S2kizzy mwenyewe anafanya kazi sehemu moja tu siku hizi.
Mara nyingi studio ndio zinabebwa na wasanii na ndio maana wasanii hasa wakubwa wana kiburi, studio nyingi wanarekodi bure.
Producer akiwadai pesa wanahama.
Weusi walihama The Industry wakaenda kwa Luffa.
Alikiba alihama Combination akaenda kwa Moco Genius.
Diamond alikuwa anafanya kazi na Sheddy clever, tangu ampige chini nae kapotea. Kuna kipindi alitaka kusimamia wasanii chini studio yake lakini mpaka leo bila bila.
Lamar yupo na studio yake hata haina kazi.
Kazi ya production bongo bado hailipi wala kuheshimika. Producers wanaishi kwa hisani ya msanii.
Bora hata maDJ wameanza kujiongeza.