Ajali ya Mh Regia - tuna tatizo

Ajali ya Mh Regia - tuna tatizo

Ushabiki unatuharibu, na ukweli unaonekana kupotoshwa. Kifo cha Regia kwa vyo vyote kimechangiwa kwa vikubwa na Regia mwenyewe kwa hoja zifuatazo:
  1. Kuendesha gari akiwa mlemavu akitumia mguu mmoja alio nao tena wa kushoto
  2. Kutovaa ukanda wakati akiwa behind the wheel, maana yake alichomoka toka kwenye kioo cha mbele
  3. Kutokuwa na gari ambalo ni maalum kwa ulemavu wake
  4. Kutofuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na usalama wa over take, mwendo kasi nk
  5. Kutokuwa mfano wa kuigwa kutokana na wajibu wake kuwa mtunga sheria za nchi nii na kisha kuwa ndiye mvunjaji
  6. Kutomheshimu mwajiriwa wake (dereva wake) ni dalili ya ubinafsi
  7. Kupuuzi sheria za bima
  8. Hakuna hakika kama alikuwa na leseni ya kuendesha gari kihalali kutokana na utata wa ulemavu wake
  9. Kupuuzi utaratibu wa viongozi kuwatumia madereva wao
  10. Kujiona yuko juu ya sheria kwa hoja ya kuwa mbunge
Kuna mengi tu ingawa yanafunikwa funikwa, lakini ukweli unabaki kifo hiki ni uzembe wa hali ya juu ambao unagusa hata vyombo na mamlaka ya sheria, usalama na utoaji leseni. Tusifanya kufuru kwa Mungu kwamba Mungu alipanga wakati mambo haya yanaweza kukwepeka. Mbona mmoja aliyenusurika katika ajili hiyo aliongea kuwa kilichomwokoa ni kuvaa ukanda, na possible wengi waliomo walifanya hivyo na ndio usalama wao. Tunajifunza mengi katika ajali hii na tuongee ukweli kwa uwazi kwani yanatufunza wewe na mimi kuwa makini tuwapo behind the wheel. Hata kama taifa halitutegemei kwa uwazi kama aliyokuwa mbunge, lakini ndugu, jamaa familia na marafiki tunakuhitaji, na bado Mungu amekujalia uhai una haki na kuwajibika kuulinda vinginevyo uzembe hautapokeleka kwa utetezi wa aina ye yote.
 
Kila mtanzania ni hazina ya Taifa, wazima na walemavu

Mbona huulizi walemavu wanahudumiwa vipi kwenye hii nchi?

usisahau kuwa nchi yetu ulikuwa inaongozakwa kua ALBINO sasa jiulize wenye ulemavu mwingine wakoje hali zao?

Jibu zuri sana' halafu huyo jamaa aelewe kuwa Regia amepata ajari ambazo zinawatoke hata madereva ambao hawana ulemavu' naamini Regia amefariki kwa ajari iliyosababishwa na mwendo kasi wakati anaovateki na wala siyo kwa sababu ya ulemavu wake.
 
Nadhani hata tuliobaki tunaweza kupata somo kutokana na yale yaliyotokea. Kwa hiyo nadhani ni muhimu tukajadili hili kwa kina, si kwa maana ya kumshushia lawama marehemu, bali kupata funzo la nini kilifanywa vuisivyo na kuwa uwezekano wa chanzo cha ajali ile ili sisi tuliobaki tujiepushe kufanya kama hivyo.

Yap Mkubwa!!tunataka watu kama ww ambao kweli wana show kind of great thinking on the matters! tunapashwa kujiuliza, kutambua, kuchukua tahadhari, na mengine mengi hasa kabla ya matukio hayajatokea!!tusiongee kwa ushabiki tu. Wa JF-wenzangu ili tupate mabadiliko ya kweli kama nchi lazima tukubaliane na kukubali kubadilika.Tunatambua kuwa mpendwa wetu hayupo tena sasa ndio tusijadili yajayo?la hasha! lazima tujipange kwa mengi tuu.
 
Tulishajadili hili toka jumamosi.........mwacheni apumzike na ile ilikuwa ni ajali tu......hata Sokoine alikufa kwa ajali japo hakuwa na ulemavu


Ajali kama hii iliyokatisha maisha ya Regia Mtema, si mpango wa Mungu. Ni dhambi kubwa kusema kwamba huu ni mpango wa Mungu. Kama barabara ya kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro, ingekuwa ni ya njia nne, ajali kama hii ya Regia Mtema na nyingine nyingi zinazotokea kila wakati kwenye barabara hii zisingetokea.
 
Ajali kama hii iliyokatisha maisha ya Regia Mtema, si mpango wa Mungu. Ni dhambi kubwa kusema kwamba huu ni mpango wa Mungu. Kama barabara ya kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro, ingekuwa ni ya njia nne, ajali kama hii ya Regia Mtema na nyingine nyingi zinazotokea kila wakati kwenye barabara hii zisingetokea.

ajali hazitaepukika hadi magamba yote yatoke
 
Wakulu

Nimesukumwa kuandika haya baada ya kufuatilia tukio zima la ajali ya Mh. Mbunge ambaye sasa ni marehemu.

Mh. Regia alikuwa mlemavu wa mguu wa kulia.Gari aliyokuwa anaendesha kwa mujibu wa taarifa za jeshi la polisi lilikuwa halijafanyiwa -modification kwamba ni gari maalumu kwa ajili ya walemavu.

Sasa swali, ni mamlaka gani ilitoa leseni kwa Marehemu? wakati anajulikana kwamba ni mlemavu...... (ukizingatia kwamba kwa mujibu wa sheria zilizopo, hata ukiwa na makengeza huruhusiwi kupewa leseni)

Nauliza hili kwa uchungu tukizingatia kwamba Regia alikuwa ni hazina ya taifa...... mpaka lini tutaendelea kupoteza vijana wenye uwezo mkubwa wa kulisaidia taifa hili ...kwa kuruhusu uzembe,kutoheshimu sheria na mambo yanayofanana na hayo?

Ilikuwaje mfumo mzima kuanzia serikali kupitia vyombo vyake vya TRA, Trafiki polisi, ndugu, chama chake, marafiki zake, abiria aliokuwa nao kwenye gari kwa nyakati mbalimbali hawakuliona hili kwamba ni tatizo kwa marehemu kuendesha gari wakati yu mlemavu ? kwa nini hawakumkemea, hawakumshauri ....n.k

Sheria , kanuni na taratibu zipo kutulinda.....naamini TUNA TATIZO KUBWA KULIKO TUNAVYODHANI.....

Naomba tujadili objectively...bila jazba...

Umeangalia upande wa leseni kwa walemavu Mkuu, wakati kuna mambo mengi yamechakachuliwa. Hilo la Regia kuwa na leseni wakati ni mlemavu ni ndogo lakini umeshangaa, bado hujakuta mtu mtu hana miguu yote na hana jicho moja lkn anamiliki leseni ya Abiria
 
Nakubaliana na wanaosema kuwa ajali ya mh.Regia haikutokana na ulemavu wake bali ni kulipita gari mahali ambapo hapakustahili na hili linawatokea wengi na kwakweli linatupotezea wapendwa wetu wengi.

Ni kweli pia haipendezi kumjadili marehemu lakini kama tunaweza kujifunza kitu kutokana na waliyoyafanya waliotutangulia ni vema kwani muhimu ni sie tuliohai kujifunza ili ikiwezekana tusianguke katika jambo lilelile la wenzetu japo kifo hatutakikwepa milele.

RIP Regia Mtema.
 
Ushabiki unatuharibu, na ukweli unaonekana kupotoshwa. Kifo cha Regia kwa vyo vyote kimechangiwa kwa vikubwa na Regia mwenyewe kwa hoja zifuatazo:
  1. Kuendesha gari akiwa mlemavu akitumia mguu mmoja alio nao tena wa kushoto
  2. Kutovaa ukanda wakati akiwa behind the wheel, maana yake alichomoka toka kwenye kioo cha mbele
  3. Kutokuwa na gari ambalo ni maalum kwa ulemavu wake
  4. Kutofuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na usalama wa over take, mwendo kasi nk
  5. Kutokuwa mfano wa kuigwa kutokana na wajibu wake kuwa mtunga sheria za nchi nii na kisha kuwa ndiye mvunjaji
  6. Kutomheshimu mwajiriwa wake (dereva wake) ni dalili ya ubinafsi
  7. Kupuuzi sheria za bima
  8. Hakuna hakika kama alikuwa na leseni ya kuendesha gari kihalali kutokana na utata wa ulemavu wake
  9. Kupuuzi utaratibu wa viongozi kuwatumia madereva wao
  10. Kujiona yuko juu ya sheria kwa hoja ya kuwa mbunge
Kuna mengi tu ingawa yanafunikwa funikwa, lakini ukweli unabaki kifo hiki ni uzembe wa hali ya juu ambao unagusa hata vyombo na mamlaka ya sheria, usalama na utoaji leseni. Tusifanya kufuru kwa Mungu kwamba Mungu alipanga wakati mambo haya yanaweza kukwepeka. Mbona mmoja aliyenusurika katika ajili hiyo aliongea kuwa kilichomwokoa ni kuvaa ukanda, na possible wengi waliomo walifanya hivyo na ndio usalama wao. Tunajifunza mengi katika ajali hii na tuongee ukweli kwa uwazi kwani yanatufunza wewe na mimi kuwa makini tuwapo behind the wheel. Hata kama taifa halitutegemei kwa uwazi kama aliyokuwa mbunge, lakini ndugu, jamaa familia na marafiki tunakuhitaji, na bado Mungu amekujalia uhai una haki na kuwajibika kuulinda vinginevyo uzembe hautapokeleka kwa utetezi wa aina ye yote.

Nimependa comment yako mkuu, tuache mawazo finyu sisi binadamu!!uache kufunga mkanda, tuendeshe magari kwa speed kali tupate ajali useme Mungu amependa??? ni Mungu gani huyo anaependa watu wake wafe kwa uzembe!!!??
 
mi bado sijaelewa logic unayojenga hapa ni nini??

je unauliza swali mamlaka gani iluruhusu yeye kuendesha gari???

au unataka kutuambia kuwa ni uzembe wake???

au unailaumu serikari???

anywai ni hivi 'MHESHIMIWA MBUNGE ALIYEKUWA NA ULEMAVU WA MGUU ALIPATA AJALI YA GARI ALILOKUWA ANALIENDESHA MWENYEWE, NA ALIFARIKI DUNIA HAPO HAPO! (Sasa hayo mengine yaache kama yalivyo, kama ni uzembe wake au serikali au dreva wake poa, mungu amuweke mahari pema peponi)

Haya matatizo ya kutotaka kumweleza mfalme kwamba yu uchi yatatufikisha pabaya.Kama kweli tunayo mapenzi mema na mpendwa wetu aliyetangulia mbele ya haki, hatuwezi kukwepa kujiuliza hayo unayouliza badala ya kutoa majibu.Ni uzembe na kutowajibika kuanzia mwanzo hadi mwisho.Mamlaka iliyoruhusu RM kuendesha gari kwa kukubali kutoa Leseni bila kukagua na kujiridhisha kwamba gari atakayotumia ni maalum kwa hali yake ya ulemavu.Lakini kubwa kuliko yote yeye mwenyewe Marehemu kukamilisha uzembe wa Mamlaka husika kujiaminisha na kukamata usukani.

Tusipokuwa Wakweli na kudanganya nafsi zetu kwamba kulikuwa hakuna kosa kuanzia kwenye Mamlaka husika hadi kwa Muhusika ambaye sasa ni Marehemu, kwa kisingizio cha Oh tuna mapenzi naye hakika huo utakuwa ni unafiki ambao haujawahi hata kufikiwa na Magamba Camp katika kipindi chote cha maika 50 ya utawala wao.Mtoa hoja ana jambo la msingi kama ilivyowahi kuingizwa humu wakati wa Mazishi lakini baadhi ya Wana JF mkatsisitiza kuipotezea.
 
Mkuu Wayne Heshima Mbele

Nadhani ulikuwa na hoja nzuri lakini ukuifanya kikamilifu kwa kuweka ushahidi wa baadhi ya lawama/Shauku zako

1) Swali lako la pili unauliza ni mamlaka gani iliyotoa leseni kwa Marehemu
Nadhani kwanza ungetuwekea hiyo leseni ya Marehemu na tukaiona imetolewa ikiwa kwenye Category gani, maana najua leseni zote zinakuwa na sehemu ya kuonyesha mwenye leseni ana ugumu gani wa kuendesha gari, (Mlemavu, anavaa miwani nk)

2) umesema Polisi walilikagua gari na kuthibitisha kuwa halikufanyiwa marekebisho ya kuendana na mlemavu
hapa point kumbe sio tatizo kwa mlemavu kuendesha gari (na ndio maana wana leseni za kuendeshea), maana hata polisi wanalijua hilo na Marehemu sio Mlemavu wa kwanza kuendesha gari, kumbe tatizo ni gari alikuwa kwenye kiwango staili kwa mlemavu

Mimi nakubaliana na wewe kuwa ukiukwaji wa kanuni na sheria ulifanywa na MArehemu, kwa kutumia leseni yake kuendesha asichoruhusiwa, ni uvunjwaji wa sheria unaoonekana ni wa kawaida machoni pa watu, ni kama mtu mwenye leseni ya gari ndogo kuitumia kuendeshea malori nk

Pamoja na hayo yote, kwa mujibu wa waliopona hiyo ajali, ni kuwa hiyo ajali haihusiani na ulemavu hata kidogo, kama alikuwa anataka kuovertake na likatokea gari lingine mbele, hapo hata kama hakuwa mlemavu hali ingekuwa ni hiyohiyo tu,

Pamoja na kuwa na hoja ya kuwa kwa nini watu wa kwenye gari hawakumkemea kwa kuendesha gari, lakini nadhani wangemkemea zaidi kwa speeding, umakini wa kuangalia kabla ya kuovertake na vitu kama hivyo


Hapo pa RED sema Alivunja Sheria ya Barabara ku ovatake ama penye mlima au penye kona.
 
Nadhani ajali ni ajali tu. Mama wa kaya aliwahi kugonga mtu na msafara wake. Mumewe aliwekewa Mafuta machafu huko kaskazini. Then Gari lake tairi zilibuma huku Dar. Mwakyembe je Si alikuwa na qualified driver akala mzinga?
Kuna Mzee mwingine alikufa kwa ajali ya ndege Mbeya Kama sijakosea.
Hiyo ni mifano michache tu. Mchango wako haujengi. Angekuwa hajui kudrive asingefika hata huko Ruvu. Tumwache apumzike kwa Amani jamani.
ajali inakuwa na maana endapo umetimiza sheria zote za barabarani lakini ikatokea tu. kwa mfano umefunga mkanda, gari liko hali nzuri, umefuata sheria zote za barabarani, watu atasema kweli mungu ametwaa!!! ila hizi nyingine ni wewe kujitwalisha maana ukiwa barabarani lazima 100% brain yako iwe hapo hapo tu hasa kwenye long safari. Madereva wengine utakuwa hupo 120km/h then anakula kula au anapiga ma-story na abilia aisee!!! au anaongea na simu.... Sasa hapo wakuu si ni kum-beep islael.

Mtindo huu wa kutupia lawama kwa mola katika kila kitu siyo vizuri - hatumsemei mabaya kwa marehemu, ila sisi tuliobaki tubadilike - kuna watu wanaenda Dar - Arusha 5 hrs - harafu wanajisifu - haya ndiyo mambo tunayosema yabadilike - ajali nyingi ni za kujitakia wenyewe.

Kuna siku naenda Moshi, nimepita wami then kuna kile kipande cha barabara kimenyooka fresh, mimi nina 120km/h kuna mtu ana V8 alinipita kwa kasi ya ajabu, nafikiri alikuwa na more than 180km/h. sasa wakuu huo ndiyo udereva? je ukikutana gari bovu au lori lina-overtake lori jingine utapona kweli? au mnyama anavuka barabara utapona kweli? ukifa sisi tuliobaki tusemeje?

haya bwana, ushauri tu - mkinununa nuneni. ila ajali zingine tunazitafuta wenyewe na lazima zitokee.
 
Kila mtanzania ni hazina ya Taifa, wazima na walemavu

Mbona huulizi walemavu wanahudumiwa vipi kwenye hii nchi?

usisahau kuwa nchi yetu ulikuwa inaongozakwa kua ALBINO sasa jiulize wenye ulemavu mwingine wakoje hali zao?
Ingekua Busara ukaanzisha thread yako kuliko kuchakachua hoja iliyopo kwa kutumia hoja yenye msingi lakini tofauti.
 
wakati nachangia kwenye thread za kifo chake, niligusia suala hili japokuwa sikusema juu ya mamlaka. Nilisema yeye mwenyewe kasababisha kifo chake, kwani ni mlemavu halafu anaendesha gari MANUAL, ambayo inahitaji kutumia viuongo mbalimbali vya mwili kuliendesha.

pili nilizungumza kuwa, kitendo cha yeye kutokuwa na dereva kwa safari hiyo wakati tayari serikali inamlipa hela ya dereva tena wa daraja la juu la kuendesha viongozi wa serikali, nao ni ufisadi. kunyima vijana wenye daraja lessen C, kumemgharimu maisha, kumetugharimu watanzania kwani tulikuwa bado tunamhitaji tuendelee kupambana.

Mwisho nilisisitiza vyombo vilivyopewa mamlaka kusimamia sheria visiangalia sura ya mtu katika kusimamia sheria, japokuwa vinalalmikiwa lakini wasimame kama taasisi wawashitaki wale wanaotumia fedha za walipakodi kujinufaisha. Na waanze na wabunge ambao mpaka sasa wamekataa kuajiri madereva wenye sifa kuwaongoza safarini, huu ni ufisadi kwa wabunge
aiseeeeeeeeeeeee arifu a yu shua?
 
Nimependa comment yako mkuu, tuache mawazo finyu sisi binadamu!!uache kufunga mkanda, tuendeshe magari kwa speed kali tupate ajali useme Mungu amependa??? ni Mungu gani huyo anaependa watu wake wafe kwa uzembe!!!??

Mkuu MCHOMAMOTO nakupa bigup kinoma, baadhi yetu tumejenga tabia ya kumuhusisha MUNGU na upuuzi wetu,Ajali za kujitakia utasikia Oh Mapenzi ya MUNGU.Ujinga huo unanikera sana , MUNGU wa aina gani Mshenzi kiasi hicho anayetaka Kiumbe wake aliyemuumba kwa mfano wake akampulizia pumzi ya Uhai afe kwa Kuangukiwa na Container lenye tani 50 halafu tuseme ni mapenzi ya MUNGU, naapa MUNGU wa namna hiyo simtaki na nitajenga urafiki na Shetani ambaye hawezi kuua Wanadamu kwa mtindi huo.Lini tutakubali kwamba hizo ni kazi za shetani kupitia kwa washenzi wanaokula rushwa na kutoa Leseni nyuma ya Mlango hata kama Muhusika haja Qualify kupata hiyo Leseni.Lini tutasema Mungu amemjalia Mchomamoto juhudi katika kazi zake hadi ameweza kujenga nyumba na kununua gari, badala yake tutasema Mchomamoto ametumia nguvu za giza kupitia maombi ya Mchungaji fulani kupata pesa zilizomletea maendeleo.Simo kwenye unafiki wenu, RM amechangai kifo chake kwa 100%.Jambo la kujadili hapa ni kuwataka wengine wenye mawazo kama yake Marehemu RM,wasithubutu kurudia alichokifanya kwa kuwa LAZIMA WATAKUFA KWA AJALI na itafika mahali hata kama tunawapenda kiasi gani, kamwe sitawalilia
 
Uache uongozi wa chadema, wao wanashughulikia masuala makubwa kama Ufisadi na maandamano, usalama wa uhai wa mtu kama marehemu Regia kwao sio muhimu, ingekua muhimu wangemshauri awe na dereva japo kwa safari ndefu kama hizo.

kama mtu umekosa la kusema bora ukae kimya mkuu ,Chadema inahusika vip na kifo cha Regia,?

Mwacheni dada wa watu apumzike kwa amani.wote tuko njia moja tunafatia
 
Kwa kweli kwenye hili kuna maswali mengi sana ambayo kwa mtu yeyote lazima utajiuliza,na hii inaonyesha jinsi waTz wengi walivyo waoga kuwa-kosoa/onya/kemea... wapendwa au marafiki/ndugu zao.
 
Subirini na wengine watapata ajali barabara hiyo hiyo ndo mtajua kuwa swala si ulemavu tu na wala sio ubunge pia!!
 
Pumzika kwa amani da Regia E. Mtema, nilikupenda sana kama my Political Icon!
 
Nadhani tungejadili kuhusu usalama barabarani na sio kujiuliza maswali yasiyo na tija na majibu kwasasa..Mum kalala nadhani tuangalie mengine,hasa usalama barabarani,maana kuna uchafu unafanyika barabarani kupita kawaida.
 
Back
Top Bottom