Ajali ya Dr. Mwakyembe na yatokanayo

Ajali ya Dr. Mwakyembe na yatokanayo

Kuna vitu vingi sana huwa vinatokea hapo tz kiaina aina.
Haya magari wakati mwingine yanatumika kama silaha. Inabidi tuwe macho sana. Ningewashauri wahusika wachunguze mahali alifanyia service au matengenezo ya mwisho ya hilo gari kabla ya safari.
 
Mkuu Mpita Njia naungana nawe kwamba shimo linaloonekana kwenye picha ni dogo sana kusababisha ajali mbaya kama hiyo hasa kwa gari ya kazi kama landcruiser. Hata hivyo maelezo ya dereva anasema kuwa, wakati yupo kwenye jitihada za kukwepa shimo, lori likagonga kwa nyuma na kusababisha gari kupinduka mara 4. (Hii ni kwa mujibu wa bbc/swahili

Na kama ni kweli tairi lilichomoka, basi clue ya mahali lilipolala gari (Makambako) ni muhimu.

...hapo mnazungumzia split-sec decisions, ...mfano,angekuwa ana overtake @ 120kph angehitaji sekunde ngapi 'kujitahidi' kulikwepa shimo lililo mita 12 toka kwenye gari lake..?

...akubali tu alikuwa kwenye mwendo mkali, aliyumba na kusababisha ajali. Kama kagongwa kwa nyuma mbona gari haijabonyea? Asimtie dereva mwenziwe matatani bure.
 
... soma habari ya jamaa wa Iringa kwenye blog yake wametoa link, ameelezea yaliyotokea. Baada ya hapo ndiyo uanze haya maelezo yake si vizuri kuhukuma kama hujafanya utafiti wa kutosha. Ajali ni kitu cha kawaida kabisa katika nchi zetu ambazo barabara zetu ni mbovu. Kama umesafiri barabara ya Dar Mbeya utakubaliana nami, naweza kusema hii barabara imeharibika sana hasa kipande cha Iringa mjini mafinga ukiachilia mbali kipate cha iyovi mpaka iringa mjini ambacho ukarabati wake umeanza pia hizi barabara zetu hazina alama zote za barabarani ambazo zingweza kusaidia kuonyesha tahadhari. Pia wakati mwingine husababishwa na uzembe wa madereva kutofuata alama za barabarani na kanuni za kuovertake.

Eti barabara zikoje? Stop it, hakuna asiye ijua Bongo hapa. Hiki kishimo kwa hali halisi ya Tanzania hii njia ni mkeka super highway hii! Shimo cha mtoto hili nalo shimo hili la kuimwaga shangingi, unless uko nduki au tingas.

i390_Shimo.JPG


Unakubali kwamba ni uzembe wa gari lao ku overtake na ku speed halafu unanambia nifanye utafiti kwenye link ya "jamaa wa Iringa." Jamaa wa Iringa alikuwepo ndani ya gari? Tunataka a free and full testimony from the driver tujue kama alikuwa under duress ya bosi kama dereva wa hayati Mbatia alivyokuwa anashinikizwa kila mara ku speed ovyo ovyo. Tunataka a fair and full fledged inquiry hapa.

Tunakemea janga la ma ajali halafu magari ya viongozi ndio yamekuwa vinara vya uendeshaji reckless?
 
Last edited:
Tunataka a free and full testimony from the driver tujue kama alikuwa under duress ya bosi kama dereva wa hayati Mbatia alivyokuwa anashinikizwa kila mara ku speed ovyo ovyo. Tunataka a fair and full fledged inquiry hapa.

Inquiry ya nini tena wakati tayari umeshetengeneza idea?

Tunakemea janga la ma ajali halafu magari ya viongozi ndio yamekuwa vinara vya uendeshaji reckless?
inquiry ya nini tena wakati umeshakuwa na idea?
 
Na kama ni kweli tairi lilichomoka, basi clue ya mahali lilipolala gari (Makambako) ni muhimu.
Kwamba tairi liling'oka nilizungumza na Advicate Nyombi (RPC wa Iringa) akaniambia hivyo
 
Mkuu Mpita Njia naungana nawe kwamba shimo linaloonekana kwenye picha ni dogo sana kusababisha ajali mbaya kama hiyo hasa kwa gari ya kazi kama landcruiser. Hata hivyo maelezo ya dereva anasema kuwa, wakati yupo kwenye jitihada za kukwepa shimo, lori likagonga kwa nyuma na kusababisha gari kupinduka mara 4. (Hii ni kwa mujibu wa bbc/swahili

Na kama ni kweli tairi lilichomoka, basi clue ya mahali lilipolala gari (Makambako) ni muhimu.

Shangaa kuwa licha ya first insight kutoka kwa wana JF kuhusiana na ajali hii,bado kuna contradictions nyingi sana tu.

Sasa hapo juu ina maana kuwa ni magari matatu yamehusika kwenye ajali ama ni mawili tu? Maana inawezekana vipi kugongwa kwa nyuma na gari ambalo uko kwenye process ya kuli overtake?

No wonder dereva yuko chini ya ulinzi wa polisi kwasababu inawezekana ana ya kujibu kutokana na stories tofauti tofauti anazozitoa kuhusiana na nini haswa kilichosababisha ajali hiyo,na inconstencies kama hizo hupelekea mawazo ya wanachi kuwander na kujiuliza how come?

Dillunga,kama unajuwa,then ni wazi utaelewa ninachotaka kusema,kipindi cha nyuma na pengine hadi sasa,matajiri wakipata taarifa ya ajali ya gari ama lori lake,basi kitu cha kwanza wanachouliza ni hali ya gari na si hali ya dereva,ilikuwa ni kama utamaduni na baadhi yao waliligunduwa hilo na kuanza kuulizia hali ya dereva na konda,then hali ya gari. Mfano huu hapo juu hauko directly linked na uliyasema hapo nyuma kuwa Mwakyembe alitakiwa amtake care dereva. Ikija kwenye ajali,wote ni victims tu. MKJJ keshaelezea kwenye posting yake na hivyo sioni umuhimu wa kuendeleza yale yale ambayo yameshasemwa,cha msingi ni kwamba wote walikuwa wakihitaji huduma za matibabu na wako under control huku madaktari wakiwa monitor na kuwapa ushauri wa hapa na pale kama kumpumzika,kutoongea nk. Kuna uwezekano mkubwa sana kuwa Mwakyembe alimuulizia mgonjwa/victim mwenzake,mara nyingi sana victims waliopata ajali pamoja huwa wanaulizia kuhusu wenzao.

Nguvu unayotaka aitumie Mwakyembe haina anything to do with hospital's rules and regulations na ushauri wa madokta,labda kama ulijisahahu ukadhani yuko bungeni na kwahivyo anatakiwa kupiga kelele.

Dokta pamoja na udokta na ubunge wake, hawezi kuingilia shughuli za profeesionals na wakati na wakati hawezi kujifanyia uchunguzi wenyewe ili kuweza kujua ni madhara kiasi gani amepata. Hata alipopelekwa MOI,si yeye aliamuwa ni madaktari,kwa maana kwamba anaweza akawa alivunjika ama kupata fracture. Kujaribu kusema Mwakyembe alitakiwa kutoa uamuzi wa nini kifanyike kimatibabu kwa dereva wake ni uonevu usiokuwa na mpango.
 
Pole sana Dr. Mwakyembe. Lakini tutumie fursa hii kujadili. Ajali Tanzania, Nani wa kumlaumu? Serikali, Madereva? au wengineo?. Kwa mujibu wa miongozo, watumiaji barabara wanapaswa kuendesha KM 80 kwa saa. Viongozi (hasa Mbunge, mwanasheria) haeshimu agizo hili. Matokeo yake tutasema shimo limesababisha ajali, au njama, au vinginevyo. NATOA POLE SANA KWA SOTE TUNAOGUSWA NA AJALI ZA BARABARANI.
 
Ogah,

Wapo kazini... Wangejua kuna mambo wanakosa wakiwa guests...!

Mkuu invinsible nilitarajia wewe ndio utakuwa wa kwanza kufahamu kuwa kuonyesha "guest" haimaanishi kuwa anayesoma hapa si memba. Kuna memba wanasoma tu kabla ya kulog-in ni wazi watatokea kama wageni.
Halafu hii limitation imeanza lini kuwa JF is 'exclusive' for members only? Ni heri hao wanaosoma tu kama wapita njia kuliko members wasiotaka kuona JF inazidishiwa uhai, if you figure out what I mean.
 
Ninapata tabu kidogo na jinsi hizi habari mzilivyoripotiwa maana nimesikiliza BBC wanasema kuwa wamefanya mahojiano na Dereva wa Mh Mwakyembe na akasema kuwa lori liliwagonga kwa nyuma sasa huko kwengine twaambiwa shimo ndo limesababisha dah,, N'way naamini atakapopata nafuu atazungumza yeye mwenyewe binafsi maana natambua ujasili alionao kama kuna baya lilipangwa juu yake basi atalisema wazi.
Mungu akujalie uzima na amani upone haraka
Amen
 
Miaka yote eneo hili barabara kuwa na mashimo ni kawaida, sijui kwa nini mashimomashimo tu, hata katika barabara kubwa inayounganisha mataifa.
Mungu amjalie afya njema mheshimiwa wetu.
 
basi angeonyesha leadership, angesema kutoka kitandani, jamani mnanipeleka Muhimbili, mwenzangu yuko wapi, kapona? Kama kaumia zaidi, anakuja na mimi kwa ma specialists? Tusimtelekeze mwananchi wangu.


kutoka Mwananchi:

''Hivi ninavyozungumza (jana saa 11 jioni) tayari amefikishwa Muhimbili na tayari anashughulikiwa na madaktari,'' alisema Dk. Kashilila na kuongeza kuwa Dk Mwakyembe alikuwa akizungumza kwa shida wakati na kulalamikia maumivu ya kichwa na mabega.

naona ungependa apewe karatasi aandike "jHivi ninavyozungumza (jana saa 11 jioni) tayari amefikishwa Muhimbili na tayari anashughulikiwa na madaktari,''

au kutumia ishara ya mikono kuonesha uzalendo wake.
 
Dr. Mwakyembe na dereva wako nawapa pole.

Kama wengi walivyochangia ajali haina kinga. Inaweza ikatokea wakati wowote na kwa yeyote.Nimeshawishika kukubali kwamba hiyo ilikuwa ni ajali kama nyingine ingawaje I am also not ruling out possibility of conspiracy. Whatever the case, huyu Bwana tushukuru Mungu hayuko katika hali mbaya na kwa taarifa za Mzee Invisible tayari yuko Muhimbili.

Kitendo cha huyu Bwana kufikishwa muhimbili kwa mawazo yangu mepesi, kina mu-expose kwenye hatari zaidi na hivyo inabidi serikali iweke ulinzi wa kutosha (ingawaje serikali hiyo hiyo inaweza isifurahie kuyasikia haya) na kuhakikisha huyu bwana ana Dr. maalumu na nesi wanao muhudumia ili kutotoa nafasi kwa mafisadi (RA, EL na wengine) kuitumia hiyo nafasi kumdhuru. Ni rahisi kumnunua nesi akaingia pale na kumchoma sindano ya sumu ambayo itamuua pole pole hata baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali.

Inabidi tuwe macho. Naogopa kuipa serikali mzigo huu wa kumlinda Dr. Mwakyembe kwani nayo ni sehemu ya ufisadi (mafisadi ndio watawala).

Otherwise, I wish Dr. Mwakyembe and his drive a quick recovery.

Tiba
 
Naangalia Chenel ten sasa ivi inaonekana ndo anafikishwa dar kwa uchunguzi zaidi .Tumuombee mungu apone haraka shujaa wetu.
 
we have been here before.. and we are going to be here again.. until we hate and reject totally and unequivocally to be here again.. otherwise.. we stuck in this time warp continuum..
 
Mungu wasaidie wapone haraka, kinga mkono wako na wachanganye lugha mafisadi wasielewane ili wasi mdhuru Dk. Mwakyembe.
 
Mwanakijiji, hiyo taarifa ina details zaidi. Mwakyembe wanasema kachubuka tu, Bunge limesema ameenda Muhimbili kuchekiwa chekiwa tu. Dereva Joseph Msuya kaumia kichwa lakini kaachiwa aende zake:

"Mbunge wa Kyela, Dr. Harrison Mwakyembe... alipata michubuko kidogo...

Hata hivyo, mganga mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa, Oscar Gabone alisema Dk Mwakyembe aliumia taya na hali yake sio mbaya sana kwani mfupa wa taya haukuvunjika.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashilila aliiambia Mwananchi kuwa Mwakyembe aliwasili jijini kwa ndege iliyotua jana alasiri na kupelekwa hadi Muhimbili....


...na kulazwa kwenye wodi ya kitengo cha mifupa cha MOI.


Mara baada ya ajali hiyo, Dk Mwakyembe alipelekwa katika hospitali ya mkoa wa Iringa kwa ajili ya matibabu na baadaye ofisi ya Bunge ilimtumia ndege kumchukua na kumkimbiza jijini Dar es Salaam kwa uchunguzi zaidi wa afya yake.

Alieleza kuwa wakati mbunge huyo amepelekwa Dar es Salaam, dereva wake aliyeumia kichwani na kukimbizwa pamoja naye katika hospitali ya mkoa wa Iringa, alitibiwa na kuruhusiwa.

Dk. Kashilila alisema kuwa Ofisi ya Bunge ipo tayari kutoa msaada kwa mbunge huyo kutibiwa hata ikiwa ni nje ya nchi, lakini akasisitiza itategemea ushauri wa wataalamu wanaomtibu.
``

Source: Hakimu Mwafongo, Iringa na Leon Bahati Da

Duu, Mbunge kachubuka chubuka, anachunguzwa zaidi, hohehahe kaumia kichwani kaachiwa lwake ajiju!
 
Mwanakijiji, hiyo taarifa ina details zaidi. Mwakyembe wanasema kachubuka tu, Bunge limesema ameenda Muhimbili kuchekiwa chekiwa tu. Dereva Joseph Msuya kaumia kichwa lakini kaachiwa aende zake:



Duu, Mbunge kachubuka chubuka, anachunguzwa zaidi, hohehahe kaumia kichwani kaachiwa lwake ajiju!

nimeyasoma yote hayo.. lakini sijaona kosa la Mwakyembe ni lipi kiasi cha kutuhumiwa kumtekeleza mgonjwa mwingine ambaye ameruhusiwa na madaktari au mtu mwingine kwenda nyumbani wakati ameumia kichwani? Kuna mahali popote panadokeza Dr alikuwa anajua dereva kaumia kichwani au karuhusiwa kwenda nyumbani?
 
mtakatifu dilunga bana.....yaani mwakyembe anakosa tena?
 
Back
Top Bottom