Afya ya Wananchi ni kitu muhimu kuliko vyote. Kwanini tusitoe ruzuku kwenye mifuko hii ya bima za afya zinazosuasua?

Afya ya Wananchi ni kitu muhimu kuliko vyote. Kwanini tusitoe ruzuku kwenye mifuko hii ya bima za afya zinazosuasua?

Dr Akili

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2011
Posts
5,119
Reaction score
4,569
Afya ya wananchi ndiyo kitu muhimu kuliko vyote. Shughuli zote za uchumi wa nchi zinategemea sana afya za wazalishaji kuwa na afya njema ya kimwili, kisaikolojia, kiakili na kiroho.

Hii mifuko ya bima za afya ambazo ndiyo tegemeo kuu kwa afya za wananchi zimekuwa zikisuasua kutokana na ukata.

Haziwezi kumudu kujitegemea bila ya kuwakamua sana wateja wake, jambo ambalo haliwezekani kwani wengi wa hao wateja watarajiwa hawana cha kukamuliwa kihivyo. Huu ndiyo ukweli, tutake tusitake.

Sasa kama tunaweza kutoa ruzuku kwa maeneo mbali mbali hususani kwenye mbolea, kwa nini tusifanye hivyo kwenye mifuko hii ya bima za afya?

Tumesikia mfuko wa NHIF ukilalamika kuelemewa na gharama kubwa ya matibabu ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza hususani yale ya saratani, kisukari, figo na moyo ambayo gharama zake zinafikia shilingi bilioni 99 kwa mwaka.

Kwa nini serikali kwa kuanzia isitoe ruzuku ya shillingi billion 100 kila mwaka kwa mfuko huu kutoka kwenye bajeti yake ya mwaka?

Na iendelee hivyo hivyo hadi mifuko hii itakapokuwa na uwezo wa kujitegemea kwa asilimia 100. Kupanga ni kuchagua.

Kwa heshima na taadhima naomba kuwakilisha ombi hili.
 
Nilijia tu in the long run kuwa toto afya card itafail.

Na hili la bima kwa wote nalo litafail pia lazima mifuko ifirisike labda kama lengo ni kukusanya pesa halafu huduma zisitolewe
 
Nilijia tu in the long run kuwa toto afya card itafail.

Na hili la bima kwa wote nalo litafail pia lazima mifuko ifirisike labda kama lengo ni kukusanya pesa halafu huduma zisitolewe
Ni jukumu la wananchi kuhakikisha kuwa haya yasitokee. Toto na mama mjamzito pamoja na wazee na wasiona uwezo wote lazima wapate huduma ya afya bila kujali wana bima au hawana. Wana haki ya kimsingi na ya kikatiba ya kulindwa uhai wao! Haki ya kuishi. Mtu ye yote asipoteze maisha yake kwa sababu tu hana fedha. Hili halikubaliki po pote duniani na mbinguni.
 
20230317_233851.jpg
 
Hakika ulichotujuza ni sahihi. Maana uchumi wa nchi yoyote ile duniani utegemea afya za wananchi, hivyo basi kama itawezekana ni bora serekali izingatie huduma za afya kuwa kipaombele kwa watanzania wote na zipatikane kwa bei rafiki.
 
Back
Top Bottom