Ajifungua na kutupa kichanga maeneo ya Shule

Mjanja M1

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2018
Posts
4,058
Reaction score
14,382
MWANAMKE ambaye hajafahamika jina lake na anayedaiwa kuwa ana ulemavu wa akili, amejifungua mtoto mchanga kisha kumtupa kwenye eneo la shule ya msingi Msali "A" iliyopo kijiji cha Ngararambe kata ya Nyakahura wilayani Biharamulo mkoani Kagera, huku baba wa mtoto huyo akiwa hajulikani.

Akizungumza na Nipashe Digital shuhuda wa tukio hilo ambaye pia ni Diwani wa viti maalumu kata ya Nyakahura, Ziyuni Hussein, amesema kuwa alipokea taarifa za tukio hilo kwa njia ya simu kutoka kwa baadhi ya walimu wa shule hiyo na kwamba alipofika eneo la tukio alishuhudia kichanga hicho kikiwa kimetupwa kwenye mchanga na kulazimika kukichukua kwaajili ya kukihudumia ili kunusuru maisha yake.

Chanzo: Nipashe
 
Kwanini baadhi ya wanaume wanapenda kudinya wanawake wenye matatizo ya akili?
Au ni madomo zege au hawana pesa za kuhonga??
Wanaleta vichanga visivyo na baba.
 
Mada hizi zikitimiza 10k comment naomba kuwa babu shetani.labda tunda kimasiara
 
Kuna wanaume ni useless kabisa.

Unampaje mimba kichaa, na ukimpa si uhudumie mtoto sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…