Ahmed Rajab akosoa historia ilivyoandikwa na Dr.Ghassany!!

Ahmed Rajab akosoa historia ilivyoandikwa na Dr.Ghassany!!

JokaKuu

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2006
Posts
34,188
Reaction score
62,952
..hii ni introduction ya makala ya Ahmed Rajab ktk gazeti la Raia Mwema.

..It is an interesting reading, mnaweza kuifuatilia ktk link niliyotoa hapo chini.

TANBIHI YA MKUTANO WANGU NA HANGA-- Ahmed Rajab

KUMBUKUMBU na usahaulifu. Kalima hizo mbili zina umuhimu mkubwa katika fani ya uandishi wa historia. Katika fani hiyo, "kumbukumbu" na "usahaulifu" huwa na siasa zake na nguvu za aina yake. Uandishi wa historia una miiko na maadili yake. Ni mwiko kwa wanahistoria pamoja na waandishi wa mambo ya kihistoria kupotosha historia kwa kutoa maelezo kinyume na matukio halisi yalivyotukia. Na huo ni mwiko mkubwa. Miongoni mwa maadili ya uandishi wa historia ni kwanza, kuyafatiisha mambo na kuyachunguza kwa kina; na pili, kutoa maelezo yaliyo sahihi bila ya upendeleo. Hii si kazi nyepesi hasa kwa wale wenye misimamo ya kisiasa. Kwa hakika, hiyo si kazi nyepesi hata kwa wasio na misimamo ya kisiasa kwa sababu mara nyingine kutokuwa na msimamo wa kisiasa kwenyewe ni sawa na kuwa na msimamo wa kisiasa. Uandishi wa historia unazidi kutatanisha pale mwandishi anayeandika kuhusu matukio ya kihistoria anapowategemea wasimulizi wenye hakika kwamba ni wao tu wenye ukweli. Wasimulizi hao hutegemea kumbukumbu zao bila ya kusaidiwa na ushahidi wa maandishi wenye kuthibitisha wanayoyakumbuka.

SOURCE :http://raiamwema.co.tz/tanbihi-ya-mkutano-wangu-na-hanga#sthash.W4a4N8tY.dpuf

cc Mohamed Said, Ritz, Nguruvi3, Mag3, Barubaru, Mzee Mwanakijiji
 
Last edited by a moderator:
..hii ni introduction ya makala ya Ahmed Rajab ktk gazeti la Raia Mwema.

..It is an interesting reading, mnaweza kuifuatilia ktk link niliyotoa hapo chini.

TANBIHI YA MKUTANO WANGU NA HANGA-- Ahmed Rajab

KUMBUKUMBU na usahaulifu. Kalima hizo mbili zina umuhimu mkubwa katika fani ya uandishi wa historia. Katika fani hiyo, “kumbukumbu” na “usahaulifu” huwa na siasa zake na nguvu za aina yake. Uandishi wa historia una miiko na maadili yake. Ni mwiko kwa wanahistoria pamoja na waandishi wa mambo ya kihistoria kupotosha historia kwa kutoa maelezo kinyume na matukio halisi yalivyotukia. Na huo ni mwiko mkubwa. Miongoni mwa maadili ya uandishi wa historia ni kwanza, kuyafatiisha mambo na kuyachunguza kwa kina; na pili, kutoa maelezo yaliyo sahihi bila ya upendeleo. Hii si kazi nyepesi hasa kwa wale wenye misimamo ya kisiasa. Kwa hakika, hiyo si kazi nyepesi hata kwa wasio na misimamo ya kisiasa kwa sababu mara nyingine kutokuwa na msimamo wa kisiasa kwenyewe ni sawa na kuwa na msimamo wa kisiasa. Uandishi wa historia unazidi kutatanisha pale mwandishi anayeandika kuhusu matukio ya kihistoria anapowategemea wasimulizi wenye hakika kwamba ni wao tu wenye ukweli. Wasimulizi hao hutegemea kumbukumbu zao bila ya kusaidiwa na ushahidi wa maandishi wenye kuthibitisha wanayoyakumbuka.

SOURCE :Raia Mwema - Tanbihi ya mkutano wangu na Hanga

cc Mohamed Said, Ritz, Nguruvi3, Mag3, Barubaru, Mzee Mwanakijiji
JokaKuu , unakumbuka niliwahi kumuuliza Mohamed Said kama Mapinduzi ya Zanzibar ni halali au ni haramu. Hakuwahi kuwa na jibu.

Nilimuuliza kwasababu yeye anasema mapinduzi ni kazi ya Nyerere na ilifanywa na wamakonde wa Kipumbwi.
Ndipo nilipomuuliza, hivi kila January 12 wznz wanasherehekea mapinduzi, je ni mazezeta wasiojua ukweli wa mapinduzi?
Hakuwa na jibu

Katika wiki hiyo hiyo, Ahmed Rajab akaandika Raia mwema kuwa 'inatagemea mtu alikuwa upande gani'' akimaanisha kwa Waarabu, waburushi na Wamanaga mhhhh iiii, kwa weusi yalikuwa mwa!

Ukimsoma Ghesany sehemu kubwa sana anaonyesha Zanzibar ilikuwa nzuri sana kabla ya mapinduzi akitumia neno Uhuru kurudi miaka ya nyuma. Yaani znz ilikuwa nzuri kuanzia ilipopata uhuru na kurudi nyuma na si mapinduzi

Ghesany na Mohamed Said wameshirikiana kuandika kitabu. Hivyo ni sahihi kusema Mohamed na Ghesany hawayakubali mapinduzi. Swali linabaki, je ni halali au si harami? Hana jibu la moja kwa moja, Ahmed anasema inategemea upande, naye akiegesha jibu lake

Ukisoma kipande hicho, Ahmed anamtupia Mohamed dongo la usoni, pwaa!

Ndio maana tunasema historia hizi tunazoambiwa za ukweli zina walakini sana. Mtu anategemea kusikia kwa baba yake na kuuchukulia kauli hizo ni facts bila kujua baba yake naye ni mwanadamu
 
JokaKuu , unakumbuka niliwahi kumuuliza Mohamed Said kama Mapinduzi ya Zanzibar ni halali au ni haramu. Hakuwahi kuwa na jibu.<br>
<br>
Nilimuuliza kwasababu yeye anasema mapinduzi ni kazi ya Nyerere na ilifanywa na wamakonde wa Kipumbwi. <br>
Ndipo nilipomuuliza, hivi kila January 12 wznz wanasherehekea mapinduzi, je ni mazezeta wasiojua ukweli wa mapinduzi?<br>
Hakuwa na jibu<br>
<br>
Katika wiki hiyo hiyo, Ahmed Rajab akaandika Raia mwema kuwa 'inatagemea mtu alikuwa upande gani'' akimaanisha kwa Waarabu, waburushi na Wamanaga mhhhh iiii, kwa weusi yalikuwa mwa!<br>
<br>
Ukimsoma Ghesany sehemu kubwa sana anaonyesha Zanzibar ilikuwa nzuri sana kabla ya mapinduzi akitumia neno Uhuru kurudi miaka ya nyuma. Yaani znz ilikuwa nzuri kuanzia ilipopata uhuru na kurudi nyuma na si mapinduzi<br>
<br>
Ghesany na Mohamed Said wameshirikiana kuandika kitabu. Hivyo ni sahihi kusema Mohamed na Ghesany hawayakubali mapinduzi. Swali linabaki, je ni halali au si harami? Hana jibu la moja kwa moja, Ahmed anasema inategemea upande, naye akiegesha jibu lake<br>
<br>
Ukisoma kipande hicho, Ahmed anamtupia Mohamed dongo la usoni, pwaa!<br>
<br>
Ndio maana tunasema historia hizi tunazoambiwa za ukweli zina walakini sana. Mtu anategemea kusikia kwa baba yake na kuuchukulia kauli hizo ni facts bila kujua baba yake naye ni mwanadamu
<br>
<br>
<strong>Nguruvi3,</strong><br>
Kuwa mimi sikuwa na jibu sikumbuki lini nimekuwa sina jibu lakini hiki si muhimu.<br>
Jina linaandikwa, <strong>"Ghassany,"</strong> siyo <strong>"Ghesany."</strong><br>
<br>
Unapoandika kwa staili hii masomaji yoyote atakutoa maanani kwa kukuona si mtu<br>
makini.<br>
<br>
<strong>Ahmed Rajab</strong> anitupie mimi dongo kwa lipi ilhali mimi si mwandishi wa kitabu<br>
hiki kilicho hapa jamvini?<br>
<br>
Hapa napo umekosa tena umakini.<br>
<strong>Ahmed Rajab </strong>anamjibu <strong>Dr. Ghassany</strong> si mie.<br>
<br>
Soma jibu la <strong>Dr. Ghassany</strong> kwa <strong>Ahmed Rajab</strong>:<br>
<a href="http://www.mohammedsaid.com/2015/06/dr-harith-ghassany-aeleza-usahihi-wa.html" target="_blank">Mohamed Said: DR. HARITH GHASSANY AELEZA USAHIHI WA UTAFITI WA KITABU CHAKE: "KWAHERI UKOLONI KWAHERI UHURU"</a><br>
<br>
Ukimaliza kusoma In Sha Allah rejea tena hapa<strong> Majlis</strong> tujadili.<br><br><strong>Nguruvi3,</strong><br>Niangalia hapa niko ofisini kwa <strong>Ahmed Rajab </strong>London na katika moja ya "past time zetu"<br>ilikuwa kuzungumza historia ya Zanzibar na marehemu <strong>Abdulrahman Babu </strong>akiwepo.<br><br>Nitazame vyema hapo nilikuwa kijana mdogo na miaka mingi sasa imepita.<br>Najua mengi katika historia ya Zanzibar kutoka ndimi za Wazanzibari wenyewe:<br><br><img src="https://lh6.googleusercontent.com/-VyAChOqKoFA/VXcwdyaOr2I/AAAAAAAAaKM/LQE-U7Tpejs/w406-h541-no/20150530_010608%2B%25281%2529.jpg"><br><br>
 
<br>
<br>
<strong>Nguruvi3,</strong><br>
Kuwa mimi sikuwa na jibu sikumbuki lini nimekuwa sina jibu lakini hiki si muhimu.<br>
Jina linaandikwa, <strong>"Ghassany,"</strong> siyo <strong>"Ghesany."</strong><br>
<br>
Unapoandika kwa staili hii masomaji yoyote atakutoa maanani kwa kukuona si mtu<br>
makini.<br>
<br>
<strong>Ahmed Rajab</strong> anitupie mimi dongo kwa lipi ilhali mimi si mwandishi wa kitabu<br>
hiki kilicho hapa jamvini?<br>
<br>
Hapa napo umekosa tena umakini.<br>
<strong>Ahmed Rajab </strong>anamjibu <strong>Dr. Ghassany</strong> si mie.<br>
<br>
Soma jibu la <strong>Dr. Ghassany</strong> kwa <strong>Ahmed Rajab</strong>:<br>
<a onclick="_gaq.push(['_trackEvent', 'Outgoing', 'www.mohammedsaid.com', '/2015/06/dr-harith-ghassany-aeleza-usahihi-wa.html']);" rel="nofollow" href="http://www.mohammedsaid.com/2015/06/dr-harith-ghassany-aeleza-usahihi-wa.html" target="_blank">Mohamed Said: DR. HARITH GHASSANY AELEZA USAHIHI WA UTAFITI WA KITABU CHAKE: "KWAHERI UKOLONI KWAHERI UHURU"</a><br>
<br>
Ukimaliza kusoma In Sha Allah rejea tena hapa<strong> Majlis</strong> tujadili.<br><br><strong>Nguruvi3,</strong><br>Niangalia hapa niko ofisini kwa <strong>Ahmed Rajab </strong>London na katika moja ya "past time zetu"<br>ilikuwa kuzungumza historia ya Zanzibar na marehemu <strong>Abdulrahman Babu </strong>akiwepo.<br><br>Nitazame vyema hapo nilikuwa kijana mdogo na miaka mingi sasa imepita.<br>Najua mengi katika historia ya Zanzibar kutoka ndimi za Wazanzibari wenyewe:<br><br><img src="https://lh6.googleusercontent.com/-VyAChOqKoFA/VXcwdyaOr2I/AAAAAAAAaKM/LQE-U7Tpejs/w406-h541-no/20150530_010608%2B%25281%2529.jpg"><br><br>

Ndugu zangu Wanamajlis,
Imekuwaje bandiko langu limechafuliwa?

Picha hiyo hapo chini nimemuwekea Nguruvi3 ili tufahamiane vizuri na nikaweka
na maelezo kuwa niko na Ahmed Rajab London miaka mingi sana iliyopita nikiwa
mtoto na tukizungumza mengi katika historia ya Zanzibar mbele ya marehemu
Abdulrahman Babu.

Nimejifunza mengi sana kutoka kwa Ahmed Rajab na naweza kusema ni yeye
ndiye aliyenitia katika dunia hii ya uandishi.

20150530_010608%2B%25281%2529.jpg
 
Migogoro kuhusu ukweli wa historia ya Zanzibar inatokana na uhusika wa Nyerere ambaye alikuwa mkristo. Wakati Mtume Muhammad anaazisha uislamu, Harith Gassani alikuwa mkristo na mfalme wa Damascus; wala hakuwa na chuki dhidi ya dini ya uislamu japo yeye mwenyewe alienedelea kuwa mkirsto.
 
Ndugu zangu Wanamajlis,
Imekuwaje bandiko langu limechafuliwa?

Picha hiyo hapo chini nimemuwekea Nguruvi3 ili tufahamiane vizuri na nikaweka
na maelezo kuwa niko na Ahmed Rajab London miaka mingi sana iliyopita nikiwa
mtoto na tukizungumza mengi katika historia ya Zanzibar mbele ya marehemu
Abdulrahman Babu.

Nimejifunza mengi sana kutoka kwa Ahmed Rajab na naweza kusema ni yeye
ndiye aliyenitia katika dunia hii ya uandishi.


20150530_010608%2B%25281%2529.jpg
Nguruvi3,
Kuwa mimi sikuwa na jibu sikumbuki lini nimekuwa sina jibu lakini hiki si muhimu.
Jina linaandikwa, "Ghassany," siyo "Ghesany."

Unapoandika kwa staili hii masomaji yoyote atakutoa maanani kwa kukuona si mtu
makini.

Ahmed Rajab anitupie mimi dongo kwa lipi ilhali mimi si mwandishi wa kitabu
hiki kilicho hapa jamvini?

Hapa napo umekosa tena umakini.
Ahmed Rajab anamjibu Dr. Ghassany si mie.

Soma jibu la Dr. Ghassany kwa Ahmed Rajab:
Mohamed Said: DR. HARITH GHASSANY AELEZA USAHIHI WA UTAFITI WA KITABU CHAKE: "KWAHERI UKOLONI KWAHERI UHURU"

Ukimaliza kusoma In Sha Allah rejea tena hapa Majlis tujadili.

Nguruvi3,
Niangalia hapa niko ofisini kwa Ahmed Rajab London na katika moja ya "past time zetu"
ilikuwa kuzungumza historia ya Zanzibar na marehemu Abdulrahman Babu akiwepo.

Nitazame vyema hapo nilikuwa kijana mdogo na miaka mingi sasa imepita.
Najua mengi katika historia ya Zanzibar kutoka ndimi za Wazanzibari wenyewe:

20150530_010608%2B%25281%2529.jpg
Mohamed Said, kwanza nimuombe radhi huyo Ghassany kwa kulikoseoa jina lake, huo ndio uungwana wala haondoi weledi na umakini wa mtu. Waungwana huwa hatukimbilii dharau, kejeli na matusi! tumefunzwa adabu za kuongea na jamii.

Wapo wanaoandika Mohamed, Mohamad, Mohammad n.k.

Kauli zako za tafstiti zinaonyesha umejawa na ghadhabu, tuliza moyo, adabu za mnakasha hazitaki taharuki

Hoja zote niziloweka hapo juu hujajibu hata moja, ulichojibu ni kusahihisha jina, wasomaji hawana interest na jina, wanachotaka kusikia ni hiki

1. Kwavile unadai mapinduzi yamefanywa na Nyerere kwa kutumia wamakonde wa Kipumbwi
a)Mapinduzi ya znz ni halali au ni haramu
b) Je, wazanzibar wanafanya makosa kusherehekea Jan 12
c) Nini mchango wa wznz katika mapinduzi yale ya 1964 na wale waliokufa, je, wamekufa kishujaa au kama vibaraka?
d) Ahmed, anaposema mapinduzi yanategeme mtu alikuwa upande, mwandishi Mohamed unatufafanuliaje

Tuendelee sheikh
 
Mohamed Said, kwanza nimuombe radhi huyo Ghassany kwa kulikoseoa jina lake, huo ndio uungwana wala haondoi weledi na umakini wa mtu. Waungwana huwa hatukimbilii dharau, kejeli na matusi! tumefunzwa adabu za kuongea na jamii.

Wapo wanaoandika Mohamed, Mohamad, Mohammad n.k.

Kauli zako za tafstiti zinaonyesha umejawa na ghadhabu, tuliza moyo, adabu za mnakasha hazitaki taharuki

Hoja zote niziloweka hapo juu hujajibu hata moja, ulichojibu ni kusahihisha jina, wasomaji hawana interest na jina, wanachotaka kusikia ni hiki

1. Kwavile unadai mapinduzi yamefanywa na Nyerere kwa kutumia wamakonde wa Kipumbwi
a)Mapinduzi ya znz ni halali au ni haramu
b) Je, wazanzibar wanafanya makosa kusherehekea Jan 12
c) Nini mchango wa wznz katika mapinduzi yale ya 1964 na wale waliokufa, je, wamekufa kishujaa au kama vibaraka?
d) Ahmed, anaposema mapinduzi yanategeme mtu alikuwa upande, mwandishi Mohamed unatufafanuliaje

Tuendelee sheikh

Nguruvi3,
Umebadilika sana ndugu yangu.
Si Nguruvi3 yule niliyemzoea.

Mimi si niliyedai kuwa kuna jeshi lilitoka Kipumbwi.

Walosema hayo ni Victor Mkello na Mohamed Omari Mkwawa na wakataja
wahusika walikuwa Ali Mwinyi Tambwe na Jumanne Abdallah.

Hayo mengine wakujibu si mie atajibu mwandishi wa kitabu, "Kwaheri Ukoloni
Kwaheri Uhuru" Dr. Ghassany ikiwa ataona iko haja ya kufanya hivyo.

Mwisho nitakudokeza kitu.

Kuna taarifa mpya ya "mole" aliyekuwa ndani ya TAA hadi TANU na alihusika
sana na kambi ya Kipumbwi.
 
Nguruvi3,
Umebadilika sana ndugu yangu.
Si Nguruvi3 yule niliyemzoea.

Mimi si niliyedai kuwa kuna jeshi lilitoka Kipumbwi.

Walosema hayo ni Victor Mkello na Mohamed Omari Mkwawa na wakataja
wahusika walikuwa Ali Mwinyi Tambwe na Jumanne Abdallah.

Hayo mengine wakujibu si mie atajibu mwandishi wa kitabu, "Kwaheri Ukoloni
Kwaheri Uhuru" Dr. Ghassany ikiwa ataona iko haja ya kufanya hivyo.

Mwisho nitakudokeza kitu.

Kuna taarifa mpya ya "mole" aliyekuwa ndani ya TAA hadi TANU na alihusika
sana na kambi ya Kipumbwi.
Mohamed, sasa kama huna uhakika na habari unazoandika, unapata wapi nguvu za kusimamia hoja hiyo tena ukisema historia ya kweli

Ni mara ngapi katika mnkasha huu umetuwekea mabandiko ukiwanukuu watu waliohusika?

Leo unawezaje kutuambia hujui, ikiwa wewe ndiye unaeleza kuhusu Kipumbwi?

Ndio maana tunasema, kuna walakini, tena mkubwa. Leo Mohamed hawezi kusema mapinduzi ni halali au ni haramu. Kesho anatualmbia Nyerere mbaya sana, kaenda kuua watu Znz!

Mohamed, wapi unaposimama katika hili. Mapinduzi ni halali au ni haramu
Unawaeleza nini Wazanzibar, kwamba waendelee kuyaenzi au waachane na 'udhalimu' wa Nyerere?

Vijana wamechanganyikiwa, tuwekee sawa mzee wetu
 
Shekh unamakusudi sana, ni kweli unashindwa kujibu kwamba mapinduzi ni haramu na waznz wanakosea sana, na kuhusu nchango wa waznz ni mdogo sana ukilinganisha na wabara km kambona,okello,nyerere nk.

Pia kuhusu ahmed rajabu na ye aje na tafiti kutengua maandishi ya watu makini km Ghassany
 
Huwezi kusema mapinduzi halali wakati yaliegemea kwenye propaganda za kibaguzi km zile alizozieleza noor shariff katika" propaganda za udini tz"
 
Huwezi kusema mapinduzi halali wakati yaliegemea kwenye propaganda za kibaguzi km zile alizozieleza noor shariff katika" propaganda za udini tz"
Kama si halali, unasema ni haramu?
Mengine mwachie mhusika aliyeandika vitabu ajibu
 
Mohamed, sasa kama huna uhakika na habari unazoandika, unapata wapi nguvu za kusimamia hoja hiyo tena ukisema historia ya kweli

Ni mara ngapi katika mnkasha huu umetuwekea mabandiko ukiwanukuu watu waliohusika?

Leo unawezaje kutuambia hujui, ikiwa wewe ndiye unaeleza kuhusu Kipumbwi?

Ndio maana tunasema, kuna walakini, tena mkubwa. Leo Mohamed hawezi kusema mapinduzi ni halali au ni haramu. Kesho anatualmbia Nyerere mbaya sana, kaenda kuua watu Znz!

Mohamed, wapi unaposimama katika hili. Mapinduzi ni halali au ni haramu
Unawaeleza nini Wazanzibar, kwamba waendelee kuyaenzi au waachane na 'udhalimu' wa Nyerere?

Vijana wamechanganyikiwa, tuwekee sawa mzee wetu

Nguruvi 3,
Unataka mimi ndiye niseme kuwa mapinduzi ni haramu.
Haya nikishasema hilo ndiyo iwe nini?

Nani kakuambia kuwa mimi sina uhakika na niyasemayo?
Mimi nakupa habari ambazo hujapata kuzisikia popote duniani.

Nyie mlimjua Mzee Mkwawa Kamanda wa Jeshi la Kipumbwi?

Ali Mwinyi Tambwe, Jumanne Abdallah, Victor Mkello...watafiti
wameandika historia ya Mapinduzi ya Zanzibar lakini wahusika hawa
hawakuwako katika kurasa zao.

Ngoja nikuongeze kitu kingine usichojua.
Kuhusu mauaji...

Wazee wetu wengi walihusika katika namna moja au nyingine katika
yale mapinduzi lakini hii leo hakuna anaetaka jina lake lihusishwe na
mapinduzi kwa sababu ya yale mauaji yasiyokuwa ya lazima kamwe
yaliyotokea wakati serikali tayari ilikuwa imeshaanguka.

Unajua Abdul Sykes alimwambia nini Issa Nasser Al Ismaily
alipomuuliza kuhusu yaliyotokea Zanzibar?

Issa Nasser ndiye aliyeandika, "Kinyang'anyiro na Utumwa Zanzibar."
Ikiwa huyajui majibu ya Abdul Sykes nifahamishe nitakueleza.

Ali Mwinyi Tambwe kapewa medali ya mapinduzi katika kusheherekea
miaka 50 ya mapinduzi lakini alipokuwa hai hakutaka kabisa jina lake
lihusishwe na kadhia hiyo.

Sisi ni Waislam na tunajua dhima ya kutoa roho pasi na haki.
 
Sidhani anayemzungumza Ahmed Rajab, kama alimfahamu Ahmed Rajab kwenye gazeti Raia Mwema.

Ahmed Rajab, hakuingia ndani ya mapinduzi. Kwani hata hao akina Ahmed Rajab, vijana wa Umma Party ama umaaufu wao ma komredi, wao hawakuhusika na mapinduzi hayo. Ushiriki wao ni kama kudandia daladala. Lazima ukumbuke, wengi wao, walikuwa ni kutoka ZNP na walipata mafunzo ya kijeshi CUBA, Russia na sehemu nyengine kwa Msaada wa A. M. Babu na Ali Sultan Issa. Ali Sultan Issa, amebahatika kuandika kitabu, na anathibitisha hayo kuwa hawakuhusika na mipango hayo. Na wao komredi, mara nyingi, husema, kwamba wao, ndio waliosaidia KUEPUSHA MAUWAJI, kwani yulee mlaanifu wa OKELO, alifuutu ada, akawa na hamu yakuwamaliza waarabu wote na hata wanachama wa ZNP na ZPPP>

Kila mtu anajuwa, kwamba Okello, ndiye aliyekuwa jemedari wa Mapinduzi yale au sisi Wazanzibari husema machafuzi! Okello ni nani. Okello, ameingia Zanzibar mwishoni mwa miaka ya hamsini. Akafikia Pemba. Huko alipotoka, alikwisha pata usumbufu huko Kenya na kufungwa. Mzee wangu akimkumbuka vyema Okello, alipokuwa Chake Chake.Kwa vile alikuwa ni Mudir, ilikuwa rahisi kumtamua. Na alikuja kukumbana naye tena alipohamia Nungwi. Wakati washapinduwa, Aboud Jumbe, ambaye ni ASP, hata yeye naye hakuwa na taaifa ya mapinduzi hayo. Na walikuwa wanaulizana pale Rahaleo, huyu jamaa ni nani hasaaa. Ilikuwa ni kiasi yakumpa muda, na alipoanza kuanza kutoosha mali na kuzipeleka KWAO UGANDA, huo ndio ulikuwa mwanya wa kumdhibiti.

Tulikuwa tunafunzwa kuwa ati Karume ndiye aliyeongoza Mapinduzi. Lakini Maehemu Ali Nabwa, ambaye anayajuwa mengi ya Zanzibar, aliandika undani wa KARUME. Aliandika kwa uthibitisho wapi alikuwepo Karume siku ya Mapinduzi na sipengine bali huko kwa Mwalimu NYerere Dar.

Ukichukuwa meelezo ya wazanzibari wengi waliokuwa wakiishi mjini kwa wakati ule na wakijihusisha na siasa, basi ndipo unapopata kujuwa ni kweli haya hayakuwa mapinduzi. Ahmed ajab huyo huyo, anamzungumzia Kassim Hanga, alivyowaelezea kosa walilolifanya baada mapinduzi ikiwemo kuuuwa na ubaguzi. Anaelezea, vipi Kassim Hanga alivyoanza kuchukiwa kwa kuanza kuwapatia ajira wale wazanzibari waliokimbia mapinduzi yale au kukimbia mateso yale ya 1964 na kuhamia Dar na yeye kuanza kuwapa ajia. Anavyosema Hanga, kwake yeye, angi si kitu, yeye akiwachukilia ni wazanzibari tu.

Kassim Hanga, aliwaelezea akina Ahmed Rajab, ubaya wa ubaguzi walioufanya na kumuomba Mungu amsamehe kwa hilo. Mwishowe ulianza kuwala wenyewe kwa wenyewe...
 
Nguruvi 3,
Unataka mimi ndiye niseme kuwa mapinduzi ni haramu.
Haya nikishasema hilo ndiyo iwe nini?

Nani kakuambia kuwa mimi sina uhakika na niyasemayo?
Mimi nakupa habari ambazo hujapata kuzisikia popote duniani.

Nyie mlimjua Mzee Mkwawa Kamanda wa Jeshi la Kipumbwi?

Ali Mwinyi Tambwe, Jumanne Abdallah, Victor Mkello...watafiti
wameandika historia ya Mapinduzi ya Zanzibar lakini wahusika hawa
hawakuwako katika kurasa zao.

Ngoja nikuongeze kitu kingine usichojua.
Kuhusu mauaji...

Wazee wetu wengi walihusika katika namna moja au nyingine katika
yale mapinduzi lakini hii leo hakuna anaetaka jina lake lihusishwe na
mapinduzi kwa sababu ya yale mauaji yasiyokuwa ya lazima kamwe
yaliyotokea wakati serikali tayari ilikuwa imeshaanguka.

Unajua Abdul Sykes alimwambia nini Issa Nasser Al Ismaily
alipomuuliza kuhusu yaliyotokea Zanzibar?

Issa Nasser ndiye aliyeandika, "Kinyang'anyiro na Utumwa Zanzibar."
Ikiwa huyajui majibu ya Abdul Sykes nifahamishe nitakueleza.

Ali Mwinyi Tambwe kapewa medali ya mapinduzi katika kusheherekea
miaka 50 ya mapinduzi lakini alipokuwa hai hakutaka kabisa jina lake
lihusishwe na kadhia hiyo.

Sisi ni Waislam na tunajua dhima ya kutoa roho pasi na haki.
Mohamed
Thamani ya maandishi si wino au rangi, ni kile msomaji anachopata.

Hapa hatuulizi habari zingine, tuna mjadala unaotokana na maandishi yako.

Ahmed Rajabu anasema inategemea mtu alikuwa upande gani katika mapinduzi.


Tunakuuliza wewe uliyeandika mengi sana kuhusu &#8216;udhalimu' wa Nyerere.

Umetamka kwa ulimi , umeandika kwa kalamu yako. Tumekusoma sasa tunahitaji ufahamu si nyongeza ya majina ya watu


1 Mohamed, kwa mtazamo, maoni na ufahamu wako, mapinduzi ya Zanzibarni halali au ni haramu? Na kwa sababu zipi

2 Je, unawaambia nini wananchi wa Zanzibar, waendelee kuenzi au waachane na &#8216;upuuzi' alioupeleka Nyerere?

Kama mwandishi hawezi kusema kitu moja kwa moja na kwa jinsi kilivyohojiwa, maana yake haeleweki.

Asipoeleweka maana nzima ya ujumbe inapotea. Na wala mwandishi hapaswi kuogopa kuudhi au kuudhiwa, anapaswa kusimama na kutetea hoja zake bila ubabaishaji au kuumba umba.


Hoja ni hizo hapo juu(mbili tu)
 
Mohamed
Thamani ya maandishi si wino au rangi, ni kile msomaji anachopata.

Hapa hatuulizi habari zingine, tuna mjadala unaotokana na maandishi yako.

Ahmed Rajabu anasema inategemea mtu alikuwa upande gani katika mapinduzi.


Tunakuuliza wewe uliyeandika mengi sana kuhusu &#8216;udhalimu' wa Nyerere.

Umetamka kwa ulimi , umeandika kwa kalamu yako. Tumekusoma sasa tunahitaji ufahamu si nyongeza ya majina ya watu


1 Mohamed, kwa mtazamo, maoni na ufahamu wako, mapinduzi ya Zanzibarni halali au ni haramu? Na kwa sababu zipi

2 Je, unawaambia nini wananchi wa Zanzibar, waendelee kuenzi au waachane na &#8216;upuuzi' alioupeleka Nyerere?

Kama mwandishi hawezi kusema kitu moja kwa moja na kwa jinsi kilivyohojiwa, maana yake haeleweki.

Asipoeleweka maana nzima ya ujumbe inapotea. Na wala mwandishi hapaswi kuogopa kuudhi au kuudhiwa, anapaswa kusimama na kutetea hoja zake bila ubabaishaji au kuumba umba.


Hoja ni hizo hapo juu(mbili tu)

Nguruvi3,
Hebu rejea kwenye makala ya Ahmed Rajab uisome upya.

Ahmed Rajab hayuko katika mjadala ni mimi yeye yuko katika mjadala na
Dr. Ghassany mwandishi wa kitabu cha Mapinduzi ya Zanzibar.

Nyongeza ya majina nakuwekea kama nilivyokuwekea picha kukuelekeza
tufahamiane vyema.

Ungekuwa makini angalau ungetaka kujua nani huyu, "mole," aliyetiwa
na Waingereza toka enzi za TAA na akadumu hadi TANU.

Huyu kachero wa Special Branch kawaumiza kiasi gani viongozi hawa
wapigania uhuru?

Issa Nasser Ismaily na Abdul Sykes kipi kati yao katika mapinduzi?

Walaa...
Haya si muhimu kwako umekuwa kama sahani ya santuri iliyochimbika
na kila kichwa cha gramafoni kikifika hapo kinarudia na kinarudia na
kinarudia hapo hapo...haramu, haramu, haramu...

Mimi Alhamdulilah naeleweka sana.

Fasaha ya lugha haijapata kuwa tatizo kwangu.
Nimeandika "paper," na makala hata hesabu yake sizijui.

Baadhi zipo hapa Majlis na zimesomwa na wengi.
Kitabu cha historia ya TANU ndiyo hiki kila leo tuko nacho Majlis.

"Udhalimu," wa Nyerere, "upuuzi," wa Nyerere wapi nimeandika maneno
hayo?

Unaweza kuleta ushahidi kuwa nimeandika maneno hayo?

Sasa nakurudisha katika Mapinduzi ya Zanzibar.
Unataka mimi nikuambie kama ni haramu...

Halafu nikishakuambia ndiyo iwe nini?
 
Nguruvi3,
Hebu rejea kwenye makala ya Ahmed Rajab uisome upya.

Ahmed Rajab hayuko katika mjadala ni mimi yeye yuko katika mjadala na
Dr. Ghassany mwandishi wa kitabu cha Mapinduzi ya Zanzibar.

Nyongeza ya majina nakuwekea kama nilivyokuwekea picha kukuelekeza
tufahamiane vyema.

Ungekuwa makini angalau ungetaka kujua nani huyu, "mole," aliyetiwa
na Waingereza toka enzi za TAA na akadumu hadi TANU.

Huyu kachero wa Special Branch kawaumiza kiasi gani viongozi hawa
wapigania uhuru?

Issa Nasser Ismaily na Abdul Sykes kipi kati yao katika mapinduzi?

Walaa...
Haya si muhimu kwako umekuwa kama sahani ya santuri iliyochimbika
na kila kichwa cha gramafoni kikifika hapo kinarudia na kinarudia na
kinarudia hapo hapo...haramu, haramu, haramu...

Mimi Alhamdulilah naeleweka sana.

Fasaha ya lugha haijapata kuwa tatizo kwangu.
Nimeandika "paper," na makala hata hesabu yake sizijui.

Baadhi zipo hapa Majlis na zimesomwa na wengi.
Kitabu cha historia ya TANU ndiyo hiki kila leo tuko nacho Majlis.

"Udhalimu," wa Nyerere, "upuuzi," wa Nyerere wapi nimeandika maneno
hayo?

Unaweza kuleta ushahidi kuwa nimeandika maneno hayo?

Sasa nakurudisha katika Mapinduzi ya Zanzibar.
Unataka mimi nikuambie kama ni haramu...

Halafu nikishakuambia ndiyo iwe nini?
Ungekuwa makini ungetambua maana ya alama hizi '' '' katika maandishi.
Usingeniuliza ushahidi wa wapi umesema. Ni alama za kawaida sana kwa waandishi makini

Mimi sihitaji kujua hao wazee, natumia akili yangu kutafakari na kujiuliza.
Si mtu wa kukaa na kumeza tu, au kusema hewala bwana. Ukiona mtu anasema hivyo, ujue kuna tatizo.

Mohamed, tatizo linalokukabili na sijui kama unalijua ni kushindwa kujibu maswali. Umeulizwa kitu unaleta hadithi za akina Mole.

Maandishi yako leo unashindwa kuyatetea

Waandishi na watu wanaokuhoji huwa najiuliza sana kama kweli wanasoma maandishi yako na kuyaelewa

Unataka tuisukume santuri iende mbele tu, wakati kuna nyimbo zako hatujui maana yake.

Moja ni hii ya kumzungumza sana Nyerere na mapinduzii, kipumbwi n.k.
leo huwezi kusimama ma kusema kwa mtazamo wako Mapinduzi ya Zanzibar yanasimama wapi.

Kwa mintaarafu hiyo, ni dhambi kumsema Nyerere.

Mohamed, unajua maana ya neno fitna! Fitna imezungumzwa sana katika vitabu vya dini.
 
Ungekuwa makini ungetambua maana ya alama hizi '' '' katika maandishi.
Usingeniuliza ushahidi wa wapi umesema. Ni alama za kawaida sana kwa waandishi makini

Mimi sihitaji kujua hao wazee, natumia akili yangu kutafakari na kujiuliza.
Si mtu wa kukaa na kumeza tu, au kusema hewala bwana. Ukiona mtu anasema hivyo, ujue kuna tatizo.

Mohamed, tatizo linalokukabili na sijui kama unalijua ni kushindwa kujibu maswali. Umeulizwa kitu unaleta hadithi za akina Mole.

Maandishi yako leo unashindwa kuyatetea

Waandishi na watu wanaokuhoji huwa najiuliza sana kama kweli wanasoma maandishi yako na kuyaelewa

Unataka tuisukume santuri iende mbele tu, wakati kuna nyimbo zako hatujui maana yake.

Moja ni hii ya kumzungumza sana Nyerere na mapinduzii, kipumbwi n.k.
leo huwezi kusimama ma kusema kwa mtazamo wako Mapinduzi ya Zanzibar yanasimama wapi.

Kwa mintaarafu hiyo, ni dhambi kumsema Nyerere.

Mohamed, unajua maana ya neno fitna! Fitna imezungumzwa sana katika vitabu vya dini.

Nguruvi,
Naijua "fitna."

Na katika kitabu cha Abdul Sykes nimeieleza fitna hiyo.
Ikiwa umekisoma kitabu umeiona hiyo fitna iliyopitika hata ikawa jina la
Abdul likafutwa katika historia ya TANU.

Naijua fitna vizuri sana.

Nakueleza tena.

Mjadala ni kati ya Ahmed Rajab na Dr. Ghassany kuhusu Mapinduzi ya
Zanzibar.

Sijapatapo kushindwa kujibu swali lako lolote na ndiyo maana kila ukiandika na
mimi nakupa jibu bahati mbaya majibu yangu huyapendi.

Ikiwa wewe huelewi mziki wangu kuna wengi wanaupata vizuri sana.
Sasa wa kulaumiwa ni nani.

Mpiga ala au msikilizaji?
Umemleta tena Nyerere bila ya ushahidi.
 
Back
Top Bottom