Aina ya Bangi inayovutwa Tanzania imeachwa kuvutwa Marekani na ulaya tangu miaka ya 1970, watanzania wanaendelea kuvuta na kuyasifia makapi

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Inashangaza sana kuona hadi leo watanzania wanavuta makapi yaliyoachwa kuvutwa miaka ya 1970, yani mpaka leo hawajastuka tu.

Makapi haya yanasifiwa kwa majina kama "Cha Arusha", "Tarime one", "Cha malawi", "Skanka ya Moro" n.k, kwa kujidanganya ni kiwango sawa na bangi za Marekani, ni uthibitisho usio na shaka kwamba watanzania wanaovuta bado wapo gizani na hawana elimu ya kilevi wanachotumia, ndio maana huwa sishangai vituko vya watumiaji wa huu mmea.

Ni kwamba Kuanzia miaka ya 1970 bangi inayolimwa haina mbegu, ni huku Tanzania na nchi nyingi Africa bado tupo gizani, ukitaka kuniamini watanzania hawajui chchote kuhusu hili ukiwajuza watakwambia "huwezi kutuambia chochote kuhusu bangi, Cha Arusha ndio chenyewe na hakuna bangi isiyo na mbegu", ni wabishi vibaya mno.

Bangi ni mmea na kwa elimu ya shule ya msingi tulijifunza kwamba ili mmea utoe mbegu, inabidi mmea wa kike (female blant) unase polen za mmea wa kiume (male pant), polen huwa ni kama unga zinafikia mmea wa kike kwa upepo, kuhamishwa na wadudu, ndege, n.k. zikifikia mmea wa kike kuna mbegu zitaanza kuota.

hivyo ili bangi isiwe na mbegu inabidi mkulima apambane sana shambani kuzuia pollen isifikie mmea wa kike, yaani inabidi autunze sana mmea wa kike azuie pollen za mmea wa kiume zisifike.

Bangi inavyoota ikizuiwa kuzalisha mbegu matokeo yake mmea unaweka nguvu zote kuzalisha kilevi, huzalisha maua makubwa zaidi yenye kilevi pure, hii ndio bangi inayokuwa na viwango na salama kwa afya.

Huku Tanzania bangi inapandwa msituni inaachwa ijiotee bila uangalizi inasubiriwa kuvunwa tu, ni lazima ukute ina mbegu, huwezi vuta moja ndio maana unawaona watu wanazichambua kwenye vihanja kutoa mbegu na bado huwa kuna chembechembe zisizoonekana zitabaki,

mbegu hutolewa sababu zinafanya kichwa kiume, zinapunguza nguvu za kiume, zikivutwa zinapasuka kwa sauti kali zikiangukia kwenye nguo zinatoboa, hufanya macho yawe mekundu zaidi kuliko bangi isiyo na mbegu, pia huwa zinaathiri mishipa ya ubongo.

Halafu kuna huu ushamba mwengine unaoonyesha wazi watanzania wanaovuta hawajui hata elimu ya mimea, mtu anasifia "hili ni ganja dume, ni kitu original", hawana hata elimu kujua kwamba sehemu ya kiume ya mmea kazi yake ni kuzalisha polen sio maua yanayovutwa, sehemu pekee inayovutwa ni maua yanayozalishwa na upande wa kike wa mmea.

Bangi ya Tanzania ipo hivi, unaweza kuona hizo mbegu zilivyojaa,



Bangi isiyo na mbegu hii hapa

 
Kwa akili yako unahisi bangi inajiotesha tu polini watu wanaenda kuvuna tu et?

Sio kila wanachofanya mzungu na huku kwetu tukifanye.

Ukimaliza uje na kwenye matunda yenye mbegu na yasio nambegu
 
Kwa akili yako unahisi bangi inajiotesha tu polini watu wanaenda kuvuna tu et?
Sio kila wanachofanya mzungu na huku kwetu tukifanye.
Ukimaliza uje na kwenye matunda yenye mbegu na yasio nambegu
kwa hapa bongo wakulima wakipanda wanaiacha inajiotea wanakuja kuvuna tu, kama hujaishi sehemu wanakolima huwezi jua chochote,
 

Bangi inayovutwa Arusha ndiyo inayovutwa Jamaica....!

Na tutaivuta hiyohiyo...hiyo ya Marekani isiyo na mbegu inavutwa na wanawake wajawazito

Ingekuwa ni kuwa Hanithi kina Bob Marley, Joseph Hill na wengine wasingekuwa na rundo la watoto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…