Air Tanzania yasimamisha Ndege zote za Airbus A220 kutokana na matatizo ya injini

Ungekuwa ni uamuzi wa manufacturer, obvious ndege zote zenye injini za aina hii zingekuwa grounded dunia nzima
Kwani ndege zingine za aina hii "dunia nzima" bado zinaruka ?

News report ya mada hii imesemaje kuhusu hali ya ndege nyingine kama hizo "dunia nzima" ?

Umesoma article yote mwanzo mpaka mwisho ????
 
Kumbe sie ndio tulioipanda kimwishimwisho huku asubuhi hiyo hiyo wenzetu wakielekea Bukoba kutumia PW.

Nilidhangaa siku ya kurudi tumebadilishiwa ATR badala ya Airbus A220.
 
Yule msukuma alikuwa anayazoa tu kama ananunulia toy watoto wake huko chato
 
Shida inaonekana ni manufacturer's defect,na nina uhakika hizo ndege bado zitakuwa ndani ya warrant kwahiyo sidhani kama ATCL wataingia gharama za matengenezo,ila tu ki biashara watakuwa kwenye maumivu,sasa sijajua kama hapo kutakuwa na maswala ya compansation au ndio imekula kwao,maana unaweza kukuta ni yale mambo ya kununua bila ya risiti ya EFD😀😀...
 
Andiko la London liko wapi banah ?

Ndio haya mambo nimeona kwenye TBC vitoto vya shule vinafundishwa kuimba London Bridge is falling down wakati hatujaliona hilo London Bridge na sisi tuna ma Wami Bridge na Mfugale Bridge yanazama kwenye mvua hatuyaimbi. Tusijadili article za London ambazo hatujaziona.

Andiko tulilo nalo hapa la bandiko la kwanza la mada hii limesemaje kuhusu fidia kutoka kwa manufacturer ????
 

Hata hao Ethiopia Kuna wakati walitengeneza hasara iliyoibua mjadala mkali sana bungeni.
 
Mkuu SemperFI , asante sana kwa story hii, kwanza, ukiondoa gazeti la the Citizen na Mwananchi, hakuna media ya Tanzania ina vichwa vya kuandika kitu kama hii!.

Humo kuna vitu Matinde hakusema ambavyo vinaligharimu taifa kwa ujuha tuu wa viongozi wetu, kununua ndege kwa cash kama unavyonunua nazi sokoni, wamama wa uswahilini wakinunua nazi wana ipasua pale pale kwa mnunuzi ili ikiwa mbovu inakuwa replaced, ukinunua nazi, ukaenda nayo nyumbani, ikotokea ni mbovu, imekula kwako!.

Manunuzi yote ya mitambo zikiwemo ndege hufanywa by order na kulipiwa by hire purchase, ili kutumika kama warranty na guarantee ya manufactures liability on defects, ukitokea kuna uharibifu wowote uliotokana na manufactures defect, ni manufacture ana gharimia. Ukinunua kwa cash, likitokea la kutokea, utajibeba!, hivyo ule ujinga wa kununua midege sokoni kama unanunua nazi, unai cost ATC na kutu cost Watanzania kwa ujuha tuu!.

Ujinga mwingine ni umiliki wa ndege kwa TGFA, halafu ATC inakodisha!. TGFA ni 100% government, ATCL ni 100% government, ATCL inakodisha ndege za TGFA, wakati wote midege hii iko grounded, yeye TGFA, anakula tuu kodi yake ya ukodishaji, ATCL inalipia midege iliyosimama, hivyo kwenye hesabu za ATCL kunaonekana ina operates on loss!.
Taarifa ya CAG ya mwaka huu imeonyesha ATC inaendeshwa kwa hasara na mpaka sasa deni la TGFA ni dola $132.77 milioni!. Halafu serikali inachota dola $194 milioni toka mfuku mkuu wa hazina kui bail out ATCL!, huu ni nini kama sio ujinga?!. Mama Samia asiukubali ujinga huu uendelee!. Mkataba wa ATC wa ukodishaji ndege za TGFA uvunjwe!, ATCL izitumie ndege bure, zikiwa kwenye operations na kuzalisha faida ndipo TGFA agaiwe faida, siku ndege ziko grounded hazizalishi kitu kama sasa, hizo Airbus, TGFA isilipwe chochote!.

Najua lengo la kuziweka ndege chini ya umiliki wa TGFA ni ku mitigate zisikamatwe na wadeni wa ATCL, nashauri, serikali yetu, lipeni madeni ya nchi, kuzuia ndege zetu kushikiliwa, kisha ipeni ATCL hiyo midege ili ATCL iwe huru kufanya chochote.

Ila pia tukubali tukatae ATCL bado kuna issues, mengine tusiseme kwa uzalendo, ila tusiendekeze ujinga kwa jina la uzalendo!.
P
 
Hahaha kuna viandiko vingi hebu pitia na haka

 
Kwa hiyo hizo ndege tumepigwa? bongolala chenga sana.....
 
Mara ngapi?, kwani kafara ile haijatosha?, au hujui kuwa ni kafara?.
P

Yaani ni afadhali wangekusanya watoto wa miaka 15 zaidi ya 500 wakawasomesha professional mbalimbali kwa vitendo kuliko huo upumbavu.

Hao vijana tungewatumia miaka mingi na wale wenye makaratasi yao ndani wangeenda kulima.

Mchina alicheza hakukosea na wale vijana hawakutetereka walifanyakazi kwa uzalendo na nchi yao Leo haitarudi nyuma.

Haya mambo ya kununua mavx 8 mandege tuachane naya. Tuwekeze kwa watoto wapate uzalendo was kuopenda nchi yao. Walimu Happ Tanzania wameshashindwa kuproduce watenda kazi. Wanazalisha watu wa porojo na matapeli.
 
Huu umaskini na unyonge si tumekubaliana tuahane nao, tusiwe na mawazo ya kimaskini?
 
Hili unalosema wwe lipo kwenye Mkataba wa manunuzi ya hizo Ndege!? Au ndiyo limejulikana Sasa!!??
Wala sio suala la mkataba. ndege sio bus kwambaa ukinunua ikipata ajali utajua mwenyewe. Ndege ukinunua lazima manufacturer ahakikishe muda wote ni salama, tatizo dogo linaweza kuleta shida kubwa. Kumbuka hivi karibuni kisa Cha Boeing na zile Max
 
Katika kitu namsifu Magufuli ni kununua hizo ndege cash. Angechukua kwa kukopeshwa Leo mngetukana matusi yote kuwa kaondoka kaiacha nchi na madeni ya ndege. Ni Kama alijua vile
 
Lakini si umeona mashirika mengine ya ndege yanayotumia hizo injini na yenyewe yametakuwa kufanya hivyo? Au ni Mimi lugha inanipiga chenga?
Sasa hili tangazo kwetu lilisubiri nini kutolewa huko nyuma kwa wakati muafka, linakuja kutolewa wakati huu? Kama ndege zingine ziko Maastricht tangu January 2022, kwa nini hatukujulishwa tangu hiyo Januari, tunakuja kujulishwa sasa?
 
Sasa hili tangazo kwetu lilisubiri nini kutolewa huko nyuma kwa wakati muafka, linakuja kutolewa wakati huu? Kama ndege zingine ziko Maastricht tangu January 2022, kwa nini hatukujulishwa tangu hiyo Januari, tunakuja kujulishwa sasa?

Kombora la Dr. Bashiru! Limetoa nyoka mapangoni. Hauoni matamko na ziara vimefumuka upya?
 
Katika kitu namsifu Magufuli ni kununua hizo ndege cash. Angechukua kwa kukopeshwa Leo mngetukana matusi yote kuwa kaondoka kaiacha nchi na madeni ya ndege. Ni Kama alijua vile

Madeni ni madeni tuu. Kama hakukopa kununua ndege, alikopa kwa mahitaji mengine. Tunarudi pale pale, nchi ni fukara na ina shida kibao.
 
Hv hizi ndehe zinafanya Internatinal routes...zinaenda wapina wapi?
 
Duuh! Yaani mnunuzi wa hizi ndege kwa cash ni juha na mjinga!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…