Ajali ya Dr. Mwakyembe na yatokanayo

Ajali ya Dr. Mwakyembe na yatokanayo

- Katika dunia ya kibepari kama tuliyonayo Tanzania sasa hivi, haya maneno ni ya kawaida sana na ni vyema sisi wananchi tukaji-tune na kuyakubali ili tuondokane na zile attitude za kijamaa jamaa, za kutambea na kandambili huku ni millionea kwa sababu ya kuogopa kuonekana unaringa na jamii,

- Yale mambo ya darasa la saba Mwenyekiti wa tawi la CCM kiwandani, kushindana na PhD yaani Director wa kiwanda na kuishia kuwa taifa la kwanza duniani kuwa na viwanda vya Sigara na Bia visivyoleta faida kwa taifa, sasa yameisha kama wewe ni bingwa wa fani yoyote ile, ubepari inataka useme tena sana au wazi bila kuficha kwa sababu under siasa ya ubepari tuliyonayo sasa hivi, huwezi jua opportunity ita-strike wapi na wakati gani,

- Bila majivuno ubepari hauwezi kushamiri, hakutakuwepo na competition katika biashara, hakutakua na competition katika siasa, tutaishia kurudi kule kule tulikotoka, kama ni majivuno basi hata mashindano ya uzuri wa kinadada zetu ni dhambi na majivuno kwani wanaoshindwa maana yake ni nini kama sio ugly? Je wewe uliowatoa kwenye mashindano unaweza kuwaumba ndio hizo mentality za kudai ukweli ni majivuno, hazina nafasi tena katika taifa letu,

Mwakyembe either ni bingwa sheria au sio, lakini ndio anayo haki zote kujitangaza kwa public na dunia, ndio ubepari tunaoutaka unavyotaka ndio maana unaona watu kama Michuzi sasa wanapeta maana anachikifanya kule Michuzi blog ndio hasa maana ya ubepari, indivualism kwanza!

Ahsante Wakuu.

William.

Naona na hapa Tanzania tuanzishe Club ya kujisifu. Nchi nyingine kuna Club za aina hiyo. Utaratibu unakuwa kwanza unasimama mwenyewe unajisifu wee na baadaye wana member wengine wanasimama kumsifu aliye jisifu na humo humo wanajisifu mwenyewe. "Majisifu si upinde". Siungi mkono kuiga mambo ambayo hayana faida na taifa kwa kisingizio cha ubepari.
 
Si ameingia katika siasa mwenyewe ? Si alitaka uwaziri mkuu huyu baada ya mwandosya kushinda uraisi kama angepata ? Si ndio huyu huyu alimtibua sana kikwete wakati yuko katika mchakato kule dodoma si anajua siasa mchezo mchafu ?

Cheap thinking always ends up in cheap talk/writing.
I can almost pick the brains of this gentleman.
 
Mambo mengine yanaumiza kichwa na wakati mwingine yanatia hasira; kwenye ajali iliyomhusisha marehemu Chacha Wangwe tulishuhudia polisi wakifanya uchunguzi kwa utaalamu wanaojua wao na dereva kufungwa.

Ajali ya Mh Chenge; polisi waliunda tume/kamati kufanya uchunguzi; hakuna ripoti iliyowekwa (sorry kama walitoa), Chenge kama mhusika mkuu pamoja na kuendesha gari bila bima na kusababisha vifo aliendelea kudunda uraiani huku polisi wakimsaka mwenye bajaji (sio dereva) ambapo alijisalimisha na kuswekwa mahabusu kwa siku kadhaa lakini Chenge hata chumba cha mahabusu Oysterbay hakuingizwa.

Hii ya Mh Mwakyembe polisi wameunda kamati ya uchunguzi haraka na kutoa taarifa ambayo inamsafisha dereva wa lori ambalo linadhaniwa kusababisha ajali huku mwadhirika wa ajali akiambiwa kuwa ni mzembe.

Swali la kujiuliza; Polisi wetu wanafanya kazi kwa kufuata maelekezo ya mtu/utashi wa kundi fulani la watu ama wanazo taratibu zinazotakiwa kufuatwa katika kutekeleza majukumu yao?, kama wanazo taratibu zao; mbona haziko sawa kwa kila mtu ama tukio lililokusudiwa katika uchunguzi?

Inashangaza kuona taratibu zinakuwa tofauti pale inapohusu mathalani kiongozi wa Serikali vs Raia wa kawaida, mwanachama/kada wa CCM vs mwanachama wa chama kingine cha siasa na vinginevyo.

Tusipokuwa makini mtindo huu wa utendaji kazi unaweza kuzaa hali ambayo sio nzuri kwa jamii yetu, mfano raia kuamua kujichukulia sheria mikononi inatokana na wao kutokuwa na imani na vyombo vya dola hususani polisi.
 
Kwi kwi kwi!! Sikujua Wanyaki mna majivuno hivyo! Toka lini majivuno na kujiamini vikawa na maana moja? Hivi uelewa mpana na wa kina unapimwa vipi?

Kazi kweli kweli TZ!

Na wasio na majivuno wana wivu sana. Na mimi naoan ni bora mwenye majivuno kuliko mwenye wivu.Mimi naona msubiri tu kwenye kinyang'anyiro utapeta tu wewe si mtu wa watu!
 
Last edited:
Yaani hapa mimi ndo ninapochoooooka kabisa............... siasa nitaomba niwe nakusoma magazetini na kukusikia maredioni tu. Mimi wewe sikuwezi nalikimbiza bawa langu.
 
Hakika ni vizuri sana tukajua nani mmiliki wa Lorry linalohusishwa na ajali hii. Lilitokea wapi, linaelekea wapi?
 
Hivi Mwakyembea mbona muongo hivi huyu Mbunge? Leo anadai alisema toka awali hii ni ajali, na hiki nini:

wewe hujamuelewa.....
hio ndio kauli yake ya kwanza......wewe umerukia kauli yake ya pili
uwe unaelewa mkuu..

Mkuu Yo Yo,

Huyo hawezi kuelewa kama akili yake haitaki kuelewa ukweli halisi, itang'ang'ania kile tu ambacho masikio yake na ubongo wake unapenda kusikia na kuona!
 
mwakyembe ana mawazo ila siasa imechanganyika zaidi kutokana na nafasi yake na hali ya kisiasa kwa sasa nchini...

nina maswali
1. je jeshi letu la polisi haliaminiki?
2. jeshi la polisi linatumika kwa masilahi ya kikundi fulani?
3. je mwakyembe anatumia ushawishi alionao kwenye jamii kwa sasa kulidhalilisha jeshi la polisi?
 
hii hapa chini ni taarifa ya dk mwakyembe ambayo ameituma kwenye kampuni ya guardian limited baada ya kuona hata jeshi la polisi limeingia kwenye upotoshaji;




siasa, siasa, saiasa.??????????????​
 
Mwakyembe ugua upone. katika hili nadhani kuna mtu anatufunga kamba kidogo tu lakini. kwani speed za hayo magari zilikuwa kiasi gani? maana kama mtu anamuovertake mtu aliye ni speed 100 inamaana anaenda sio pungufu ya 110 na ukungu na baridi na umande hamadi shimo hili hapa, unategemea nini? tuwe wakweli jamani. Tusitimie ajali kujikweza kisiasa na tuwasamehe polisi kwa kusema kweli.
 
1. je jeshi letu la polisi haliaminiki?
2.

Ndiyo. Unaweza kulitumia utakavyo. Kwa mfano, kuna siku gari langu liligongwa kwa nyuma na jamaa mmoja kwenye foleni. Alichofanya huyo jamaa ni kwamba alimpigia simu trafiki mmoja pale Oysterbay wakaongea kilugha halafu akaja akapima ajali na kunitia hatiani. Ndiyo polisi wetu hao.

2. jeshi la polisi linatumika kwa masilahi ya kikundi fulani?

Ndiyo. Kwa mfano ukiwa na hela angalau kidogo unaweza kumtumia polisi utakavyo. Jaribu.

3. je mwakyembe anatumia ushawishi alionao kwenye jamii kwa sasa kulidhalilisha jeshi la polisi?

Sidhani na haiwezekani kwamba alipanga hii ajali itokee ili apate nafasi ya kulidhalilisha jeshi la polisi.
 
''ni nani katika kamati hiyo ana utaalamu kunipita mimi?''

hakya mungu nchi hii!!!!!?

we acha tu.
 
Jamani hivi Mwakyembe kosa lake nini hadi achukiwe vibaya hivi? kusoma riport ya Richmond! au kuwa mwenyekiti wa tume iliyo wakaanga kina Lowassa!?
Yaani hata humu JF wako watu wanamchukia hadi naamini wangesikia kafa wangeshangilia! Lakini mimi nawaambia kati ya giza walilolichagua ni NURU ndiyo itakayoshinda!
Mnalitumikia giza kwa makusudi au kwa "ujinga" tu wa kupenda ubishi wa kitoto.
Haya mambo yako wazi kuyaunganisha, Mwakyembe anapigwa vita na serikali kwa kutumia vyombo vyake vya dola, na baadhi ya watu wajingajinga tu... kwa kosa a kusema kweli, kweli? Mnashabikia mtu asie nakosa auliwe!?
 
FMES Na KAMAUDOULTON Heshima kwenu!!!
Nimeusoma ushauri wenu umetulia sana na nafikiri Dr. Mwakwembe anapaswa kuufuata na kuachana na malumbano yenye lengo la kumwondoa kwenye point.

Kwa kawaida ya mchezo wa ngumi ukiwa kama bondia inapofikia wakati umefanikiwa kumumiminia bondia wenzio ngumi nyingi basi unatakiwa kuongeza speed kubwa yakuendelea kumimina makonde ili uweze kushinda na kinachoendelea sasa ni kwamba Makonde ya vita ya ufisadi yamepungua na yanahitajika kumiminwa sana na watu wengi sana na sio Dr mwakyembe peke yake,Dr mwakyembe ongeza speed ya kumimina makumbora zaidi wataishiwa pumzi na kusalimu amri.
 
Na wasio na majivuno wana wivu sana. Na mimi naoan ni bora mwenye majivuno kuliko mwenye wivu.Mimi naona msubiri tu kwenye kinyang'anyiro utapeta tu wewe si mtu wa watu!

Mkuu Shalom,
"Mtu wa watu" kwi kwi kwi!! nimeipenda hii na nitaiweka kwenye manifesto yangu ya kugombea ubalozi wa mtaa hapa kijijini kwangu.

Mwenye wivu si ni yule anayekwamisha vijana wa Kyela wasiendelee? Mtu akiona vijana wanafanya kweli kiroho kinaanza kumpanda? Utamwonea wivu mtu anayeshindwa ku deliver ili iweje?

Mkuu nimekwambia tafuta sababu nyingine lakini huko kwenye majivuno au wivu hutanikuta. Kama Wanyika mmejaaa majivuno huku mnashindwa kufanya la maana kule kwenu mtakuwa wajinga kweli kweli.

Elimu ya kweli ni ile inayokusaidia kutatua matatizo yanayokuzunguka, sio ile ya kutamba mitaani na kutundika vyeti ofisini.

Elimu nzuri ni kama Dr. aliyoitumia kule kwenye Richmond, wala hakuhitaji kutamba, ile report ilikuwa inajiuza yenyewe.
 
- Shujaa wangu Mwakyembe, achana na haya malumbano lumbano yasiyo na faida,rudi kwenye ku-focus na ishu muhimu za taifa kama zamani ulivyokuwa,

- Hivi nyinyi mlio karibu naye mmegundua kuwa ni muda mrefu sana sasa mafisadi wamemuondoa kwenye focus ya taifa na kumuweka kwenye ulingo wa kuji-defend defend tu all the time kwa muda mrefu sasa...
Valid, timely observation and ushauri pia. Labda sasa wanaanza 'kulipiza kisasi' maana nimesikia maneno maneno yakisemwa.... 'kama vile alivyomfanyia Lowassa kushindwa kumhoji kwenye sakata la Richmond....'
Lakini hatutaki kupelekwa huko. Lets return to the issues
 
Inakumbusha wakati ule, Inspekta Zombe aliongea na press na kusema something like..wananchi wakae kimya hawana utaalamu kama wao Jeshi la Polisi. Wao, Jeshi, wanafanya mambo kisayansi etc etc. Sasa kama yale aliyosema Dk. Mwakyembe hospitali kuhusu ajali ni uongo basi hiyo "ndoto" ya lori kuwabana na kufanya watoke nje ya barabara ilikua a very very lucid dream. I wish I could dream like that..
 
Back
Top Bottom