Tetesi: Ajali Lucky Vincent School: Uzembe, Tamaa, Ubadhirifu na Kutokujali Usalama wa Wanafunzi

Tetesi: Ajali Lucky Vincent School: Uzembe, Tamaa, Ubadhirifu na Kutokujali Usalama wa Wanafunzi

231ec751a0ee037267cb0fc4876d9432.jpg
b076608e3a5bafde5e094c077583137a.jpg
Magari mazuri sana.
Naipongeza hii shule.
Lakini magari haya pia yanaweza kupata ajali mbaya siku moja.
Tuwe makini, tutimize wajibu ipasavyo na tumuombe Mungu.
 
Mkuu kwa haraka basi lile siyo basi la shule Ile sababu mabasi yao ni mawili Na daladala lile lilikodishwa asubuhi sana kwa akili ya safari hiyo Na dereva hajawahi kuendelsha gari bara bara ya karatu ambayo inakona na milima mikali pia gari ilikuwa Na tatizo la brake system na stearing ilikuwa Na shida iliyopelekea kushindwa kupiga gari ukutani wala kukamata brake hata za ghafla Na gari kupaa hadi kutua chini
ulishawahi kuwa dereva mkuu
 
Kwanza kabisa nianze kwa kutoa pole kwa Familia zote zilizokumbwa na huu Msiba mzito na mkubwa kabisa, pili nitoe pole zangu za dhati kabisa kwa Wana Arusha wote bila kumsahau Mkuu wao wa Mkoa Comrade Mrisho Gambo na mwisho kwa Watanzania wote kwa janga hilo lililotokea hapa nchini Kwetu Tanzania na tumuombe Mwenyezi Mungu azipokee roho na Watoto wetu wote, Walimu na Dereva wa gari lile la Shule ya Lucky Vicent aziweke mahala pema peponi Amin / Inshaallah.

Kwa mtazamo wangu binafsi naweza nikapingana na Mtoa mada juu ya baadhi ya lawama zake alizoziweka hapo juu japo nikiri wazi pia kuwa kuna mahala pengine amesema mambo ya wazi na ya kweli kabisa ambayo Mamlaka husika zinapaswa kuyachukua na kuyafanyia Kazi.

Najua kuwa wengi wetu tunaweza kumtupia lawama yule Dereva wa lile Basi ila niseme tu wazi kuwa ile ajali ya jana imetokea kwa BAHATI MBAYA sana na haina cha kumlaumu. Ukiona ajali yoyote ile inayohusisha Mabasi ya Abiria halafu hadi Dereva na zingine Dereva na Utingo / Kondakta wake nao ' wamekufa ' basi jua ya kwamba hiyo Gari hata Yeye ( Dereva ) ilimshinda na siyo ya kawaida.

Inasemekana kwamba sababu kubwa hadi iliyopelekea hiyo ajali ni kwamba Basi lilikuwa katika Spidi kiasi na siyo kubwa kama ambavyo tunaanza kupeana ' Sumu ' mitandaoni na kwamba Gari lilipofika katika huo Mlima kulitokea ' Ukungu ' mkubwa mno wa ghafla hali ambayo ulimchanganya Dereva kiasi cha kutaka kupunguza kidogo Spidi ili aende kwa ' tahadhari ' ndipo Gari lile ( Basi ) likaanza ' kuyumba ' huku likisaidiwa na ' utelezi ' uliokuwepo pale na ambao ulitokana na hali ya ' unyevu unyevu ' hali ambayo ilifanya Gari lile likose mwelekeo na kuanza kuyumba yumba hadi likaingia ' Korongoni ' pale na kusababisha yale ' mauti ' ya kutukuka ya Watoto wetu wapendwa, Walimu wao na Dereva.

Nadhani kwa maoni yangu kama tukisema tutupe lawama mahala fulani basi itapendeza sana kama tukizipeleka hizi lawama zetu kubwa kwa Mamlaka husika hasa Tanroads ya Mkoa wa Arusha na hata Serikali vile vile kwa kuweza ' kuzembea ' kuweka angalau ' Vizuizi ' vya pembeni ( Kingo ) ili kuweza kuepusha ' Ajali ' kama hii kwani hata ukiangalia tu ile sehemu ilipotokea ajali utaona ni barabara nzuri tu ila hapo katika bonde hakuna ' Kingo ' zozote hivyo ni rahisi mno kwa Gari lolote kutumbukia humo pindi pakitokea ' hitilafu ' yoyote.

Mwisho kabisa nimalizie tu kwa kusema kuwa kuanza kuwalaumu Walimu wa Shule au Mmiliki wa Shule au sijui Madereva wa wale Wanafunzi hakutosaidia kitu kwani wao kama wao walitimiza wajibu wao na bahati nzuri ni kwamba kumbe hii siyo mara ya Kwanza hao Watoto wanaenda kufanya hiyo mitihani ya ujirani mwema na kwamba ni mara ya tatu isipokuwa tu sisi kama Wanadamu tutambue kuwa kuna bahati mbaya maishani na siamini kabisa kama Walimu au Mmiliki wa Shule hiyo ya Lucky Vicent alipanga hili kutokea au hata amelifurahia.

Ni ajali tu ya bahati mbaya hivyo kikubwa tu kama Wanadamu kuanzia sasa tunatakiwa tuchukue tahadhari siyo tu hapo Karatu bali hata maeneo mengine ambapo tunajua kuna miundo mbinu mibovu au hali ya barabara siyo nzuri pindi pakiwa na mvua na hata Wahusika hasa TANROADS nao wanapashwa kuhakikisha kuwa sehemu zote hatarishi za barabara Kuu za Mabasi usalama wake hasa wa Kingo za bondeni umezingatiwa ili basi Tanzania isije ikapata tena ' Mkasa ' mkubwa kama huu.

Poleni sana Watanzania wote na GENTAMYCINE nipo nanyi katika ' majonzi ' katika kipindi hiki kigumu kabisa cha huu Msiba kikubwa tuwape ushirikiano mkubwa na wa hali na mali ' Wafiwa ' wote, tuwafariji na tuwaombee Mwenyezi Mungu awape moyo wa ' subira / uvumilivu ' mpaka pale tutakapowapumzisha ' Wapendwa ' wetu katika Nyumba zao za Milele na wala hakuna haja ya kuanza kuichukia Shule ya Lucky Vicent au kumchukia sijui Mwalimu Mkuu au Mmiliki wake kwani hili jambo lingeweza kutokea mahala popote pale na hata kumtokea Mtu yoyote yule.

Muinto Obrigado nyote na tupo pamoja.
Ninaungana nawe Gentamycine
Umeongea kwa busara sana.
Sidhani kuwa ajali hii imetokana na mwendo kasi uliopitiliza (maana walioshuhudia ajali na magari waliyoongozana wangeshasema)..au kubeba uzito mkubwa kuliko uwezo wa gari ukizingatia abiria wengi ni wanafunzi ambao kwa wastani wa uzito hawazidi 50kg.

Hii ni ajali mbaya na ni hulka ya binadam kutafuta pa kutupa lawama baada ya maafa.
Tujizuie sote. Tuomboleze kwa amani.
 
baada ya msiba tunaomba Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi wa kina na litoe taarifa juu ya chanzo na sababu ya ajali hii mbaya!!
 
Mkuu kwa haraka basi lile siyo basi la shule Ile sababu mabasi yao ni mawili Na daladala lile lilikodishwa asubuhi sana kwa akili ya safari hiyo Na dereva hajawahi kuendelsha gari bara bara ya karatu ambayo inakona na milima mikali pia gari ilikuwa Na tatizo la brake system na stearing ilikuwa Na shida iliyopelekea kushindwa kupiga gari ukutani wala kukamata brake hata za ghafla Na gari kupaa hadi kutua chini
90449aafb608d9a5c8e3dae8e90c7460.jpg
 
Pale ilipojipigiza nyuma yake kuna mti mkubwa tu lakini basi ilipaa juu ya huu mti na kutua mbele yake.
 
Kwa kiasi flani yaweza kuwa kweli juu ya utunzaji wa kumbukumbu za service lakini kwa uzi wako mzima si lazima ikawa hivyo. Zipo sababu nyingi za kiufundi na kimazingira ambazo zinaweza kusababisha ajali. Kwa muda mwingine ajali haingalii umefanya service leo au jana, mazingira husika yanaweza kukufanya pia ukapata ajali. Cha msingi kila mtu atimize wajibu wake japo kila mtu atakufa kwa muda wake na style yake.
 
Imetokea,tunahitaji kujifunza hakuna haja ya kutuhumu watu....R.I.P
 
Wazazi poleni kwa msiba huu uliowapata watoto wetu wapendwa wa Lucky Vicent na walimu wao! Hakika ni majonzi makubwa sana! Lakini yafaa tutafakari kwa kina kwanini janga kama hili liwafike watoto hawa, tumaini la maisha yetu! Maswali ni mengi, na kwa kweli yana hitaji majibu ya kina.

Kwa tunaozunguka kutwa barabarani, mtakubaliana na mimi kuwa, vipo viashiria vingi hatarishi kwa watoto wetu wanapotumia mabasi ya shule zao. Shule nyingi zinatumia mabasi ambayo zamani yalitumika kama daladala, na baada ya kuchoka yakabadilishwa na kuwa mabasi ya shule. Huku madereva wakiendesha kwa mwendo usiostahili kabisa kubeba watoto.

Hatari zaidi, mabasi haya ya shule hubeba idadi kubwa ya wanafunzi kuzidi uwezo halisi wa gari, na kutokuzingatia taratibu zote za kiusalama kama vile kufunga mikanda. Mfano wa hili ni hii ajari ya Lucky Vicent. Wanasema "eti gari lili feli breki" ndo sababu ya ajari! Binafsi sikubaliani nalo.

Kwa wale ambao wameendesha magari makubwa kwa weledi na kwa kipindi kirefu, watakubaliana na mimi kuwa, kubeba uzito zaidi ya uwezo wa gari pamoja na mwendo kasi husababisha mfumo wa breki za gari kushidwa kuhimili, hivyo kutokukamata pale dereva anapozitumia.

Sababu nyingine ya kujiuliza, je ni kweli haya mabasi ya shule yanafanyiwa matengenezo na ukaguzi wa mara kwa mara, kwa maana ya motor vehicle service! Hapa inatiashaka! *A motor vehicle service is a series of maintenance procedures carried out at a set time interval or after the vehicle has travelled a certain distance.* Shule ya Lucky Vicent lazima ithibitishe kwa kuonyesha *service na log books* za hilo gari, majibu utayaona, hakuna kumbukumbu ya service.*The completed services are usually recorded in a service book which is rubber stamped by the service centre upon completion of each service.* Mashule mengi yanahuo udhaifu, na hii inatokana na uzembe, tamaa, ubadhirifu wa watendaji wao, kutokujali maisha ya wanafunzi na kutokuwa waangalifu huku wakiweka mbele masilahi yao na kupata faida.

Matengenezo muhimu na ya mara kwa mara kwa gari *motor vehicle service* ni kama ifuatavyo;
-Change the engine oil & oil filter
-Replace the air filter & fuel filter
-Tune the engine
-Check level & refill brake fluid/clutch fluid
-Check Brake Pads/Liners, Brake Discs/Drums, and replace if worn out.
-Check level and refill power steering fluid
-Refill Manual Transmission Fluid,Grease and lubricate components inspect.
-Check condition of the tires
-Check for proper operation of all lights, wipers etc.

Vipuri vingine vyote vinavyo weza kulifanya gari lisiwe salama kwa matumizi ya barabara hukaguliwa na kubadilishwa wakati wa kufany *service* je mashule yetu wanafanya haya! Kama haya hayafanyiki ni wakati sasa wazazi wa watu wote wenye matashi mema kuchukua hatua za kuwawajibisha wahusika wote ili kuokoa maisha ya watoto wasio na hatia.

Gereji yako iko wapi mkuu
 
Hivi mwili wa dereva ulitambuliwa na kufanyiwa uchunguzi kujua kuwa alilewa au la? Sijui kuna utaratibu gani wa kiuchinguzi unaofanyika kujua hasa chanzo cha ajali ili ikiwezekana tahadhari zichukuliwe siku za usoni.
 
Ni kweli wamiliki wanaangalia faida kuliko usalama wa wateja wao
Ajali hii imenikumbusha Mwaka 74 kabla ya tv na internet huko Arusha ilitokea ajali pale Usa River ikaua watu 70. Walikuwa kwenye bus la kampuni ya TTBS. Watu wakapachika magari hayo Twende Tukafe Bila Sababu. Ulikuwa ni msiba wa kitaifa. RIP Our Little Angels. Sikumbuki vema jinsi serikali ilivyohandle huo msiba nilikuwa bado ufahamu si sana.
 
Back
Top Bottom