Ajira mpya hakuna, halafu hela mnakula wenyewe, Good God will pay you

Ajira mpya hakuna, halafu hela mnakula wenyewe, Good God will pay you

Wanaukumbi.

Serikali tuliiamini na tukavumilia mateso ya mtaani tukijipa matumaini makubwa kuwa mnaijenga nchi baadae mambo yatakuwa mazuri, kumbe fedha zinatumiwa hovyo, mlikuwa na uwezo wa kuajiri kila mwaka na kuongeza mishahara ila mliamua kubana ili hizo hela za umma na kufanya ufisadi kama ripoti ya CAG, inavyosema.

CAG anaonesha namna mabeberu wetu walivyokuwa wanaitafuna hii nchi, huku wamejificha kwenye kimvuli cha uzalendo.

Ripoti hii ya CAG imetuonyesha kuwa:
  • Tunahitaji taasisi imara na siyo fikra za mtu mmoja anayejidai imara
  • Tunahitaji wanasiasa visionary wanaojali maslahi ya muda mrefu ya Watanzania na vyama imara vya siasa.
Baba yako kasemaje?
 
Toka Cag atoe taarifa napata wageni wengi wakuwaagua wanakuja na yale magari makubwa meusi na vioo vyake vyeusi
 
Inakera Sana yaani😔😔😔nmejifunga mkanda miaka 6 nikiamini nawekeza kwa ajili ya vizazi vijavyo,kumbe pesa inachezewa na wanaojiita WAZALENDO!

Mama Samia tupandishe madaraja waajiliwa wa 2014 maana vichwa vinauma,pia usisahau kuongeza mishahara na annual increments,TUMEVUMILIA SANA,TUMECHOKA SASA!!
 
Kasema Mama yako leo aje nyumbani leo usiku mkiwa mmelala.
Ila meko aliwapiga sana kudadeki.
Ma UDA yote yake aliyafyekelea mbali
Hadi nasikia ulishindwa kulipa ada za watoto.
Inaabidi uchunguzi huru ufanyike nyie ndio mmepiga ndumba
 
Sisi wana wa maskini tuna miaka takribani 6 sasa mtaani bila ajira baada ya kuhitimu vyuo. Wanatwambia wanajenga uchumi imara kwanza ndipo watuajiri.

Kumbe kujenga uchumi ndiko huku? Mamilioni kwa Mabilioni kwa matrilioni, wametafuna. Sisi tunateseka mtaani bila ajira,huku HESLB nao wakituongezea zigo liitwalo retention fee.

Wanataka tuandamane?

Ila ngoja, Mungu wetu ni Mungu wa haki.

ATALIPA TENA.
Shangaa na wewe eti ajira milioni nane zilitengenezwa!
 
Watu wanajifunza kutokana na makosa yao au ya wengine.

Natumai wanafunzi wa sasa hivi wanajifunza hapa.
 
Jiwe nilimuona wa ajabu sanaa.

Kunyanyasa vijana kutoajiri huku akitoa ahadi hewa.
Bora aende tuu , hakuwa na faida yyte , unatengeneza ndege hewa bil 3 na ushehe, hasara mabill ya kutosha , malipo hewa mara kibao , mara ujenge uwanja wa ndege chato , alaf nyongeza ya mishahara hamna , ajira hamna , kwenye Kodi tunakabana koooo.... jamaa linatia hasira sana
 
kwa haya madudu, marehem anatakiwa afukuriwe atandikwe viboko na kabur lake linyewe juu
Anatia hasira basi tuu , alaf lilikuwa halitaki watu waseme , huyu jamaa wakat anaingia madarakani nilikuwa fan wake Ila kuanzia 2019 ndo niliona jamaa ni wa hovyo saana
 
Ila meko aliwapiga sana kudadeki.
Ma UDA yote yake aliyafyekelea mbali
Hadi nasikia ulishindwa kulipa ada za watoto.
Inaabidi uchunguzi huru ufanyike nyie ndio mmepiga ndumba
Tabia za mashoga utazijua tu unajifanya unanijua hahahahha.
 
Si tulikubaliana ni mabeberu wametuchezea sana jamani sasa mbona mnaanza kulalamikaaaaa
 
Tabia za mashoga utazijua tu unajifanya unanijua hahahahha.
Ila mwanangu punguza matusi.

Najua sio wewe hapa nakuzingua tu.
Ila hata kama sio wewe lakini meko aliwaweza sana.
Dingilee alimpigania akamuweka pale juu ila jamaa likawageuka.
Likageuka kila mtu.
Yaani hatutosahau.

Ila kiufupi long live mshua.
 
Kaka sijajua umesomea nini, lakini kwa ntu yoyote aliyesoma mambo ya biashara mfano uhasibu, masomo, uchumi n.k alikuwa anajua kabisa uchumi wa nchi tunauweka chini.

Sikuwahi kuuelewa utawala awamu ya 5 kabisa. Toka aingie madarakani jamaa hakuajiri kabisa, huku mtaani mpaka vyeti vinanuka.

Watoto zao wana vipato, sisi huku tunalia na hali ya maisha kila siku.
 
Back
Top Bottom