Air Tanzania ingeshusha viwango vya nauli, tungesafirisha Watanzania wengi ndani na nje ya nchi

Air Tanzania ingeshusha viwango vya nauli, tungesafirisha Watanzania wengi ndani na nje ya nchi

Mimi nililipa, 42500, 66000, 94000 na 154000 one way
Hizi ni bei rafiki sana.

Wateja wetu wengi hutuomba tuwafikishie malalamiko yao katika idara husika na kututaka tukahoji; hayo mashirika mengine yaliwezaje hadi ATC lishindwe kuweka bei hizi?

Kupitia uzi huu watayaona pia. Tunatazamia kheri.
 
Kwa sasa hata ukiliombea shirika la ATCL life ni ngumu kwani idadi ya abiria kwa kila route sio ndogo. Mapendekezo yangu;
1. Kama mtanzania naungana na wote tunaotaka nauli zipungue. Inawezekana na itasaidia shirika letu kuwa na abiria wengi zaidi.
2. Route za southern corridor zirejeshwe, kama vile mtwara, songea na iringa. Maana viwanja vimeshakarabatiwa.
3. Tukimaster route zote za ndani twende route za nje kama london, guanhzou nk.
 
Kwa sasa hata ukiliombea shirika la ATCL life ni ngumu kwani idadi ya abiria kwa kila route sio ndogo. Mapendekezo yangu;
1. Kama mtanzania naungana na wote tunaotaka nauli zipungue. Inawezekana na itasaidia shirika letu kuwa na abiria wengi zaidi.
2. Route za southern corridor zirejeshwe, kama vile mtwara, songea na iringa. Maana viwanja vimeshakarabatiwa.
3. Tukimaster route zote za ndani twende route za nje kama london, guanhzou nk.
Umeiweka vizuri sana mdau
 
Ghar
View attachment 1679043

Salaam Great Thinkers,
Tumeanza kutoa huduma ya kusafirisha abiria wanaotumia ndege kusafiri, iwe ni ndani ya nchi au kimataifa, kwa miaka kadhaa sasa. Uzoefu tulionao umepelekea tuzifahamu changamoto nyingi kupitia feedback tunazozipata kutoka kwa wateja/abiria.

Miongoni mwa changamoto hizo tumejaribu kuzitolea elimu na ufafanuzi kwenye threads zetu zilizopita. Leo tumeona tugusie changamoto ya bei ya nauli.

Bei za Tiketi za #AirTanzania zimekuwa zikilalamikiwa na kufanya usafiri wa anga kuwa anasa badala ya huduma. Ni mara nyingi mno tumelazimika kutumia nguvu ya ziada kushawishi wateja kuona kwamba gharama hizi zinaendana na viwango vya huduma nzuri zitolewazo na ATC. Pia tunatumia kete ya kuwasihi watanzania kutanguliza uzalendo kwani Shirika hili bado linajipanga kibiashara, lakini inafikia hatua tunaishiwa sera!

Baadhi ya threads hapa JF ambazo zimeongelea gharama za ndege za ATCL kuwa sio rafiki na hazivumiliki ni pamoja na;




Kwa utafiti wetu ambao sio rasmi, tumegundua Watanzania wengi wanatamani kutumia usafiri huu lakini wanaogopa bei, hasa wale wenye kipato cha kawaida. Routes mpya za Chato na Arusha zilitia hamasa lakini bei zimewarudisha wengi wao nyuma baada ya kukutana na bei tata. Ni idadi kubwa ya watu ambayo ingeweza kulizalishia shirika faida na kurahisisha safari za masafa marefu zikiwemo za kutoka Dar kwenda Mwanza, Kagera, Kigoma n.k. na kinyume chake.

Tunafahamu, lengo la Serikali na Shirika ni kuhakikisha Ndege hizi zilizonunuliwa kwa wingi zinakuwa affordable kwa watanzania wanaofanya safari (ndani na nje ya nchi). Na sisi kwa uzoefu wetu na tabia za wateja tunaliona hili la bei kuwa kikwazo namba moja kinachosababisha hata rate ya wasafiri ku-book ndege hizi za ndani ikishuka au kushindwa kuongezeka katika kiwango kinachoridhisha.

Imefikia hatua zipo baadhi ya routes za ndani zina gharama ya juu zaidi kulinganisha na gharama za ndege kupitia mashirika mengine kwenda nje ya nchi. Hatuingilii mamlaka, tunajaribu tu kufikisha 'picha halisi' kutoka kwa watumiaji wa huduma na mtazamo wetu wadau wa sekta hii muhimu kwa maendeleo ya taifa.

Ni matarajio yetu wanaofanya maamuzi wataliangalia hili kwa ukaribu na kulifanyia kazi haraka. Wakishusha bei, tutasafirisha watanzania wengi popote pale kwa kweli na ndege hazitasafiri tupu, kwani wengi wapo tayari tatizo ni hilo tu- BEI!

Au abiria wazoefu na watarajiwa mnasemaje?
Gharama za undeshaji lazima uzingatiwe, tuko kwenye uchumi wa kati wananchi wengi wana uwezo wa kupanda Ndege.
 
Hivi ukisafiri na ndege ukapanda izo place mfano business, economy ndege ikianguka ci mnakufa wote?
Tofauti ya madaraja (classes) katika Ndege ni ubora wa huduma anazopatiwa mteja kulingana na hadhi ya daraja husika.

Kuna daraja la uchumi (economy class), daraja la biashara (business class) na daraja la kwanza (first class).

Ajali na matokeo yake ni suala lingine.

Asante.
 
Ungeweka figures ingependeza zaidi. Compare & contrast!
Ukipitia uzi vizuri, utaona bei mbalimbali zimetajwa sambamba na shuhuda.

Habari njema ni kwamba maoni na taarifa zinazoandikwa kwenye uzi huu tayari zimefika mezani kwa ofisi kuu ya ATCL.

Yote yanayoandikwa hapa yanafuatiliwa ili kufanyiwa kazi haraka mwaka huu.

Asante.
 
View attachment 1679043

Salaam Great Thinkers,
Tumeanza kutoa huduma ya kusafirisha abiria wanaotumia ndege kusafiri, iwe ni ndani ya nchi au kimataifa, kwa miaka kadhaa sasa. Uzoefu tulionao umepelekea tuzifahamu changamoto nyingi kupitia feedback tunazozipata kutoka kwa wateja/abiria.

Miongoni mwa changamoto hizo tumejaribu kuzitolea elimu na ufafanuzi kwenye threads zetu zilizopita. Leo tumeona tugusie changamoto ya bei ya nauli.

Bei za Tiketi za #AirTanzania zimekuwa zikilalamikiwa na kufanya usafiri wa anga kuwa anasa badala ya huduma. Ni mara nyingi mno tumelazimika kutumia nguvu ya ziada kushawishi wateja kuona kwamba gharama hizi zinaendana na viwango vya huduma nzuri zitolewazo na ATC. Pia tunatumia kete ya kuwasihi watanzania kutanguliza uzalendo kwani Shirika hili bado linajipanga kibiashara, lakini inafikia hatua tunaishiwa sera!

Baadhi ya threads hapa JF ambazo zimeongelea gharama za ndege za ATCL kuwa sio rafiki na hazivumiliki ni pamoja na;




Kwa utafiti wetu ambao sio rasmi, tumegundua Watanzania wengi wanatamani kutumia usafiri huu lakini wanaogopa bei, hasa wale wenye kipato cha kawaida. Routes mpya za Chato na Arusha zilitia hamasa lakini bei zimewarudisha wengi wao nyuma baada ya kukutana na bei tata. Ni idadi kubwa ya watu ambayo ingeweza kulizalishia shirika faida na kurahisisha safari za masafa marefu zikiwemo za kutoka Dar kwenda Mwanza, Kagera, Kigoma n.k. na kinyume chake.

Tunafahamu, lengo la Serikali na Shirika ni kuhakikisha Ndege hizi zilizonunuliwa kwa wingi zinakuwa affordable kwa watanzania wanaofanya safari (ndani na nje ya nchi). Na sisi kwa uzoefu wetu na tabia za wateja tunaliona hili la bei kuwa kikwazo namba moja kinachosababisha hata rate ya wasafiri ku-book ndege hizi za ndani ikishuka au kushindwa kuongezeka katika kiwango kinachoridhisha.

Imefikia hatua zipo baadhi ya routes za ndani zina gharama ya juu zaidi kulinganisha na gharama za ndege kupitia mashirika mengine kwenda nje ya nchi. Hatuingilii mamlaka, tunajaribu tu kufikisha 'picha halisi' kutoka kwa watumiaji wa huduma na mtazamo wetu wadau wa sekta hii muhimu kwa maendeleo ya taifa.

Ni matarajio yetu wanaofanya maamuzi wataliangalia hili kwa ukaribu na kulifanyia kazi haraka. Wakishusha bei, tutasafirisha watanzania wengi popote pale kwa kweli na ndege hazitasafiri tupu, kwani wengi wapo tayari tatizo ni hilo tu- BEI!

Au abiria wazoefu na watarajiwa mnasemaje?
Yaani bei ni shida jamani tena sasa hivi naona zimeongezeka zaidi, maana juzi tu hapa nimefanya booking sema sikulipia , baada ya siku kadhaa nakuja kufanya tena booking ya siku nyingine naona bei zimeongezeka, hata ukitafuta za siku za mbeleni huko.
 
Yaani bei ni shida jamani tena sasa hivi naona zimeongezeka zaidi, maana juzi tu hapa nimefanya booking sema sikulipia , baada ya siku kadhaa nakuja kufanya tena booking ya siku nyingine naona bei zimeongezeka, hata ukitafuta za siku za mbeleni huko.
Pole sana kajojo. Tuliwasiliana na menejiment ya #AirTanzania na viongozi wa idara wakasema watakuwa wanapitia uzi huu mara kwa mara. Bila shaka wataona malalamiko haya na kuyafanyia kazi.
 
Yaani bei ni shida jamani tena sasa hivi naona zimeongezeka zaidi, maana juzi tu hapa nimefanya booking sema sikulipia , baada ya siku kadhaa nakuja kufanya tena booking ya siku nyingine naona bei zimeongezeka, hata ukitafuta za siku za mbeleni huko.
siku hzi hakuna za kukata mapemaaaaaaa kabla ya chrismass??maisha haya tunateseka na mengi jamani
 
Pole sana kajojo. Tuliwasiliana na menejiment ya #AirTanzania na viongozi wa idara wakasema watakuwa wanapitia uzi huu mara kwa mara. Bila shaka wataona malalamiko haya na kuyafanyia kazi.
ishu watende haki mambo ya kupitia uzi kila siku sio suluhisho ishu ni bei imekuwa shida !!!!!swala la kusema ndege ni zetu mbna gharama ni kubwa sana pia
 
yote ya yote ataalamu wa mambo ya auditing wanakwambia bado kampuni nyingi za ndege zinajiendesha kiahasara sana..wengi wao wanahemea juuujuu
 
Dar-Dodoma nilipe sijui 325,000 wallah nitakufa. Shabiby na Kibinyiko zile za Alfajili ni Tshs 20,000/= halafu unapita Pwani Kibaha, Morogoro kisha Dodoma. Upo angani unapita wapi. Sikataki kupanda mwewe ila kwa route za humu ndani hapa kbs biashara ya kupunguziana K-Vant na mbuzi choma. Pandeni tu. Wengine tutakufa na IT na Mafusso kwa route za ndani. Ama magari ya Magazeti yale ya Posta.
 
Ajabu ni rahisi kupanda ndege congo kuliko Tanzania, Alaumiwe aliewatoa fastjet angani tulijua ATCL ni shirika letu la kizalendo litajopanga kibiashara kwa huduma nzuri na bei rafiki lakini kubaki peke yao imekua mzigo kwao, wajitafakari bila hivo naona Baada ya Rais Magufuli na shirika litakufa tena.
 
Back
Top Bottom