastahili pongezi, huyo mkojani amepewa tu dhamana ya kuwakilisha walipa kodi.
 
EEEeeHEeee, Kagame hawezi kukubali ujinga huo. Ndiyo maana alitaka aunganishe na Mombasa, badala ya Dar!
Najua kama angekuwa ni Kagame shilingi moja isingeibiwa na wapigaji wangeozea ndani.
 
Dar es Salaam. Benki ya Maendeleo ya Afrika imeidhinisha kifurushi cha ufadhili cha dola milioni 696.41 kwa Burundi na Tanzania ili kuanza Awamu ya Pili ya mradi wa Reli ya Pamoja ya Tanzania-Burundi- DR Congo Standard Gauge (SGR).

Awamu hii itashuhudia ujenzi wa kilomita 651 za reli ya njia moja inayotumia umeme, kuunganisha Burundi na mtandao uliopo wa Tanzania na hatimaye bandari ya Dar es Salaam.

Mradi umegawanywa katika sehemu tatu: Tabora-Kigoma (kilomita 411) na Uvinza-Malagarasi (kilomita 156) nchini Tanzania, na Malagarasi-Musongati (kilomita 84) nchini Burundi.

Hii itaunganisha Burundi moja kwa moja na bandari ya Dar es Salaam, na kufungua fursa mpya kwa sekta yake ya madini na kilimo.

Ahadi ya AfDB ni pamoja na $98.62 milioni kama ruzuku kwa Burundi na $597.79 milioni kama mikopo na dhamana kwa Tanzania.

Zaidi ya hayo, Benki itafanya kazi kama Mpangaji Mkuu wa Mamlaka ya Awali (IMLA), ikikusanya hadi dola bilioni 3.2 kutoka kwa benki za biashara, Taasisi za Kifedha za Maendeleo (DFIs), Wakala wa Mikopo ya Mauzo ya Nje (ECAs), na wawekezaji wa taasisi. Gharama ya jumla ya mradi inakadiriwa kuwa karibu dola bilioni 3.93.

Mradi huu kabambe unatarajiwa kuwa na matokeo ya mageuzi katika ukanda huu. Upatikanaji wa huduma ya usafiri wa masafa marefu yenye ufanisi na yenye gharama nafuu itachochea uchimbaji mkubwa wa madini na kilimo cha kibiashara, hasa nchini Burundi pamoja na amana zake kubwa za nikeli.

Mradi huu unaendana na mikakati kadhaa muhimu ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na Mpango Mkuu wa Reli wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Mpango wa Umoja wa Afrika wa Maendeleo ya Miundombinu Barani Afrika (PIDA), na vipaumbele vya Benki yenyewe vya "High 5" na "Integrate Africa".

Pia inaendana na Waraka wa Mkakati wa Benki katika Kanda ya Afrika Mashariki na Hati zake za Mkakati wa Nchi kwa Tanzania na Burundi.

View attachment 2841405
Source: The Citizen Tanzania
For more info read: AfDB approves $696 million for joint Tanzania-Burundi SGR

Maneno mengi ya kupamba, lakini nakuhakikishia hata kama mradi utakuja kukamilika, hali za mataifa haya, hakuna cha pekee kitabadilika.

Tulijenga ya TAZARA, Dar hadi Kaprimposhi, zambia. Tukasema itafungua fursa mbalimbali kwanchi zote kusini mwa Afrika. Je, hizo fursa umeziona? Mpaka tumekosa pesa ya kuendeshea, sasa imebidi tuwarudishie Wachina, waliotujengea. Hii ya SGR tutakaposhindwa kuiendesha, sijui tutamrudushia nani!!

Serikali za Afrika zinaendeshwa na watu wenye upeo mdogo sana, wasio na maarifa yoyote, na wanaojifikiria wenyewe na familia zao kuliko mataifa yao, ndiyo maana hakuna mradi ambao huwa unaendeshwa na Serikali, halafu ukafanikiwa. Wala tusitegemee cha pekee hata kwenye hii SGR itakapomalizika. Malori kwa kuwa ni ya watu binafsi ndiyo yataendelea kuwa ndiyo njia kuu ya kusafirishia mizigo. Ni ajeri hiyo pesa ingetumika kujenga bara maalum ya malori toka Dar mpaka Bujumbura Burundi, mpaka DRC ili itumike na malori ya makampuni binafsi.
 
Hiyo Reli kweli itarudisha fedha kweli? Burundi mizigo yake ni kidogo sana.

Mizigo ya Rwanda ni mingi sana.
Kamwe pesa haitarudi. Mkopo utalipwa kutoka kwenye kodi za mishahara ya wafanyakazi na biashara zinazokamliwa kila siku na TRA. Ikishindikana wataenda kukopa WB, halafu wanaenda kulipa Africa Development Bank.
 
Leo kwa mara ya kwanza umeandika ukweli.
Mimi nina matumaini.
Naamini tumefikia ukingoni mwa ndoto hii mbaya ya CCM. Tutaanza ukurasa mpya; hata kama itakuwa ni chini ya CCM iliyojibadilisha; siyo hii iliyo chini ya huyu mama.

Siioni CCM hii ikidumu hata kidogo.
 
KUna faida gani sisi kukupeshwa, kwanini tusikope pamoja na burudi, ili kushare deni?
 
Hata inayoenda katavi. Hiyo ya katavi ni inahitaji meli mpya ya mizigo. Halafu inabidi pawe na bandari kubwa kwenye ziwa Tanganyika upande wa Tanzania na upande wa Congo. Halafu pawe na Barabara nzuri au reli upande wa congo toka bandari ya ziwa Tanganyika mpaka mashariki au kule kusini kwenye migodi ya congo. Ila hapo kwenye meli, bandari na Barabara/reli Drc ni Changamoto
Meli Tunajenga Tanzania na kazi ya ujenzi wa meli Mpya inaendelea na ukarabati wa meli za zamani unaendelea pia.

Nakumbuka Kuna MoU ya Tzn na DRC ya kujenga Barabara na reli Hadi Kisangani na pia kujenga Barabara na reli Hadi Lubumbashi kutokea huku Lake Tanganyika
 
Mimi nina matumaini.
Naamini tumefikia ukingoni mwa ndoto hii mbaya ya CCM. Tutaanza ukurasa mpya; hata kama itakuwa ni chini ya CCM iliyojibadilisha; siyo hii iliyo chini ya huyu mama.

Siioni CCM hii ikidumu hata kidogo.
I concur with you bro.
 
Back
Top Bottom