Aibu kwa TRA idara ya forodha Rusumo; Mhuri nyeti huachiwa nyoka (kijana)

Aibu kwa TRA idara ya forodha Rusumo; Mhuri nyeti huachiwa nyoka (kijana)

Suzy Elias

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2021
Posts
1,067
Reaction score
6,200
20220406_144017.jpg

Mida ya usiku pale kwenye geti la kutokea Tanzania kuingia Rwanda maafisa wetu wa forodha huwa wanafanya uzembe unaohatarisha usalama wa taifa letu kwa wao kwenda majumbani ama nyakati zingine kwenda kuangalia mpira na pengine kwenda bar na mhuri huo hapo juu huachiwa vijana wa ving'amuzi kuutumia kwa kuwagongea madereva ama wenye mizigo kuruhusu kutoka upande wa Tanzania.

Hoja hapa siyo kuharibu kibarua cha mtu bali ni uzalendo.

Iweje afisa forodha azingatie starehe na kumilikisha kijana asiye na sifa kutumia mhuri nyeti namna hiyo?

Binafsi nilipeleka bidhaa zangu huko Rwanda na ajabu tena ikiwa mapema saa 2100 usiku mimi,agent wangu na dereva wangu pia tulikuta afisa mhusika wa zamu hayupo na tukaelezwa mhuri anao yule kijana wa ving'amuzi jambo lililonisononesha sana!

Jamani Watanzania wenzangu hasa mliopewa dhamana mahali fulani tujitahidi tuwe na uzalendo japo kiduchu kwa nchi yetu.
 
Hii nchi hii ww acha tu kuna uozo mwingi sana kuna watu watakuja na hoja ooh magu hayupo wakati haya madudu yapo mda tu sijui tunamfumo gani sisi Tanzania.

Pale Nala Dodoma mzani kuna Dokta wa mifugo huwezi pita pale km hujagongewa muhuri kwenye permit huyo Dokta mda wote amelewa chakari yaani anayumba toka 2020 yupo [emoji3][emoji1787][emoji2960] tukipita mida ya usiku around 07:00 na kuendelea. Sasa hivi nilikuwa najiuliza huyu magu natumbua tumbua alafu huyu mtu yuko Capital City hii serikali imelala [emoji1787][emoji3] nahisi mpaka leo yupo.

Tulikuwa tukipita zetu kwa vile mlevi msumbufu tunamzungua unampa 2,000 ya bia siku tunamchenjia tunasepa sasa nikawa najiuliza hivi hapa kuna ufanisi wa kazi kweli huyu sianapitisha hata mifugo imekufa, imekonda kwa walaji. [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Wacha watu wapige hela we nenda kwenu Rwanda, Meko alitusumbua mno we vuka usilipe ushuru ishia zako kimpango wako bana inakuuma nini?
 
Hizi ni tuhuma kali sana kuleta picha ya muhuri peke yake sio uthibitisho tosha wa tuhuma zako. Tutajuaje huenda ni chuki dhidi ya Customs officcer unayemtuhumu hapa? hebu Mkuu leta ushahidi zaidi tuliamini hili jambo.
 
Hii nchi hii ww acha tu kuna uozo mwingi sana kuna watu watakuja na hoja ooh magu hayupo wakati haya madudu yapo mda tu sijui tunamfumo gani sisi Tanzania...
Nchi ishakufa kaka si mijini tu ila hata vijijini yanayoendelea si Sawa, nimebahatika kuitembelea mbeya vijijini , katika kijiji kinaitwa ISUTO wao wanaita umalila, pale kuna zahanati ya kijiji hivi uliwahi jua kupimwa UKIMWI kwenye hospitali za serikali ni gharama? Basi ni hapa kwenye hiki kijiji watu wanalipishwa sana lakini pia wengi wameathirika na bado hakuna ethics kwa hawa madaktari maana wakikupima kukutangaza ni kawaida.

Oooh Tanzania ya nyerere iko wapi?
 
Hizi ni tuhuma kali sana kuleta picha ya muhuri peke yake sio uthibitisho tosha wa tuhuma zako. Tutajuaje huenda ni chuki dhidi ya Customs officcer unayemtuhumu hapa? hebu Mkuu leta ushahidi zaidi tuliamini hili jambo.
Ulitaka afanyaje sasa watumishi wako wengi wanafanya huo uozo yaani ikifika usiku ni vitimbi wengine walevi mpaka unamzuia mtu asianguke eti yuko kazini [emoji3][emoji3][emoji1787]. Taarifa inatosha mamlaka husika zifanyie kazi wachunguze.
 

Mida ya usiku pale kwenye geti la kutokea Tanzania kuingia Rwanda maafisa wetu wa forodha huwa wanafanya uzembe unaohatarisha usalama wa taifa letu kwa wao kwenda majumbani ama nyakati zingine kwenda kuangalia mpira na pengine kwenda bar na mhuri huo hapo juu huachiwa vijana wa ving'amuzi kuutumia kwa kuwagongea madereva ama wenye mizigo kuruhusu kutoka upande wa Tanzania.

Hoja hapa siyo kuharibu kibarua cha mtu bali ni uzalendo.

Iweje afisa forodha azingatie starehe na kumilikisha kijana asiye na sifa kutumia mhuri nyeti namna hiyo?

Binafsi nilipeleka bidhaa zangu huko Rwanda na ajabu tena ikiwa mapema saa 2100 usiku mimi,agent wangu na dereva wangu pia tulikuta afisa mhusika wa zamu hayupo na tukaelezwa mhuri anao yule kijana wa ving'amuzi jambo lililonisononesha sana!

Jamani Watanzania wenzangu hasa mliopewa dhamana mahali fulani tujitahidi tuwe na uzalendo japo kiduchu kwa nchi yetu.
Majungu ni ujinga pata elimu ili upunguze majungu.
 
Wacha watu wapige hela we nenda kwenu Rwanda, Meko alitusumbua mno we vuka usilipe ushuru ishia zako kimpango wako bana inakuuma nini?
Yanasemwa kimzaha mzaha vile, kumbe ndiyo tabia yenyewe hiyo aliyonayo mtu.

Kuna siku atapatikana mzalendo wa kweli anayejali maslahi ya nchi hii. Watu kama nyinyi mtalia na kusaga meno.

Usiniambie, na wala sitaki kusikia ukimtaja Magufuli kama mfano wa MZALENDO huyo. Yupo, yuko njiani. Mtakoma tu!

'Bondpost', inanilazimu nikukumbuke tokea sasa, kama mmoja wa maadui wa nchi yetu.
 
Bar ni kiungo muhimu cha kukuza uchumi wetu.

Wapongezwe kwa kuendeleza uwekezaji wa ndani.
 
Back
Top Bottom