Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Nashauri magari yote ya abiria yafungwe tracking systém halafu yawe monitored kwenye speed, ajali nyingi ni mwendo kasi, ndo maana magari huwa yanachanika kama makaratasi.
 
Kwanza kama Mwananchi na mdau wa usafiri ninaumizwa sana na hizi ajali ambazo zinaendelea kuchukua uhai wa ndugu, jamaa na marafiki huku zikiacha wengi wakiwa na ulemavu.

Mkuu wa kitengo cha Usalama barabarani jana ametoa kauli ya kutoa matumaini sana kwa watanzania.

Kwa uzoefu uliopo ajali nyingi zinatokana na madereva wasio na elimu na kazi waifanyayo na kukosekana mikataba ya kazi na si mwendo kasi kama tunavyoamini sasa.
Mpinga ametangaza kuanzia jumatatu kila dereva atembee na cheti chake kilichomwezesha kupata leseni ya udereva kwa ajili ya ukaguzi.

Tuwe wakweli na wawazi madereva wengi wa haya magari ya abiria hawana sifa ya kuendesha hayo magari ila wanalindwa na askari wa Usalama barabarani hatimae kusababisha ajali na vifo.

Magari yanayokimbia sana yanajulikana, lakini ni nadra sana kusikia hizo bus kupata ajali Sababu madereva wanaelewa jukumu lao wakiwa barabarani.

Mwisho niombe tu wote kwa pamoja tushirikiane kuwafichua madereva wanaotumia vilevi njiani.

Kutembea na vyetu haitoshi ndugu yangu, ikiwa leseni zenyewe wanapata kwa rushwa, nchi za wenzetu mpaka wakupe leseni ujue umefaulu kweli na hata mwenyewe utajisikia raha ukiipata na ukileta uzembe unanyang'anywa, kuja kuipata tena ni lazima uende shule tena kwa kipindi kirefu sana.
 
Hapana ni ubabaishaji wetu sisi wa tz lazima tubadilike,yaani sisi ni wa kimya sana sijui ndio 'amani' au nini,utakuta mtu kapakiwa kwenye bodaboda dereva anaendesha kwa spidi anayotaka mtu kakaa tu nyuma kimya kama mzigo hii tunaiona kila siku,kwenye mabasi ni hivyohivyo spidi ya ajabu overtake bila mpangilio baada ya ajari majeruhi utawasikia ooohh dereva alikuwa amelewa sijui spidi ilikuwa kali nk,kwenye daladala pia konda anatuambia gari bado kujaa inayojaa ni chupa tunashindiliwa kama nyanya,Basi kutoka Dar kwenda Mwanza linatakiwa lifike saa tano lakini mengine yanaingia mpaka saa tatu dereva anasifiwa na kupewa sifa nyingi,ubabaishaji huu hapo Kenya tu hauwezi kuuona.
 
nadhani kwa hili hata taasisi zinazotoa mafunzo ya udereva zikaguliwe upya
 
Hii ndio bongo bana hizo ni mbwembwe tu kama zile za speed gavana,mwisho wa siku tunaludi kwenye maisha yetu ya kimazoea.
 
Hiyo ni long term plan Mkuu, wanasiasa kwenye ilani za vyama vyao watakua nazo hizo..ila sasa itachukua 25 years ku implement hilo kwa viongozi wetu.Ngoja tujadili kinachowezekana sasa maana Vifo kila kukicha vinatokea wala havisubiri hizo barabara pana,treni za kisasa,ndege na Meli.
Khaa!! ™©[® Basi tuendelee kufa tu kama kuku kama tunawategemea wanasiasa waje watuletee hali nzuri
Mimi nimauhakika hawatakuja
 
Mkuu umejaribu kueleza maoni yako kwa ufasaha ukimaanisha kua ndio dawa ya kutokomeza kabisa hili janga sugu la ajali za barabarani.Naomba unijibu maswali haya ili nijue kua umewaza mbali! 1.Je, kwanini nchi nyingi zilizoedelea huwezi kusikia ajali za magari zaidi ya matetemeko ya ardhi, moto,vimbunga, mafriko n.k? 2.Je,Mamlaka husika hutafuta angalao ushuari toka nchi zilizoendelea ili kulinusuru taifa na hili janga? 3 Kama wamepewa ushauri impact yake iko wapi? 4.Je, kama kuna taasisi zimelifanyia hili suala utafiti wa kutosha report ni kwa manufaa gani? 5.Je,nani alaumiwe?6.Ivi ni kwanin Tz imeshafikia sasa mtu ukisafiri usala wa maisha yako unakua"Fifty fifty"?
 
Mkuu umejaribu kueleza maoni yako kwa ufasaha ukimaanisha kua ndio dawa ya kutokomeza kabisa hili janga sugu la ajali za barabarani.Naomba unijibu maswali haya ili nijue kua umewaza mbali! 1.Je, kwanini nchi nyingi zilizoedelea huwezi kusikia ajali za magari zaidi ya matetemeko ya ardhi, moto,vimbunga, mafriko n.k? 2.Je,Mamlaka husika hutafuta angalao ushuari toka nchi zilizoendelea ili kulinusuru taifa na hili janga? 3 Kama wamepewa ushauri impact yake iko wapi? 4.Je, kama kuna taasisi zimelifanyia hili suala utafiti wa kutosha report ni kwa manufaa gani? 5.Je,nani alaumiwe?6.Ivi ni kwanin Tz imeshafikia sasa mtu ukisafiri usala wa maisha yako unakua"Fifty fifty"?

Unapozungumzia nchi zilizoendelea ina imply vitu vingi sana kwanza vyombo vyao vya usafiri ni bora na salama kuliko vyetu, Mianya ya rushwa ni kidogo ukilinganisha na sisi hivyo si rahisi kumuhonga traffic hata kama gari lako lina makosa,Mamlaka zinazosimamia masuala ya usafiri ni makini na zinachukua hatua kuliko sisi ...yaani huwezi kukuta kiongozi anamiliki chombo cha usafiri hivyo ni rahisi kwa mmiliki wa chombo cha usafiri kuchukuliwa hatua endapo ataenda kinyume,Barabara zao ni bora na salama zaidi kuliko sisi, madereva wao wanalipwa mishahara mizuri kuliko sisi na wala hawaokotwi tu mtaani kama ilivyo kwetu, et al., Mamlaka husika hata kama ikipata ushauri ni kazi bure mpaka nilichokisema hapo juu kizingatiwe..Wakulaumiwa hebu na wewe fikiria kwa makini kwa sababu nilizotoa hapo kisha utamjua ni nani anafaa kulaumiwa.
 
Hapo umesema kweli, lakini tujiulize nani wa kumshughulikia mwenzie, Labda kiundwe chombo kingine cha kuwachukulia hatua hawa askari.



Ni kweli nchi hii inahitaji tume huru kuanzia ngazi ya familia hadi taifa maana mizengwe imekithiri
 
ni kweli madereva wanachangia ajali ila kwa upande wa pili miundombinu yetu sio rafiki haimpi driver alternatives za kutosha anapokutana hali ya hatari.
barabara zikiboreshwa ajali zitapungua kwa kiac kikubwa mno.
 
Unapozungumzia nchi zilizoendelea ina imply vitu vingi sana kwanza vyombo vyao vya usafiri ni bora na salama kuliko vyetu, Mianya ya rushwa ni kidogo ukilinganisha na sisi hivyo si rahisi kumuhonga traffic hata kama gari lako lina makosa,Mamlaka zinazosimamia masuala ya usafiri ni makini na zinachukua hatua kuliko sisi ...yaani huwezi kukuta kiongozi anamiliki chombo cha usafiri hivyo ni rahisi kwa mmiliki wa chombo cha usafiri kuchukuliwa hatua endapo ataenda kinyume,Barabara zao ni bora na salama zaidi kuliko sisi, madereva wao wanalipwa mishahara mizuri kuliko sisi na wala hawaokotwi tu mtaani kama ilivyo kwetu, et al., Mamlaka husika hata kama ikipata ushauri ni kazi bure mpaka nilichokisema hapo juu kizingatiwe..Wakulaumiwa hebu na wewe fikiria kwa makini kwa sababu nilizotoa hapo kisha utamjua ni nani anafaa kulaumiwa.

Yeah umejibu vizuri sana mkuu! Lakini kwa nchi ilyojaa rasirimali kama yetu haya yote si yanawezekana? Tembelea nchi ndogo tu jiran ya Rwanda utazame systems zao ndo ujiulize hapa kwetu kunani?
 
Mkuu hata vianzishwe vyuo vikuu, kamausalama barabarani ni hawa hawa tunatwangamaji kwenye kinu. Kwanza hiki kikosi kivunjwe wawe askari wa kawaida watafutwe wenye woga wa Mungu kufanya hii kazi. Kamanda wa usalama barabarani aache siasa afanye kazi ya kiaskari. Leseni za udereva zisiwahusishe polisi kabisa!!!! Wafanye TRA kazi yote. Sina imani na trafic kwa kifupi.
 
Haswaa vyeti bila miundombinu imara ni bure
ni kweli madereva wanachangia ajali ila kwa upande wa pili miundombinu yetu sio rafiki haimpi driver alternatives za kutosha anapokutana hali ya hatari.
barabara zikiboreshwa ajali zitapungua kwa kiac kikubwa mno.
 
serikali ilitumia kodi zetu nyingi kujenga mkonga wa taifa wa internet lakini bado haujatusaidia sana. Tuutumie huu mfumo kufunga camera barabarani kama zifanyavyo nchi zilizoendelea. Hii manpower ya kikosi cha usalama barabarani kutwa kushinda barabarani ingetumika kushinda kwenye computer na ku-monitor madereva wasiotii sheria za barabarani
 
serikali ilitumia kodi zetu nyingi kujenga mkongo wa taifa wa internet lakini bado haujatusaidia sana. Tuutumie huu mfumo kufunga camera barabarani kama zifanyavyo nchi zilizoendelea. Hii manpower ya kikosi cha usalama barabarani kutwa kushinda barabarani ingetumika kushinda kwenye computer na ku-monitor madereva wasiotii sheria za barabarani

Nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa.
Lkn pia kama inawezekana kutazama upya mfumo wa udhibiti wa magari ya abiria thru technolojia internet kuputia mkonga wa taifa wa nawasikiano kwa mabasi yote yafungwe kifaa maalum ambacho kitakuwa linked na saver za mamlaka husika let say SUMATRA na backup iwe pengine wizarani. Mfumo uwe automated kiasi cha kureport overspeed, kiasi cha abiria na kila kitu kitakachomfanya dereva awe anajua yupo monitored all the time.

Na ikitokea amevunja taratibu basi system ina alert in real time na hapo fine kubwa ambayo kabisa let say milioni 100 kwa kosa lolote la uvunjifu wa sheria.
 
Leo ndio jumatatu na imetokea ajali mbaya kuliko ya juzi. leo wamepoteza maisha watu 48
 
Kwanza kabisa nikupongeze kwa kuguswa na hili na kutuletea mada yanye tija kwa kila mmoja wetu,nategemea kuwaona watu mkiweka maoni yenu hapa kuliko kushabikia siasa zinazojadili watu badala ya mijadala yenye tija kama hii.

Naungana na yote uliyoyasema isipokuwa hilo la mabasi kusafiri na Askari.

Mawazo yangu ili kudhibiti ajali ni lazima kwanza kutambua vyanzo vya ajali,

pamoja na vyanzo kuwa vingi lkn mwendo kasi na uzembe wa madereva ndio chanzo kikuu cha ajali za barabarani.

Suluhisho ni kuwapangia muda madereva kufika kwenye vituo.

Mfano mabasi yaondoke Dar saa 12.00 alfajiri na yafike morogoro saa 4:00 yafike Dodoma saa 8:00,yafike manyoni saa 9:30,Singida Saa 11:00,Misigiri saa 12.30, Igunga saa 1:50,Nzega Saa 2:30 na hatimae kahama saa 4:00.


Masaa hayo yapangwe kitaalamu na watu wa sumatra baada ya kujiridhisha umbali toka eneo moja kwenda eneo jingine,

Kila kituo kiwe na askari ambao wapo serious na kuwepo na utaratibu kama ule wa treni wa kupewa line clear,hivyo mtu atachukua kibali maalum mahala anapoanzia safari kinachoonyesha muda na atapaswa kukabidhi kibali hicho kwenye kituo cha mbele na kupewa kingine kinachomruhusu kuendelea na safari,afanye hivyo mpaka mwisho wa safari yake,.

ili kuepusha usumbufu maeneo vinapotolewa vibali pawepo na vyoo pamoja na hotel za kula chakula,lengo ni kutumia mudaa wa kuonyesha kibali huku abiria wakiruhusiwa kuchimba dawa na kupata chakula,hivyo hakutakuwa na malalamiko,

Kama hilo halitoshi tunaweza kuyatumia maeneo mizani kama check point ya muda wa kuwasili eneo husika.

tukifanya hivi italeta self control ya madereva ,adhabu yake iwe kuahirishwa safari na abiria kuwekwa katika mabasi mengine kwa kibali maalum na dereva kuwekwa ndani mwezi mmoja na gari kufungiwa kusafirisha abiria kwa muda wa mwezi mmoja.


kama tutafanya hayo hakika hakuna dereva wala mmiliki wa gari atakaefika eneo husika kabla ya wakati.

Kufanya hivyo kutawafanya madereva kutembea mwendo wa kawaida na hivyi kupunguza ajali kwa kiwango kikubwa.

Pendekezo hili ni baada ya safari yangu toka Dodoma,gari ya kwanza kufika Dodoma ilikuwa campuni ya KISBO ikiduatiwa na Leina na CITY BOY.


Hizi ni basi zilizojizolea umaarufu kwa kukimbia kupita kiasi kiasi cha kufika kahama saa 12:30 badala ya saa tatu usiku.

Tulipofika manyoni walisimama petrol station na kutueleza abiria kuwa tunasubiri muda wa kufika Singida.

ilikuwa saa 7:20 za mchana na singida tulipaswa kuingia kuanzia saa 10.30 au zaidi ya hapo.

Hivyo tulilazimika kukaa muda wa saa moja na nusu ndipo tukaendelea na safari,


Gari zoote zilizotoka Dar zilikuwa kama msafara na hakuna aliethubutu kukimbia,waliogopa faini kubwa ambayo hutozwa singida endapo Gari itafika kabla ya muda uliopangwa.

Mwisho ni kwetu wapiga kura ambao ndio wahanga wa ajali hizi,tusiwachague tena wafanyabishara kuwa wabunge wetu,maana wengi wao hutumia fursa ya vyeo vyao kuwafanya hata askari Polisii wayaogope magari yao.
 
Sumatra haina meno...,Pengine ngoja tuone huyu mkurugenzi mkuu mpya MR GILIAD NGEWE aweza kuleta mabadiriko, maana namfahamu km mchapa kazi mzuri tu huko nyuma, ila kama naye atakumbatia utaratibu uliokuwepo hapo nyuma wakubebana bila kujali elimu katika kitendo husika ,Akasema kubebana km walivyojaa wachagga mle ,mambo hayataenda kabisa, nakumbuka wamewahi kutangaza kazi pale ya LICENCING OFFICER, shart awe na degree, ila aliyeajiliwa alikuwa na diploma tena na matokeo ya semista ya mwisho alikuwa hajapewa,watu tukahudhuria interview kumbe tiyar wana mtu wao.tena ana diploma .
 
Back
Top Bottom