Airbus A380 - Emirates - King of the Sky

Wewe jenga hoja roho ya kwanini utakufa maskini, badala ya kujiuliza vipi hawa wameweza sisi tunakwama wapi? Hawa ni watu walikuwa wanajuwa wanataka kwenda wapi, haya unayo yaona ya Emirates ni mipango ilikuwepo toka siku ya kwanza wanaanzisha hii shirika kwa kukodi ndege toka Pakistan Air, ndege yao ya kwanza ya kukodi. Kama una mawazo ya kijinga eti sisi ndio tumewatajirisha mzee rudi shule, ujiulize hivi hawa uchumi wao wanategemea nini haswa. Budget ya Dubai tu sisemi UAE nasema Dubai tu ni mara 4 ya budget ya Tanzania yote.
 
Sawa sawa mkuu nimekuelwa vizuri sana
 
Asante kwa Elimu uliyotoa hapa hususani Emirates kukodi ndege yao ya kwanza toka Pakistan air. Leo imebaki stori
 
Tanzania inawezekana sema tupate mtu makini na apewe Uhuru wa kutosha sio mtu WA kupewa Vimemo. Ndege ziwe zinazunguka kubeba makada kila mkoa
 
First class yake ni 4mil aakati sogea tukae ni dolar1000
 
Mkuu kwann wanazigeuza cargo Kwa abiria hailipi?
Gharama za uendeshaji kuwa kubwa zaidi kumbuka Ile ni jumbo jet ni ndege kubwa yenye injini 4, Airbus wali introduce A 350 kama replacement ya A 380 mwaka 2019.
Dunia nzima zilitengenezwa 251 ila mpaka sasa ni 150 pekee ndo zipo angani na hazizalishwi Tena kiwandani.
 
A350 naona ni pacha wa B787 niliipanda hiyo A350 Singapore airlines aisee zinga la mashine hata ndugu zetu Ethiopian airlines wanazo za kutosha. Zanzibar airlines wanaweza kuamua kuanza nazo
 
Hamas wapo bize kujilipua. Wakati waarabu wenzao dini moja wanasaka noti
 


Airbus waliamua kuchukua route nyingine, A350 ni ndogo kidogo ila ni more efficient, more advanced n.k
 
Hivi huu uwekezaji wa Ndege kwanini sisi tunaushindwa kabisa? shida ni viongozi wetu au tunaletewa ndege feki?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…