Hakika Rais Samia anaupepo kwelikweli | Aie Holding Ltd kampuni toka Israel kuwekeza TZS 575bl kwenye kilimo na kutoa ajira za moja kwa moja elfu 70
" Hakuna kama Rais Samia "
Wakati uwekezaji kwa miezi sita ya Rais Samia ukikua kwa 400% kutoka $510M March 2021 hadi $2.98bl Sept karibu 7trilioni mambo yanazidi kunoga na kicheko kwa Watanzania kinazidi kukolea,
Moja ya faida kubwa ya Uwekezaji toka nje ( FDI ) ni kutuletea fedha za kigeni,teknolojia,ongezeko la thamani kwenye bidhaa na huduma pamoja na ajira kwa wazawa,Taarifa za TPSF zinaonesha Sekta binafsi inabeba zaidi ya 90% ya ajira zote Tanzania,Lakini inachangia 80% ya mapato yote ya Serikali na inabeba 60% ya uwekezaji wote wa nchi,
Wakati FY 2021|22 Serikali imepanga kuajiri watu elfu 40 Aie Holding LTD pekee wanakuja kuajiri watu elfu 70 kwa Mkupuo sawa na 175% ya ajira zote mpya za serikali kwa mwaka wa fedha wa 2021|2022 ndio maana Rais Samia ameondoa jumla ya tozo 232 nahii ndio sababu kamapuni kama hii ilisajiliwa mwaka 2020 ila uwekezaji inaufanya mwaka wa Rais Samia,
Aie Holding LTD kampuni toka Israeli itawekeza kwenye biashara ya kilimo ,kilimo, elimu ya kilimo pamoja na Vifaa vya kilimo na mashine na itahitaji jumla ya hekta 25,000,Makao makuu yatakuwa D'salaam vituo vingine vitakuwa Mwanza, Morogoro,Njombe,Kagera na Bagamoyo na watatumia zaidi umeme wa jua,
Aie Holding LTD inawekeza jumla ya $250M sawa na Tshs 575BL huku $200 itatumika kujenga miundombinu na $50M itakuwa ni mtaji wa kuanzia biashara,Kazi hii itafanywa kwa ubia na baadhi ya mabenki makubwa matano bila kubali majina ya benki husika huku Staff watakaoajiriwa na kampuni hii kupelekwa kozi ya miezi kati ya 6|7 nchini Israel vijana changamkeni,
View attachment 1956881