Ajabu ya uteuzi wa Waziri Mkuu wa Uingereza

Ajabu ya uteuzi wa Waziri Mkuu wa Uingereza

AJABU YA UTEUZI WA WAZIRI MKUU UINGEREZA 🇬🇧
Na JumaKilumbi,

05.09.2022

Uingereza ni nchi ya kidemokrasia, Demokrasia iliyokomaa hasa, ila ina Malkia mwenye mamlaka ambayo huizidi katiba kwa sehemu.

Kuna mengi ya kuuliza kuhusu ‘Demokrasia’ yao ila leo tuzungumze kuhusu kupatikana kwa Waziri Mkuu wao.

WAZIRI MKUU NI NANI HASA?
Ni kiongozi wa Serikali mwenye mamlaka ya teuzi zote za juu; Teuzi za mabalozi, Teuzi za Baraza la mawaziri na Teuzi za maafisa wa Jeshi.

Pia ana mamlaka juu ya Utungaji wa sheria Utungaji wa sera na Utumaji Majeshi nje.

Muhimu ya yote ana sikio la Malkia, aweza mshauri kitu Malkia naye akafuata, kama vile Kuvunja Bunge!


WAINGEREZA 🇬🇧 HAWACHAGUI WAZIRI MKUU WAO

Tofauti na Tanzania 🇹🇿 ambapo huku kila baada ya miaka mitano tunapiga kura kumchagua kiongozi wa serikali, Rais, wao humchagua mtu mmoja tu, Mbunge.

Hao Wabunge wakienda Bungeni hujitazama, Chama kipi kitakuwa na Wabunge wengi?

Kama ni Labor basi Malkia atamteua kiongozi wa chama cha Labour kuwa Waziri Mkuu, na kama ni ‘Conservative’ vivyo hivyo.

Kwahiyo WAINGEREZA HAWCHAGUI WAZIRI MKUU!


SAKATA LA KUANGUKA KWA BORIS JOHNSON!
NB: Boris Johnson = BJ

  • SKENDO YA CHRIS PINCHER
BJ Alimteua bwana Pincher kuwa Mnadhimu wa chama chake cha Conservative. June 29, 2022 Picher alienda klabu alilewa sana akaanza kubambia wanaume wawili. Ikazuka skendo kubwa na nyingine kumhusu zilizowahi tokea huko nyuma. Watu wakasema ndiyo tabia yake.

Alipoulizwa BJ akadai hajui chochote kuhusu tabia za Mnadhimu Pincher, lakini watu wakazidi kusema kuwa BJ alikuwa anajua fika.

Baadae BJ alikiri kuwa alikua anajua tabia ya mnadhimu wake na akaomba radhi kumteua. Hili likamtafuna polepole.

  • ‘PARTYGATE SCANDAL’
Hili lilikuwa zito, si unaikumbuka Covid-19? Lockdown je? Basi ilipozuka Uviko-19 BJ na serikali yake wakaweka katazo la watu kuchangamana ili kuepusha kusambaa kwa virusi.

👉 Mwezi may 2020 walifanya ‘party’ kwenye bustani iliyopo Downing street (makazi ya Waziri Mkuu) na BJ alikuwepo.

👉 Mwezi Juni 2020 BJ alienda kwenye sherehe ya ‘birthday’ yake, ambapo ilisemekana kanuni za ‘Lockdown’ zilivunjwa.

Yote ilikuwa siri lakini Novemba 2021 gazeti la ‘Daily Mirror’ likaripoti matukio haya, ripoti nyingi zaidi zikafuata ila alipoulizwa BJ alisema kanuni za ‘social distancing’ zilifuatwa! Na uongozi wa Makazi ya ‘Downing Street’ (makazi na ofisi za Waziri Mkuu) walisema hakukuwa na ‘party’ yoyote.

Wiki moja baadae Video ikasambaa mtandaoni kumuonesha mkuu wa kitengo cha habari na mwenzie wakifanya mzaha kuhusu kanuni za ‘lockdown’. Shughuli ikaanzia hapo, Bunge likaunda kamati kuchunguza nini hasa kilitokea.

Miezi ikapita Januari 2022 ripoti ikatoka ikieleza kinaga ubaga kuwa sheria za ‘lockdown’ zilivunjwa kwenye ‘party’ ya mwezi mei 2020. BJ akajitokeza kukiri kuwani kweli alienda kwenye ‘party’ na kuomba radhi.

Iliposambaa ile video ya mkuu wa kitengo cha habari BJ aliunda chombo cha kuchunguza ambacho kilitoa ripoti mwezi mei 2022 ambayo ilieleza kuwa Watu walilewa sana kwenye ‘party’ hiyo na wengine walifanya vitendo vya dharau kwa wafanyakazi za usafi na ulinzi jengoni hapo.

ATHARI ZA SKENDO
Baada ya mambo kuwa dhahiri BJ akapoteza uungwaji wa wananchi wengi, Wabunge wa Upinzani na chama chake wakataka ajiuzulu. Wakafikia kupiga kura ya kutokuwa na Imani nae, BJ akashinda kura hiyo.

Lakini tarehe 7 Julai 2022 BJ akatangaza kujiuzulu nafasi ya Kiongozi wa chama chake cha ‘Conservative’ na Uwaziri Mkuu, lakini ataendelea kuwa Waziri Mkuu mpaka atakapopatikana mrithi wake.

KILICHOFUATA
Basi chama chenye serikali kiliendesha mchakato wa kupiga kura kumchagua Kiongozi mpya wa chama hicho, ambaye moja kwa moja ndiye atakaekuwa Waziri Mkuu mpya wa Uingereza.

Mchakato ulimalizika kwa Bi. Liz Truss kushinda nafasi hiyo na 6.09.2022 alienda Scotland kwenye kasri la Balmoral alipokuwa Malkia Elizabeth II kuagizwa kuunda serikali, Maana Malkia ndiye humtafuta mtu wa kuunda Serikali .

KWAHIYO WAZIRI MKUU ANAPATIKANAJE?
Malkia ndiye anateua Waziri Mkuu, na moja ya sifa za mtu huyo ni awe na wafuasi wengi Bungeni, kwa kesi hii mtu toka chama cha Conservative ndiye mwenye wafuasi wengi Bungeni. Hivyo Mchakato wa wanachama 160,000 wa ‘Conservative’ kupiga kura kumchagua Kiongozi wao mpya ndiyo kumechagua Waziri Mkuu mpya wa Uingereza yenye watu Milioni 67.


View attachment 2348993
Mkuu naomba nikuweke sawa kidogo kwenye hoja yako kuhusu mambo mawili.

1. Waziri mkuu wa Uingereza huchaguliwa na wananchi kupitia chama chake ambapo kikishinda uchaguzi na kuwa na idadi kubwa ya wabunge, kiongozi wake ndie huja kuwa waziri mkuu.

Hivyo basi, wananchi wa nchi hiyo huchagua waziri mkuu kupitia chama chake.

Ikitokea waziri mkuu anajiuzulu nafasi hiyo basi chama hufanya mchakato wa kutafuta kiongozi mwingine ambae akipitishwa huja kuwa kiongozi na pia waziri mkuu.

Moja ya mamlaka ya waziri mkuu ni kuitisha uchaguzi wa haraka ambao huitwa "snap election" ili kutafuta wingi zaidi wa wabunge ambao utamsaidia kupoitisha ajenda kadhaa bila kusumbuliwa. Hatua hii ni ina madhara kwani yahitaji waziri mkuu kuwa na uhakika wa asilimia 100 kuwa atashinda.

Boris Johnson alifanya hivyo mwaka 2019 na akashinda uchaguzi kwa kishindo na kuwa na idadi kubwa ya wabunge na kwa kuwa yeye ni bingwa wa ushawishi alikonga nyoyo za waingereza wengi.

2. Malkia wa Uingereza hachagui waziri mkuu bali humuidhinisha rasmi baada ya chama chake kushinda uchaguzi na kumruhusu kuunda baraza lake la mawaziri. Pia Malkia ni lazima aidhinishe kujiuzulu kwa waziri mkuu ikiwa kiongozi huyo amelazimika kujiuzulu.

Na mwisho ni kwamba Malkia hajishughulishi na aina yoyote ya siasa za nchi hiyo na hata akisema kitu fulani (kuhusu siasa) basi Buckingham Palace huombwa kutoa ufafanuzi ili kuondoa dhana kwamba ana ushawishi juu ya mada fulani.
 
Mkuu naomba nikuweke sawa kidogo kwenye hoja yako kuhusu mambo mawili.

1. Waziri mkuu wa Uingereza huchaguliwa na wananchi kupitia chama chake ambapo kikishinda uchaguzi na kuwa na idadi kubwa ya wabunge, kiongozi wake ndie huja kuwa waziri mkuu.

Hivyo basi, wananchi wa nchi hiyo huchagua waziri mkuu kupitia chama chake.

Si kweli, Kwenye Uchaguzi mkuu ambao huitwa kila baada ya miaka 5 Wananchi hupiga kura ya kumchagua Mbunge wa eneo lake tu.

Wabunge wakishaenda Bungeni hupatikana chama chenye Wabunge wengi, kisha mtukufu Malkia humteua/‘appoint’/humualika Mbunge mmoja toka chama chenye Wabunge wengi kuunda serikali, hapa huwa ni Kiongozi wa chama hicho. Kwa mtiririko huo Waingereza wao humchagua Mbunge tu. Waziri Mkuu hutokana na Chama chenye Wabunge wengi ambaye huwa ‘appointed’ na Mtukufu Malkia kama sehemu ya mamlaka yake.

Na pia tovuti ya Bunge la Uingereza umeweka wazi nini hutokea wakati wa Uchaguzi mkuu.


Ikitokea waziri mkuu anajiuzulu nafasi hiyo basi chama hufanya mchakato wa kutafuta kiongozi mwingine ambae akipitishwa huja kuwa kiongozi na pia waziri mkuu.

Naam, ni kweli kabisa.


Moja ya mamlaka ya waziri mkuu ni kuitisha uchaguzi wa haraka ambao huitwa "snap election" ili kutafuta wingi zaidi wa wabunge ambao utamsaidia kupoitisha ajenda kadhaa bila kusumbuliwa. Hatua hii ni ina madhara kwani yahitaji waziri mkuu kuwa na uhakika wa asilimia 100 kuwa atashinda.

Boris Johnson alifanya hivyo mwaka 2019 na akashinda uchaguzi kwa kishindo na kuwa na idadi kubwa ya wabunge na kwa kuwa yeye ni bingwa wa ushawishi alikonga nyoyo za waingereza wengi.

Kweli kabisa.

2. Malkia wa Uingereza hachagui waziri mkuu bali humuidhinisha rasmi baada ya chama chake kushinda uchaguzi na kumruhusu kuunda baraza lake la mawaziri. Pia Malkia ni lazima aidhinishe kujiuzulu kwa waziri mkuu ikiwa kiongozi huyo amelazimika kujiuzulu.

Nadhani tunapishana lugha tu, kiprotokali Baada ya Uchaguzi mkuu Malkia humwita Kiongozi wa chama chenye Wabunge wengi na kumuagiza/kumuomba kuunda serikali, hapo ndipo anateuliwa kuwa Waziri Mkuu.

Ama kwa maneno mengine ni kwamba, Malkia ndiye mwenye mamlaka ya kuteua Waziri Mkuu, lakini uteuzi huo haufanyi kwa utashi wake, ila huongozwa kufanya hivyo kwa kufuata vigezo na moja ya kigezo hiko ni mtu huyo atakayemteua ni lazima awe na wafuasi wengi Bungeni.

Na mwisho ni kwamba Malkia hajishughulishi na aina yoyote ya siasa za nchi hiyo na hata akisema kitu fulani (kuhusu siasa) basi Buckingham Palace huombwa kutoa ufafanuzi ili kuondoa dhana kwamba ana ushawishi juu ya mada fulani.

Ni sahihi kabisa kwa maana Malkia anapaswa kuwa nembo ya Muungano kitaifa hivyo hajihusishi na mivutank yeyote ya kisiasa.
 
Si kweli, Kwenye Uchaguzi mkuu ambao huitwa kila baada ya miaka 5 Wananchi hupiga kura ya kumchagua Mbunge wa eneo lake tu.

Wabunge wakishaenda Bungeni hupatikana chama chenye Wabunge wengi, kisha mtukufu Malkia humteua/‘appoint’/humualika Mbunge mmoja toka chama chenye Wabunge wengi kuunda serikali, hapa huwa ni Kiongozi wa chama hicho. Kwa mtiririko huo Waingereza wao humchagua Mbunge tu. Waziri Mkuu hutokana na Chama chenye Wabunge wengi ambaye huwa ‘appointed’ na Mtukufu Malkia kama sehemu ya mamlaka yake.

Na pia tovuti ya Bunge la Uingereza umeweka wazi nini hutokea wakati wa Uchaguzi mkuu.




Naam, ni kweli kabisa.




Kweli kabisa.



Nadhani tunapishana lugha tu, kiprotokali Baada ya Uchaguzi mkuu Malkia humwita Kiongozi wa chama chenye Wabunge wengi na kumuagiza/kumuomba kuunda serikali, hapo ndipo anateuliwa kuwa Waziri Mkuu.

Ama kwa maneno mengine ni kwamba, Malkia ndiye mwenye mamlaka ya kuteua Waziri Mkuu, lakini uteuzi huo haufanyi kwa utashi wake, ila huongozwa kufanya hivyo kwa kufuata vigezo na moja ya kigezo hiko ni mtu huyo atakayemteua ni lazima awe na wafuasi wengi Bungeni.



Ni sahihi kabisa kwa maana Malkia anapaswa kuwa nembo ya Muungano kitaifa hivyo hajihusishi na mivutank yeyote ya kisiasa.
Mkuu, mimi nimeishi Uingereza (kama miaka 3 na ushei hivi)na nimepiga kura nikiwa raia wa Jumuiya ya Madola.

Raia wa Jumuiya hiyo wanaruhusiwa kupiga kura.

Hivyo ni jambo la hekima kunifahamu.

Pale wapiga kura yako, mbunge unaemchagua ndiyo wakichagua chama chake kwenda bungeni.

Chama chenye wabunge wengi walochaguliwa ndicho hushinda uchaguzi.

Wao watumia mfumo wa "First Past The Post" yaani mwenye wingi wa kura ndio mshindi hata kama mgombea apata chini ya asilimia 50 jambo linoweza kutokea iwapo kuna wagombea wawili maarufu. Mfumo huu huvisaidia vyama ambavyo vina wafuasi wengi katika maeneo makubwa.

Kwa mfano chama cha wahafidhina uchaguzi wa 2019 kilishinda kwa kura nyingi maeneo ya katikati ya nchi (Midlands) na kaskazini, kwasababu wazungu wengi wasopenda wageni nchini humo walipenda Boris Johnson awe waziri mkuu ili tu kutimiliza ajenda yao ya Brexit yaani kutoka kwenye Umoja wa Ulaya.

Hivyo Boris Johnson akaenda kupata wabunge wengi Bungeni yaani "majority" na mambo mengi yakapitishwa bungeni kwa kuzingatia kuwa yeye ana dhamana (mandate) alopewa na wananchi.
 
Mkuu, mimi nimeishi Uingereza (kama miaka 3 na ushei hivi)na nimepiga kura nikiwa raia wa Jumuiya ya Madola.

Raia wa Jumuiya hiyo wanaruhusiwa kupiga kura.

Hivyo ni jambo la hekima kunifahamu.

Pale wapiga kura yako, mbunge unaemchagua ndiyo wakichagua chama chake kwenda bungeni.

Chama chenye wabunge wengi walochaguliwa ndicho hushinda uchaguzi.

Wao watumia mfumo wa "First Past The Post" yaani mwenye wingi wa kura ndio mshindi hata kama mgombea apata chini ya asilimia 50 jambo linoweza kutokea iwapo kuna wagombea wawili maarufu. Mfumo huu huvisaidia vyama ambavyo vina wafuasi wengi katika maeneo makubwa.

Kwa mfano chama cha wahafidhina uchaguzi wa 2019 kilishinda kwa kura nyingi maeneo ya katikati ya nchi (Midlands) na kaskazini, kwasababu wazungu wengi wasopenda wageni nchini humo walipenda Boris Johnson awe waziri mkuu ili tu kutimiliza ajenda yao ya Brexit yaani kutoka kwenye Umoja wa Ulaya.

Hivyo Boris Johnson akaenda kupata wabunge wengi Bungeni yaani "majority" na mambo mengi yakapitishwa bungeni kwa kuzingatia kuwa yeye ana dhamana (mandate) alopewa na wananchi.
Nashukuru kufahamu, vipi maisha kule Uingereza? Natamani kuzuru siku moja.

Ila kama nilivyosema, tunapishana lugha tu,
Ila ngoja twende sawa, kwenye ‘Ballot paper’ kuna chaguzi ya kumchagua Waziri mkuu kama ilivyo huku kwetu kwa upande wa rais?
 
Nashukuru kufahamu, vipi maisha kule Uingereza? Natamani kuzuru siku moja.

Ila kama nilivyosema, tunapishana lugha tu,
Ila ngoja twende sawa, kwenye ‘Ballot paper’ kuna chaguzi ya kumchagua Waziri mkuu kama ilivyo huku kwetu kwa upande wa rais?
Maisha ya pale UK ni magumu kama hujajiandaa kwa maana ya aina ya ukaazi wako.

Lakini kama uko poa kifedha na kikazi waweza kwenda pale kutembea. Waweza jiandaa kwenda kushuhudia uchaguzi unokuja.

Ila Uingereza kwenye uchaguzi huwekwa wagombea wa vyama na utaratibu ni kuchagua wabunge ambao ndo huenda bungeni na kura hiyohiyo huchagua waziri mkuu.
 
Ile nchi ya kipuuzi sana familia iyo moja tokea mwaka 1066 inatawala tuu nchi mpaka leo alafu wao wamekalia kuzisema royal family nyingine kwamba hazina Democrasia na wakati wao pia hawana democrasia...
Vip mifumo ya nchi Yao ni kama ya kwetu? Au Iko imara sana
 
Hata Mimi namshangaa. Skendo ya kuwa mtoa habari wa Russia ndiyo iliyomvuruga zaidi na kuonekana hafai hata ndani ya chama chake
Jamaa Wana mifumo imara sana ya taasisi zake.

Wananchi wake wanajielewa sana. Ndo maana ukileta shida tu unaondolewa chapu. Hawataki upuuzi. Angalia upuuzi unafanywa na viongozi wetu. Wao ni miungu watu na Wala hawahitaji kukosolewa kama aliyeondoka
 
Jamaa Wana mifumo imara sana ya taasisi zake.

Wananchi wake wanajielewa sana. Ndo maana ukileta shida tu unaondolewa chapu. Hawataki upuuzi. Angalia upuuzi unafanywa na viongozi wetu. Wao ni miungu watu na Wala hawahitaji kukosolewa kama aliyeondoka
Yaani uko sawa asilimia 101.
 
Mkuu naomba nikuweke sawa kidogo kwenye hoja yako kuhusu mambo mawili.

1. Waziri mkuu wa Uingereza huchaguliwa na wananchi kupitia chama chake ambapo kikishinda uchaguzi na kuwa na idadi kubwa ya wabunge, kiongozi wake ndie huja kuwa waziri mkuu.

Hivyo basi, wananchi wa nchi hiyo huchagua waziri mkuu kupitia chama chake.

Ikitokea waziri mkuu anajiuzulu nafasi hiyo basi chama hufanya mchakato wa kutafuta kiongozi mwingine ambae akipitishwa huja kuwa kiongozi na pia waziri mkuu.

Moja ya mamlaka ya waziri mkuu ni kuitisha uchaguzi wa haraka ambao huitwa "snap election" ili kutafuta wingi zaidi wa wabunge ambao utamsaidia kupoitisha ajenda kadhaa bila kusumbuliwa. Hatua hii ni ina madhara kwani yahitaji waziri mkuu kuwa na uhakika wa asilimia 100 kuwa atashinda.

Boris Johnson alifanya hivyo mwaka 2019 na akashinda uchaguzi kwa kishindo na kuwa na idadi kubwa ya wabunge na kwa kuwa yeye ni bingwa wa ushawishi alikonga nyoyo za waingereza wengi.

2. Malkia wa Uingereza hachagui waziri mkuu bali humuidhinisha rasmi baada ya chama chake kushinda uchaguzi na kumruhusu kuunda baraza lake la mawaziri. Pia Malkia ni lazima aidhinishe kujiuzulu kwa waziri mkuu ikiwa kiongozi huyo amelazimika kujiuzulu.

Na mwisho ni kwamba Malkia hajishughulishi na aina yoyote ya siasa za nchi hiyo na hata akisema kitu fulani (kuhusu siasa) basi Buckingham Palace huombwa kutoa ufafanuzi ili kuondoa dhana kwamba ana ushawishi juu ya mada fulani.
Sasa malikia kazi zake hasa ni zipi ndani ya taifa?
 
Ile nchi ya kipuuzi sana familia iyo moja tokea mwaka 1066 inatawala tuu nchi mpaka leo alafu wao wamekalia kuzisema royal family nyingine kwamba hazina Democrasia na wakati wao pia hawana democrasia...

Hili jambo tutaliangaziq siku moja.
 
Maisha ya pale UK ni magumu kama hujajiandaa kwa maana ya aina ya ukaazi wako.

Lakini kama uko poa kifedha na kikazi waweza kwenda pale kutembea. Waweza jiandaa kwenda kushuhudia uchaguzi unokuja.

Ila Uingereza kwenye uchaguzi huwekwa wagombea wa vyama na utaratibu ni kuchagua wabunge ambao ndo huenda bungeni na kura hiyohiyo huchagua waziri mkuu.

Oh sawa sawa.
 
Rudi shule ujifunze topic ya democracy ipo form two na uielewe vizuri. Ni kwamba kuna aina tatu za democracy ambazo zinadetermine nguvu za viongozi wa nchi husika. Ya kwanza inaitwa representative democracy kwa kiswahili ni demokrasia ya uwakilishi ambapo wanachi jukumu lao ni kwachagua wawakili wao kwenye vyombo maamuzi na hao wawakilishi ndo wanachagua mkuu wa serikali mfano wa hizo serikali ndo kama Uingereza n.k Uingereza waziri mkuu. Aina ya pili ni Presidential democracy ambapo katika aina hii wanachi wanapiga kura kwa kumchagua raisi na wawakilishi. Hivyo kwenye hiyo serikali Raisi ndo mkuu wa serikali na mkuu wa nchi, hakuna mambo ya waziri mkuu, mfano wa hizi serikali ni kama U.S.A, Kenya n.k. Aina ya tatu na ya mwisho ndo inaitwa mixed democracy ambapo wanachi wanapiga kura kumchagua raisi na wawakilishi, baadae raisi anapendekeza waziri mkuu na wawakilishi wana haki ya kumpitisha au kumkataa mfano ni Tanzania. Kwahiyo hapo kila nchi inachagua ni aina gani inatumia.

Andiko langu nimelipa jina ‘Ajabu ya uteuzi wa waziri mkuu wa Uingereza’ .

Hakuna pahali nimesema SIO YA KIDEMOKRASIA.

Tafadhali soma tena kisha karibu kwa mjadala juu ya upatikanaji wake, kama unaona nimekosea kueleza ama kufafanua karibu kukosoa.

Halafu wakati mwingine tujadili AINA YA DEMOKRASIA mada unayoonekana unapenda sana kuijadili.

Karibu Mkuu.
 
Ile nchi ya kipuuzi sana familia iyo moja tokea mwaka 1066 inatawala tuu nchi mpaka leo alafu wao wamekalia kuzisema royal family nyingine kwamba hazina Democrasia na wakati wao pia hawana democrasia...
Wao wqnajiheshimu na kuheshimu wenhine,sisi tunajiina miungu watu
 
Back
Top Bottom