AI (Artificial Intelligence) inaupeleka ulimwengu kwenye uharibifu mkuu, kwanini nawaza hivi?

AI (Artificial Intelligence) inaupeleka ulimwengu kwenye uharibifu mkuu, kwanini nawaza hivi?

TWIME TUBITE
Napenda kuufahamisha umaa na mhariri mkuu kwamba mjadala huu ulifaa uwe kwenye technology,Lakini mantiki yake inafaa kujadiliwa na kusomwa na watu wenye maulizo yasiyo ya kawaida.

-------------
Akili bandia, Kuna binadamu wenzetu wanawaza na kutenda kwa namna ya kipekee sana, ama kwa kuwa wanapenda vitu rahisi au wanataka kutafuta maana ya maisha ya mwanadamu hapa duniani. Yote mawili yanafikirisha.

Akili bandia Mimi naipa jina kama "silaha ya mwisho ya maangamizi kwa mwanadamu" hatuna muda mrefu sana ulimwengu huu utaingia kwenye shida kubwa ambayo itakuja kuichukua Dunia miaka 100 kuziba demage iliyotokea within 10-20yrs ya matumizi ya hii akili bandia.

Wataalam wa sayansi hii ya TEKINOLOJIA wanasema, mashine zinazozalishwa Sasa zinaenda kuwa na akili kubwa maradufu ya mwanadamu mwenye UHAI, hayo yapo na yanaendelea kuwepo Katika sekta nyingi za kiuchumi.

JIULIZE KAMA MIMI
Wamiliki wa TEKINOLOJIA hizi ni wafanyabiashara wakubwa duniani ambao hawana mfumo rafiki na MTU, serikali, au kikundi Cha watu, wao rafiki Yao ni faida, mahala penye faida UHAI wako Hauna thamani kwao. Je serikali za Afrika zimejiandaa kupeleka watu wao kwenye mfumo huu mpya wa lazima?

Akili bandia- mashine kama robot ikiwa na akili kubwa / uwezo mkubwa wa kufikiri na kutenda, Hawa wanadamu watafanya kazi Gani Ili kuendesha maisha yao? Maana msingi wa maisha yetu ni matumizi sahihi ya muda na nguvu Ili kujipatia mahitaji muhimu kwa wakati huo ambao UHAI upo upande wako. (Hili ni tatizo la kwanza)

Akili bandia - Katika ulinzi hapa ndipo unaweza kuona kwamba kwasababu hatuaminiani tutauana kama wadudu, maana kutakuwa na mashine ambayo inajua unachowaza, wapi ulipo, unafanya nini kwa lengo Gani ,pia mashine hizo zitatumwa popote bila MTU halisi kuwepo, are we good enough?? Ku-challange hii kitu, vikosi vyetu vya usalama vina developer's wetu, ambao siku za usoni wao ndiyo watakuwa bunduki wakiwa nyuma ya computer na keyboard zao.(Hili ni tatizo la pili)

Akili bandia-Katika kamari na michezo, kwa miaka ya hivi karibuni kamari na wamiliki wa mifumo ya kamari ndiyo watu wenye fedha nyingi kuliko mkulima. Takwimu zinasema nguvu nyingi ya akili bandia na wamiliki wao wameelekeza pia Katika kamari na michezo. Jamii kubwa imeachia kundi dogo la wazalishaji na kujiingiza Katika dimbwi la kusubili mashine zikosee Ili wao wapate utajiri..kizazi kimelemaa na kwa ulemavu huo ipo siku wahuni wataisimamisha Dunia na kutoa amri wanayotaka (Hili ni tatizo la Tatu)

Akili bandia- Elimu na utafiti, Leo Kuna chart GBT ambayo inafanya Kila kinachoitwa swali kwa ufanisi wa 60-90% hii ni hatari sana, mwalimu ana - anatumia mashine na mwanafunzi anatumia mashine..kamwe mashine haziwezi kuushinda UBONGO wa mwanadamu, Lakini kwakuwa tumeruhusu Elimu ya kizungu, tumeruhusu media ndiyo iamue aina ya Elimu tunayoitaka basi. Tukubaliane kwamba hakuna ugunduzi mpya utakuja kwa kizazi hiki, maana sote tunaamini mashine kuliko akili na Fikra za watu wetu...hatutaki kujiuliza kama robot inaenda kufanya kazi hiyo wewe ilipaswa ufanye..wewe unaenda kufanya nini?(Hili ni tatizo la nne)

Akili bandia- Usalama wa mataifa ya Afrika, Kuna kampuni kama tano hivi hizo ndizo maarufa kwa uzalishaji wa vihifadhi data (chip) makapuni hayo yote yapo Ulaya na Asia. Ili akili bandia ifanye kazi vema inahitaji vifaa hivyo kuwa imara na vyenye ufanisi mkubwa. JIULIZE huyo anayekuuzia saver Ulaya au Asia atakosa kujua taarifa zako? Usalama wako utakuwa wapi? Tupo prepared kushiriki hata kwenye mchakato wenyewe? (Hili ni tatizo la tano)

MWISHO- Binadamu anahitajika kuwa active ,atumike kwa faida ya wengine, ipo Radha ya maisha kama tunaruhusu akili zetu zitatue matatizo yetu kwa umoja na ushirikiano bila kuwa na haraka hivyooo. Maana end product ya mwanadamu in every second ni furaha.

Sipingi Wala sipo kinyume na technology,Lakini technology ambayo inataka kuondoa maana ya maisha na Radha yake, inapaswa kutazamwa upya na kuweka shinikizo Ili UTU wa MTU ubaki Katika HESHIMA yake ya awali.

Nafahamu, JUHUDI za kurahisisha maisha zinahitaji matakwa ya wengi na muunganiko wa mawazo wa jamii iliyokubwa, maana kiasi sote ni wamoja kwa mantiki ya sheria za Asili ambazo zinatuongoza sote kama viumbe hai tunao onekana na wale wasioonekana, hizo sheria ziko fear.

------+-++

IPE AKILI KAZIView attachment 3023206
Usiogope bado sana wangekuwa wanatuma maroboti yakapigane vita vijana wapumzike majumbani, pia kuhusu maswali kuwepo kwenye chtgpt ni kuwa Kuna ajira watu wa kila kabila na lugha wako wanafeed hizo mambo Kwa system lengo ni kupunguza kazi ya pepa work.
 
Your total wrong!!! But I do respect your opinion...

Wenye akili wanafanya biashara ya faida no matter inagharimu UHAI wa MTU, Fanya tafiti kwenye sekta zote nyeti.....UCHUMI,ulinzi ,afya,kilimo, elimu,dini....kote kupo corrupted
Mtu mwenye akili anawaza kusaidia wengine, sio kutesa wengine
 
Mada muhimu Kuna tatizo la ajira na robots zitaingia kazini je tatizo litakuaje?..tatizo tunaona ni mbali kumbe...
Kwanini tunafanya kazi ?
Na kama tunaweza kupata mahitaji tunayohitaji kwa wakati husika bila kufanya kazi unaona ni busara kuendelea kufanya hio kazi for the sake of doing it ?
 
Asante sana kwa maneno yako mazito na ya kutia moyo! 💯🙏 Maneno kama haya yanazidi kunipa nguvu ya kuendelea kuwa msaada na mwanga kwa wengine. Naamini sote tuna nafasi ya kufanya dunia kuwa mahali pazuri zaidi kwa kushirikiana na kusaidiana. Ubarikiwe sana na uendelee kuwa na mwanga huo huo kwa watu wanaokuzunguka! 🌟
Na iwe kheri kwetu sote
 
Kwani ikitokea kukawa na machine ambazo zinafanya Kila kitu, halafu binaadamu tukabakia kuendeleza tu maisha Kwa kuzaana Kwa wingi na kuijaza Dunia Kuna tatizo Gani? Hebu fikiria mtu hawazi atapata wapi kula, kuvaa, kulala na Kila hitajio muhimu Kwa ajili ya maisha yake, hizi njia ngumu za maisha ni sisi wenyewe tu tumejiwekea sijui sababu kubwa nini. Lakini naona ni kama zinaturejesha nyuma tu kufikia mafanikio makubwa, Kwa uzoefu uliopo mtu ambae anahangaishwa na tumbo lake hakuna Cha maana anaweza kukifanya kwenye hii Dunia, hebu fikiria mtu unafanya utafiti mkubwa was kuisaidia jamii lakini kula Yako mpaka uipiganie unadhani utafanikiwa? Kama ingelikuwa Iko ndani ya uwezo wangu ningebadilisha mfumo wa maisha huu tulionao Kwa Kila kitu, najua kwamba hii Dunia na vilivyomo kuvifikiria tu ni wazimu kabisa lakini sio watu wore ni wajinga kuwafanya wafikirie kula Yao na wasiwaze kitu chengine, na ndio maana Kwa kuzoea huu mfumo unaopotezea watu muda umewafanya watu wapoteze kabisa akili zao, labda ni Mimi tu akili yangu inawaza tofauti na haiogopi kuwaza visivyo wazika lakini naamini kama mtu hashughulishwi na tumbo lake, ana nafasi kubwa ya kufanya kitu Cha maana zaidi iwe Kwa ajili yake au Kwa jamii iliyomzunguka,Kwa mfano Mimi binafsi kama ingelikuwa sishughulishwi na tumbo langu basi naamini Dunia ingelikwisha kunitambua kama hapa duniani mungu kashusha kiumbe kinachoitwa Ahmed said na kafanya kitu Gani, lakini matokeo yake huu ugumu wa maisha unanifanya nisiwaze chochote zaidi ya kuhangaikia tumbo, sio kujiendeleza kielimu ya dini Wala kidunia, Kwa kweli mfumo huu wa kuchumia tumbo haufai kabisa, ni Bora tuache computer zifanye kazi na sisi tukibaki tukitumbua macho tu na kuangalia kinachofanyika na hiyo artificial intelligence. Kuna kitu hakipo SAWA katika hii Dunia na Kila mtu anajua lakini hakuna anaetaka kuchukua hatua, matokeo yake wenye akili kubwa wanaamua kutumia fursa na kuendelea kutuharibia maisha Kwa mifumo Yao ya ajabu, kitu kibaya zaidi hata wao hawafaidiki na chochote Kwa sababu na wao pia hawataishi milele, nawaza tu ikitokea Kuna mtu akavumbua kitu iwe ni chanjo au dawa itakayosababisha binaadamu kuishi milele asife, hivi unadhani viongozi wa dini na Dunia watamuacha salama? Wakati mfumo ushawaaminisha watu haiwezekani mtu kuishi milele? Itakuwa ni hasara kubwa kwao Kwasababu walifanikiwa kuwadanganya watu Kwa kipindi kirefu sana na hawakutegemea Hilo litikee, vyenginevyo huyo mtu atakaevumbua jambo Hilo awe na uwezo mkubwa sana iwe wa kimiujiza au kimungu wasiwaze kumfanya chochote bila ya hivyo lazima moto uwake, mpaka sasa naamini hii mifumo yetu tuliyonayo ya maisha ni kama gereza linalofanya tuweze kuona uhalisia. Utashangaa mtu anaposhindwa kumfanya jambo lake atamtupia mzigo wake mungu na kusema hili haliwezekani tusubirie miujiza ya mungu, utafikiri hiyo miujiza ya mungu nikitu ambacho Kiko mbali naye wakati miujiza mikubwa Iko mbele ya macho yake lakini anashindwa kuona Wala kuhisi, binaadamu mwenyewe ni miujiza mikubwa kuwepo kwake katika hii Dunia, hivi mtu anashindwa hata kufikiri maisha yake yalivyo anavyoishi, anavyotembea, anavyokula na Kila anachokifanya anaona ni kawaida sio miujiza? Bahati mbaya haya mambo yote yameelezwa mpaka kwenye vitabu vya dini lakini kutokana na huu mfumo wa kuhangaikia tumbo mtu anashindwa hata kujitambua yeye mwenyewe. Ni jambo la kusikitisha Kwa kweli lakini tumuimbe mungu atusaidie, maana mfumo umetubana hatufurukuti na tumeukubali Kwa nguvu zote, kiasi ambacho hatuhitaji kitu chengine chochote kitakachotusaidia kuuondoa huu mfumo wa kuchumia tumbo. Nawasilisha
 
Wakristo mlivyo na shida mnataka mpaka Ai iwatendee wema ndio muone ya kuwa inatenda haki,

Ai ni mwanzo sahihi wa kuitoa akili kwenye huu mwili uliojaa vikwazo vingi na kuiweka huru, halafu pia unaogopa vipi kitu ambacho hakina conscious? Hakioni, hakisikii, hakinusi, hakihisi,

Kwangu mimi tafsiri halisi ya Ai ni akili ya mwanadamu iliyohamishiwa kwenye mashine, kwahiyo kuiogopa Ai ni sawa na kuiangalia akili yako inavyofanya kazi nje ya mwili na kuamua kuiogopa...

Akili bandia ni mwanzo tuu katika hii safari ya kumuondoa organic being na kuleta super being ambaye hahitaji kutimiza mahitaji ya mwili kama tafsiri ya maisha.
Kwa tafsiri nyepesi ni mtu kuogopa kivuli chake mwenyewe
 
Back
Top Bottom