Ajali Tanzania: Mawazo mbadala kuhusu udhibiti wa ajali Tanzania

Wanavyotofautisha leseni za abiria wanatakiwa pia kutofautisha adhabu. Ukiwa name class C basis ukifanya kiss hukumu take I we Mara mbili Saudi ya dreva wa kawaida. Hawezekani umebeba abiria halafu ufanye kosa huukumiwe sawa na mwenye Vitz.
Ni kweli mkuu...maana watazunguka kila kona kutafuta dawa ya ajali hazitoisha...kwa sababu zinasababishwa na madereva zaidi kuliko ubovu wa magari...adhabu kali zinaweza kuwatia adabu kiukweli
 

Jamani, hebu tuwe realistic tuache ndoto za alinacha. Hivi kweli nchi kama Tanzania unaweza kutengeneza barabara kama hii toka Dar hadi Kigoma au Tunduma? Hata nchi nyingi zilizoendelea hakuna kitu kama hicho, bali hizo zinakuwa barabara katika eneo la karibu na mjini, au ukanda wa kilometa 50 toka mji mkubwa.

Hata bondeni ambako wenzetu wameendelea, ukiangalia barabara zao kubwa mbili, N1 na N2, si kwamba N1 iko hivyo toka Johannesburg hadi Cape Town, na N2 iko hivyo toka Durban hadi Cape Town. N1 na N2 zinafanywa kuwa dual carriageway maeneo ya karibu na mijini tu, ukisha toka nje ya mji zinakuwa na kawaida single lane.
 
Hoja yangu ni, madereva wa mabasi wapimwe akili na matumizi ya madawa ya kulevya mf,bangi, pombe kituo hadi kituo. Pili, ukaguzi wa leseni na vyeti liwe ni zoezi la kudumu. Tatu, trafiki wanaokula rushwa waendelee kufukuzwa kazi, nne, wamiliki wa mabasi walazimishwe kutoa mkataba wa ajira kwa madereva wawili kwa kila gari.
 
Niambie kama kuna kipimo cha akili na kinapatikana wapi , na uniambie kinaitwa nini , kama tunavyofahamu ukitaka kupima joto unatumia thermometer sasa ukitaka kupima akili utatumia nini?
 
Tano, mabasi yafanyiwe ukaguzi na Sumatra/Askari, kabla ya kuanza safari
 
Naunga mkono hoja,nimeshtuka nimesoma kwenye gazeti Mwananchi la leo kuna habari inayosema na imethibitishwa na kamanda Mpinga kwamba kuanzia Juni/Agost mwaka huu ajali zimeuwa watu 1,078 na kujeruhi watu 3,715,yaani miezi mitatu ajali zinauwa na kujeruhi idadi hiyo je mwaka mzima watakufa wangapi???wakati mwengine abiria tunakuwa hatuna umoja,unakuta may be mpo safarini dereva haendeshi kwa usalama ukijaribu kumkanya abiria wenzako wanakukebehi utasikia "huyo ndo mara yake ya kwanza kupanda bus anasikilizia"wengine wanakwambia ww unaenda kwenu ssi tunawahi biashara zetu,ukipiga cm polisi akija konda anashuka wanaenda nyuma ya gari akirudi anagonga bodi bus linaondoka mwendo ni ule ule tena umezidi,Tanzania yetu omba kwa Mungu akufikishe kwa miujiza yake tu ila sheria zetu zimeingiliwa hazitulindi tena tuwapo barabarani.
 

Sababu ulizotaja sio mbaya ila hazijangatia mazingira halisi ya kitanzania kwa sababu hazitekelezeki katika muda mfupi. Kwangu mimi sababu kuu ya ajali hizi ni:

1. Madereva kutopata muda wa kutosha wa kupumzika. Hii huwafanya kukimbia sana ili kuokoa muda na kupata muda wa kutosha wa kupumzika.
2. Sheria kuzuia magari kutembea usiku. Kwa magari kutembea mchana tu, husababisha wear and tear kuwa kubwa. Pia muda wa service hautoshi kwa sababu ya muda. Mathalani Kwa gari linalofika Dar saa 4 au 6 usiku na kutakiwa kugeuka saa 12 asubuhi, ni wazi kuwa mafundi hawatapata muda wa kutosha wa kufanya service.

3. Mabasi mengi kuondoka kwa wakati mmoja.

SULUHISHO

Ili kuondoa tatizo hilo, ni kuondoa kikwazo cha magari kutembea kwa masaa 24 na kisha kuweka interval ya magari yanayoelekea sehemu moja kuondoka kila baada ya saa moja.
SULUHISHO
 
Cha Muhimu ni kurudisha nakuboresha zaidi usafiri wa reli uwe wa kisasa.Hii itapunguza utitiri wa mabasi barabarani..Nchi hii wameuwa reli ili vigogo wafanye biashara ya mabasi
 
Mabasi huwa yanakimbia sana , hii inasababisha impact kubwa inapotokea ajali, kuna kitu kinaitwa tracking system wangeanza na hiyo, mabasi yote yafungwe na yawe monitor kwa speed isizidi 80km/hr , mfano mzuri ofisini kwetu tulikuwa hatuna limit yani gari zilikuwa zinakimbizwa kama ndege ya chini mpaka jasho linakutoka, wameweka hii kitu mwendo ni 80km/hr tu unasafiri ukiwa na amani.
 
ishu kubwa kwangu naona magari yanayotembea zaidi ya masaa10 na kufika vituoni ama mwisho wa safari kuanzia saa4 usiku yasiruhusiwe kuendelea na safari kesho yake ili gari ifanyiwe service bora na si bora service.Siku moja niliwahi kuwa pale Nyegezi basi fulani iliingia saa6:30 usiku alafu saa10 ikawa stand tena inapakia kurudi dar ..kwa hari kama hii tunatarajia nini hili lije kufika tena ubungo saa3/4 usiku?
 
Cha Muhimu ni kurudisha nakuboresha zaidi usafiri wa reli uwe wa kisasa.Hii itapunguza utitiri wa mabasi barabarani..Nchi hii wameuwa reli ili vigogo wafanye biashara ya mabasi

Mkuu,tayari hapo kwenye red wewe mwenyewe unakiri kua usafiri wa reli umefanywa wa kusuasua maksudi ili wafanye biashara ya Mabasi ..sasa unafikiri wazo la kurudisha usafiri wa reli kwa sasa ni rahisi kama utatuzi wa haraka kunusuru hali mbaya ya ajali zinazoendelea??????
 
Nimetafakari sana namna watanzania tunavyoteketea kwa ajali za mabasi. Nimejiuliza maswali mengi nikakosa majibu. Labda wanaJF wenzangu mnaweza kushare nami. Mfano hivi upeo wa traffic police wetu unaishia tu kukagua driving licence, kadi ya Gari, honi, headlights, bima, road licence, uchakavu wa matairi tuu? Vipi mechanical wellbeing ya Gari? Vipi speed governors zilizogharimu watu hela nyingi? Tutakufa sana kwa upeo wa hawa maafande wetu.
 
Mimi nadhani hata tukiwajengea boarding school madereva wasome miaka mitano itakuwa solution. Hii issue ni uzembe zembe na kujiamini sana bila tija.

Hata wasomi wetu mambo ni haya mikataba mibovu wanaingia, Ma-doctor hivyo hivyo, wakandarasi wanajenga chini ya kiwango, Jamaa wa bodaboda fujo tu yani kila kona hakuna hafadhali. Labda tuweke double road kama walivyo shauri wengine.
 

Nafuwewe.
 
Kwa kuwa ajali za kutisha hasa za mabasi ya abiria zinazidi kuteketeza maisha ya Watanzania kuna haja jeshi la polisi baada ya mabadiliko ya sheria za barabarani litumie askari wake kuendesha magari haya ya abiria badala ya madereva wa kiraia wanaovunja sheria za barabarani kila siku hali inayosababisha kutokea ajali hizi kila siku.

Ninatumaini makamanda wa polisi wa kila mkoa wataweka utaratibu wa askari wao kuendesha mabasi haya ya abiria.Ni ukweli usiopingika iwapo askari wakitumika kuendesha mabasi ya abiria uwezekano wa kutokea ajali ni mdogo.Utaratibu huu uwekwe kwa magari ya njia ndefu na mwendo uwe kilometa 50 kwa saa.

Hivyo jeshi la polisi lifanye mazungumzo na wamiliki wa magari ili wawaachie jukumu la udereva wa mabasi yao ili kupunguza ajali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…