Aibu! Boda ya Rusumo Mgeni haingii nchini bila rushwa

Aibu! Boda ya Rusumo Mgeni haingii nchini bila rushwa

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Tusipoyaandika au kuyapigia kelele vilivyo, mama aliye busy na kuifungua nchi atayasikia vipi na hasa kama wenye dhamana ni sehemu ya mchezo wenyewe?

Baada ya kuyasikia nilijivinjari kufika mpakani Rusumo kujiridhisha.

Huu ndiyo ulio ukweli mchungu:

Mgeni haingii nchini bila kutoa rushwa. Rushwa inaombwa waziwazi bila ya aibu. Rushwa imefanywa kuwa sehemu ya malipo halali ya waliopewa dhamana mbalimbali mpakani hapo.

Mambo ya aibu kubwa.

(Nitajivinjari mipaka mingine pia kuipata ladha kamili ya huko nako. Tutege masikio).

Mchezo uko hivi:
Mgeni akifika hupaswa kuanzia kitengo cha afya. Kuna mabwana na mabibi afya hapo. Cha mno huuliziwa kadi ya yellow fever.

Mgeni akiwa nayo hupewa ki memo cha kupeleka kwa afisa uhamiaji. Bila hiyo kadi, memo pia hupatikana kwa njia mbadala - pesa, wala si chanjo. Makubwa maana madogo yana nafuu!

Kihunzi hicho cha kwanza mgeni akikiruka, kwa afisa uhamiaji anaweza kuulizwa kuthibitisha kama kachanjwa korona.

Uhamiaji na korona wapi na wapi wandugu wakati kipo kitengo cha afya? Akikosa uthibitisho si kuwa atalazimika kuchanjwa, la hasha. Hapa napo chanjo mbadala ni pesa!

Mgeni akiruka viwili hivi mengi mengine yaja. Atatakiwa kueleza madhumuni ya safari, namba za simu za jamaa kama ana mwenyeji, jina la Hoteli atajayofikia kama hana mwenyeji, nk. Lini mla rushwa aliwahi kupungukiwa longolongo au visingizio?

Ole wake aseme kaja kufuata biashara. Makaratasi sasa yatakayotakiwa hapo kwa jina la leseni, vibali nk ili mradi mlengwa hawezi kutoboa. Kazi kweli kweli.

Au ole wake asijue jina la Hoteli au guest house atakayofikia, hapo napo ni kimbembe kingine cha kutosha! Bottom line kunatakiwa pesa na pesa lazima itoke.

Ama kweli kuna watu wako kwenye kulamba asali na kula kwa urefu wa kamba zao.

Ninakazia: Nani mwenye kuyaangazia haya, mama anapokuwa busy akiifungua nchi?

Pumzika kwa amani JPM yawezekana ulikuwa sahihi kuwa tutakukumbuka.
 
Daaah hapo sasa watasababisha watu waanze kuvuka kinyemela kwa kutumia mitumbwi kupitia huo mto Ruvuvu. Na hii itakuwa ni hatari sana kwa usalama.
 
Madhila wanayokutana nayo wa Tanzania wakiwa wanavuka border kwenda nchi nyingine husemi unawasemea wageni wanaoingia Tanzania.
 
Madhila wanayokutana nayo wa Tanzania wakiwa wanavuka border kwenda nchi nyingine husemi unawasemea wageni wanaoingia Tanzania
Hizi ndiyo zile akili zetu sasa. Ndiyo maana tupo tulipo na itatuchukua miaka mingi sana.

Hivi tunajipangaje na wewe mkuu kudai haki zetu na ustawi wa taifa hili kwa akili kama hizi?

Au wewe ni mshirika mwaminifu tu wa magenge haya ya kihalifu?

Bure kabisa.

Pamoja na yote apumzike kwa amani JPM.
 
Ni mipaka yote tu imeoza kupita maelezo halafu uhamiaji wala rushwa wakubwa basi ni vile hatuwasemi sana humu

"Hii nchi ni ngumu sana." Alisikika mwuungwana mmoja aliyekata tamaa akilalama.
 
Wanasema “This is Africa”

Kuna moja nilipita manyovu narudi Tanzania kuona tu ppt ya kijani ina bei yake 5000 ya Kitanzania. No way lazima ulipe upate exit ya kuingia nyumbani Tanzania.

Pia kuna border ya Rwanda nilivuka salama kuingia immigration ya Burundi tayari lazima uache chenji, ila kwa warundi nishawazoelea nawapa franga 1000 wao wanaita ya primus.
 
Mkuu hivi hapo boda kuna gari za kwenda mpaka Kigali maana 2020 kwenye korona si zilizuiwa.

Halafu vipi kuingia Rwanda lazima uchanje ule utopolo wa korona.

Halafu nao wageni wanaibiwaje wakati maafisa wa ujamiaji wa Rwanda na Tanzania wako jengo moja.
 
Mkuu hivi hapo boda kuna gari za kwenda mpaka Kigali maana 2020 kwenye korona si zilizuiwa.


Halafu vipi kuingia Rwanda lazima uchanje ule utopolo wa korona

Halafu nao wageni wanaibiwaje wakati maafisa wa ujamiaji wa Rwanda na Tanzania wako jengo moja

Mkuu chanjo si ilishadhibiti Corona duniani kote na boda zikafunguliwa?

Boda kufunguka ina maana human traffic hata kwa punda - back and forth si inakuwa ruksa? Au nasema uongo ndugu yangu?

Hii kuwa chumba kimoja haihusu idara ya afya.

Mahojiano ya afisa na mteja si kwa kila mtu kusikia. Zaidi sana kuna chumba cha faragha kwa ajili ya mahojiano nyeti yenye tija ya tumbo binafsi kama haya.

Kwenye ukwasi wa kupindukia wa wajumbe wetu hawa haikuwa point ya kuanzia kulala mbele na magenge kama haya?

Nini source ya ukwasi wao?

Pumzika kwa amani JPM leo ni mwendo wa kijipimia kwa urefu wa kamba ya mtu.
 
Kwahiyo hapo Rusumo watu wanavuka kama zamani bila kuombana cheti cha kupima korona
Kwa mujibu wa mada ambayo imefanyiwa kazi vilivyo, uthibitisho wa chanjo huhitajika kimagumashi kuingia Tanzania tu.

Habari ndiyo hiyo.
 
Kwa mujibu wa mada ambayo imefanyiwa kazi vilivyo, uthibitisho wa chanjo huhitajika kimagumashi kuingia Tanzania tu.

Habari ndiyo hiyo.
Mkuu, nimepanga Decemba kupita border ya Rusumo, Destination yangu ni Goma DRC.
Vipi barabara kutoka Nyakanazi hadi Rusumo iliisha karabatiwa?
Vipi kuhusu chanjo za corona, kwa kuingia Rwanda ni lazima uchanjwe au wanafanya test za corona?
Kama una taarifa nyepesi nyepesi naomba tupeane maujanja.... Asante
 
Back
Top Bottom