AFYA: Wizara ya Afya inasemaje kuhusu utafiti huu?

Nguruka

Senior Member
Joined
Dec 6, 2006
Posts
189
Reaction score
129
Kuna tafiti imechapishwa katika tovuti ya https://www.mdpi.com/2079-6382/11/9/1222?type=check_update&version=2 unaohusu upatikanaji wa mabaki ya dawa katika nyama za kuku tunazokula hususani wale wa broiler. Utafiti umefanyika Ilala na Kinondoni mkoani Dar es Salaam.

Utafiti huo umebeba kichwa ' Determination of Sulphonamides and Tetracycline Residues in Liver Tissues of Broiler Chicken Sold in Kinondoni and Ilala Municipalities, Dar es Salaam, Tanzania' swali langu je wataalam wetu wa afya wanasemaje kuhusu matokeo ya utafiti huo kwani inaonesha uwepo wa kiwango kikubwa cha dawa ghizo katika nyama na tunavila kila siku na kuviingiza katika miili yetu.

Utafiti ulibaini uwepo wa mabaki ya Tetracycline katika sampuli zote za ini zilizochukuliwa na Sulphonamide kuwa ni wa asilimia 21.4 (n=18), wakati kiwango kama hicho cha asilimia 21.4 cha sulphonamide na tetracycline vilibainika.
Utafiti huu umeeleza kuwa kiwango cha mabaki ya sulfonamidi vilikuwa vya kiwango cha juu zaidi cha mabaki (MRL). Asilimia 90.5 ya sampuli zilikuwa na viwango vya tetracycline vilivyozidi kiwango kinachokubalika cha kila siku (ADI)

Nimeambatanisha utafiti huo.

 
Kuleni dawa ndo tiba yenyewe, kifo ni ahadi ya uhakika….. iko pale pale.
 
Nasikia hata hizi “Hormone” wazonyweshwa kuku wanenepe pia zinaathiri binadamu na kuugua Mara kwa Mara.
 
Hao watafiti wafunguliwe mashtaka kwa mujibu wa Sheria ya Takwimuya mwaka 2016 pia wameleta taharuki
 
Nilikuwa nafikilia nikanunue boiler nilikandamize, kwa namna hii hapana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…