Ajira Portal inahitaji mabadiliko, inakatisha ndoto za vijana wengi kwenye kuomba ajira

Ni
Kweli mzee kule amna upendeleo ila naona pale kwenye academic wamerekebisha tofaut na mwanzo
 
Changamoto #2 naiona sio changamoto kabisa.
Unajua mtu akiwa na njaa ya ajira hata akiwa na PhD ukimwambia nitakulipa laki 4 anakubali.
Ukimwajiri tu akizoea mazingira ataanza kuona anaonewa, ataanza kupoteza morali, ataanza kuibia serikali kwa hasira.
Atasema nalipwa mshahara mdogo kuliko elimu yangu, kuna watu tuko na level moja ya elimu au nimewazidi lakini wanalipwa ndefu.
Haya umeajiriwa kwa certificate lakini una diploma, na degree kabatini, na kazini supervisor wako aidha ana degree au diploma utajisikiaje?
Serikali ina akili kuliko wewe
 
Tatizo sio Portal..., Tatizo ni Hizo Ajira hazitoshi / hazikidhi mahitaji; unadhani demand ingekuwa kubwa kuliko supply wangetoa hata pesa na ku-advertise kwenye maluninga, matovuti na sms hata wale wasio na simu janja au vishikwambi waweze kujisetiri....

Yaani wewe sio kuomba tena / Kuapply bali ni kubembelezwa; ila ndio hivyo tena....
 
Aisee pole sana hii kitu inasumbua wengi sana na sijui kwaniin
Wale walioenda leo dodoma kufanya usaili wa BAKITA ...msanifu lugha na mchunguzi lugha walitoa maswali gani na mangapi?
 
Nakwambia ni disaster
 
Kama umewahi kufanya application ya maombi ya kazi kupitia mfumo wa ajira portal utakubaliana na mimi huu ni mfumo wa kijinga sana kuwahi kutokea

Just imagine wametangaza nafasi za kazi za Tutoria Assistant(Accounting and Finance). Wanataka mtu aliesomea ACCOUNTING AND FINANCE or BUSINESS ADMINISTRATION IN ACCOUNTING AND FINANCE, kama inavyoonesha hapa chini;



Sasa mtu amesomea chuo Bachelor of business administration in accounting na mfumo unakukubali kuomba kazi unaomba, mwisho wa siku wanakuja kusema hauna qualification na wakati G.P.A iko sawa kisa tu iyo finance😭😭



Halafu unawapigia simu wanasema mtu unakua umeucheat mfumo wakati vyeti na kila kitu umewawekea, how can this be possible..huu mfumo wa portal ni wa kipumbavu...otherwise hizi changamoto zinakatisha ndoto za watu wengi na ukizingatia majina yenyewe wanachelewa kuita watu.
 
Kama vile ambavyo wanafunzi wanaosoma vyuoni kushindwa kuelewa kwamba unaweza kupata kazi kwa kutumia hata module moja tu..ndivyo hivyo hivyo hao watu wa PSRS wanavyokariri kwamba lazima usome accounting nkt hata mtu aliesoma Finance kuna maswala yanamuwezesha kufanya..kwenye accounting
 
Ni wajinga sana mkuu
 

Udhaifu, Maoni na Mapendekezo kwa Tume ya Ajira "PSRS"
 
Asante mkuu labda mods wataangalia namna gan wauweke uzi wangu kwenye post yako maana hata mimi nimepiga simu kapokea mdada ambaye kabisa ni kama hajui anachokisema..kuna haja hata ya makatibu siku moja moja kupiga simu za hao jamaa waone watu wao walivo hawana weledi na majukumu yao..iyo system ya kishenzi na kipuuzi
 
Ushauri wa bure..kama una umri wa miaka 30 una degree yako ni mwaka wa 3 unatafuta ajira hujaipata achana na hizo ishu unapoteza muda, kuna umri ukifika watu hawatotaka kujua umesoma mpaka wapi ila wao watataka waone maendeleo yako tu...........
 
Wakuu naombeni msaada, kila ninapojaribu ku update picha naona ina load tu lakini haibadiliki.

Picha iliyopo sasa hivi niliiweka wakati nipo certificate, sasa haikuwa ya passport size ilikuwa ni picha ya kawaida tu ya photo shoot.

Kwa anaejua namna ya ku update picha nyingine naomba anisaidie maana kila nikijaribu inagoma, msaada wakuu tafadhali.
 
Subiri usiku mtaandao ukikaa vizuri jaribu tena hapo ni ishu ya network tu wala sio kingine
 
na huenda ushaiupoad sema hiyo search engine ndo inakupa huo mrejesho.

fanya hivi tumia search engine nyingine kulogin kwa mf..kama ulisearch na samsung internet/google now tumia chrome then login...!

Au tumia device nyingine kulogin.Kama ulitumia simu yako kusearch(kuplload) now tumia simu/laptop nyingine kulogin.

then, lete mrejesho.
 
Shukrani mkuu itabidi nijaribu njia hii nikifanikiwa ntaleta mrejesho ndugu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…