Afrika tumepoteza utamaduni wetu, madam Rais amevaa kimagharibi

Afrika tumepoteza utamaduni wetu, madam Rais amevaa kimagharibi

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
1611804967893.png


Afrika tumepoteza utamaduni wetu. Rais ni alama ya nchi, madam Rais angevaa vazi la asili la Ethiopia angeweza kuitangaza nchi yake zaidi.

Nikiwa shule ya msingi , Waziri Mkuu wa India, Bi Indira Ghandi (RIP) alitembelea Tanzania akiwa ndani ya vazi la Sari. Sijawahi kumuona mama huyu enzi za uhai wake akiwa nje ya vazi la Sari.

Mbali na kupoteza utamaduni wetu, pia tunanufaisha makampuni ya Magharibi. Usishangae gauni la Madam Rais kuwa ni brand ya Chanel na lilimgharimu US$ 2,000 (Sina uhakika na hili).

Ninawasifu wa Afrika Magharibi, wameamua kufanya kitenge kuwa vazi la asili. Nilishaweka historia ya vitenge hapa. Ni vazi Wa Dutch waliiga Indonesia wakati wana tawala. Waindonesia walipogoma kununua kopi ya vazi lao iliyotengenezwa na Mdutch, soko lilitafutwa Afrika.

1611805967404.jpeg


Nguo ya asili ya Ethiopia.
 
Wewe unavaa hayo mavazi ya asili? hununui hizo nguo za kimagharibi kama unavyoziita?
Kufaidisha makampuni yakimagharibi ni jambo lisilokwepeka kwasasa,kama utaacha kununu hizo nguo toka kwao,vipi kuhusu bidhaa zingine?

Utaacha kununua Magari,dawa,mashine,vifaa vya Hospitali,Simu.....kisa usiwafaidishe wa Magharibi? hata hao wa Magharibi pia kua vitu wananunua toka nchi zingine na ndio biashara ilivyo.
 
Wewe unavaa hayo mavazi ya asili? hununui hizo nguo za kimagharibi kama unavyoziita?
Kufaidisha makampuni yakimagharibi ni jambo lisilokwepeka kwasasa,kama utaacha kununu hizo nguo toka kwao,vipi kuhusu bidhaa zingine?

Utaacha kununua Magari,dawa,mashine,vifaa vya Hospitali,Simu.....kisa usiwafaidishe wa Magharibi? hata hao wa Magharibi pia kua vitu wananunua toka nchi zingine na ndio biashara ilivyo.
Kwa bidhaa nyingine ni sawa lakini kwa mavazi, tungekuwa na mavazi yetu hata Chanel wangeweza kuiga kuwapata wateja wenye kipato kikubwa. Sari ya celebrity Channel wanatengeneza.
 
Nimependa tuu kupata dondoo za asili ya vitenge,
Maana nilikua najiuliza jee vimeanzia africa au kwa wazungu,
Haraka haraka nisingekua na shaka kama chanzo ni nje, ila nikawa najiuliza kwa nini wakija kwetu kutalii ndio utaona wananunua na kuvaa, ila wakiwa kwao ni nadra sana, hii ilinifanya nihisi asilu yake ni Africa.
 
Bila wazungu viongozi wa Afrika wangefyatuka kama siafu, wazungu ndio wamepunguza makali ya viongozi wa Afrika.
Kwa hili naungana na wewe..
Viongozi wengi wa kiafrica Hofu yao katika kufanya maovu, haipo kwa wananchi wao, Democrasia wala Mungu wao ila Wazungu.

Waarabu pekeee angalau Wao ndio Humtaja Mungu, japo njia zao nazo baadhi naona kama wanamsingizia tuu Mungu, japo sikuhizi kuna walioamua kumfuata Mmarekani na Muisraeli.
 
Nimependa tuu kupata dondoo za asili ya vitenge,
Maana nilikua najiuliza jee vimeanzia africa au kwa wazungu,
Haraka haraka nisingekua na shaka kama chanzo ni nje, ila nikawa najiuliza kwa nini wakija kwetu kutalii ndio utaona wananunua na kuvaa, ila wakiwa kwao ni nadra sana, hii ilinifanya nihisi asilu yake ni Africa.
1611807793638.jpeg

Hii ndiyo asili ya vitenge, Indonesia wanachora maua kwa mikono na wanatumia nta ya nyuki ili kukandamiza rangi. Ndiyo asili ya vitenge vya wax.
 
Nimependa tuu kupata dondoo za asili ya vitenge,
Maana nilikua najiuliza jee vimeanzia africa au kwa wazungu,
Haraka haraka nisingekua na shaka kama chanzo ni nje, ila nikawa najiuliza kwa nini wakija kwetu kutalii ndio utaona wananunua na kuvaa, ila wakiwa kwao ni nadra sana, hii ilinifanya nihisi asilu yake ni Africa.
Kuna mdau alishaniambia mzalishaji mkubwa wa vitenge quality ni Mholanzi na soko lake lipo Africa kwao haitumiki kabisa.
 
Kuna mdau alishaniambia mzalishaji mkubwa wa vitenge quality ni Mholanzi na soko lake lipo Africa kwao haitumiki kabisa.
Baada ya WWII, Mfalme wa Holland alijenga kiwanda cha kutengeneza vitenge. Alipatia vijana wengi sana ajira katika jitihada za kuondokana na recession. Soko kuu likiwa Ghana. Vikitoka Ghana na Nigeria vinafika Congo mpaka Kigoma.
 
Kuna mdau alishaniambia mzalishaji mkubwa wa vitenge quality ni Mholanzi na soko lake lipo Africa kwao haitumiki kabisa.
Ohoooo, Kuna mwingine alisema humu hata hivi vinavyotoka Congo, watu wanaita vutenge vya congo, sio kama vinatengenenezwa Congo, ila ile ni njia tuu ya kuja Tz, akadai vinatokea Zambia, mwingne akapinga, sasa nikabaki tuu na mwaswali yasio na majibu.
 
Back
Top Bottom