Political Jurist
Senior Member
- Sep 6, 2021
- 143
- 120
Katika pita pita zangu mtandaoni nimekutana na taarifa iliyozua gumzo ambayo inahusu Hospitali ya Aga Khan kuiiomba NHIF isitishe mkataba wake wa utoaji wa huduma kwa sababu za kiuendeshaji.
Ilinistua na nikalazimika kwenda mbali zaidi ili kujua sababu ya suala hilo. Hakika niliumia sana kuona hospitali hii inalazimisha ilipwe mamilioni ya fedha na NHIF katika utoaji wa huduma zake, bei ambazo hata katika Hospitali nyinginezo tena zilizo ngazi ya juu ya rufaa ya matibabu.
Katika uchunguzi wangu nilioufanya nimebaini madudu mengi ambayo Aga Khan inataka kuibebesha Serikali mzigo wa kuongeza gharama zaidi za huduma kwa wateja wa NHIF kuliko kiwango cha juu kabisa cha malipo kwa huduma.
Nitatoa mifano michache ya huduma za kawaida kabisa ambazo Aga Khan imekuwa ikidai kuongezewa gharama hizo kwenye huduma wanazotoa kwa wateja wa NHIF.
Ifahamike kuwa Aga Khan sio Hospitali ngazi ya Taifa hivyo bado rufaa zao zote wanalazimika kuzipeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili, hata kama ni Hospitali Binafsi ukiweka gharama za juu pamoja na huduma za ziada hawapaswi kuwa na tofauti kubwa ambayo inatishia uhai wa Mfuko.
Kama Taifa ifike mahali tutafakari endapo Aga Khan wana nia kweli ya kutoa huduma za matibabu au la? Je ni wananchi wangapi wataweza kupata huduma kwa gharama hizi katika hospitali hii? Au wamelenga tabaka gani la kulitibia?
Hata hivyo niipongeze sana Serikali kwa hatua kubwa ya kuboresha huduma za matibabu nchini huduma ambazo awali yawezekana zilipatikana nje ya nchi lakini sasa zinapatikana katika hospitali zetu za umma. Kwa hili kongole kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Viongozi wa na Watendaji wa Wizara ya Afya wakiongozwa na Waziri jembe kabisa Mhe. Ummy Mwalimu.
Ninaamini kwamba katika utoaji wa huduma za matibabu, utu hupaswa kuwa kipaumbele cha kwanza na kuweka maslahi mapana ya kuokoa maisha ya binadamu.
Kwa leo niwaache na tafakari hii ya gharama kubwa zisizo na uzalendo za Aga Khan.
Ilinistua na nikalazimika kwenda mbali zaidi ili kujua sababu ya suala hilo. Hakika niliumia sana kuona hospitali hii inalazimisha ilipwe mamilioni ya fedha na NHIF katika utoaji wa huduma zake, bei ambazo hata katika Hospitali nyinginezo tena zilizo ngazi ya juu ya rufaa ya matibabu.
Katika uchunguzi wangu nilioufanya nimebaini madudu mengi ambayo Aga Khan inataka kuibebesha Serikali mzigo wa kuongeza gharama zaidi za huduma kwa wateja wa NHIF kuliko kiwango cha juu kabisa cha malipo kwa huduma.
Nitatoa mifano michache ya huduma za kawaida kabisa ambazo Aga Khan imekuwa ikidai kuongezewa gharama hizo kwenye huduma wanazotoa kwa wateja wa NHIF.
- Hospitali ya Aga Khan wanataka kutoza Shilingi 6,000,000/= kwa huduma za kujifungua kwa njia ya upasuaji wakati Hospitali nyingine zenye hadhi sawa ya rufaa ya Kanda wanatoza kiasi cha Shilingi 230,000/= huku bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ikijumlisha na huduma ziada hutoza kiasi cha Shilingi 600,000/=. Aga Khan wanataka kulipwa maradufu kwa asilimia 100 zaidi kuliko Hospitali nyingine.
- Huduma ya kulaza wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Aga Khan wanataka kulipwa kiasi cha Shilingi 2,278,933, huduma hii kwenye Hospitali nyingine huwa ni kiasi cha shilingi 500,000/= na Shilingi 700,000/= ambayo ni bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ukijumuisha na huduma za ziada.
- Aga Khan wanataka kutoza kiasi cha Shilingi 334,546 kwa huduma za uchunguzi kwa kupitia CT-Scan huku Hospitali nyingine zinatoza 120,000 hadi 150,000 ikiwa ni bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ukijumuisha na huduma za ziada. Kwanini bei iwe juu hivi? CT-Scan hizi hizi ambazo tumeona Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan amezinunua na sasa huduma zinapatikana nchi nzima kwenye Hospitali zote za Rufaa za Mikoa na nyinginezo ngazi za juu. Najiuliza Gharama zote hizo zinakuja kwa msingi upi?
Ifahamike kuwa Aga Khan sio Hospitali ngazi ya Taifa hivyo bado rufaa zao zote wanalazimika kuzipeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili, hata kama ni Hospitali Binafsi ukiweka gharama za juu pamoja na huduma za ziada hawapaswi kuwa na tofauti kubwa ambayo inatishia uhai wa Mfuko.
Kama Taifa ifike mahali tutafakari endapo Aga Khan wana nia kweli ya kutoa huduma za matibabu au la? Je ni wananchi wangapi wataweza kupata huduma kwa gharama hizi katika hospitali hii? Au wamelenga tabaka gani la kulitibia?
Hata hivyo niipongeze sana Serikali kwa hatua kubwa ya kuboresha huduma za matibabu nchini huduma ambazo awali yawezekana zilipatikana nje ya nchi lakini sasa zinapatikana katika hospitali zetu za umma. Kwa hili kongole kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Viongozi wa na Watendaji wa Wizara ya Afya wakiongozwa na Waziri jembe kabisa Mhe. Ummy Mwalimu.
Ninaamini kwamba katika utoaji wa huduma za matibabu, utu hupaswa kuwa kipaumbele cha kwanza na kuweka maslahi mapana ya kuokoa maisha ya binadamu.
Kwa leo niwaache na tafakari hii ya gharama kubwa zisizo na uzalendo za Aga Khan.